< 2 Rois 16 >
1 En la dix-septième année de Phacée, fils de Romélie, régna Achaz, fils de Joatham, roi de Juda,
Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
2 Achaz avait vingt ans lorsqu’il commença à régner, et il régna seize ans à Jérusalem: il ne fit point ce qui était agréable en la présence du Seigneur son Dieu, comme David son père;
Ahazi alikuwa na miaka ishirini alipoanza kutawala, akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na sita. Tofauti na Daudi baba yake, hakufanya yaliyo mema machoni pa Bwana, Mungu wake.
3 Mais il marcha dans la voie des rois d’Israël; de plus il consacra même son fils, le faisant passer par le feu, selon le culte des idoles des nations qu’avait dissipées le Seigneur devant les enfants d’Israël.
Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, na hata akamtoa mwanawe kafara katika moto, akifuata njia za machukizo za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele ya Waisraeli.
4 Il immolait aussi des victimes, et offrait de l’encens sur les hauts lieux, sur les collines, et sous tout arbre couvert de feuillage.
Akatoa kafara na kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu, juu ya vilima, na chini ya kila mti uliotanda.
5 Alors Rasin, roi de Syrie, et Phacée, fils de Romélie, roi d’Israël, montèrent à Jérusalem pour livrer bataille, et quoiqu’ils tinssent Achaz assiégé, ils ne purent pas le vaincre.
Kisha Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli wakaondoka kwenda kupigana dhidi ya Yerusalemu na kumzunguka Ahazi kwa jeshi, lakini hawakuweza kumshinda.
6 En ce temps-là, Rasin, roi de Syrie, rendit Aila à la Syrie, et chassa les Juifs d’Aila; et les Iduméens vinrent à Aila, et ils y ont habité jusqu’à ce jour.
Wakati ule, Resini mfalme wa Aramu akaurudisha Elathi kwa Aramu kwa kuwafukuza watu wa Yuda. Kisha Waedomu wakahamia Elathi, nao wanaishi huko mpaka leo.
7 Alors Achaz envoya des messagers à Théglathphalasar, roi des Assyriens, disant: Je suis votre serviteur et votre fils; montez, sauvez-moi de la main du roi de Syrie et de la main du roi d’Israël, qui se sont levés ensemble contre moi.
Ahazi akatuma wajumbe kumwambia Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru kwamba, “Mimi ni mtumishi na mtumwa wako. Njoo na uniokoe kutoka mkononi mwa mfalme wa Aramu na wa mfalme wa Israeli, ambao wananishambulia.”
8 Et ayant amassé l’argent et l’or qui put être trouvé dans la maison du Seigneur et dans les trésors du roi, il envoya au roi des Assyriens des présents.
Naye Ahazi akachukua fedha na dhahabu zilizopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme, na kuzituma kama zawadi kwa mfalme wa Ashuru.
9 Celui-ci acquiesça à sa volonté: le roi des Assyriens, en effet, monta à Damas, et la ravagea; il en transféra les habitants à Cyrène, mais il tua Rasin.
Mfalme wa Ashuru akamwitikia kwa kushambulia Dameski na kuiteka. Akawahamishia wenyeji wake huko Kiri, na kumuua Resini.
10 Alors le roi Achaz alla à la rencontre de Théglathphalasar, roi des Assyriens, à Damas; et lorsqu’il eut vu l’autel de Damas, le roi Achaz en envoya au prêtre Urie le modèle et la représentation d’après tout le travail de cet autel.
Kisha Mfalme Ahazi akaenda Dameski kukutana na Tiglath-Pileseri wa Ashuru. Akaona madhabahu huko Dameski, naye akamtumia Uria kuhani mchoro wa hayo madhabahu, pamoja na maelezo ya mpango kamili wa ujenzi wake.
11 Urie, le prêtre, construisit donc l’autel; selon tout ce que le roi Achaz avait ordonné de Damas, ainsi fit le prêtre Urie, jusqu’à ce que le roi Achaz vint de Damas.
Kwa hiyo Uria kuhani akajenga madhabahu kulingana na mipango yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ameituma kutoka Dameski, na akamaliza ujenzi kabla ya Mfalme Ahazi kurudi.
12 Et lorsque le roi fut venu de Damas, il vit cet autel, et il le révéra; puis il monta, et immola les holocaustes, et son sacrifice;
Mfalme aliporudi kutoka Dameski na kuona hayo madhabahu, akayasogelea na kutoa sadaka juu yake.
13 Et il fit des libations, et répandit le sang des hosties pacifiques qu’il avait offertes sur l’autel.
Akatoa sadaka yake ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka, akamimina sadaka ya kinywaji na kunyunyizia damu ya sadaka zake za amani juu ya hayo madhabahu.
14 Quant à l’autel d’airain qui était devant le Seigneur, il le transféra de devant la face du temple, de la place de l’autel et de la place du temple du Seigneur, et il le mit à côté de l’autel, vers l’aquilon.
Mfalme Ahazi akayaondoa madhabahu ya zamani ya shaba kutoka hapo mbele ya Hekalu la Bwana, yaliyokuwa yamesimama kati ya ingilio la Hekalu na hayo madhabahu mapya, naye akayaweka upande wa kaskazini mwa hayo madhabahu mapya.
15 Le roi Achaz ordonna aussi à Urie, le prêtre, disant: Offre sur le grand autel l’holocauste du matin et le sacrifice du soir, l’holocauste du roi et son sacrifice, l’holocauste de tout le peuple, leurs sacrifices et leurs libations; mais tout le sang des holocaustes et tout le sang des victimes, tu le répandras sur cet autel; et quant à l’autel d’airain, il sera préparé selon ma volonté.
Ndipo Mfalme Ahazi akatoa amri zifuatazo kwa Uria kuhani: “Juu ya hayo madhabahu kubwa mapya, toa sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa na sadaka ya jioni ya nafaka, sadaka ya mfalme ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa ya watu wote wa nchi, pamoja na sadaka yao ya nafaka na sadaka yao ya kinywaji. Unyunyize juu ya hayo madhabahu damu yote ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu. Lakini mimi nitatumia hayo madhabahu ya zamani ya shaba kwa ajili ya kutafuta uongozi.”
16 Ainsi Urie, le prêtre, fit tout selon ce qu’avait ordonné le roi Achaz.
Naye Uria kuhani akafanya kama Mfalme Ahazi alivyoagiza.
17 Or le roi Achaz enleva les bases ciselées et le bassin qui était dessus, et il ôta la mer de dessus les bœufs d’airain, qui la soutenaient, et il la mit sur le pavé, qui était de pierre.
Mfalme Ahazi akaondoa mbao za pembeni na kuondoa masinia kwenye vile vishikilio vilivyohamishika. Akaondoa ile Bahari kutoka kwenye mafahali wa shaba walioishikilia, na kuiweka kwenye kitako cha jiwe.
18 Même le Musach du sabbat, qu’il avait bâti dans le temple, et l’entrée extérieure du roi, il les transporta dans le temple du Seigneur, à cause du roi des Assyriens.
Kwa heshima ya mfalme wa Ashuru, akaliondoa pia pazia la Sabato lililokuwa limewekwa ndani ya Hekalu, na akaondoa ile njia ya kifalme ya kuingia kwenye Hekalu la Bwana.
19 Mais le reste des actions d’Achaz, qu’il a faites, n’est-il pas écrit dans le Livre des actions des jours des rois de Juda?
Matukio mengine ya utawala wa Ahazi na yale aliyoyafanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
20 Et Achaz dormit avec ses pères, et fut enseveli avec eux dans la cité de David, et Ezéchias, son fils, régna en sa place.
Ahazi akalala na baba zake, naye akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Hezekia mwanawe akawa mfalme baada yake.