< 2 Chroniques 9 >

1 La reine de Saba aussi, ayant appris la renommée de Salomon, vint à Jérusalem pour l’éprouver par des énigmes, avec de grandes richesses, et des chameaux qui portaient des aromates, et une grande quantité d’or, et des pierres précieuses. Et lorsqu’elle lut venue vers Salomon, elle lui dit tout ce qui était en son cœur.
Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni, huyo malkia akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu. Alifika akiwa na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani, alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
2 Et Salomon lui expliqua tout ce qu’elle avait proposé, et il n’y eut rien qu’il ne lui éclaircît.
Solomoni akamjibu maswali yake yote, wala hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwake asiweze kumwelezea.
3 Après qu’elle eut vu ces choses, c’est-à-dire la sagesse de Salomon et la maison qu’il avait bâtie,
Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
4 Ainsi que les mets de sa table, les logements de ses serviteurs, les emplois de ceux qui le servaient, et leurs vêtements; de plus, ses échansons, leurs habits, et les victimes qu’il immolait dans la maison du Seigneur, son esprit n’était plus en elle, à cause de son étonnement.
chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika Hekalu la Bwana alipatwa na mshangao.
5 Et elle dit au roi: il est véritable, le récit que j’avais ouï dans mon pays, de vos vertus et de votre sagesse.
Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
6 Je n’ai pas cru à ceux qui me parlaient, jusqu’à ce que je sois venue moi-même, que mes yeux aient vu, et que j’aie reconnu que la moitié de votre sagesse ne m’avait pas été racontée: vous avez surpassé la renommée par vos vertus.
Lakini sikuamini yaliyosemwa hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana kuliko ile taarifa niliyoisikia.
7 Heureux vos sujets, et heureux vos serviteurs, qui sont devant vous en tout temps, et qui écoutent votre sagesse!
Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
8 Béni soit le Seigneur votre Dieu, qui a voulu vous placer sur son trône, roi du Seigneur votre Dieu. Parce que Dieu aime Israël, et qu’il veut le conserver à jamais, c’est pour cela qu’il vous a établi roi sur lui, pour rendre les jugements et la justice.
Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe, na akakuweka juu ya kiti chake cha ufalme utawale kwa niaba ya Bwana Mungu wako. Kwa sababu ya upendo wa Mungu wako kwa Israeli na shauku yake ya kuwadhibitisha milele, amekufanya wewe mfalme juu yao, ili kudumisha haki na uadilifu.”
9 Or elle donna au roi cent vingt talents d’or, des aromates en très grande quantité, et des pierres précieuses: il n’y a pas eu d’aromates tels que ceux que donna la reine de Saba à Salomon.
Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa vikolezi vizuri kama vile Malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
10 Mais aussi les serviteurs d’Hiram avec les serviteurs de Salomon apportèrent de l’or d’Ophir, des bois odorants, et des pierres très précieuses.
(Watumishi wa Hiramu na wa Solomoni wakaleta dhahabu kutoka Ofiri, tena wakaleta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
11 Le roi fit avec ces bois odorants des degrés dans la maison du Seigneur et dans la maison du roi, et aussi des harpes et des psaltérions pour les chantres: jamais on n’a vu dans la terre de Juda de tels bois.
Mfalme akatumia hiyo miti ya msandali kuwa ngazi kwa ajili ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa Yuda tangu siku ile.)
12 Or le roi Salomon donna à la reine de Saba tout ce qu’elle voulut et ce qu’elle demanda, et beaucoup plus qu’elle ne lui avait apporté; et la reine, s’en retournant, s’en alla en son pays avec ses serviteurs.
Mfalme Solomoni akampa Malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, zaidi ya vile alivyokuwa amemletea mfalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
13 Or le poids de l’or qu’on apportait à Salomon chaque année était de six cent soixante-six talents d’or,
Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
14 Outre la somme que les députés de diverses nations et les marchands avaient accoutumé d’apporter, ainsi que tous les rois d’Arabie, et tous les gouverneurs des provinces, qui apportaient de l’or et de l’argent à Salomon.
mbali na mapato yaliyoletwa na wafanyabiashara na wachuuzi. Wafalme wote wa Arabuni na watawala wa nchi wakamletea Solomoni dhahabu na fedha.
15 Le roi Salomon fit donc deux cents lances d’or, d’une somme de six cents sicles d’or, qui étaient dépensés pour chaque lance;
Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa. Kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
16 Et de plus trois cents boucliers d’or de trois cents sicles d’or avec lesquels chaque bouclier était couvert; et le roi les plaça dans l’arsenal, qui était planté d’un bois.
Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
17 Le roi fit encore un grand trône d’ivoire, et le revêtit d’un or très pur;
Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
18 Et de plus six degrés par lesquels on montait au trône, un marchepied d’or, deux petits bras de chaque côté, et deux lions qui étaient près des deux petits bras,
Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na mahali pa kuwekea miguu vyote vya dhahabu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
19 Et aussi douze autres petits lions qui étaient sur les six degrés, d’un côté et de l’autre: il n’y a pas eu un tel trône dans aucun royaume.
Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
20 Tous les vases de la table du roi étaient également d’or, et tous les vases de la maison du bois du Liban aussi d’un or très pur; car l’argent, au jour de Salomon, était réputé comme rien,
Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo wakati wa Solomoni.
21 Attendu que les vaisseaux du roi allaient en Tharsis avec les serviteurs d Hiram une fois tous les trois ans; et ils apportaient de là de l’or, de l’argent, de l’ivoire, des singes, et des paons.
Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizoendeshwa na watu wa Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
22 Le roi Salomon surpassa donc tous les rois de la terre en richesse et en gloire.
Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
23 Et tous les rois de la terre désiraient voir la face de Salomon, pour écouter la sagesse que Dieu avait mise en son cœur;
Wafalme wote wa dunia wakatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
24 Et ils lui envoyaient des présents, des vases d’argent et d’or, des vêtements, des armes, des aromates, des chevaux et des mulets, à chaque année.
Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja, alileta zawadi, vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
25 Salomon eut encore quarante mille chevaux dans des écuries, douze mille chars et autant de cavaliers, et il les plaça dans les villes des quadriges, et où était le roi, dans Jérusalem.
Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 kwa ajili ya farasi na magari ya vita, farasi 12,000 ambao aliwaweka katika miji ya magari ya vita na katika Yerusalemu pamoja naye.
26 Il exerça aussi sa puissance sur tous les rois, depuis le fleuve d’Euphrate jusqu’à la terre des Philistins et jusqu’aux frontières d’Égypte.
Solomoni akatawala juu ya wafalme wote kuanzia Mto Frati mpaka kwenye nchi ya Wafilisti na kuendelea hadi mpaka wa Misri.
27 Et il procura une abondance d’argent dans Jérusalem comme celle des pierres, et une multitude de cèdres, semblable à celle des sycomores qui sont produits dans les plaines.
Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
28 Or on lui amenait des chevaux d’Égypte et de tous les pays.
Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka nchi nyingine zote.
29 Mais le reste des actions de Salomon, des premières et des dernières, est écrit parmi les paroles de Nathan, le prophète, dans les livres d’Ahias, le Silonite, et aussi dans la vision d’Addo, le Voyant, contre Jéroboam, fils de Nabath.
Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Nathani, katika unabii wa Ahiya Mshiloni na katika maono ya Ido mwonaji kuhusu Yeroboamu mwana wa Nebati?
30 Or Salomon régna à Jérusalem sur tout Israël, pendant quarante ans.
Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
31 Et il s’endormit avec ses pères; et on l’ensevelit dans la cité de David; et Roboam, son fils, régna à sa place.
Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Chroniques 9 >