< 2 Chroniques 25 >
1 Amasias avait vingt-cinq ans lorsqu’il commença à régner, et il régna vingt-neuf ans à Jérusalem: le nom de sa mère était Joadan de Jérusalem.
Amazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani kutoka Yerusalemu.
2 Et il fit le bien en la présence du Seigneur, mais non avec un cœur parfait.
Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kwa moyo wake wote.
3 Et, lorsqu’il vit son empire affermi, il fit égorger les serviteurs qui avaient tué le roi son père;
Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake.
4 Mais leurs enfants, il ne les tua point, comme il est écrit dans le Livre de la loi de Moïse, où le Seigneur a ordonné, disant: Des pères ne seront pas mis à mort pour des enfants, ni des enfants pour des pères; mais chacun mourra pour son péché.
Hata hivyo hakuwaua watoto wao, lakini akafanya sawasawa na ilivyoandikwa katika Sheria, katika Kitabu cha Mose, ambako Bwana aliamuru: “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto hawatauawa kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
5 Amasias assembla donc Juda, et il les établit par familles, tribuns et centurions dans tout Juda et Benjamin; et il les recensa depuis vingt ans et au-dessus, et il trouva trois cent mille jeunes hommes qui pouvaient sortir pour les combats, et porter une lance et un bouclier.
Amazia akawaita watu wa Yuda pamoja, akawaweka chini ya majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia kufuatana na jamaa zao katika Yuda yote na Benyamini. Kisha akawahesabu wale wenye umri wa miaka ishirini au zaidi na akakuta kwamba walikuwa wanaume 300,000 watu walio tayari kwa utumishi wa jeshi, walio na uwezo wa kutumia mkuki na ngao.
6 Il engagea aussi cent mille hommes robustes d’Israël au prix de cent talents d’argent.
Akawaajiri pia watu 100,000 wapiganaji kutoka Israeli kwa talanta 100 za fedha.
7 Or un homme de Dieu vint vers lui, et dit: ô roi, que l’armée d’Israël ne sorte pas avec vous; car Dieu n’est point avec Israël, ni avec les enfants d’Ephraïm.
Lakini mtu wa Mungu akamjia na kumwambia, “Ee mfalme, haya majeshi kutoka Israeli kamwe usiyaruhusu yaende pamoja na wewe kwa kuwa Bwana hayuko pamoja na Israeli, wala hayupo pamoja na yeyote wa watu wa Efraimu.
8 Que si vous croyez que la guerre consiste dans la force de l’armée, Dieu fera que vous serez vaincu par vos ennemis; car c’est à Dieu à secourir et à mettre en fuite.
Hata kama ukienda na kupigana kwa ujasiri katika vita, Mungu atakufanya ukimbie mbele ya adui, kwa kuwa Mungu anao uwezo wa kusaidia au wa kuangusha.”
9 Et Amasias demanda à l’homme de Dieu: Que sera-t-il donc fait des cent talents que j’ai donnés aux soldats d’Israël? Et l’homme de Dieu lui répondit: Le Seigneur a de quoi pouvoir vous donner beaucoup plus que ces cent talents.
Amazia akamuuliza yule mtu wa Mungu, “Lakini itakuwaje kwa zile talanta 100 za fedha nilizolipa kwa ajili ya haya majeshi ya Israeli?” Yule mtu wa Mungu akajibu, “Bwana aweza kukupa zaidi sana ya hizo.”
10 C’est pourquoi Amasias sépara l’armée qui lui était venue d’Ephraïm, afin qu’elle retournât en son lieu; mais c’est violemment irritées contre Juda que ces troupes retournèrent dans leur contrée.
Hivyo Amazia akayaondoa yale majeshi yaliyokuwa yamekuja kutoka Efraimu na kuyarudisha nyumbani. Waliwakasirikia sana Yuda, nao wakarudi nyumbani wakiwa na hasira kali.
11 Or Amasias, conduisit son peuple résolument; il alla dans la vallée des Salines, et il battit les enfants de Séir au nombre de dix mille.
Ndipo Amazia akajitia nguvu na kuliongoza jeshi lake kwenye Bonde la Chumvi, ambako aliua watu 10,000 wa Seiri.
12 Et les enfants de Juda prirent dix autres mille hommes; ils les amenèrent sur le pic du rocher, et les précipitèrent du haut en bas, et tous furent brisés.
Jeshi la Yuda pia likawateka watu 10,000 wakiwa hai, likawapandisha juu ya jabali na kuwatupa chini kwa nguvu hata wote wakavunjika vipande vipande.
13 Mais l’armée qu’Amasias avait renvoyée, afin qu’elle n’allât pas avec lui au combat, se répandit dans les villes de Juda, depuis Samarie jusqu’à Béthoron, et, trois mille hommes tués, elle enleva un grand butin.
Wakati huo yale majeshi Amazia aliyoyarudisha na ambayo hakuyaruhusu kushiriki katika vita, yalivamia miji ya Yuda kuanzia Samaria hata Beth-Horoni. Yakawaua watu 3,000 na kuchukua kiasi kikubwa sana cha mateka.
14 Or Amasias, après avoir taillé en pièces les Iduméens et avoir emporté les dieux des enfants de Séir, en fit des dieux pour lui-même; il les adorait, et leur brûlait de l’encens.
Amazia aliporudi kutoka kuwachinja Waedomu, alileta pia kutoka huko miungu ya watu wa Seiri. Akaisimamisha kama miungu yake mwenyewe, akaisujudia na kuitolea kafara za kuteketezwa.
15 C’est pourquoi le Seigneur, irrité contre Amasias, envoya vers lui un prophète pour lui dire: Pourquoi avez-vous adoré les dieux qui n’ont pas délivré leur peuple de votre main?
Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Amazia, naye akamtuma nabii kwake, ambaye alisema: “Kwa nini unauliza kwa miungu ya hawa watu, ambayo haikuweza kuwaokoa watu wake wenyewe kutoka mkononi mwako?”
16 Comme le prophète disait ces choses, Amasias lui répondit: Est-ce que tu es conseiller du roi? Tais-toi, de peur que je ne te tue. Alors le prophète se retirant: Je sais, dit-il, que Dieu a résolu de vous tuer, parce que vous avez fait ce mal, et que de plus vous n’avez pas voulu acquiescer à mes conseils.
Wakati nabii alipokuwa angali anazungumza, mfalme akamwambia, “Je, wewe tumekuchagua kuwa mshauri wa mfalme? Nyamaza, ya nini uuawe?” Hivyo nabii akanyamaza lakini akasema, “Najua kuwa Mungu ameazimia kukuangamiza kwa sababu umefanya jambo hili na hukusikiliza shauri langu.”
17 Ainsi Amasias, roi de Juda, ayant pris une détestable résolution, envoya vers Joas, fils de Joachaz, fils de Jéhu, roi d’Israël, disant: Venez, et voyons-nous mutuellement.
Baada ya Amazia mfalme wa Yuda kushauriana na washauri wake akatuma ujumbe kwa Yehoashi, mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli kusema: “Njoo tukabiliane uso kwa uso.”
18 Mais Joas renvoya les messagers, disant: Le chardon qui est au Liban envoya vers le cèdre du Liban, disant: Donnez votre fille à mon fils pour femme; et voilà que les bêtes qui étaient dans la forêt du Liban passèrent et foulèrent aux pieds le chardon.
Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda, “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti.
19 Vous avez dit: J’ai battu Edom, et c’est pourquoi votre cœur s’élève jusqu’à l’orgueil. Demeurez en votre maison: pourquoi provoquez-vous un malheur pour que vous tombiez, et vous et Juda avec vous?
Wewe unasema moyoni mwako kwamba umemshinda Edomu, nawe sasa unajigamba na kujivuna. Lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini utafute matatizo na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”
20 Amasias ne voulut pas l’écouter, parce que la volonté du Seigneur était qu’il fût livré dans les mains des ennemis, à cause des dieux d’Edom.
Hata hivyo, Amazia hakutaka kusikia, kwa kuwa Mungu alifanya hivyo ili awatie mikononi mwa Yehoashi, kwa sababu waliitafuta miungu ya Edomu.
21 Joas, roi d’Israël, monta donc, et les deux armées se mirent en présence. Or Amasias, roi de Juda, était campé à Bethsamès de Juda;
Hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akakwea kuwashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakabiliana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda.
22 Et Juda tomba devant Israël, et s’enfuit dans ses tabernacles.
Yuda ikashindwa na Israeli na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake.
23 Pour Amasias, roi de Juda, fils de Joas, fils de Joachaz, Joas, roi d’Israël, le prit dans Bethsamès, et l’emmena à Jérusalem; et il détruisit aussi son mur, depuis la porte d’Ephraïm jusqu’à la porte de l’angle, espace de quatre cents coudées.
Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akamleta Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.
24 Il emporta encore tout l’or et l’argent et tous les vases qu’il avait trouvés dans la maison de Dieu et chez Obédédom, et même dans les trésors de la maison royale; il ramena aussi à Samarie les fils des otages.
Akachukua dhahabu yote, fedha na vyombo vyote vilivyopatikana katika Hekalu la Mungu, ambavyo vilikuwa chini ya uangalizi wa Obed-Edomu, pamoja na hazina za jumba la mfalme na mateka, kisha akarudi Samaria.
25 Or Amasias, fils de Joas, roi de Juda, vécut quinze ans après que fut mort Joas, fils de Joachaz, roi d’Israël.
Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.
26 Mais le reste des actions d’Amasias, des premières et des dernières, est écrit dans le Livre des rois de Juda et d’Israël.
Kwa habari ya matukio mengine katika utawala wa Amazia, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na wa Israeli?
27 Après qu’Amasias eut abandonné le Seigneur, on lui tendit des embûches dans Jérusalem; et, comme il se fut enfui à Lachis, on envoya, et on le tua là.
Kuanzia wakati ule Amazia alipogeuka na kuacha kumfuata Bwana walifanya shauri baya dhidi yake huko Yerusalemu naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi nao wakamuulia huko.
28 Et le rapportant sur les chevaux, on l’ensevelit avec ses pères dans la cité de David.
Akarudishwa kwa farasi na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Yuda.