< 2 Chroniques 16 >

1 Mais à l’année trente-sixième de son règne, Baasa, roi d’Israël, monta en Juda, et environna d’un mur Rama, afin que nul du royaume d’Asa ne pût sûrement sortir et entrer.
Katika mwaka wa thelathini na sita wa utawala wa Asa, Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
2 Asa prit donc de l’argent et de l’or des trésors de la maison du Seigneur, et des trésors du roi, et envoya à Bénadad, roi de Syrie, qui habitait à Damas, disant:
Ndipo Asa akachukua fedha na dhahabu kutoka hazina ya Hekalu la Bwana na kutoka jumba lake mwenyewe la kifalme na kumpelekea Ben-Hadadi mfalme wa Aramu, ambaye alikuwa anatawala huko Dameski.
3 Il y a une alliance entre moi et vous; mon père aussi et le vôtre ont entretenu la concorde; c’est pourquoi je vous ai envoyé de l’argent et de l’or, afin que, rompant l’alliance que vous avez faite avec Baasa, roi d’Israël, vous l’obligiez à s’éloigner de moi.
Akasema, “Pawepo na mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
4 Cette nouvelle reçue, Bénadad envoya les princes de ses armées contre les villes d’Israël, lesquels frappèrent Ahion, et Dan, et Abelmaïm, et toutes les villes de Nephthali murées.
Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Wakashinda Iyoni, Dani, Abel-Maimu na miji yote ya hazina ya Naftali.
5 Lorsque Baasa l’eut appris, il cessa de bâtir Rama, et interrompit son ouvrage.
Baasha aliposikia jambo hili, akasimamisha kujenga Rama na kuacha kazi yake.
6 Or le roi Asa prit tout Juda avec lui, et ils enlevèrent les pierres de Rama et les bois qu’avaient préparés Baasa pour bâtir, et il en bâtit Gabaa et Maspha.
Ndipo Mfalme Asa akawaleta watu wote wa Yuda, nao wakachukua mawe na miti ambayo Baasha alikuwa anavitumia huko Rama. Kwa vitu hivyo akajenga Geba na Mispa.
7 En ce temps-là, Hanani, le prophète, vint vers Asa, roi de Juda, et lui dit: Parce que vous avez eu confiance dans le roi de Syrie, et non dans le Seigneur votre Dieu, c’est pourquoi l’armée du roi de Syrie s’est échappée de votre main.
Ikawa wakati huo mwonaji Hanani akamjia Mfalme Asa wa Yuda na kumwambia: “Kwa sababu ulimtegemea mfalme wa Aramu nawe hukumtegemea Bwana Mungu wako, jeshi la mfalme wa Aramu limeponyoka mkononi mwako.
8 Est-ce que les Ethiopiens et les Libyens n’étaient pas beaucoup plus nombreux en quadriges, en cavaliers et en une multitude considérable? Et comme vous aviez cru au Seigneur, il les livra en votre main.
Je, hukumbuki lililotendeka kwa Wakushi na Walibia, hawakuwa jeshi lenye nguvu na magari mengi ya vita na wapanda farasi? Hata hivyo, ulipomtegemea Bwana yeye aliwatia mkononi mwako.
9 Car les yeux du Seigneur contemplent toute la terre, et ils donnent de la force à ceux qui d’un cœur parfait croient en lui. Vous avez donc agi follement, et à cause de cela dès à présent des guerres s’élèveront contre vous.
Kwa kuwa macho ya Bwana hukimbiakimbia duniani kote ili kujionyesha mwenye nguvu kwa ajili ya wale ambao mioyo yao inamtegemea kwa ukamilifu. Umefanya jambo la upumbavu na kuanzia sasa na kuendelea utakuwa na vita.”
10 Mais Asa, irrité contre le Voyant, commanda qu’il fût mis dans les chaînes; car il avait été très indigné de ses paroles; et il tua en ce temps-là un grand nombre de personnes d’entre le peuple.
Asa akamkasirikia mwonaji kwa sababu ya jambo hili. Alikuwa ameghadhibika sana hata akamweka gerezani. Wakati huo huo Asa akaanza kuwatesa na kuwaonea baadhi ya watu kwa ukatili.
11 Or les actions d’Asa, les premières et les dernières, sont écrites dans le Livre des rois de Juda et d’Israël.
Matukio ya utawala wa Asa, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
12 Asa fut aussi malade, la trente-neuvième année de son règne, d’une douleur aux pieds très violente, et dans son infirmité il ne chercha point le Seigneur; mais il se confia davantage en l’art des médecins.
Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wake, Asa alipatwa na ugonjwa kwenye miguu yake. Ingawa ugonjwa wake ulimzidia sana, hata katika kuugua kwake hakutafuta msaada kutoka kwa Bwana bali kwa matabibu tu.
13 Et il dormit avec ses pères; et il mourut l’an quarante et unième de son règne.
Katika mwaka wa arobaini na moja wa utawala wa Asa, alikufa na kulala na baba zake.
14 Et on l’ensevelit dans son sépulcre qu’il s’était creusé dans la cité de David; et on le mit sur son lit rempli d’aromates et d’essences de femme de mauvaise vie, composées selon l’art des parfumeurs, et on les brûla sur lui en très grand appareil.
Nao wakamzika katika kaburi lile alilokuwa amejichongea mwenyewe katika Mji wa Daudi. Wakamzika kwa jeneza lililowekwa vikolezi na mchanganyiko wa manukato ya aina mbalimbali yaliyotengenezwa kwa utaalamu wa mtengeneza marashi, nao wakawasha moto mkubwa kwa heshima yake.

< 2 Chroniques 16 >