< 1 Timothée 2 >

1 Je demande donc instamment avant tout, qu’on fasse des supplications, des prières, des demandes, des actions de grâces pour tous les hommes,
Kwa hiyo awali ya yote, nahitaji maombi, na dua, na maombezi, na shukrani vifanyike kwa ajili ya watu wote,
2 Pour les rois et tous ceux qui sont en dignité, afin que nous menions une vie paisible et tranquille, en toute piété et chasteté.
kwa ajili ya wafalme na wote ambao wako kwenye mamlaka, ili kwamba tuweze kuishi maisha ya amani na utulivu katika utauwa wote na heshima.
3 Car cela est bon et agréable à notre Sauveur Dieu,
Hili ni jema na lenye kukubalika mbele za Mungu Mwokozi wetu.
4 Qui veut que tous les hommes soient sauvés, et viennent à la connaissance de la vérité,
Yeye hutamani kuwa watu wote waokolewe na wapate kuijua kweli.
5 Car il n’y a qu’un Dieu et qu’un médiateur entre Dieu et les hommes, le Christ Jésus homme,
Kwa kuwa kuna Mungu mmoja, na kuna mpatanishi mmoja kati ya Mungu na mwanadamu ambaye ni Kristo Yesu.
6 Qui s’est livré lui-même, pour la rédemption de tous, comme un témoignage temps.
Alijitoa mwenyewe kama fidia kwa wote, kama ushuhuda kwa wakati muafaka.
7 C’est pourquoi j’ai été établi moi-même prédicateur et apôtre (je dis la vérité, je ne mens point), docteur des nations dans la foi et la vérité.
Kwa sababu hii, mimi mwenyewe nilifanywa kuwa mjumbe wa injili na mtume. Nasema kweli. Sisemi uongo. Mimi ni mwalimu watu Mataifa katika imani na kweli.
8 Je veux donc que les hommes prient en tout lieu, élevant des mains pures, sans colère et sans contention.
Kwa hiyo, nataka wanaume kila mahali waombe na kuinua mikono mitakatifu bila ghadhabu na mashaka.
9 Pareillement, que les femmes, en vêtements décents, se parent avec pudeur et modestie, et non avec des cheveux frisés, ou de l’or, ou des habits somptueux;
Vivyo hivyo, nataka wanawake wajivike mavazi yanayokubalika, kwa heshima na kujizuia. Wasiwe na nywele zilizosukwa, au dhahabu, au Lulu, au mavazi ya gharama kubwa.
10 Mais comme il convient à des femmes qui font profession de piété par de bonnes œuvres.
Pia nataka wavae mavazi yanayowastahili wanawake wanaokiri uchaji kwa kupitia matendo mema.
11 Que la femme écoute en silence et dans une entière soumission.
Mwanamke na ajifunze katika hali ya utulivu na kwa utii wote.
12 Je ne permets point à la femme d’enseigner ni de dominer sur l’homme; mais qu’elle garde le silence.
Simruhusu mwanamke kufundisha, au kuwa na mamlaka juu ya mwanaume bali aishi katika hali ya ukimya.
13 Car Adam fut formé le premier, ensuite Eve,
Kwa kuwa Adamu aliumbwa kwanza, kisha Eva.
14 Et Adam ne fut point séduit, mais la femme séduite tomba dans la prévarication.
Adamu hakudanganywa, lakini mwanamke alidanganywa kabisa katika uasi.
15 Toutefois elle sera sauvée par la génération des enfants, si elle demeure dans la foi, la charité et la sainteté jointe à la tempérance.
Hata hivyo, ataokolewa kwa kupitia kuzaa watoto, kama wataendelea katika imani na upendo na katika utakaso na akili njema.

< 1 Timothée 2 >