< 1 Samuel 30 >
1 Or, lorsque David et ses hommes arrivèrent à Siceleg, au troisième jour, les Amalécites avaient fait une irruption du côté austral, contre Siceleg, avaient battu Siceleg et l’avaient mise à feu.
Ikawa, Daudi na watu wake walipokuwa wamefika Ziklagi siku ya tatu, Waamaleki walifanya mashambulizi katika Negevu na Ziklagi. Waliupiga Ziklagi, wakauchoma moto mji,
2 Et ils avaient emmené les femmes captives, et depuis le plus petit jusqu’au grand: ils n’avaient tué personne; mais ils avaient tout emmené avec eux, et ils s’en allaient par leur chemin.
na kuwachukua mateka wanawake na kila mmoja aliyekuwa ndani yake, mkubwa kwa mdogo. Wao hawakuua hata mmoja, lakini waliwachukua watu na kuondoka nao.
3 Lors donc que David et ses hommes furent arrivés à la ville, et qu’ils eurent trouvé qu’elle avait été mise à feu, et que leurs femmes, leurs fils et leurs filles avaient été emmenées captives,
Daudi na watu wake walipofika kwenye mji, ulikuwa umechomwa moto - na wake zao, watoto wao wakiume na wakike walichukuliwa mateka.
4 David et le peuple qui était avec lui élevèrent leurs voix, et pleurèrent jusqu’à ce que les larmes leur manquèrent.
Ndipo Daudi na watu aliokuwa nao wakapaza sauti zao na kulia hadi walipokuwa hawana nguvu zaidi za kulia.
5 Car même les deux femmes de David, Achinoam de Jezraël, et Abigaïl, femme de Nabal du Carmel, avaient été emmenées captives.
Wake wawili wa Daudi walichukuliwa mateka, yaani Ahinoamu Myezreeli, na Abigaili aliyekuwa mke wa Nabali Mkarmeli.
6 Et David fut très contristé; car le peuple voulait le lapider, parce que l’âme de chacun était dans l’amertume à cause de ses fils et de ses filles; mais David se fortifia dans le Seigneur son Dieu.
Daudi aliguswa sana, maana watu walikuwa wanaongea kuhusu kumpiga mawe, kwa sababu roho za watu wote walihuzunika, kila mtu kwa ajili ya mtoto wake wakiume na wakike, lakini Daudi alijiimarisha katika BWANA, Mungu wake.
7 Et il dit à Abiathar, le prêtre, fils d’Achimélech: Approchez-moi l’éphod. Et Abiathar approcha l’éphod de David.
Daudi akamwambia Abiathari, kuhani, mwana wa Ahimeleki, “Tafadhali, niletee hapa ile naivera.”Abiathari akaileta hiyo naivera kwa Daudi.
8 Et David consulta le Seigneur, disant: Poursuivrai-je ces brigands, et les prendrai-je, ou non? Et le Seigneur lui répondit: Poursuis, car, sans doute, tu les prendras, et tu recouvreras le butin.
Daudi akamwomba BWANA kwa ajili ya mwongozo, akisema, “Je, kama nikiliandama jeshi hili, nitalipata?” BWANA akamjibu, “Wafuate, maana kweli utawapata, na kwa hakika utarudisha kila kitu.”
9 David s’en alla donc, lui et les six cents hommes qui étaient avec lui, et ils vinrent jusqu’au torrent de Bésor; et quelques-uns fatigués s’arrêtèrent.
Kwa hiyo Daudi akaenda, yeye na wale watu mia sita waliokuwa pamoja naye; nao wakafika katika kijito cha Bethori, mahali walipokaa wale walioachwa nyuma.
10 Mais David les poursuivit avec quatre cents hommes; car deux cents s’étaient arrêtés, qui, fatigués, ne pouvaient passer le torrent de Bésor.
Lakini Daudi aliendelea kuwafuata, yeye na watu mia nne; maana wale mia mbili walibaki nyuma, wakiwa wamechoka kiasi cha kutoweza kuvuka kijito cha Besori.
11 Et ils trouvèrent un Egyptien dans la campagne, et ils l’amenèrent à David, et ils lui donnèrent du pain pour manger, et de l’eau pour boire;
Nao walimkuta Mmisri shambani na wakamleta kwa Daudi; wakampatia mkate, na akala; wakampa maji ya kunywa;
12 Et de plus une partie d’une panerée de figues sèches et deux grappes de raisins secs. Lorsqu’il eut mangé ces choses, ses esprits revinrent, et il fut restauré; car il n’avait pas mangé de pain ni bu d’eau pendant trois jours et trois nuits.
kisha walimpa kipande cha keki ya tini na vishada viwili vya zabibu. Alipomaliza kula, akapata nguvu tena, kwa kuwa alikuwa hajala mkate wala kunywa maji, siku tatu mchana na usiku.
13 C’est pourquoi David lui demanda: À qui es-tu? et d’où es-tu? et où vas-tu? Celui-ci répondit: Je suis un jeune Egyptien, esclave d’un Amalécite; mais mon maître m’a abandonné, parce que je tombai malade avant-hier.
Ndipo Daudi akamuuliza, “Wewe ni mtu wa nani? Je, unatoka wapi?” Naye akajibu, “Mimi ni kijana wa Misri, mtumishi wa Mwamaleki mmoja; bwana wangu aliniacha, kwa sababu siku tatu zilizopita nilikuwa mgonjwa.
14 Car nous, nous avons fait une sortie vers la région australe du Céréthien, et contre Juda, et vers le midi de Caleb, et nous avons mis Siceleg à feu,
Tulifanya mashambulizi dhidi ya Negevu ya Wakerethi, na iliyochini ya Yuda, na ile Negevu ya Kalebu, na kuichoma moto Ziklagi.”
15 Et David lui dit: Peux-tu me conduire vers cette troupe? L’Egyptien répondit: Jurez-moi par Dieu, que vous ne me tuerez point, et que vous ne me livrerez point aux mains de mon maître, et moi je vous conduirai vers cette troupe. Et David lui jura.
Daudi akamwambia, “Je, utanipeleka hadi kwa jeshi lililofanya mashabulizi?” Huyo Mmisri akasema, “Uniapie kwa Mungu kwamba hautaniua au kunisaliti na kuniweka katika mikono ya bwana wangu, nami nitakupeleka liliko hilo jeshi.”
16 Et lorsque l’Egyptien l’eut conduit, voilà que les Amalécites étaient couchés sur la face de toute la terre, mangeant et buvant, et comme célébrant un jour de fête, pour tout le butin, et les dépouilles qu’ils avaient enlevés de la terre des Philistins, et de la terre de Juda.
Yule Mmisri alipompeleka huko Daudi, hao wateka nyara walikuwa wametawanyika kila sehemu, wakila na kunywa, na wakicheza, kwa sababu ya nyara zote walizokuwa wamezitwaa kutoka nchi ya Wafilisti na kutoka nchi ya Yuda.
17 Et David les battit depuis le soir jusqu’au soir du jour suivant, et il n’en échappa aucun, sinon quatre cents jeunes hommes qui étaient montés sur les chameaux, et s’étaient enfuis.
Daudi akawashambulia tangu jua lilipozama hadi jioni ya siku ya pili. Hakuna mtu aliyeponyoka isipokuwa vijana mia nne, waliopanda ngamia na kukimbia.
18 David donc reprit tout ce que les Amalécites avaient emporté, ainsi il reprit ses deux femmes.
Daudi akarudisha vyote ambavyo Waamaleki walikuwa wamevichukua; na Daudi akawaokoa wake zake wawili.
19 Et rien ne manqua, depuis le petit jusqu’au grand, tant des fils que des filles, ni des dépouilles; car tout ce qu’ils avaient pris, David le ramena entièrement.
Hakuna kilichopotea, si kidogo wala kikubwa, si watoto wa kiume wala wa kike, si mali iliyotekwa, wala chochote ambacho wavamizi alikichukuwa kwa ajili yao. Daudi akawa amerejesha kila kitu.
20 Il retira donc tous les troupeaux de menu et de gros bétail, et les fit marcher devant lui; et on disait: Voici le butin de David.
Akachukua makundi yote ya kondoo na ng'ombe, ambayo watu waliyatanguliza mbele ya ng'ombe wengine. Wakisema, “Hizi ni nyara za Daudi.”
21 David vint ensuite vers les deux cents hommes, qui, fatigués, s’étaient arrêtés et n’avaient pu suivre David, et à qui il avait commandé de rester au torrent de Bésor; ceux-ci sortirent au devant de David et du peuple qui était avec lui. Or, David s’approchant du peuple, le salua pacifiquement.
Daudi akafika kwa wale watu mia mbili waliokuwa wamechoka kufuatana naye, wale walioachwa wakae katika kijito cha Besori. Watu hawa wakajitokeza kumlaki na watu waliokuwa naye.
22 Mais tout homme très méchant et inique, d’entre les hommes qui étaient allés avec David, répondant, dit: Parce qu’ils ne sont pas venus avec nous, nous ne leur donnerons rien du butin que nous avons repris; mais que chacun se contente de sa femme et de ses enfants; et, lorsqu’ils les auront reçus, qu’ils se retirent.
Ndipo watu wote waovu na wasiofaa miongoni mwa waliokwenda na Daudi wakasema, “Kwa sababu watu hawa hawakwenda nasi, hatutawapa chochote kutoka katika nyara tulizorudisha. Isipokuwa kila mtu aweza kuchukuwa mke na watoto wake, wawatoe na kwenda zao.”
23 Mais David dit: Ce n’est pas ainsi, mes frères, que vous disposerez des biens que le Seigneur nous a livrés, il nous a conservés, et a mis en nos mains les brigands qui étaient sortis violemment contre nous;
Ndipo Daudi akasema, “Ndugu zangu, msifanye hivyo, kwa vitu ambavyo BWANA ametupatia. Ametuhifadhi na kuwaweka mkononi mwetu wavamizi waliotuinukia.
24 Et nul ne vous écoutera sur cette parole; car égale sera la part de celui qui est descendu au combat, et de celui qui est resté près des bagages, et ils partageront également.
Ni nani atawasikiliza kuhusu jambo hili? Kwa maana mgawo ni kwa yeyote aendae vitani, basi pia mgawo ni kwa yeyote aliyelinda mizigo; Nao watapata tena kilicho sawa.”
25 Or, c’est ce qui a été fait depuis ce jour-là, et dans la suite établi, fixé, et comme une loi dans Israël jusqu’à ce jour.
Ilikuwa hivyo tangu siku hiyo hadi leo, maana Daudi aliamua iwe sheria na amri kwa Israeli.
26 David donc vint à Siceleg, et il envoya des dons du butin pris aux anciens de Juda, ses proches, disant: Recevez cette bénédiction du butin des ennemis du Seigneur;
Daudi alipofika Ziklagi, alituma sehemu ya nyara kwa wazee wa Yuda, kwa rafiki zake, akisema, “Tazama, hii ni zawadi yenu kutokana na nyara za adui wa BWANA.”
27 À ceux qui étaient à Béthel, à ceux qui étaient à Ramoth vers le midi, à ceux qui étaient à Jéther,
Zawadi zilienda kwa wazee waliokuwa Bethueli, na kwa hao waliokuwa Ramothi iliyoko kusini, na kwa hao waliokuwa Yatiri,
28 À ceux qui étaient à Aroer, à ceux qui étaient à Séphamoth, à ceux qui étaient à Esthamo.
na kwa hao waliokuwa Aroeri, na kwa hao waliokuwa Sifmothi, na kwa hao waliokuwa Eshtemoa
29 À ceux qui étaient à Rachat, à ceux qui étaient dans le? villes de Jéraméel, à ceux qui étaient dans les villes de Céni,
Pia kwa wazee waliokuwa Rakali, na kwa hao waliokuwa katika miji ya Wayerameeli, na kwa hao waliokuwa katika miji ya Wakeni,
30 À ceux qui étaient à Arama, à ceux qui étaient sur le lac d’Asan, à ceux qui étaient à Athach,
na kwa hao waliokuwa Horma, na kwa hao waliokuwa Borashani, na kwa hao waliokuwa Athaki,
31 À ceux qui étaient à Hébron, et aux autres qui étaient dans les lieux dans lesquels avaient demeuré David, lui-même, et ses hommes.
na kwa hao waliokuwa Hebroni, na kwa sehemu zote ambazo Daudi mwenyewe na watu wake walizoea kwenda.