< 1 Rois 16 >

1 Or la parole du Seigneur fut adressée à Jéhu, fils d’Hanani, contre Baasa, disant:
Ndipo neno la Bwana likamjia Yehu mwana wa Hanani dhidi ya Baasha, kusema:
2 Quand je t’ai élevé de la poussière, et je t’ai établi chef sur mon peuple Israël, toi au contraire, tu as marché dans la voie de Jéroboam, et tu as fait pécher mon peuple Israël, pour m’irriter par leurs péchés:
“Nilikuinua kutoka mavumbini na kukufanya kiongozi wa watu wangu Israeli, lakini ukaenenda katika njia za Yeroboamu na kusababisha watu wangu Israeli kutenda dhambi na kunikasirisha kwa dhambi zao.
3 Voilà que moi, je moissonnerai la postérité de Baasa et la postérité de sa maison, et je ferai de ta maison ce que j’ai fait de la maison de Jéroboam, fils de Nabath.
Basi nitamwangamiza Baasha pamoja na nyumba yake, nami nitaifanya nyumba yako kama ile ya Yeroboamu mwanawe Nebati.
4 Celui de la race de Baasa qui mourra dans la ville, les chiens le mangeront, et celui qui mourra dans la campagne, les oiseaux du ciel le mangeront.
Mbwa watawala watu wa Baasha watakaofia mjini na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani.”
5 Mais le reste des actions de Baasa, et tout ce qu’il fit, et ses combats, n’est-ce pas écrit dans le Livre des actions des jours des rois d’Israël?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Baasha, aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
6 Baasa dormit donc avec ses pères, et il fut enseveli à Thersa; et Ela son fils régna en sa place.
Baasha akalala na baba zake naye akazikwa huko Tirsa. Naye Ela mwanawe akawa mfalme baada yake.
7 Mais lorsque par l’entremise de Jéhu le prophète, fils d’Hanani, la parole du Seigneur eut été adressée contre Baasa, contre sa maison, et contre tout le mal qu’il avait fait devant le Seigneur, pour l’irriter par les œuvres de ses mains, afin que sa maison devînt comme la maison de Jéroboam, Baasa pour ce motif même le tua, c’est-à-dire, Jéhu, fils d’Hanani le prophète,
Zaidi ya hayo, neno la Bwana likamjia Baasha pamoja na nyumba yake kupitia kwa nabii Yehu mwana wa Hanani, kwa sababu ya maovu yote aliyokuwa ametenda machoni pa Bwana, akamkasirisha kwa mambo aliyotenda, na kuwa kama nyumba ya Yeroboamu, na pia kwa sababu aliiangamiza.
8 La vingt-sixième année d’Asa, roi de Juda, Ela, fils de Baasa, régna sur Israël à Thersa pendant deux ans;
Katika mwaka wa ishirini na sita wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ela mwana wa Baasha akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala huko Tirsa kwa miaka miwili.
9 Car son serviteur Zambri, chef de la moitié de sa cavalerie, se révolta contre lui; or Ela était à Thersa buvant et ivre, dans la maison d’Arsa, gouverneur de Thersa.
Zimri, mmoja wa maafisa wake, aliyekuwa na amri juu ya nusu ya magari yake ya vita, akafanya hila mbaya dhidi ya Ela. Wakati huo Ela alikuwa Tirsa, akilewa katika nyumba ya Arsa, mtu aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme huko Tirsa.
10 Zambri donc se jetant sur lui, le frappa et le tua la vingt-septième année d’Asa, roi de Juda, et il régna en sa place.
Zimri akaingia, akampiga na kumuua katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda. Kisha Zimri akaingia mahali pake kuwa mfalme.
11 Et lorsqu’il fut roi et qu’il fut assis sur son trône, il tua toute la maison de Baasa, et il ne laissa d’elle aucun urinant contre une muraille, ni ses proches, ni ses amis.
Mara tu alipoanza kutawala na kuketi juu ya kiti cha ufalme, aliua jamaa yote ya Baasha. Hakumwacha mwanaume hata mmoja, akiwa ni ndugu au rafiki.
12 Ainsi Zambri détruisit toute la maison de Baasa, selon la parole que le Seigneur avait dite à Baasa par l’entremise de Jéhu le prophète,
Hivyo Zimri akaangamiza jamaa yote ya Baasha, kulingana na neno la Bwana lililonenwa dhidi ya Baasha kupitia nabii Yehu:
13 À cause de tous les péchés de Baasa et des péchés d’Ela son fils, qui avaient péché et fait pécher tout Israël, provoquant le Seigneur Dieu d’Israël par leurs vanités.
kwa sababu ya dhambi zote Baasha na mwanawe Ela walizokuwa wametenda na wakasababisha Israeli kuzitenda, basi wakamkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli kwa sanamu zao zisizofaa.
14 Mais le reste des actions d’Ela, et tout ce qu’il fit, n’est-ce pas écrit dans le Livre des actions des jours des rois d’Israël?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Ela, na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
15 La vingt-septième année d’Asa, roi de Juda, Zambri régna pendant sept jours à Thersa: or l’armée d’Israël assiégeait Gebbethon, ville des Philistins.
Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Zimri akatawala huko Tirsa siku saba. Jeshi lilikuwa limepiga kambi karibu na Gibethoni, mji wa Wafilisti.
16 Et lorsqu’il eut appris que Zambri s’était révolté et avait tué le roi, tout Israël se donna pour roi Amri, qui était prince de la milice d’Israël, et en ce jour-là dans le camp.
Wakati Waisraeli waliokuwa kambini waliposikia kuwa Zimri alikuwa amefanya hila mbaya dhidi ya mfalme na kumuua, wakamtangaza Omri, jemadari wa jeshi, kuwa mfalme wa Israeli siku iyo hiyo huko kambini.
17 Amri monta donc, et tout Israël avec lui, de Gebbethon, et ils assiégeaient Thersa.
Ndipo Omri na Waisraeli wote pamoja naye wakaondoka Gibethoni na kuizingira Tirsa.
18 Or Zambri, voyant que la ville allait être prise d’assaut, entra dans le palais et se brûla avec la maison royale: et il mourut
Wakati Zimri alipoona kuwa mji umechukuliwa, alikwenda ndani ya ngome ya jumba la kifalme na kulichoma moto jumba la kifalme na kujiteketeza ndani yake. Kwa hiyo akafa,
19 Dans ses péchés qu’il avait commis, faisant le mal devant le Seigneur, et marchant dans la voie de Jéroboam et dans le péché par lequel il avait fait pécher Israël.
kwa sababu ya dhambi alizofanya, akitenda maovu machoni pa Bwana na kuenenda katika njia za Yeroboamu na katika dhambi alizofanya na kusababisha Israeli kuzifanya.
20 Mais le reste des actions de Zambri, de ses embûches et de sa tyrannie, n’est-ce pas écrit dans le Livre des actions des jours des rois d’Israël?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Zimri, na uasi alioutenda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
21 Alors le peuple d’Israël fut divisé en deux parties: la moitié du peuple suivait Thebni, fils de Gineth, pour l’établir roi, et l’autre moitié. Amri.
Ndipo watu wa Israeli wakagawanyika katika makundi mawili, nusu wakamuunga mkono Tibni mwana wa Ginathi ili awe mfalme na nusu nyingine wakamuunga mkono Omri.
22 Mais le peuple qui était avec Amri l’emporta sur le peuple qui était avec Thebni, fils de Gineth; or Thebni mourut, et Amri régna.
Lakini wafuasi wa Omri wakajionyesha wenye nguvu kuliko wale wa Tibni mwana wa Ginathi. Hivyo Tibni akafa na Omri akawa mfalme.
23 Depuis la trente-unième année d’Asa, roi de Juda, Amri régna sur Israël pendant douze ans: à Thersa, il régna six ans.
Katika mwaka wa thelathini na moja wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala kwa miaka kumi na miwili, sita kati ya hiyo katika Tirsa.
24 Et il acheta la montagne de Samarie à Somer, pour deux talents d’argent; et il la bâtit, et il appela la ville qu’il avait construite Samarie, du nom de Somer, le maître de la montagne.
Alinunua kilima cha Samaria kutoka kwa Shemeri kwa talanta mbili za fedha na akajenga mji juu ya hicho kilima, akiuita Samaria, kutokana na Shemeri, jina la mmiliki wa kwanza wa kilima hicho.
25 Mais Amri fit le mal en la présence du Seigneur, et il agit méchamment, plus que tous ceux qui furent avant lui.
Lakini Omri akatenda maovu machoni pa Bwana na kutenda dhambi kuliko wote waliomtangulia.
26 Et il marcha dans toute la voie de Jéroboam, fils de Nabath, et dans ses péchés par lesquels il avait fait pécher Israël, pour irriter le Seigneur Dieu d’Israël par ses vanités.
Akaenenda katika njia zote za Yeroboamu mwana wa Nebati na katika dhambi zake, ambazo alisababisha Israeli kutenda, hivyo basi wakamkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli kwa sanamu zao zisizofaa.
27 Mais le reste des actions d’Amri et les combats qu’il donna, n’est-ce pas écrit dans le Livre des actions des jours des rois d’Israël?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Omri, yale aliyofanya na vitu alivyovifanikisha, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
28 Et Amri dormit avec ses pères et fut enseveli à Samarie, et Achab, son fils, régna en sa place.
Omri akalala pamoja na baba zake na akazikwa huko Samaria. Ahabu mwanawe akatawala mahali pake.
29 Mais Achab, fils d’Amri, régna sur Israël la trente-huitième année d’Asa, roi de Juda. Et Achab, fils d’Amri, régna sur Israël à Samarie pendant vingt-deux ans.
Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ahabu mwana wa Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala Israeli akiwa Samaria kwa miaka ishirini na miwili.
30 Et Achab, fils d’Amri, fit le mal en la présence du Seigneur plus que tous ceux qui furent avant lui.
Ahabu mwana wa Omri akafanya maovu zaidi machoni mwa Bwana kuliko yeyote aliyewatangulia.
31 Et il ne lui suffit pas de marcher dans les péchés de Jéroboam, fils de Nabath; de plus, il prit pour femme Jézabel, fille d’Ethbaal, roi des Sidoniens, et il alla, et servit Baal et l’adora.
Kama vile haikutosha kuishi kama Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti wa Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, naye akaanza kumtumikia Baali na kumwabudu.
32 Et il éleva un autel à Baal dans le temple de Baal qu’il avait bâti à Samarie,
Akajenga madhabahu kwa ajili ya Baali katika hekalu la Baali lile alilolijenga huko Samaria.
33 Et il planta le bois sacré; et Achab ajouta à son œuvre en irritant le Seigneur Dieu d’Israël plus que tous les rois d’Israël qui furent avant lui.
Pia Ahabu akatengeneza nguzo ya Ashera na kufanya mengi ili kumkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli, kuliko walivyofanya wafalme wote wa Israeli waliomtangulia.
34 Pendant ses jours, Hiel, de Béthel, bâtit Jéricho: il en jeta les fondements sur Abiram, son premier-né, et il en posa les portes sur Ségub, son dernier fils, selon la parole que le Seigneur avait dite par l’entremise de Josué, fils de Nun.
Katika wakati wa Ahabu, Hieli, Mbetheli, akaijenga upya Yeriko. Aliweka misingi yake kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza Abiramu, na kuweka malango yake kwa gharama ya mwanawe mdogo Segubu, kulingana na neno la Bwana alilosema kupitia Yoshua mwana wa Nuni.

< 1 Rois 16 >