< 1 Rois 15 >

1 Ainsi en la dix-huitième année du règne de Jéroboam, fils de Nabath, Abiam régna sur Juda.
Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
2 Il régna trois ans dans Jérusalem; le nom de sa mère était Maacha, fille d’Abessalom.
naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
3 Et il marcha dans tous les péchés que son père avait commis avant lui, et son cœur n’était point parfait avec le Seigneur son Dieu, comme le cœur de David son père.
Alitenda dhambi zote baba yake alizotenda kabla yake; moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana Mungu wake kama moyo wa Daudi baba yake ulivyokuwa.
4 Mais, à cause de David, le Seigneur son Dieu lui donna une lampe dans Jérusalem, en sorte qu’il suscita son fils après lui, et maintint Jérusalem,
Pamoja na hayo, kwa ajili ya Daudi, Bwana Mungu wake akampa taa katika Yerusalemu kwa kumwinua mwana atawale badala yake na kwa kuifanya Yerusalemu kuwa imara.
5 Parce que David avait fait ce qui était droit aux yeux du Seigneur, et qu’il ne s’était point détourné de tout ce qu’il lui avait commandé, durant tous les jours de sa vie, excepté le fait touchant Urie, l’Héthéen.
Kwa kuwa Daudi alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana na hakushindwa kushika maagizo yote ya Bwana siku zote za uhai wake, isipokuwa katika habari ya Uria, Mhiti.
6 Cependant il y eut guerre entre Roboam et Jéroboam, pendant tout le temps de la vie de Roboam.
Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu wakati wote wa maisha ya Abiya.
7 Mais le reste des actions d’Abiam, et tout ce qu’il fit, n’est-ce pas écrit dans le Livre des actions des jours des rois de Juda? Et il y eut une bataille entre Abiam et Jéroboam.
Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Abiya na yote aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
8 Et Abiam dormit avec ses pères, et on l’ensevelit dans la cité de David; et son fils Asa régna en sa place.
Naye Abiya akalala na baba zake akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake.
9 Ainsi en la vingtième année de Jéroboam, roi d’Israël, Asa, roi de Juda, régna.
Katika mwaka wa ishirini wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa akawa mfalme wa Yuda,
10 Et il régna quarante-un ans dans Jérusalem. Le nom de sa mère était Maacha, fille d’Abessalom.
naye akatawala katika Yerusalemu miaka arobaini na mmoja. Bibi yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
11 Et Asa fit ce qui était droit en la présence du Seigneur, comme David son père;
Asa akatenda yaliyo mema machoni mwa Bwana, kama alivyokuwa ametenda Daudi baba yake.
12 Et il chassa les efféminés du pays, et le purifia de toutes les souillures des idoles que ses pères avaient fabriquées.
Akawafukuza mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu kutoka nchi na kuondoa sanamu zote ambazo baba zake walikuwa wametengeneza.
13 De plus, il éloigna même sa mère Maacha, afin qu’elle ne fût pas préposée aux sacrifices de Priape, et à son bois sacré qu’elle avait consacré; et il renversa sa caverne, et il brisa le simulacre très obscène, et le brûla dans le torrent de Cédron.
Hata akamwondoa bibi yake Maaka kwenye wadhifa wake kama mama malkia, kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
14 Mais il ne détruisit pas les hauts lieux. Toutefois le cœur d’Asa fut parfait avec le Seigneur durant tous ses jours;
Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
15 Il porta aussi ce qu’avait consacré son père, et qu’il avait voué dans la maison du Seigneur, de l’argent, de l’or, et des vases.
Akaleta ndani ya Hekalu la Bwana fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
16 Or il y eut guerre entre Asa et Baasa, roi d’Israël, durant tous leurs jours.
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli siku zote za utawala wao.
17 Et Baasa, roi d’Israël, vint contre Juda et bâtit Rama, afin que personne ne pût sortir ou entrer du côté d’Asa, roi de Juda.
Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
18 C’est pourquoi Asa, prenant tout l’argent et l’or qui étaient demeurés dans les trésors de la maison du Seigneur et dans les trésors de la maison du roi, les mit entre les mains de ses serviteurs, et les envoya à Bénadad, fils de Tabremon, fils d’Hézion, roi de Syrie, qui habitait à Damas, disant:
Kisha Asa akachukua fedha yote na dhahabu iliyokuwa imeachwa katika hazina za Hekalu la Bwana na za jumba lake mwenyewe la kifalme. Akawakabidhi maafisa wake na kuwatuma kwa Ben-Hadadi mwana wa Tabrimoni, mwana wa Hezioni, mfalme wa Aramu, aliyekuwa akitawala Dameski.
19 Il y a alliance entre moi et vous, et entre mon père et votre père: c’est pourquoi je vous ai envoyé des présents, de l’argent et de l’or, et je vous prie de venir, et de rendre vaine l’alliance que vous avez avec Baasa, roi d’Israël, afin qu’il se retire loin de moi.
“Akasema na pawepo mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea zawadi ya fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
20 Bénadad, écoutant le roi Asa, envoya les princes de son armée contre les villes d’Israël, et ils prirent d’assaut Ahion, Dan, Abel maison de Maacha, et Cennéroth tout entière, c’est-à-dire toute la terre de Nephthali.
Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Akaishinda miji ya Iyoni, Dani, Abel-Beth-Maaka na Kinerethi yote, pamoja na Naftali.
21 Ce qu’ayant appris, Baasa cessa de bâtir Rama, et revint à Thersa.
Wakati Baasha aliposikia hili, akaacha kuijenga Rama na akaenda kuishi Tirsa.
22 Or le roi Asa envoya un messager dans tout Juda, disant: Que personne ne soit exempté. Et on emporta les pierres de Rama et les bois avec lesquels Baasa avait bâti, et le roi Asa en construisit Gabaa en Benjamin, et Maspha.
Kisha Mfalme Asa akatoa amri kwa Yuda yote, pasipo kumbagua hata mmoja, kubeba mawe na mbao kutoka Rama, ambazo Baasha alikuwa akitumia huko. Mfalme Asa akazitumia kujengea Geba iliyoko Benyamini na Mispa pia.
23 , Mais le reste de toutes les actions d’Asa, tous ses traits de courage, tout ce qu’il fit, et les villes qu’il bâtit, n’est-ce pas écrit dans le Livre des actions des jours des rois de Juda? Cependant dans le temps de sa vieillesse, il souffrit de ses pieds;
Kwa matukio yote ya utawala wa Asa, mafanikio yake yote, yote aliyofanya na miji aliyoijenga, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Katika uzee wake, hata hivyo, alipata ugonjwa wa miguu.
24 Et il dormit avec ses pères, et il fut enseveli avec eux dans la cité de David son père. Et Josaphat, son fils, régna eu sa place.
Kisha Asa akalala pamoja na baba zake na kuzikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Naye Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake.
25 Or Nadab, fils de Jéroboam, régna sur Israël la seconde année d’Asa, roi de Juda; et il régna deux ans sur Israël.
Nadabu mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Asa wa Yuda, naye akatawala Israeli kwa miaka miwili.
26 Et il fit ce qui est mal en la présence du Seigneur, et il marcha dans les voies de son père et dans les péchés par lesquels il fit pécher Israël.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za baba yake na katika dhambi yake, ambayo alisababisha Israeli kuifanya.
27 Mais Baasa, fils d’Ahias, de la maison d’Issachar, lui tendit des embûches et le tua près de Gebbethon, qui est une ville des Philistins; vu que Nadab et tout Israël assiégeaient Gebbethon.
Baasha mwana wa Ahiya wa nyumba ya Isakari akafanya shauri baya dhidi yake, naye akamuua huko Gibethoni, mji wa Wafilisti, wakati Nadabu na Israeli yote walipokuwa wameuzingira.
28 Baasa tua donc Nadab, et il régna en sa place, la troisième année d’Asa, roi de Juda.
Baasha akamuua Nadabu katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, naye Baasha akaingia mahali pake kuwa mfalme.
29 Et lorsque Baasa fut devenu roi, il tua toute la maison de Jéroboam: il n’en laissa pas même une seule âme de sa race, jusqu’à ce qu’il l’eût exterminée, selon la parole que le Seigneur avait dite par l’entremise de son serviteur Ahias, le Silonite,
Mara tu alipoanza kutawala, aliua jamaa yote ya Yeroboamu. Hakumwachia Yeroboamu yeyote aliyekuwa hai, bali aliwaangamiza wote, kulingana na neno la Bwana lililotolewa kupitia kwa mtumishi wake Ahiya Mshiloni,
30 À cause des péchés que Jéroboam avait commis et par lesquels il avait fait pécher Israël, et à cause du péché par lequel il avait irrité le Seigneur Dieu d’Israël.
kwa sababu ya dhambi alizokuwa amezitenda Yeroboamu na kusababisha Israeli kuzitenda, tena kwa sababu alimkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli.
31 Mais le reste des actions de Nadab, et tout ce qu’il fit, n’est-ce pas écrit dans le Livre des actions des jours des rois d’Israël?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Nadabu na yote aliyofanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
32 Et il y eut guerre entre Asa et Baasa, roi d’Israël, durant tous leurs jours.
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli wakati wote wa utawala wao.
33 La troisième année d’Asa, roi de Juda, Baasa, fils d’Ahias, régna sur tout Israël à Thersa pendant vingt-quatre ans.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya akawa mfalme wa Israeli yote huko Tirsa, naye akatawala kwa miaka ishirini na minne.
34 Et il fit le mal devant le Seigneur, et il marcha dans la voie de Jéroboam et dans les péchés par lesquels il avait fait pécher Israël.
Akatenda maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za Yeroboamu na dhambi yake, ambayo alikuwa amesababisha Israeli kuitenda.

< 1 Rois 15 >