< 1 Rois 14 >
1 En ce temps-là, Abia, fils de Jéroboam, fut malade,
Wakati ule Abiya mwana wa Yeroboamu akaugua,
2 Et Jéroboam dit à sa femme: Lève-toi, change de vêtement, pour qu’on ne sache point que tu es femme de Jéroboam, et va à Silo, où est Ahias le prophète, qui m’a dit que je devais régner sur ce peuple.
naye Yeroboamu akamwambia mke wake, “Nenda ukajibadilishe, ili watu wasijue kwamba wewe ni mke wa Yeroboamu. Kisha uende Shilo. Nabii Ahiya yuko huko, yule aliyeniambia kuwa nitakuwa mfalme juu ya watu hawa.
3 Prends aussi en ta main dix pains, une galette et un vase de miel, et va vers lui; car lui-même t’indiquera ce qui doit arriver à cet enfant.
Chukua mikate kumi, maandazi kadhaa na gudulia la asali na umwendee. Atakuambia kitakachotokea kwa kijana.”
4 La femme de Jéroboam fit comme il avait dit; et, se levant, elle alla à Silo, et vint dans la maison d’Ahias; mais celui-ci ne pouvait voir, parce que ses yeux s’étaient obscurcis à cause de sa vieillesse.
Basi mke wa Yeroboamu akafanya kama alivyosema mumewe, akaenda kwenye nyumba ya Ahiya huko Shilo. Wakati huu Ahiya alikuwa kipofu naye alishindwa kuona kwa sababu ya umri wake.
5 Or le Seigneur dit à Ahias: Voilà que la femme de Jéroboam vient te consulter sur son fils qui est malade: tu lui diras ceci et cela. Comme donc elle entrait, et dissimulait qui elle était,
Lakini Bwana alikuwa amemwambia Ahiya, “Mke wa Yeroboamu anakuja kukuuliza kuhusu mwanawe, kwa kuwa ni mgonjwa, nawe utamjibu hivi na hivi. Atakapowasili, atajifanya kuwa ni mtu mwingine.”
6 Ahias entendit le bruit de ses pieds lorsqu’elle entrait à la porte, et il dit: Entrez, femme de Jéroboam: pourquoi feignez-vous d’être une autre? Pour moi, je vous suis envoyé comme un messager funeste.
Hivyo Ahiya aliposikia kishindo cha hatua zake mlangoni, akasema, “Karibu ndani, mke wa Yeroboamu. Kwa nini kujibadilisha? Nimetumwa kwako nikiwa na habari mbaya.
7 Allez, et dites à Jéroboam: Voici ce que dit le Seigneur Dieu d’Israël: Je t’ai élevé du milieu du peuple, et je t’ai établi chef sur mon peuple Israël;
Nenda, ukamwambie Yeroboamu kwamba hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Nilikuinua miongoni mwa watu na kukufanya kiongozi juu ya watu wangu Israeli.
8 Et j’ai divisé le royaume de la maison de David et te l’ai donné; et tu n’as point été comme mon serviteur David, qui a gardé mes commandements, et qui m’a suivi en tout son cœur, faisant tout ce qui était agréable en ma présence;
Nikararua ufalme kutoka kwa nyumba ya Daudi na kukupa wewe, lakini hukuwa kama mtumishi wangu Daudi, ambaye aliyashika maagizo yangu na kunifuata kwa moyo wake wote, akifanya tu lile lililokuwa sawa machoni pangu.
9 Mais tu as fait plus de maux que tous ceux qui ont été avant toi, et tu t’es fait des dieux étrangers et jetés en fonte, pour me provoquer au courroux, et tu m’as rejeté derrière toi.
Umefanya maovu mengi kuliko wote waliokutangulia. Umejitengenezea miungu mingine, sanamu za chuma, umenighadhibisha na kunitupa nyuma yako.
10 C’est pourquoi voilà que j’amènerai des maux sur la maison de Jéroboam, et je frapperai de Jéroboam celui qui urine contre une muraille, celui qui est renfermé, et celui qui est le dernier dans Israël; et je nettoyerai les restes de la maison de Jéroboam, comme on a coutume de nettoyer le fumier, jusqu’à ce que tout soit net.
“‘Kwa sababu ya hili, nitaleta maafa juu ya nyumba ya Yeroboamu. Nitakatilia mbali kutoka kwa Yeroboamu kila mzaliwa wa mwisho wa kiume katika Israeli, mtumwa au mtu huru. Nitachoma nyumba ya Yeroboamu mpaka iteketee yote kama mtu achomaye kinyesi.
11 Ceux de Jéroboam qui mourront dans la ville, les chiens les mangeront, et ceux qui mourront dans la campagne, les oiseaux du ciel les dévoreront, parce que c’est le Seigneur qui a parlé.
Mbwa watawala wale walio wa nyumba ya Yeroboamu watakaofia ndani ya mji na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani. Bwana amesema!’
12 Vous donc, levez-vous, et allez en votre maison; et, à l’entrée même de vos pieds dans la ville, l’enfant mourra,
“Kukuhusu wewe, rudi nyumbani. Wakati utakapotia mguu katika mji wako, kijana atakufa.
13 Et tout Israël le pleurera et l’ensevelira; car c’est le seul de Jéroboam qui sera porté dans un sépulcre, parce qu’il a été trouvé en lui quelque chose de bon par le Seigneur Dieu d’Israël dans la maison de Jéroboam.
Israeli yote itamwombolezea na kumzika. Kwa sababu ni yeye pekee wa nyumba ya Yeroboamu atakayezikwa, kwa sababu ni yeye peke yake ndani ya nyumba ya Yeroboamu ambaye Bwana, Mungu wa Israeli, ameona kitu chema kwake.
14 Mais le Seigneur s’est établi un roi sur Israël, qui frappera la maison de Jéroboam en ce jour et en ce temps;
“Bwana atajiinulia mwenyewe mfalme juu ya Israeli ambaye ataikatilia mbali jamaa ya Yeroboamu. Siku ndiyo hii! Nini? Naam, hata sasa hivi.
15 Et le Seigneur Dieu frappera Israël comme le roseau a coutume d’être agité dans l’eau, et il arrachera Israël de la bonne terre qu’il a donnée à leurs pères, et il les dispersera au-delà du fleuve, parce qu’ils se sont fait des bois sacrés pour irriter le Seigneur.
Naye Bwana ataipiga Israeli, hata iwe kama unyasi unaosukwasukwa juu ya maji. Ataingʼoa Israeli kutoka nchi hii nzuri aliyowapa baba zao na kuwatawanya ngʼambo ya Mto Frati, kwa sababu wamemghadhibisha Bwana kwa kutengeneza nguzo za Ashera
16 Et le Seigneur livrera Israël à cause des péchés de Jéroboam, qui a péché et qui a fait pécher Israël.
Naye atawaacha Israeli kwa ajili ya makosa ya Yeroboamu aliyoyatenda na kusababisha Israeli kuyatenda.”
17 C’est pourquoi la femme de Jéroboam se leva, s’en alla, et vint à Thersa; et lorsqu’elle entrait sur le seuil de la porte de sa maison, l’enfant mourut,
Kisha mke wa Yeroboamu akainuka, akaondoka kwenda Tirsa. Mara alipokanyaga kizingiti cha mlango, kijana akafa.
18 Et on l’ensevelit. Et tout Israël le pleura, selon la parole du Seigneur qu’il avait dite par l’entremise de son serviteur Ahias, le prophète.
Wakamzika na Israeli yote ikamwombolezea, kama Bwana alivyokuwa amesema kupitia mtumishi wake, nabii Ahiya.
19 Mais le reste des actions de Jéroboam, comment il combattit, et comment il régna, voilà que c’est écrit dans le Livre des actions des jours des rois d’Israël.
Matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, vita vyake na jinsi alivyotawala, vimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
20 Or les jours durant lesquels Jéroboam régna furent de vingt-deux ans, et il dormit avec ses pères, et Nadab, son fils, régna en sa place.
Yeroboamu akawatawala kwa miaka ishirini na miwili, kisha akalala na baba zake. Naye Nadabu mwanawe akawa mfalme baada yake.
21 Cependant Roboam, fils de Salomon régnait sur Juda. Roboam avait quarante-un ans lorsqu’il commença à régner, et il régna dix-sept ans dans la ville de Jérusalem, que le Seigneur avait choisie d’entre toutes les tribus d’Israël pour y établir son nom. Or le nom de sa mère était Naama, l’Ammanite.
Rehoboamu mwana wa Solomoni alikuwa mfalme wa Yuda. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na moja alipoanza kutawala, naye akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua kutoka makabila yote ya Israeli ili apate kuliweka humo Jina lake. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni.
22 Et Juda fit le mal aux yeux du Seigneur, et ils l’irritèrent au-delà de tout ce qu’avaient fait leurs pères, dans les péchés dont ils s’étaient rendus coupables,
Yuda wakatenda maovu machoni pa Bwana. Kwa dhambi walizotenda wakachochea hasira yake yenye wivu zaidi kuliko baba zao walivyofanya.
23 Car ils se firent, eux aussi, des autels, des statues et des bois sacrés sur toute colline élevée et sous tout arbre couvert de feuillage.
Pia wakajijengea mahali pa juu pa kuabudia miungu, mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kilichoinuka na kila mti uliotanda.
24 Il y eut aussi des efféminés dans leur terre, et ils commirent toutes les abominations de ces nations que le Seigneur avait détruites devant la face des enfants d’Israël.
Walikuwepo hata wanaume mahanithi wa mahali pa ibada za sanamu katika nchi; watu wakajiingiza katika kutenda machukizo ya mataifa ambayo Bwana aliyafukuza mbele ya Waisraeli.
25 Or en la cinquième année du règne de Roboam, Sésac, roi d’Egypte, monta à Jérusalem,
Katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu.
26 Et il enleva les trésors de la maison du Seigneur et les trésors du roi, et il pilla tout, même les boucliers d’or qu’avait faits Salomon,
Akachukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao zote za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza.
27 En la place desquels le roi Roboam fit des boucliers d’airain, et il les mit entre les mains des chefs des scutaires, et de ceux qui veillaient devant la porte de la maison du roi.
Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.
28 Et lorsque le roi entrait dans la maison du Seigneur, ceux dont l’office était de marcher devant lui portaient ces boucliers, et ensuite ils les reportaient dans l’arsenal des scutaires.
Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana, walinzi walizichukua hizo ngao, na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.
29 Mais le reste des actions de Roboam, et tout ce qu’il a fait, voilà que c’est écrit dans le Livre des actions des jours des rois de Juda.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Rehoboamu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
30 Et il y eut guerre entre Roboam et Jéroboam durant tous leurs jours.
Kulikuwa na vita vinavyoendelea kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
31 Et Roboam dormit avec ses pères, et il fut enseveli avec eux dans la cité de David. Le nom de sa mère était Naama l’Ammanite, et Abiam son fils régna en sa place.
Naye Rehoboamu akalala na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.