< 1 Corinthiens 4 >
1 Que les hommes nous regardent comme ministres du Christ, et dispensateurs des mystères de Dieu.
Hivi ndivyo mtu atuhesabu sisi, kama watumishi wa Kristo na mawakili wa siri za kweli za Mungu.
2 Or ce qu’on demande dans les dispensateurs, c’est que chacun soit trouvé fidèle.
Katika hili, kinachotakiwa kwa uwakili ni kwamba wawe wa kutumainiwa.
3 Pour moi, je me mets fort peu en peine d’être jugé par vous ou par un tribunal humain; bien plus, je ne me juge pas moi-même.
Lakini kwangu mimi ni kitu kidogo sana kuwa ninahukumiwa na ninyi au hukumu ya kibinadamu. Kwa kuwa sijihukumu hata mimi mwenyewe.
4 À la vérité, ma conscience ne me reproche rien, mais je ne suis pas pour cela justifié; celui qui me juge c’est le Seigneur.
Sijihukumu mimi mwenyewe, hii haina maana kuwa mimi ni mwenye haki. Ni Bwana anihukumuye.
5 C’est pourquoi, ne jugez pas avant le temps, jusqu’à ce que vienne le Seigneur, qui éclairera ce qui est caché dans les ténèbres, et manifestera les pensées secrètes des cœurs; et alors chacun recevra de Dieu sa louange.
Kwa hiyo, msitamke hukumu juu ya lolote kabla ya wakati, kabla ya kuja kwa Bwana. Atayaleta nuruni mambo yaliyofichika gizani na kufunua makusudi ya mioyo. Ndipo kila mmoja atapokea sifa yake kutoka kwa Mungu.
6 Au reste, mes frères, j’ai personnifié ces choses en moi et en Apollo à cause de vous, afin que vous appreniez, par notre exemple, à ne pas, contrairement à ce que je vous ai écrit, vous enfler d’orgueil l’un contre l’autre pour autrui.
Sasa, kaka na dada zangu, mimi mwenyewe na Apolo nimetumia kanuni hizi kwa ajili yenu. Ili kwamba kutoka kwetu mnaweza kujifunza maana ya usemi, “Usiende zaidi ya kilivyoandikwa.” Hii ni kwamba hakuna mmoja wenu ajivunaye juu ya mwingine.
7 Car qui te discerne? et qu’as-tu que tu n’aies reçu? Que si tu l’as reçu, pourquoi t’en glorifies-tu, comme si tu ne l’avais pas reçu?
Maana ni nani aonaye tofauti kati yenu na mwingine? Ni nini ulicho nacho hukukipokea bure? Kama umekwisha kupokea bure, kwa nini mnajivuna kama hamkufanya hivyo?
8 Déjà vous êtes rassasiés, déjà vous êtes riches, vous régnez sans nous; et plaise à Dieu que vous régniez en effet, afin que nous régnions avec vous.
Tayari mnavyo vyote ambavyo mngetaka! Tayari mmekuwa na utajiri! Mmeanza kutawala-na kwamba mnamiliki zaidi yetu sisi! Kweli, nawatakia umililki mwema ili kwamba tumiliki pamoja nanyi.
9 Car il me semble que Dieu nous a présentés, nous les derniers des apôtres, comme destinés à la mort, puisque nous sommes donnés en spectacle au monde, aux anges et aux hommes.
Kwa hiyo ninadhani Mungu ametuweka sisi mitume kama kutuonyesha wa mwisho katika mustari wa maandamano na kama watu waliohukumiwa kuuawa. Tumekuwa kama tamasha kwa ulimwengu, kwa malaika na kwa wanadamu.
10 Nous sommes, nous, insensés à cause du Christ; mais vous, vous êtes sages dans le Christ; nous sommes faibles et vous forts; vous êtes honorés, mais nous méprisés.
Sisi ni wajinga kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye hekima katika Kristo. Tu wanyonge, lakini ninyi mna nguvu. Mnaheshimiwa, lakina sisi tunadharauliwa.
11 Jusqu’à cette heure nous souffrons et la faim et la soif, nous sommes nus, déchirés à coups de poing, et nous n’avons pas de demeure stable;
Hata saa hii tuna njaa na kiu, hatuna nguo, tuna mapigo, na tena hatuna makazi.
12 Nous nous fatiguons, travaillant de nos mains; on nous maudit, et nous bénissons; on nous persécute, et nous le supportons;
Tunafanya kazi kwa bidii, kwa mikono yetu wenyewe. Tunapodharauliwa, twabariki. Wakati tunapoteswa, twavumilia.
13 On nous blasphème, et nous prions; nous sommes devenus jusqu’à présent comme les ordures du monde, et les balayures rejetées de tous.
Tunapotukanwa, twarudisha kwa upole. Tumekuwa, na tu bado tunahesabiwa kuwa kama kukataliwa na dunia na takataka kwa mambo yote.
14 Ce n’est point pour vous donner de la confusion que j’écris ceci, mais je vous avertis comme mes fils très chers.
Siandiki mambo haya kuwaaibisha ninyi, lakini kuwarudi ninyi kama watoto wangu niwapendao.
15 Car eussiez-vous dix mille maîtres dans le Christ, vous n’avez cependant pas plusieurs pères; puisque c’est moi qui, par l’Evangile, vous ai engendrés en Jésus-Christ.
Hata kama mna waalimu makumi elfu katika Kristo, hamna baba wengi. Kwa kuwa nimekuwa baba yenu katika Yesu Kristo kupitia injili.
16 Je vous en conjure donc, soyez mes imitateurs, comme je le suis du Christ.
Hivyo ninawasihi mniige mimi.
17 C’est pourquoi, je vous ai envoyé Timothée, qui est mon fils bien-aimé, et fidèle dans le Seigneur; il vous rappellera mes voies en Jésus-Christ, selon ce que j’enseigne partout dans toutes les Eglises.
Hiyo ndiyo sababu nilimtuma kwenu Timotheo, mpendwa wangu na mtoto mwaminifu katika Bwana. Atawakumbusheni njia zangu katika Kristo, kama ninavyofundisha kila mahali na kila kanisa.
18 Quelques-uns s’enflent en eux-mêmes, comme si je ne devais plus venir vous voir.
Sasa baadhi yenu wanajisifu, wakitenda kana kwamba sitakuja kwenu.
19 Mais je viendrai vers vous bientôt, si le Seigneur le veut; et je connaîtrai non quel est le langage de ceux qui sont pleins d’eux-mêmes, mais quelle est leur vertu.
Lakini nitakuja kwenu kitambo, kama Bwana akipenda. Ndipo nitajua si maneno yao tu wanaojisifu, lakini nitaona nguvu zao.
20 Car ce n’est pas dans les paroles que consiste le royaume de Dieu, mais dans la vertu.
Kwa kuwa ufalme wa Mungu hauwi katika maneno bali katika nguvu.
21 Que voulez-vous? que je vienne à vous Avec une verge, ou avec chanté et mansuétude?
Mnataka nini? Nije kwenu na fimbo au kwa upendo na katika roho ya upole?