< 1 Chroniques 27 >

1 Or les enfants d’Israël, suivant leur nombre, les princes de familles, les tribuns, les centurions, et les préposés qui, selon leurs bandes, servaient le roi, entrant et sortant à chaque mois dans l’année, étaient chacun à la tête de vingt-quatre mille hommes.
Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.
2 Au premier mois, Jesboa, fils de Zabdiel, était à la tête de la première bande, et sous lui étaient vingt-quatre mille hommes.
Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake.
3 Il était d’entre les fils de Pharès, et le prince de tous les princes dans l’armée, au premier mois.
Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
4 Dudia, l’Ahohite, avait la bande du second mois, et après lui était un second du nom de Macelloth, qui dirigeait une partie de l’armée de vingt-quatre mille hommes.
Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
5 De plus, le chef de la troisième bande, au troisième mois, était Banaïas, le prêtre, fils de Joïada, et dans sa division étaient vingt-quatre mille hommes.
Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000.
6 C’est ce même Banaïas, le plus vaillant parmi les trente, et au-dessus des trente. Amizabad, son fils, était aussi à la tête de sa bande.
Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.
7 Le quatrième chef, au quatrième mois, était Asahel, frère de Joab, et Zabadias, son fils, après lui; et dans sa bande étaient vingt-quatre mille hommes.
Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
8 Le cinquième, au cinquième mois, Samaoth, le Jézerite; et dans sa bande étaient vingt-quatre mille hommes.
Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
9 Le sixième, au sixième mois, Hira, fils d’Accès, le Thécuite; et dans sa bande étaient vingt-quatre mille hommes.
Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
10 Le septième, au septième mois, Hellès, le Phallonite, d’entre les fils d’Ephraïm; et dans sa bande étaient vingt-quatre mille hommes.
Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
11 Le huitième, au huitième mois, Sobochaï, le Husathite, de la race de Zarahi; et dans sa bande étaient vingt-quatre mille hommes.
Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
12 Le neuvième, au neuvième mois, Abiézer, l’Anathothite, d’entre les fils de Jémini; et dans sa bande étaient vingt-quatre mille hommes.
Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
13 Le dixième, au dixième mois, Maraï, le Nétophathite, de la race de Zaraï; et dans sa bande étaient vingt-quatre mille hommes.
Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
14 Le onzième, au onzième mois, Banaïas, le Pharatonite, d’entre les fils d’Ephraïm; et dans sa bande étaient vingt-quatre mille hommes.
Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
15 Le douzième, au douzième mois, Holdaï, le Nétophathite, de la race de Gothoniel; et dans sa bande étaient vingt-quatre mille hommes.
Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
16 Quant aux tribus d’Israël, à la tête des Rubénites, était le chef, Eliézer, fils de Zechri; à la tête des Siméonites, le chef Saphatias, fils de Maacha;
Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa: Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri; kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;
17 À la tête des Lévites, Hasabias, fils de Camuel; à la tête des Aaronites, Sadoc;
kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli; kwa Aroni: Sadoki;
18 À la tête de Juda, Eliu, frère de David; à la tête d’Issachar, Amri, fils de Michaël;
kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi; kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;
19 À la tête des Zabulonites, Jesmaïas, fils d’Abdias; à la tête des Nephthalites, Jérimoth, fils d’Ozriel;
kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia; kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;
20 À la tête des fils d’Ephraïm, Osée, fils d’Ozaziu; à la tête de la demi-tribu de Manassé, Joël, fils de Phadaïa;
kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia; kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;
21 Et à la tête de la demi-tribu de Manassé en Galaad, Jaddo, fils de Zacharie; mais à la tête de Benjamin, Jasiel, fils d’Abner;
kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria; kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;
22 Et à la tête de Dan, Ezrihel, fils de Jéroham. Voilà les princes des enfants d’Israël.
kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.
23 Mais David ne voulut pas les dénombrer au-dessous de vingt ans, parce que le Seigneur avait dit qu’il multiplierait les enfants d’Israël comme les étoiles du ciel.
Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani.
24 Joab, fils de Sarvia, avait commencé à dénombrer; mais il n’acheva pas, parce que pour cela était tombée la colère du Seigneur sur Israël; et c’est pourquoi le nombre de ceux qui avaient été recensés n’a pas été relaté dans les fastes du roi David.
Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.
25 Le surintendant des trésors du roi était Azmoth, fils d’Adiel; quant aux trésors des villes, des bourgs et des tours, Jonathan, fils d’Osias, en avait la garde;
Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme. Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.
26 Mais aux travaux de la campagne et aux laboureurs qui travaillaient la terre, présidait Ezri, fils de Chélub.
Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.
27 À ceux qui cultivaient les vignes, c’était Séméias, le Romathite; mais aux celliers où on met le vin, Zabdias, l’Aphonite.
Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu. Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.
28 Aux plants d’oliviers, aux figuiers, qui étaient dans les plaines, Balanan, le Gédérite, et aux magasins d’huile, Joas.
Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi. Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.
29 Mais aux troupeaux qui paissaient en Saron, fut préposé Sétraï, le Saronite, et aux bœufs dans les vallées, Saphat, fils d’Adli;
Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni. Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.
30 Sur les chameaux, Ubil, L’Ismahélite, et sur les ânes, Jadias, le Méronathite;
Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia. Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.
31 Et sur les brebis, Jaziz l’Agaréen. Tous ceux-là étaient les intendants des biens du roi David.
Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi. Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.
32 Mais Jonathan, oncle de David, homme sage et savant, était un de ses conseillers; lui et Jahiel, fils d’Hachamoni, étaient auprès des enfants du roi.
Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.
33 Achitophel aussi était conseiller du roi; Chusaï, l’Arachite, favori du roi.
Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme. Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme.
34 Après Achitophel étaient Joïada, fils de Banaïas, et Abiathar; mais le prince de l’armée du roi était Joab.
Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari. Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.

< 1 Chroniques 27 >