< 1 Chroniques 19 >
1 Or il arriva que Naas, roi des enfants d’Ammon, mourut, et que son fils régna à sa place.
Baada ya muda, Nahashi mfalme wa Waamoni akafa, mwanawe akaingia mahali pake.
2 Et David dit: Je ferai miséricorde à Hanon, fils de Naas, parce que son père m’a rendu service. David envoya donc des messagers pour le consoler de la mort de son père. Lorsque ceux-ci furent arrivés dans le pays des enfants d’Ammon, pour consoler Hanon,
Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kwa sababu baba yake alinitendea wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe ili kumfariji Hanuni kwa ajili ya kifo cha baba yake. Watu wa Daudi walipofika kwa Hanuni katika nchi ya Waamoni ili kumfariji,
3 Les princes des enfants d’Ammon dirent à Hanon: Vous, peut-être, vous pensez que David, pour l’honneur de votre père, a envoyé ces messagers, afin de vous consoler; et vous ne remarquez pas que c’est pour explorer, sonder et scruter votre territoire que sont venus vers vous ses serviteurs.
wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni, “Hivi unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kuwatuma wajumbe kukufariji? Je, hawa watu hawakuja kuipeleleza na kuidadisi nchi ili waishinde?”
4 Ainsi Hanon rasa la tête et la barbe aux serviteurs de David, coupa leurs tuniques depuis le haut des cuisses jusqu’aux pieds, et les renvoya.
Kwa hiyo Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa ndevu akakata nguo zao katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
5 Lorsque ceux-ci s’en furent allés, et qu’ils eurent mandé cela à David, il envoya à leur rencontre (car ils avaient enduré un grand outrage), et il ordonna qu’ils demeurassent à Jéricho, jusqu’à ce que leur barbe eût crû, et qu’alors ils revinssent.
Mtu mmoja alipofika na kumpasha Daudi habari za watu hawa, akawatuma wajumbe wengine kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote, ndipo mje.”
6 Or les enfants d’Ammon, voyant que tant Hanon que le reste du peuple avaient fait injure à David, envoyèrent mille talents d’argent, pour se procurer, de la Mésopotamie, de la Syrie de Maacha, et de Soba, des chariots et des cavaliers.
Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, Hanuni na Waamoni wakatuma talanta 1,000 za fedha ili kukodisha magari ya vita pamoja na waendeshaji wa hayo magari ya kukokotwa na farasi, kutoka Aramu-Naharaimu, Aramu-Maaka na Soba.
7 Ils réunirent donc à eux trente-deux mille chariots, et le roi de Maacha avec son peuple. Lorsqu’ils furent venus vis-à-vis de Médaba, ils campèrent. Les enfants d’Ammon, s’étant aussi assemblés de leurs villes, vinrent au combat.
Wakakodisha magari ya vita 32,000 yakiwa na waendeshaji wake, pamoja na mfalme wa Maaka na vikosi vyake, wakaja na kupiga kambi karibu na Medeba. Waamoni nao wakakusanyika toka miji yao, wakatoka ili kupigana vita.
8 Ce qu’ayant appris David, il envoya Joab et toute l’armée des hommes vaillants;
Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
9 Et, étant sortis, les enfants d’Ammon rangèrent leur armée en bataille près de la porte de la ville; mais les rois qui étaient venus à leur secours se tinrent séparément dans la campagne.
Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati wale wafalme wengine waliokuja nao walijipanga kwa vita uwanjani.
10 Ainsi Joab, s’apercevant que la guerre se faisait contre lui, et par devant et par derrière, choisit des hommes très braves de tout Israël, et marcha contre les Syriens.
Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
11 Mais le reste du peuple, il le mit sous la main d’Abisaï, son frère; et ils marchèrent contre les enfants d’Ammon;
Akawaweka wale wanajeshi wengine waliobaki chini ya amri ya Abishai ndugu yake, nao wakapangwa ili wakabiliane na Waamoni.
12 Et il dit: Si les Syriens me vainquent, tu me seras en aide; mais si les enfants d’Ammon l’emportent sur toi, j’irai à ton secours.
Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itakupasa wewe unisaidie; lakini kama Waamoni watakuzidi nguvu, basi mimi nitakusaidia.
13 Fortifie-toi et agissons courageusement pour notre peuple et pour les villes de notre Dieu, et le Seigneur fera ce qui est bon en sa présence.
Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
14 Joab marcha donc, et le peuple qui était avec lui, au combat contre les Syriens, et il les mit en fuite.
Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
15 Or les enfants d’Ammon, voyant que les Syriens avaient fui, s’enfuirent, eux aussi, devant Abisaï, son frère, et ils entrèrent dans la ville; et Joab lui-même retourna à Jérusalem.
Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao pia wakakimbia mbele ya nduguye Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi Yerusalemu.
16 Mais les Syriens, voyant qu’ils avaient succombé devant Israël, envoyèrent des messagers, et firent venir les autres Syriens qui étaient au-delà du fleuve: or Sophach, prince de la milice d’Adarézer, était leur chef.
Baada ya Waaramu kuona kwamba wameshindwa na Israeli, wakapeleka wajumbe na kuwataka Waaramu wengine kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakiongozwa na Shofaki, jemadari wa jeshi la Hadadezeri.
17 Lorsque cela eut été annoncé à David, il assembla tout Israël, passa le Jourdain, fondit sur eux et rangea en face son armée en bataille, eux combattant de leur côté.
Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote na kuvuka Yordani. Akasonga mbele dhidi yao na akajipanga kuwakabili. Daudi akapanga vita ili kupigana na Waaramu, nao wakapigana dhidi yake.
18 Cependant les Syriens s’enfuirent devant Israël, et David tua des Syriens sept mille hommes qui étaient sur les chariots, quarante mille de pied, et Sophach, général de cette armée.
Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari 7,000 na askari wao wa miguu 40,000. Pia akamuua Shofaki, jemadari wa jeshi lao.
19 Or les serviteurs d’Adarézer, voyant qu’ils étaient vaincus par Israël, passèrent à David et lui furent assujettis; et la Syrie ne voulut plus donner secours aux enfants d’Ammon
Raiya wa Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya mapatano ya amani na Daudi, wakawa watumishi wake. Hivyo Waaramu hawakukubali kuwasaidia Waamoni tena.