< Marc 2 >

1 Quelques jours après, Jésus revint à Capernaüm, et l'on apprit qu'il était dans la maison.
Baada ya siku kadhaa Yesu alirudi Kapernaumu, watu wakasikia kwamba amerudi nyumbani.
2 Il s'y assembla tant de monde, qu'il n'y avait plus de place même devant la porte; et il leur annonçait la parole.
Hivyo watu wengi wakakusanyika kiasi kwamba hapakubaki nafasi yoyote hata mlangoni! Naye akawahubiria Neno.
3 Alors, il vint des gens qui lui amenaient un paralytique, porté par quatre hommes.
Ndipo baadhi ya watu wakaja wakamletea Yesu mtu aliyepooza, akiwa amebebwa na watu wanne.
4 Mais, ne pouvant arriver jusqu'à lui à cause de la foule, ils découvrirent le toit au-dessus de l'endroit où il était; et, par l'ouverture, ils descendirent le lit sur lequel le paralytique était couché.
Kwa kuwa walikuwa hawawezi kumfikisha kwa Yesu kwa ajili ya umati wa watu, walitoboa tundu kwenye paa mahali pale alipokuwa Yesu, wakamshusha yule aliyepooza kwa kitanda alichokuwa amelalia.
5 Jésus, voyant leur foi, dit au paralytique: Mon enfant, tes péchés te sont pardonnés.
Yesu alipoiona imani yao, alimwambia yule mtu aliyepooza, “Mwanangu, dhambi zako zimesamehewa.”
6 Or, il y avait là quelques scribes qui se tenaient assis, et ils faisaient ce raisonnement dans leur coeur:
Basi baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa wameketi huko wakawaza mioyoni mwao,
7 Pourquoi cet homme parle-t-il ainsi? Il blasphème! Qui peut pardonner les péchés, que Dieu seul?
“Kwa nini mtu huyu anasema hivi? Huyu anakufuru! Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
8 Aussitôt Jésus, ayant connu en son esprit qu'ils raisonnaient ainsi en eux-mêmes, leur dit: Pourquoi faites-vous ces raisonnements dans vos coeurs?
Mara moja Yesu akatambua rohoni mwake kile walichokuwa wanawaza mioyoni mwao, naye akawaambia, “Kwa nini mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
9 Lequel est le plus aisé, de dire au paralytique: Tes péchés te sont pardonnés. ou de dire: Lève-toi, prends ton lit, et marche?
Je, ni lipi lililo rahisi zaidi: kumwambia huyu aliyepooza, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uchukue mkeka wako, uende’?
10 Or, — afin que vous sachiez que le Fils de l'homme a sur la terre le pouvoir de pardonner les péchés, —
Lakini ili mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi…” Yesu akamwambia yule aliyepooza,
11 je te l'ordonne, dit-il au paralytique, lève-toi, prends ton lit, et va dans ta maison.
“Nakuambia, inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani kwako.”
12 Cet homme se leva, et aussitôt, ayant pris son lit, il sortit en présence de tout le monde; de sorte qu'ils étaient tous dans l'étonnement, et ils glorifiaient Dieu en disant: Nous n'avons jamais rien vu de pareil!
Yule mtu aliyekuwa amepooza akasimama, akachukua mkeka wake, akatembea machoni pao wote! Jambo hili likawashangaza wote, wakamtukuza Mungu, wakisema, “Hatujapata kuona jambo kama hili kamwe!”
13 Alors Jésus retourna du côté de la mer; tout le peuple venait à lui, et il les enseignait.
Yesu akaenda tena kandokando ya Bahari ya Galilaya. Umati mkubwa wa watu ukamfuata, naye akaanza kuwafundisha.
14 En passant, il vit Lévi, fils d'Alphée, assis au bureau du péage. Il lui dit: Suis-moi; et lui, se levant, le suivit.
Alipokuwa akitembea, akamwona Lawi mwana wa Alfayo ameketi forodhani mahali pa kutoza ushuru, akamwambia, “Nifuate.” Lawi akaondoka, akamfuata Yesu.
15 Comme Jésus était à table dans la maison de Lévi, beaucoup de péagers et de pécheurs se mirent à table avec lui et ses disciples; car il y en avait beaucoup qui l'avaient suivi.
Yesu alipokuwa akila chakula nyumbani mwa Lawi, watoza ushuru wengi pamoja na “wenye dhambi” walikuwa wakila pamoja naye na wanafunzi wake, kwa maana kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakimfuata.
16 Les scribes appartenant au parti des pharisiens, voyant qu'il mangeait avec des péagers et des pécheurs, disaient à ses disciples: Il mange avec des péagers et des pécheurs!
Baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa Mafarisayo walipomwona akila pamoja na watoza ushuru na “wenye dhambi,” wakawauliza wanafunzi wake: “Mbona Yesu anakula pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”
17 Jésus, ayant entendu cela, leur dit: Ce ne sont pas ceux qui se portent bien qui ont besoin de médecin, mais ceux qui se portent mal. Je ne suis pas venu appeler les justes, mais les pécheurs.
Yesu aliposikia haya akawaambia, “Watu wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa. Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.”
18 Or, les disciples de Jean et les pharisiens jeûnaient. Ils vinrent dire à Jésus: D'où vient que les disciples de Jean et ceux des pharisiens jeûnent, et que tes disciples ne jeûnent pas?
Basi wanafunzi wa Yohana pamoja na Mafarisayo walikuwa wakifunga. Baadhi ya watu wakamjia Yesu na kumuuliza, “Mbona wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo hufunga lakini wanafunzi wako hawafungi?”
19 Jésus leur répondit: Les amis de l'époux peuvent-ils jeûner pendant que l'époux est avec eux? Tant qu'ils ont l'époux avec eux, ils ne peuvent jeûner.
Yesu akawajibu, “Wageni wa bwana arusi wawezaje kufunga wakati angali pamoja nao? Wakati bwana arusi bado yuko pamoja nao, hawawezi kufunga.
20 Mais le temps viendra où l'époux leur sera ôté; alors ils jeûneront ce jour-là.
Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao. Siku hiyo ndipo watakapofunga.
21 Personne ne coud une pièce de drap neuf à un vieux vêtement; autrement, la pièce neuve emporte une partie du vieux drap, et la déchirure en devient pire.
“Hakuna mtu ashoneaye kiraka cha nguo mpya kwenye nguo iliyochakaa. Akifanya hivyo, kile kiraka kipya kitachanika kutoka ile nguo iliyochakaa, nayo itachanika zaidi.
22 Et personne ne met du vin nouveau dans de vieilles outres; autrement, le vin fait rompre les outres; le vin est perdu, et les outres aussi.
Wala hakuna mtu awekaye divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, ile divai mpya itavipasua hivyo viriba, nayo hiyo divai itamwagika na viriba vitaharibika. Lakini divai mpya huwekwa kwenye viriba vipya.”
23 Il arriva, comme Jésus passait par les blés un jour de sabbat, que ses disciples, chemin faisant, se mirent à arracher des épis.
Siku moja ya Sabato, Yesu pamoja na wanafunzi wake walikuwa wakipita katikati ya mashamba ya nafaka. Walipokuwa wakitembea, wanafunzi wake wakaanza kuvunja masuke.
24 Alors les pharisiens lui dirent: Regarde! Pourquoi font-ils ce qui n'est pas permis le jour du sabbat?
Mafarisayo wakamwambia, “Tazama, mbona wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato?”
25 Il leur répondit: N'avez-vous jamais lu ce que fit David, lorsqu'il fut dans le besoin et qu'il eut faim, lui et ceux qui étaient avec lui;
Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma kamwe alivyofanya Daudi wakati yeye na wenzake walikuwa na njaa, wakahitaji chakula?
26 comment il entra dans la maison de Dieu, du temps d'Abiathar, souverain sacrificateur, et mangea les pains de proposition — qu'il est permis aux sacrificateurs seuls de manger — et comment il en donna même à ceux qui étaient avec lui?
Daudi aliingia katika nyumba ya Mungu, wakati Abiathari alikuwa kuhani mkuu, akaila ile mikate iliyowekwa wakfu, ambayo ni halali kuliwa na makuhani peke yao. Naye pia akawapa wenzake.”
27 Puis Jésus ajouta: Le sabbat a été fait pour l'homme, et non pas l'homme pour le sabbat.
Kisha Yesu akawaambia, “Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, lakini si mwanadamu kwa ajili ya Sabato.
28 Ainsi le Fils de l'homme est maître même du sabbat.
Hivyo, Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”

< Marc 2 >