< Luc 10 >
1 Après cela, le Seigneur désigna encore soixante-dix autres disciples; et il les envoya deux à deux devant lui, dans toutes les villes et dans tous les lieux où il devait aller lui-même.
Baada ya hayo, Bwana aliwachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawiliwawili, wamtangulie katika kila kijiji na mahali ambapo yeye mwenyewe alitaka kwenda.
2 Il leur disait: La moisson est grande; mais il y a peu d'ouvriers. Priez donc le maître de la moisson d'envoyer des ouvriers dans sa moisson.
Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache. Kwa hivyo, mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake.
3 Allez! Je vous envoie comme des agneaux au milieu des loups.
Sasa nendeni; fahamuni kwamba ninawatuma ninyi kama kondoo wanaokwenda kati ya mbwa mwitu.
4 Ne portez ni bourse, ni sac, ni chaussures, et ne saluez personne en chemin.
Msichukue mfuko wa fedha, mkoba, wala viatu; msimsalimu mtu yeyote njiani.
5 Dans quelque maison que vous entriez, dites d'abord: La paix soit sur cette maison!
Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza wasalimuni hivi: Amani iwe katika nyumba hii!
6 Et s'il se trouve là un enfant de la paix, votre paix reposera sur lui; sinon, elle reviendra à vous.
Kama akiwako mwenye kupenda amani, amani yenu itakaa naye, la sivyo, itawarudieni.
7 Demeurez dans cette maison-là, mangeant et buvant ce qu'on vous donnera; car l'ouvrier est digne de son salaire. Ne passez point de maison en maison.
Kaeni katika nyumba hiyo mkila na kunywa wanavyowapeni, maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msiende mara nyumba hii mara nyumba ile.
8 Dans quelque ville que vous entriez, si l'on vous reçoit, mangez ce qu'on vous présentera.
Kama mkifika mji fulani na watu wakiwakaribisha, kuleni wanavyowapeni.
9 Guérissez les malades qui s'y trouveront, et dites-leur: Le royaume de Dieu s'est approché de vous.
Ponyeni wagonjwa walioko huko, waambieni watu: Ufalme wa Mungu umekaribia kwenu.
10 Mais, dans quelque ville que vous entriez, si l'on ne vous reçoit pas, allez sur les places publiques et dites:
Lakini mkiingia katika mji wowote, wasipowakaribisheni, tokeni; nanyi mpitapo katika barabara zao semeni:
11 Nous secouons contre vous la poussière même de votre ville, qui s'est attachée à nos pieds; sachez pourtant que le royaume de Dieu s'est approché de vous.
Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu tunawakung'utieni. Lakini, jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
12 Je vous dis qu'au dernier jour, Sodome sera traitée moins rigoureusement que cette ville.
Hakika nawaambieni, siku ile mji huo utapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Sodoma.
13 Malheur à toi, Corazin! Malheur à toi, Bethsaïda! Car si les miracles qui ont été faits au milieu de vous avaient été faits dans Tyret dans Sidon, il y a longtemps qu'elles se seraient repenties, en prenant le sac et la cendre.
“Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika kule Tiro na Sidoni, watu wake wangalikwishavaa mavazi ya gunia kitambo, na kukaa katika majivu kuonyesha kwamba wametubu.
14 C'est pourquoi, au jour du jugement, Tyr et Sidon seront traitées moins rigoureusement que vous.
Hata hivyo, Siku ya Hukumu ninyi mtapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Tiro na Sidoni.
15 Et toi, Capernaüm qui as été élevée jusqu'au ciel, tu seras abaissée jusqu'en enfer! (Hadēs )
Na wewe Kafarnaumu, unataka kujikweza mpaka mbinguni? La; utaporomoshwa mpaka Kuzimu.” (Hadēs )
16 — Qui vous écoute, m'écoute; qui vous rejette, me rejette; et qui me rejette, rejette Celui qui m'a envoyé.
Halafu akasema, “Anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; na anayekataa kuwapokea ninyi, anakataa kunipokea mimi. Yeyote anayekataa kunipokea, anakataa kumpokea yule aliyenituma.”
17 Les soixante-dix revinrent avec joie, en disant: Seigneur, les démons mêmes nous sont assujettis en ton nom.
Baadaye, wale sabini na wawili walirudi wamejaa furaha, wakisema, “Bwana, hata pepo wametutii tulipolitaja jina lako.”
18 Alors Jésus leur dit: Je voyais Satan tomber du ciel comme un éclair.
Yeye akawaambia, “Nilimwona Shetani jinsi alivyokuwa anaporomoka kama umeme kutoka mbinguni.
19 Voici que je vous ai donné le pouvoir de fouler aux pieds les serpents, les scorpions et toute la puissance de l'ennemi; et rien ne pourra vous nuire.
Naam, nimewapeni uwezo wa kukanyaga nyoka na ng'e, na uwezo juu ya nguvu zote za yule adui; hakuna chochote kitakachowadhuru.
20 Toutefois, ne vous réjouissez pas de ce que les esprits vous sont assujettis; mais réjouissez-vous de ce que vos noms sont écrits dans les cieux.
Hata hivyo, msifurahi kwa sababu pepo wamewatii, bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.”
21 A cette heure même, Jésus tressaillit de joie par le Saint-Esprit, et il dit: Je te loue, ô Père, Seigneur du ciel et de la terre, de ce que tu as caché ces choses aux sages et aux intelligents, et de ce que tu les as révélées aux petits enfants! Oui, Père, il en est ainsi, parce que tu l'as trouvé bon.
Saa ileile, Yesu akafurahi kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akasema, “Nakushukuru ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa kuwa umewaficha wenye hekima na elimu mambo haya, ukawafumbulia wadogo. Naam, Baba, ndivyo ilivyokupendeza.”
22 Toutes choses m'ont été remises par mon Père; et nul ne connaît qui est le Fils, si ce n'est le Père, ni qui est le Père, si ce n'est le Fils, et celui à qui le Fils aura voulu le révéler.
Kisha akasema, “Baba yangu ameweka yote mikononi mwangu. Hakuna amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala amjuaye Baba ni nani ila Mwana, na yeyote yule ambaye Mwana anataka kumfunulia hayo.”
23 Puis, se tournant vers ses disciples, il leur dit en particulier: Heureux les yeux qui voient ce que vous voyez!
Halafu akawaelekea wafuasi wake akawaambia, “Heri wanaoona yale mnayoyaona ninyi!
24 Car, je vous le déclare, beaucoup de prophètes et de rois ont souhaité de voir ce que vous voyez, et ils ne l'ont pas vu, et d'entendre ce que vous entendez, et ils ne l'ont pas entendu.
Hakika, manabii na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona ninyi wasiyaone, na kusikia yale mnayoyasikia wasiyasikie.”
25 Alors un docteur de la loi se leva pour mettre Jésus à l'épreuve, et il lui dit: Maître, que ferai-je pour hériter la vie éternelle? (aiōnios )
Baadaye mwalimu mmoja wa Sheria alisimama akamwuliza akitaka kumtega, “Mwalimu, nifanye nini ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios )
26 Jésus lui dit: Qu'est-ce qui est écrit dans la loi? Qu'y lis-tu?
Yesu akamwuliza, “Imeandikwa nini katika Sheria? Unaelewaje?”
27 Il répondit: «Tu aimeras le Seigneur, ton Dieu, de tout ton coeur, de toute ton âme, de toute ta force et de toute ta pensée, et ton prochain comme toi-même.»
Akamjibu, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote. Na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
28 Jésus lui dit: Tu as bien répondu fais cela, et tu vivras.
Yesu akawaambia, “Vema! Fanya hivyo, nawe utaishi.”
29 Mais cet homme, voulant se justifier, dit à Jésus: Et qui est mon prochain?
Lakini yeye akitaka kujihakikishia kuwa mwema akamwuliza Yesu, “Na jirani yangu ni nani?”
30 Jésus reprit la parole et dit: Un homme descendait de Jérusalem à Jérico. Il tomba entre les mains de brigands qui le dépouillèrent, et qui, après l'avoir couvert de blessures, s'en allèrent, le laissant à demi-mort.
Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anashuka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko. Alipokuwa njiani, alivamiwa na majambazi, wakamnyang'anya mali yake na kumpiga, wakamwacha amelala pale nusu mfu.
31 Or, il se trouva qu'un sacrificateur descendait par ce chemin-là; il vit cet homme, et il passa outre.
Kumbe, kuhani mmoja akawa anapita barabara ileile, akamwona, akapita kando.
32 Un lévite aussi, étant venu en cet endroit, s'approcha et, l'ayant vu, il passa outre.
Hali kadhalika na Mlawi mmoja, alipofika mahali akamwona, akapita kando.
33 Mais un Samaritain, qui était en voyage, arriva près de lui, et, l'ayant vu, il fut touché de compassion.
Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa anasafiri, alifika pale yule mtu alipokuwa, naye alipomwona, alimwonea huruma.
34 Il s'approcha et banda ses plaies, en y versant de l'huile et du vin; puis il le mit sur sa propre monture, le conduisit à une hôtellerie et prit soin de lui.
Akamwendea, akamtibu majeraha yake kwa kumtia mafuta na divai; na kuyafunga halafu akampandisha juu ya punda wake akampeleka katika nyumba moja ya wageni akamuuguza.
35 Le lendemain, il prit deux deniers, les donna à l'hôtelier et lui dit: Aie soin de lui; et tout ce que tu dépenseras de plus, je te le rendrai à mon retour.
Kesho yake akatoa fedha dinari mbili akampa yule mwenye nyumba, akamwambia, Muuguze mtu huyu; na chochote utakachotumia zaidi, nitakulipa nitakaporudi.”
36 Lequel de ces trois te paraît avoir été le prochain de celui qui était tombé entre les mains des brigands?
Kisha Yesu akauliza, “Kati ya hao watatu, ni yupi aliyeonyesha kuwa jirani yake yule aliyevamiwa na majambazi?”
37 Le docteur de la loi répondit: C'est celui qui a exercé la miséricorde envers lui. Jésus dit: Va, et fais de même!
Yule mwalimu wa Sheria akamjibu, “Ni yule aliyemwonea huruma.” Yesu akamwambia, “Nenda ukafanye vivyo hivyo.”
38 Comme ils étaient en chemin, il entra dans un village, et une femme, nommée Marthe, le reçut dans sa maison.
Walipokuwa safarini, waliingia katika kijiji kimoja na mwanamke mmoja, aitwaye Martha, alimkaribisha nyumbani kwake.
39 Elle avait une soeur, appelée Marie, qui, se tenant assise aux pieds du Seigneur, écoutait sa parole.
Martha alikuwa na dada yake aitwaye Maria; huyu aliketi karibu na Yesu akisikiliza mafundisho yake.
40 Or, Marthe était absorbée par divers soins; elle vint et dit à Jésus: Seigneur, ne considères-tu pas que ma soeur me laisse servir toute seule? Dis-lui donc de m'aider.
Lakini Martha alikuwa anashughulika na mambo mengi. Basi, akamwendea Yesu, akamwambia, “Bwana, hivi hujali kwamba dada yangu ameniacha nishughulike peke yangu? Mwambie basi, anisaidie.”
41 Le Seigneur lui répondit: Marthe, Marthe, tu te mets en peine et tu t'agites pour beaucoup de choses;
Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, unahangaika na kusumbuka kwa mambo mengi.
42 mais une seule chose est nécessaire. Et Marie a choisi la bonne part qui ne lui sera point ôtée.
Kitu kimoja tu ni muhimu. Maria amechagua kitu bora zaidi ambacho hakuna mtu atakayemnyag'anya.”