< Actes 27 >
1 Quand il fut décidé que nous irions par mer en Italie, on remit Paul et quelques autres prisonniers à un centenier nommé Julius, de la cohorte Augusta.
Walipokwisha amua tusafiri mpaka Italia, walimweka Paulo pamoja na wafungwa wengine chini ya ulinzi wa Yulio aliyekuwa ofisa wa jeshi katika kikosi kiitwacho “Kikosi cha Augusto.”
2 Étant montés sur un navire d'Adramytte, qui devait longer les côtes de l'Asie, nous partîmes. Aristarque, Macédonien de Thessalonique, était avec nous.
Tulipanda meli ya Adiramito iliyokuwa inasafiri na kupitia bandari kadhaa za mkoa wa Asia, tukaanza safari. Aristarko, mwenyeji wa Makedonia kutoka Thesalonika, alikuwa pamoja nasi.
3 Le jour suivant, nous arrivâmes à Sidon; et Julius, qui traitait Paul avec humanité, lui permit d'aller voir ses amis et de recevoir leurs soins.
Kesho yake tulitia nanga katika bandari ya Sidoni. Yulio alimtendea Paulo vizuri kwa kumruhusu awaone rafiki zake na kupata mahitaji yake.
4 Puis, étant partis de là, nous suivîmes les côtes de l'île de Chypre, parce que les vents étaient contraires.
Kutoka huko tuliendelea na safari, lakini kwa kuwa upepo ulikuwa unavuma kwa kasi kutujia kwa mbele, tulipitia upande wa kisiwa cha Kupro ambapo upepo haukuwa mwingi.
5 Après avoir traversé la mer de Cilicie et de Pamphylie, nous arrivâmes à Myra, en Lycie.
Halafu tulivuka bahari ya Kilikia na Pamfulia, tukatia nanga Mura, mji wa Lukia.
6 Là, le centenier trouva un navire d'Alexandrie, qui allait en Italie, et sur lequel il nous fit monter.
Hapo yule ofisa alikuta meli moja ya Aleksandria iliyokuwa inakwenda Italia, na hivyo akatupandisha ndani.
7 Après plusieurs jours d'une navigation lente et pénible, nous arrivâmes vis-à-vis de Cnide. Le vent ne nous permettant pas d'aborder, nous suivîmes les côtes de l'île de Crète, vers Salmone.
Kwa muda wa siku nyingi tulisafiri polepole, na kwa shida tulifika karibu na Nido. Kwa sababu upepo ulikuwa bado unatupinga, tuliendelea mbele moja kwa moja tukapitia upande wa Krete karibu na rasi Salmone ambapo upepo haukuwa mwingi.
8 Après l'avoir longée, non sans difficulté, nous vînmes à un endroit appelé Beaux-Ports, près de la ville de Lasée.
Tulipita kando yake polepole tukafika mahali paitwapo “Bandari Nzuri”, karibu na mji wa Lasea.
9 Comme il s'était écoulé beaucoup de temps, et que la navigation devenait dangereuse — l'époque du Jeûne étant déjà passée — Paul fit entendre ces paroles d'avertissement:
Muda mrefu ulikuwa umepita, na hata siku ya kufunga ilikuwa imekwisha pita. Sasa ilikuwa hatari sana kusafiri kwa meli. Basi, Paulo aliwapa onyo:
10 Je vois que la navigation ne se fera pas sans péril et sans de graves dommages, non seulement pour la cargaison et le bâtiment, mais aussi pour nos personnes.
“Waheshimiwa, nahisi kwamba safari hii itakuwa ya shida na hasara nyingi si kwa shehena na meli tu, bali pia kwa maisha yetu.”
11 Mais le centenier se fiait plutôt au pilote et au capitaine du navire, qu'à ce que Paul disait.
Lakini yule ofisa alivutiwa zaidi na maoni ya nahodha na ya mwenye meli kuliko yale aliyosema Paulo.
12 Comme le port n'était pas bon pour hiverner, la plupart furent d'avis d'en repartir et de tâcher de gagner Phénix, port de la Crète, qui regarde le Sud-Ouest et le Nord-Ouest, pour y passer l'hiver.
Kwa kuwa bandari hiyo haikuwa mahali pazuri pa kukaa wakati wa baridi, wengi walipendelea kuendelea na safari, ikiwezekana mpaka Foinike. Foinike ni bandari ya Krete inayoelekea kusini-magharibi na kaskazini-magharibi; na huko wangeweza kukaa wakati wa baridi.
13 Une brise du Sud s'étant mise à souffler, ils crurent qu'ils exécuteraient à leur gré leur dessein, et, ayant levé l'ancre, ils côtoyèrent de près l'île de Crète.
Basi, upepo mzuri wa kusi ulianza kuvuma, nao wakadhani wamefanikiwa lengo lao; hivyo wakang'oa nanga, wakaiendesha meli karibu sana na pwani ya Krete.
14 Bientôt après, un vent furieux, appelé Euraquilon, vint s'abattre sur l'île.
Lakini haukupita muda, upepo mkali uitwao “Upepo wa Kaskazi” ulianza kuvuma kutoka kisiwani.
15 Le navire se trouva entraîné, sans pouvoir résister à l'ouragan, et nous nous laissâmes aller à la dérive.
Upepo uliipiga ile meli, na kwa kuwa hatukuweza kuukabili, tukaiacha ikokotwe na huo upepo.
16 Ayant été poussés au-dessous d'une petite île, appelée Clauda, nous parvînmes avec peine à nous rendre maîtres de la chaloupe.
Kisiwa kimoja kiitwacho Kanda kilitukinga kidogo na ule upepo; na tulipopita kusini mwake tulifaulu, ingawa kwa shida, kuusalimisha ule mtumbwi wa meli.
17 Après l'avoir hissée, on prit des mesures de sûreté. On lia le navire par-dessous avec des cordes; puis, dans la crainte d'échouer sur les bancs de la Syrte, on amena les voiles, et on se laissa ainsi emporter par le vent.
Wale wanamaji waliuvuta mtumbwi ndani, kisha wakaizungushia meli kamba na kuifunga kwa nguvu. Waliogopa kwamba wangeweza kukwama kwenye ufuko wa bahari, pwani ya Libya. Kwa hiyo walishusha matanga na kuiacha meli ikokotwe na upepo.
18 Le lendemain, la tempête étant toujours aussi forte, on jeta la cargaison à la mer.
Dhoruba iliendelea kuvuma na kesho yake wakaanza kutupa nje shehena ya meli.
19 Le troisième jour, nous jetâmes de nos propres mains les agrès du navire.
Siku ya tatu, wakaanza pia kutupa majini vifaa vya meli kwa mikono yao wenyewe.
20 Pendant plusieurs jours, ni le soleil, ni les étoiles ne se montrèrent, et la tempête restait toujours si violente que nous perdîmes toute espérance de nous sauver.
Kwa muda wa siku nyingi hatukuweza kuona jua wala nyota; dhoruba iliendelea kuvuma sana, hata matumaini yote ya kuokoka yakatuishia.
21 Comme il y avait longtemps qu'on n'avait mangé, Paul se leva au milieu d'eux et leur dit: Mes amis, il aurait fallu me croire, et ne pas partir de Crète; nous aurions évité ce péril et cette perte.
Baada ya kukaa muda mrefu bila kula chakula, Paulo alisimama kati yao, akasema, “Waheshimiwa, ingalikuwa afadhali kama mngalinisikiliza na kuacha kusafiri kutoka Krete. Kama mngalifanya hivyo tungaliiepuka shida hii na hasara hizi zote.
22 Mais maintenant, je vous exhorte à prendre courage; aucun de nous ne périra, et il n'y aura de perte que celle du navire.
Lakini sasa ninawaombeni muwe na moyo; hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza maisha yake; meli tu ndiyo itakayopotea.
23 Cette nuit, en effet, un ange du Dieu à qui je suis et que je sers, m'est apparu
Kwa maana jana usiku malaika wa yule Mungu ambaye mimi ni wake na ambaye mimi ninamwabudu alinitokea,
24 et m'a dit: Paul, ne crains point; il faut que tu comparaisses devant César; et voici que Dieu t'a donné tous ceux qui naviguent avec toi.
akaniambia: Paulo usiogope! Ni lazima utasimama mbele ya Kaisari; naye Mungu, kwa wema wake, amekufadhili kwa kuwaokoa wote wanaosafiri nawe wasiangamie.
25 C'est pourquoi, mes amis, ayez bon courage, car j'ai cette confiance en Dieu, qu'il en sera comme il m'a été dit;
Hivyo, waheshimiwa, jipeni moyo! Maana ninamwamini Mungu kwamba itakuwa sawa kama nilivyoambiwa.
26 mais il faut que nous soyons jetés sur quelque île.
Lakini ni lazima tutatupwa ufukoni mwa kisiwa fulani.”
27 C'était déjà la quatorzième nuit que nous étions ballottés sur l'Adriatique, quand vers minuit, les matelots estimèrent qu'ils approchaient de quelque terre.
Usiku wa siku ya kumi na nne, tulikuwa tunakokotwa huku na huku katika bahari ya Adria. Karibu na usiku wa manane wanamaji walijihisi kuwa karibu na nchi kavu.
28 Ayant jeté la sonde, ils trouvèrent vingt brasses; un peu plus loin, ils la jetèrent encore, et trouvèrent quinze brasses.
Hivyo walitafuta kina cha bahari kwa kuteremsha kamba iliyokuwa imefungiwa kitu kizito, wakapata kina cha mita arobaini. Baadaye wakapima tena wakapata mita thelathini.
29 Alors, craignant de donner contre des écueils, ils jetèrent quatre ancres du haut de la poupe, et ils appelaient de leurs voeux la venue du jour.
Kwa sababu ya kuogopa kukwama kwenye miamba, waliteremsha nanga nne nyuma ya meli; wakaomba kuche upesi.
30 Mais, comme les matelots cherchaient à s'échapper du navire et mettaient la chaloupe à la mer, sous prétexte de jeter des ancres du côté de la proue,
Wanamaji walitaka kutoroka, na walikwisha kuteremsha ule mtumbwi majini, wakijisingizia kwamba wanakwenda kuteremsha nanga upande wa mbele wa meli.
31 Paul dit au centenier: Si ces hommes ne restent pas à bord, vous ne pouvez être sauvés.
Lakini Paulo alimwambia yule ofisa wa jeshi na askari wake, “Kama wanamaji hawa hawabaki ndani ya meli, hamtaokoka.”
32 Alors les soldats coupèrent les cordes de la chaloupe et la laissèrent tomber.
Hapo wale askari walizikata kamba zilizokuwa zimeshikilia ule mtumbwi, wakauacha uchukuliwe na maji.
33 Puis, en attendant que le jour vînt, Paul les exhorta tous à prendre de la nourriture. Voici, leur dit-il, le quatorzième jour que vous êtes dans l'attente, et que vous restez à jeun, sans rien manger.
Karibu na alfajiri, Paulo aliwahimiza wote wale chakula: “Kwa siku kumi na nne sasa mmekuwa katika mashaka na bila kula; hamjala kitu chochote.
34 Je vous exhorte donc à prendre de la nourriture; car cela est nécessaire à votre salut. Aucun d'entre vous ne perdra un cheveu de sa tête!
Basi, ninawasihi mle chakula kwa maana mnakihitaji ili mweze kuendelea kuishi. Maana hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.”
35 Ayant ainsi parlé, il prit du pain; il rendit grâces à Dieu, en présence de tous; puis il le rompit et se mit à manger.
Baada ya kusema hivyo, Paulo alichukua mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote, akaumega, akaanza kula.
36 Tous alors, reprenant courage, mangèrent aussi.
Hapo wote wakapata moyo, nao pia wakala chakula.
37 Or, nous étions en tout deux cent soixante seize personnes à bord.
Jumla tulikuwa watu mia mbili na sabini na sita katika meli.
38 Quand ils se furent rassasiés, ils allégèrent le navire en jetant les provisions à la mer.
Baada ya kila mmoja kula chakula cha kutosha, walipunguza uzito wa meli kwa kutupa nafaka baharini.
39 Le jour venu, ils ne reconnaissaient pas la terre; mais, ayant aperçu un golfe avec une plage, ils résolurent d'y mettre, si possible, le navire à l'abri.
Kulipokucha, wanamaji hawakuweza kuitambua nchi ile, ila waliona ghuba moja yenye ufuko; wakaamua kutia nanga huko kama ikiwezekana.
40 Ils coupèrent donc les câbles des ancres qu'ils abandonnèrent à la mer, et ils lâchèrent les amarres des gouvernails; puis, ayant mis au vent la voile d'artimon, ils tâchèrent de gagner le rivage.
Hivyo walikata nanga na kuziacha baharini, na wakati huohuo wakazifungua kamba zilizokuwa zimeufunga usukani, kisha wakatweka tanga moja mbele kushika upepo, wakaelekea ufukoni.
41 Mais, étant tombés sur un endroit battu par la mer, des deux côtés, ils y firent échouer le navire; et, tandis que la proue enfoncée restait immobile, la poupe était brisée par la violence des vagues.
Lakini walifika mahali ambapo mikondo miwili ya bahari hukutana, na meli ikakwama. Sehemu ya mbele ilikuwa imezama mchangani bila kutikisika. Sehemu ya nyuma ya meli ilianza kuvunjika vipandevipande kwa mapigo ya nguvu ya mawimbi.
42 Alors les soldats furent d'avis de tuer les prisonniers, de peur que l'un d'eux ne vînt à s'échapper à la nage.
Askari walitaka kuwaua wafungwa wote kwa kuogopa kwamba wangeogelea hadi pwani na kutoroka.
43 Mais le centenier, voulant sauver Paul, les empêcha d'exécuter leur dessein. Il ordonna à ceux qui savaient nager de se jeter à l'eau les premiers et de gagner la terre,
Lakini kwa vile yule ofisajeshi alitaka kumwokoa Paulo, aliwazuia wasifanye hivyo. Aliamuru wale waliojua kuogelea waruke kutoka melini na kuogelea hadi pwani,
44 et à ceux qui restaient, de se mettre, les uns sur des planches, les autres sur quelques débris du navire. C'est ainsi que tous parvinrent à terre, sains et saufs.
na wengine wafuate wakijishikilia kwenye mbao au kwenye vipande vya meli iliyovunjika. Ndivyo sisi sote tulivyofika salama pwani.