< Actes 2 >
1 Quand fut arrivé le jour de la Pentecôte, ils étaient tous ensemble dans le même lieu.
Siku ya Pentekoste ilipofika, waumini wote walikuwa wamekusanyika pamoja.
2 Tout à coup, il vint du ciel un bruit pareil à celui d'un vent qui souffle avec impétuosité, et il remplit toute la maison où ils étaient assis.
Ghafla, sauti ikasikika kutoka angani; sauti iliyokuwa kama ya upepo mkali, ikajaza ile nyumba yote walimokuwa wamekaa.
3 Alors ils virent paraître des langues séparées les unes des autres, qui étaient comme des langues de feu, et qui se posèrent sur chacun d'eux.
Kisha, vikatokea vitu vilivyoonekana kama ndimi za moto, vikagawanyika na kutua juu ya kila mmoja wao.
4 Ils furent tous remplis du Saint-Esprit, et ils commencèrent à parler en des langues étrangères, selon que l'Esprit leur donnait de s'exprimer.
Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema lugha mbalimbali kadiri Roho alivyowawezesha.
5 Or, il y avait, en séjour à Jérusalem, des Juifs, hommes pieux venus de toutes les nations qui sont sous le ciel.
Na huko Yerusalemu walikuwako Wayahudi, watu wamchao Mungu, waliotoka katika kila nchi duniani.
6 Quand ce bruit se fit entendre, la foule accourut, et tous furent étonnés de ce que chacun d'eux les entendait parler sa propre langue.
Waliposikia sauti hiyo, kundi kubwa la watu lilikusanyika. Wote walishtuka sana kwani kila mmoja wao aliwasikia hao waumini wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
7 Ils en étaient tous hors d'eux-mêmes et remplis d'admiration, et ils disaient: Tous ces gens-là qui parlent, ne sont-ils pas des Galiléens?
Walistaajabu na kushangaa, wakisema, “Je, hawa wote tunaowasikia wakisema hivi, si wenyeji wa Galilaya?
8 Comment donc chacun de nous les entend-il parler la propre langue du pays où il est né?
Imekuwaje, basi, kwamba kila mmoja wetu anawasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe?
9 Parthes, Mèdes, Élamites, ceux qui habitent la Mésopotamie, la Judée, la Cappadoce, le Pont, l'Asie,
Baadhi yetu ni Waparthi, Wamedi na Waelami; wengine ni wenyeji wa Mesopotamia, Yudea, Kapadokia, Ponto na Asia,
10 la Phrygie, la Pamphylie, l'Egypte, le territoire de la Libye qui est près de Cyrène, et ceux qui sont venus de Rome, tant Juifs que proselytes,
Frugia na Pamfulia, Misri na sehemu za Libya karibu na Kurene; wengine wetu ni wageni kutoka Roma,
11 Cretois et Arabes, nous les entendons parler dans nos langues des choses magnifiques de Dieu.
Wayahudi na watu walioongokea dini ya Kiyahudi; wengine wametoka Krete na Arabia. Sisi sote tunasikia wakisema kwa lugha zetu wenyewe mambo makuu ya Mungu.”
12 Ils étaient tous hors d'eux-mêmes, et ne savaient que penser, se disant l'un à l'autre: Qu'est-ce que cela veut dire?
Wote walishangaa na kufadhaika huku wakiulizana, “Hii ina maana gani?”
13 Mais d'autres disaient en se moquant: C'est qu'ils sont pleins de vin doux!
Lakini wengine wakawadhihaki wakisema, “Watu hawa wamelewa divai mpya!”
14 Alors Pierre, se présentant avec les Onze, éleva la voix et leur dit: Hommes de la Judée, et vous tous qui êtes en séjour à Jérusalem, sachez bien ceci, et prêtez l'oreille à mes paroles.
Lakini Petro alisimama pamoja na wale kumi na mmoja akaanza kuwahutubia watu kwa sauti kubwa: “Ndugu Wayahudi nanyi nyote mnaokaa hapa Yerusalemu, sikilizeni kwa makini maneno yangu.
15 Ces gens ne sont pas ivres, comme vous le supposez; car il n'est encore que la troisième heure du jour.
Watu hawa hawakulewa kama mnavyodhani; mbona ni saa tatu tu asubuhi?
16 Mais ce qui arrive a été prédit par le prophète Joël:
Ukweli ni kwamba jambo hili ni lile alilosema nabii Yoeli:
17 «Il arrivera, pendant les derniers jours, — c'est Dieu lui-même qui parle — que je répandrai de mon Esprit sur toute créature; vos fils et vos filles prophétiseront, vos jeunes gens auront des visions, et vos vieillards auront des songes.
Katika siku zile za mwisho, asema Bwana, nitawamiminia binadamu wote Roho wangu. Watoto wenu, wanaume kwa wanawake, watautangaza ujumbe wangu; vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
18 Oui, en ces jours-là, je répandrai de mon Esprit sur mes serviteurs et sur mes servantes, et ils prophétiseront.
Naam, hata watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, nitawamiminia Roho wangu, siku zile, nao watautangaza ujumbe wangu.
19 Je ferai paraître des prodiges en haut dans le ciel, et des miracles en bas sur la terre: du sang, du feu, et des tourbillons de fumée.
Nitatenda miujiza juu angani, na ishara chini duniani; kutakuwa na damu, moto na moshi mzito;
20 Le soleil sera changé en ténèbres, et la lune en sang, avant que vienne le grand et glorieux jour du Seigneur;
jua litatiwa giza, na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya kutokea ile siku kuu na tukufu ya Bwana.
21 et il arrivera que quiconque invoquera le nom du Seigneur, sera sauvé.»
Hapo, yeyote atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa.
22 Enfants d'Israël, écoutez ces paroles: Jésus de Nazareth, cet homme à qui Dieu a rendu témoignage parmi vous par les actes de puissance, les prodiges et les miracles qu'il a opérés par son moyen au milieu de vous, comme vous le savez vous-mêmes,
“Wananchi wa Israeli, sikilizeni maneno haya! Yesu wa Nazareti alikuwa mtu ambaye mamlaka yake ya kimungu yalithibitishwa kwenu kwa miujiza, maajabu na ishara Mungu alizofanya kati yenu kwa njia yake, kama mnavyojua.
23 — cet homme, livré selon le dessein arrêté et la prescience de Dieu, vous l'avez fait mourir par la main des impies, en le clouant à la croix.
Kufuatana na mpango wake mwenyewe Mungu alikwisha amua kwamba Yesu angetiwa mikononi mwenu; nanyi mkamuua kwa kuwaachia watu wabaya wamsulubishe.
24 Mais Dieu l'a ressuscité, en le délivrant des douleurs de la mort, parce qu'il n'était pas possible qu'elle le retînt en sa puissance.
Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu akamwokoa katika maumivu ya kifo kwa maana haingewezekana kabisa kifo kimfunge.
25 En effet, David dit de lui: «Je voyais toujours le Seigneur devant moi; car il est à ma droite, afin que je ne sois point ébranlé.
Maana Daudi alisema juu yake hivi: Nilimwona Bwana mbele yangu daima; yuko nami upande wangu wa kulia, na hivyo sitatikisika.
26 C'est pour cela que mon coeur s'est réjoui, et que ma langue a fait entendre un chant d'allégresse. Ma chair elle-même, remplie d'espérance, trouvera le repos;
Kwa hiyo, moyo wangu ulifurahi; tena nilipiga vigelegele vya furaha. Mwili wangu utakaa katika tumaini;
27 car tu n'abandonneras pas mon âme dans le Séjour des morts, et tu ne. permettras pas que ton Saint voie la corruption. (Hadēs )
kwa kuwa hutaiacha roho yangu katika kuzimu, wala kumruhusu mtakatifu wako aoze. (Hadēs )
28 Tu m'as fait connaître les sentiers de la vie; tu me rempliras de joie par ta présence.»
Umenionyesha njia za kuufikia uzima, kuwako kwako kwanijaza furaha!
29 Mes frères, permettez-moi de vous dire en toute liberté, au sujet du patriarche David, qu'il est mort, qu'il a été enseveli, et que son tombeau est encore aujourd'hui au milieu de nous.
“Ndugu zangu, napenda kuwaambieni waziwazi juu ya mambo yaliyompata Daudi, babu yetu. Yeye alikufa, akazikwa, tena kaburi lake liko papa hapa petu mpaka leo.
30 Mais, étant prophète et sachant que Dieu lui avait promis avec serment de faire asseoir un de ses descendants sur son trône,
Lakini kwa vile Daudi alikuwa nabii, alijua kuwa Mungu alimwapia kiapo kwamba atamtawaza mmoja wa uzawa wake kuwa mfalme mahali pake.
31 c'est la résurrection du Christ qu'il a prévue et dont il a parlé en disant: «Il n'a pas été laissé dans le Séjour des morts, et sa chair n'a pas vu la corruption.» (Hadēs )
Daudi aliona kabla mambo yatakayofanywa na Mungu na hivyo akasema juu ya ufufuo wa Kristo wakati aliposema: Hakuachwa kuzimu, mwili wake haukuoza. (Hadēs )
32 Ce Jésus, en effet, Dieu l'a ressuscité, et nous en sommes tous témoins.
Basi, Mungu alimfufua huyo Yesu na sisi sote ni mashahidi wa tukio hilo.
33 Après donc qu'il a été élevé à la droite de Dieu, et qu'il a reçu du Père le Saint-Esprit qui avait été promis, il l'a répandu, comme vous le voyez et l'entendez.
Yesu aliinuliwa juu mpaka upande wa kulia wa Mungu, akapokea kutoka kwa Baba ile zawadi aliyoahidi yaani Roho Mtakatifu; na mnachoona sasa na kusikia ni mmiminiko wa huyo Roho.
34 Car David n'est pas monté au ciel; mais il dit lui-même: «Le Seigneur a dit à mon Seigneur: Assieds-toi à ma droite,
Maana Daudi mwenyewe, hakupanda mpaka mbinguni; ila yeye alisema: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia,
35 jusqu'à ce que j'aie mis tes ennemis sous tes pieds, pour te servir de marche-pied».
hadi nitakapowafanya adui zako kibao cha kukanyagia miguu yako.
36 Que toute la maison d'Israël tienne donc pour certain que Dieu a fait Seigneur et Christ ce Jésus que vous avez crucifié.
“Watu wote wa Israeli wanapaswa kufahamu kwa hakika kwamba huyo Yesu mliyemsulubisha ninyi, ndiye huyo ambaye Mungu amemfanya kuwa Bwana na Kristo.”
37 En entendant ces paroles, ils furent touchés jusqu'au fond du coeur, et ils dirent à Pierre et aux autres apôtres: Frères, que ferons-nous?
Basi, watu waliposikia hayo, walichomwa moyo, wakawauliza Petro na wale mitume wenzake: “Ndugu zetu, tufanye nini?”
38 Pierre leur répondit: Convertissez-vous, et que chacun de vous soit baptisé au nom de Jésus-Christ pour obtenir la rémission de ses péchés; et vous recevrez le don du Saint-Esprit.
Petro akajibu, “Tubuni na kila mmoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo ili mpate kuondolewa dhambi zenu na kupokea ile zawadi ya Roho Mtakatifu.
39 Car la promesse est pour vous, pour vos enfants, et pour tous ceux qui sont au loin, en aussi grand nombre que le Seigneur, notre Dieu, en appellera.
Maana, ahadi ile ilikuwa kwa ajili yenu, kwa ajili ya watoto wenu, kwa ajili ya wote wanaokaa mbali; na kwa ajili ya kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita kwake.”
40 Puis, par beaucoup d'autres paroles, il leur adressait les exhortations les plus pressantes, en disant: Sauvez-vous du milieu de cette race perverse!
Kwa maneno mengine mengi, Petro alisisitiza na kuwahimiza watu akisema, “Jiokoeni katika kizazi hiki kiovu.”
41 Ceux qui accueillirent la prédication de Pierre furent donc baptisés; et il y eut, ce jour-là, environ trois mille personnes ajoutées à l'Eglise.
Wengi waliyakubali maneno yake, wakabatizwa. Watu wapatao elfu tatu wakaongezeka katika kile kikundi siku hiyo.
42 Or, ils persévéraient dans la doctrine des apôtres et dans la communion fraternelle; ils rompaient le pain et priaient ensemble.
Hawa wote waliendelea kujifunza kutoka kwa mitume, kuishi pamoja kidugu, kumega mkate na kusali.
43 La crainte était dans tous les coeurs, et beaucoup de prodiges et de miracles étaient opérés par les apôtres.
Miujiza na maajabu mengi yalifanyika kwa njia ya mitume hata kila mtu akajawa na hofu.
44 Tous ceux qui croyaient étaient ensemble et avaient toutes choses en commun;
Waumini wote waliendelea kuwa kitu kimoja na mali zao waligawana pamoja.
45 ils vendaient leurs propriétés et leurs biens, et ils en partageaient le prix entre tous, selon les besoins de chacun.
Walikuwa wakiuza mali na vitu vyao kisha wakagawana fedha kadiri ya mahitaji ya kila mmoja.
46 Chaque jour, tous ensemble, ils allaient assidûment au temple; dans leurs maisons, ils rompaient le pain et prenaient leurs repas avec joie et simplicité de coeur,
Waliendelea kukutana pamoja kila siku Hekaluni. Lakini wakati wa kumega mkate, walikutana katika nyumba zao na wakakishiriki chakula hicho kwa furaha na moyo mkunjufu.
47 louant Dieu et se rendant agréables à tout le peuple. Et le Seigneur ajoutait tous les jours à l'Église ceux qui étaient sauvés.
Walimtukuza Mungu, wakapendwa na watu wote. Kila siku Bwana aliwaongezea idadi ya watu waliokuwa wakiokolewa.