< Actes 13 >

1 Il y avait dans l'Église d'Antioche des prophètes et des docteurs: Barnabas, Siméon, appelé Niger, Lucius le Cyrénéen, Manahem, qui avait été élevé avec Hérode le tétrarque, et Saul.
Katika kanisa huko Antiokia ya Shamu walikuwako manabii na walimu, yaani: Barnaba, Simeoni aitwaye Nigeri, Lukio Mkirene, Manaeni aliyekuwa amelelewa pamoja na Mfalme Herode Agripa, na Sauli.
2 Pendant qu'ils célébraient le culte du Seigneur et qu'ils jeûnaient, le Saint-Esprit leur dit: Mettez à part Barnabas et Saul, pour l'oeuvre à laquelle je les ai appelés.
Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, “Nitengeeni Sauli na Barnaba kwa kazi ile maalum niliyowaitia.”
3 Alors, après avoir jeûné et prié. ils leur imposèrent les mains et les laissèrent partir.
Ndipo baada ya kufunga na kuomba, wakawawekea mikono yao na wakawatuma waende zao.
4 Eux donc, étant envoyés par le Saint-Esprit, descendirent à Séleucie, et, de là, ils firent voile vers l'île de Chypre.
Hivyo, wakiwa wametumwa na Roho Mtakatifu, wakashuka kwenda Seleukia na kutoka huko wakasafiri baharini mpaka kisiwa cha Kipro.
5 Arrivés à Salamine, ils annoncèrent la parole de Dieu dans les synagogues des Juifs; ils avaient Jean avec eux pour les aider.
Walipowasili katika mji wa Salami, wakahubiri neno la Mungu katika sinagogi la Wayahudi. Pia walikuwa na Yohana Marko kuwa msaidizi wao.
6 Ayant traversé toute l'île jusqu'à Paphos, ils trouvèrent un certain Juif, magicien et faux prophète, nommé Bar-Jésus,
Walipokwisha kupita katika nchi zote hizo wakafika Pafo, ambapo walikutana na Myahudi mmoja mchawi aliyekuwa nabii wa uongo, jina lake Bar-Yesu.
7 qui vivait auprès du proconsul Sergius Paulus, homme d'une intelligence éprouvée. Celui-ci, ayant fait appeler Barnabas et Saul, demanda à entendre la parole de Dieu.
Mtu huyu alikuwa pamoja na Sergio Paulo, mtu mwenye hekima aliyekuwa msaidizi wa mwakilishi wa mtawala wa kile kisiwa. Sergio Paulo akawaita Sauli na Barnaba akitaka kusikia neno la Mungu.
8 Mais Élymas, le magicien — c'est ce que signifie son nom — leur résistait, tâchant de détourner le proconsul de la foi.
Lakini Elima yule mchawi (hii ndiyo maana ya jina lake), aliwapinga Barnaba na Sauli na kujaribu kumpotosha yule mkuu wa kile kisiwa aiache imani.
9 Alors Saul, appelé aussi Paul, plein du Saint-Esprit, le regarda en face et lui dit:
Ndipo Sauli, ambaye pia aliitwa Paulo, akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akamkazia macho Elima huyo mchawi,
10 Homme tout rempli d'artifice et de méchanceté, enfant du Diable, ennemi de toute justice, ne cesseras-tu pas de rendre tortueuses les voies droites du Seigneur?
akamwambia, “Ewe mwana wa ibilisi, wewe ni adui wa kila kilicho haki! Umejaa kila aina ya udanganyifu na ulaghai. Je, hutaacha kuzipotosha njia za Bwana zilizonyooka?
11 Déjà la main du Seigneur est sur toi; tu seras aveugle, tu ne verras pas le soleil pendant un certain temps. A l'instant même, l'obscurité et les ténèbres tombèrent sur Élymas; et, tournant de tous côtés, il cherchait quelqu'un pour le conduire.
Nawe sasa sikiliza, mkono wa Bwana u dhidi yako. Utakuwa kipofu, wala hutaona jua kwa muda.” Mara ukungu na giza vikamfunika, naye akaenda huku na huko akitafuta mtu wa kumshika mkono ili amwonyeshe njia.
12 Alors le proconsul, voyant ce qui était arrivé, devint croyant; car la doctrine du Seigneur l'avait rempli d'admiration.
Yule mkuu wa kile kisiwa alipoona yaliyotukia, akaamini kwa sababu alistaajabishwa na mafundisho kuhusu Bwana.
13 S'étant embarqués à Paphos, Paul et ses compagnons arrivèrent à Perge, en Pamphylie. Mais Jean se sépara d'eux, et retourna à Jérusalem.
Kisha Paulo na wenzake wakasafiri toka Pafo wakafika Perga huko Pamfilia. Lakini, Yohana Marko akawaacha huko, akarejea Yerusalemu.
14 Pour eux, ayant quitté Perge, ils poursuivirent leur route et parvinrent à Antioche de Pisidie; et, étant entrés dans la synagogue le jour du sabbat, ils y prirent place.
Kutoka Perga wakaendelea hadi Antiokia ya Pisidia. Siku ya Sabato wakaingia ndani ya sinagogi, wakaketi.
15 Après la lecture de la loi et des prophètes, les chefs de la synagogue leur envoyèrent dire: Frères, si vous avez quelques paroles d'exhortation à adresser au peuple, parlez!
Baada ya Sheria ya Mose na Kitabu cha Manabii kusomwa, viongozi wa sinagogi wakawatumia ujumbe wakisema, “Ndugu, kama mna neno la kuwafariji watu hawa, tafadhali lisemeni.”
16 Alors Paul se leva, et, ayant fait signe de la main, il dit: Enfants d'Israël et vous qui craignez Dieu, écoutez:
Paulo akasimama, akawapungia mkono na kusema: “Enyi wanaume wa Israeli na ninyi nyote mnaomcha Mungu.
17 Le Dieu de ce peuple d'Israël choisit nos pères; il éleva bien haut ce peuple, pendant son séjour à l'étranger, dans le pays d'Egypte, et il l'en fit sortir par la puissance de son bras.
Mungu wa watu hawa wa Israeli aliwachagua baba zetu, akawafanya kustawi walipokuwa huko Misri, kwa uwezo mwingi akawaongoza na kuwatoa katika nchi ile.
18 Il supporta leur conduite dans le désert, pendant environ quarante ans.
Kwa muda wa miaka arobaini alivumilia matendo yao walipokuwa jangwani.
19 Puis, ayant détruit sept nations dans le pays de Canaan, il mit les Israélites en possession de leur territoire,
Naye baada ya kuyaangamiza mataifa saba waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, akawapa Waisraeli nchi yao iwe urithi wao.
20 pendant environ quatre cent cinquante ans; c'est alors qu'il leur donna des juges jusqu'au prophète Samuel.
Haya yote yalichukua kama muda wa miaka 450. “Baada ya haya, Mungu akawapa waamuzi mpaka wakati wa nabii Samweli.
21 Ensuite les Israélites demandèrent un roi. Dieu leur donna pour quarante ans Saül, fils de Kis, de la tribu de Benjamin;
Ndipo watu wakaomba wapewe mfalme, naye Mungu akawapa Sauli mwana wa Kishi wa kabila la Benyamini, aliyetawala kwa miaka arobaini.
22 puis, l'ayant rejeté. Dieu leur suscita pour roi David, auquel il rendit ce témoignage: «J'ai trouvé David, fils de Jessé, un homme selon mon coeur, qui exécutera toutes mes volontés.»
Baada ya kumwondoa Sauli katika ufalme, akawainulia Daudi kuwa mfalme wao. Mungu pia alimshuhudia, akisema, ‘Nimemwona Daudi mwana wa Yese, mtu anayeupendeza moyo wangu, atakayetimiza mapenzi yangu yote.’
23 C'est de sa postérité que Dieu, selon sa promesse, a suscité pour Israël un Sauveur, qui est Jésus.
“Kutoka uzao wa mtu huyu, Mungu amewaletea Israeli Mwokozi Yesu, kama alivyoahidi.
24 Avant sa venue, Jean avait prêché le baptême de la repentance à tout le peuple d'Israël.
Kabla ya kuja kwa Yesu, Yohana alihubiri toba na ubatizo kwa watu wote wa Israeli.
25 Et pendant que Jean poursuivait sa course, il disait: Je ne suis pas ce que vous pensez; mais il vient après moi, celui dont je ne suis pas digne de délier la chaussure.
Yohana alipokuwa anakamilisha kazi yake, alisema: ‘Ninyi mnadhani mimi ni nani? Mimi si yeye. La hasha, lakini yeye yuaja baada yangu, ambaye mimi sistahili kufungua kamba za viatu vya miguu yake.’
26 Mes frères, enfants de la race d'Abraham, et vous qui craignez Dieu, c'est à nous que ce message de salut est adressé.
“Ndugu zangu, wana wa Abrahamu, nanyi watu wa Mataifa mnaomcha Mungu, ujumbe huu wa wokovu umeletwa kwetu.
27 Car les habitants de Jérusalem et leurs chefs, ayant méconnu ce Jésus, ont accompli, en le condamnant, les paroles des prophètes qu'on lit chaque sabbat.
Kwa sababu wakaao Yerusalemu na viongozi wao hawakumtambua wala kuelewa maneno ya manabii yasomwayo kila Sabato, bali waliyatimiza maneno hayo kwa kumhukumu yeye.
28 Bien qu'ils n'eussent rien trouvé en lui qui fût digne de mort, ils demandèrent à Pilate de le faire mourir.
Ijapokuwa hawakupata sababu yoyote ya kumhukumu kifo, walimwomba Pilato aamuru auawe.
29 Après qu'ils eurent accompli tout ce qui avait été écrit à son sujet, ils le descendirent de la croix et le mirent dans un tombeau.
Walipokwisha kufanya yale yote yaliyoandikwa kumhusu, walimshusha kutoka msalabani na kumzika kaburini.
30 Mais Dieu l'a ressuscité des morts.
Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu.
31 Il a été vu, pendant plusieurs jours, par ceux qui étaient montés avec lui de la Galilée à Jérusalem, et qui sont maintenant ses témoins auprès du peuple.
Naye kwa siku nyingi akawatokea wale waliokuwa pamoja naye kuanzia Galilaya hadi Yerusalemu. Nao sasa wamekuwa mashahidi wake kwa watu wetu.
32 Quant à nous, nous vous annonçons une bonne nouvelle: La promesse faite à nos pères.
“Nasi tunawaletea habari njema, kwamba yale Mungu aliyowaahidi baba zetu
33 Dieu l'a accomplie pour nous, leurs enfants, en ressuscitant Jésus, ainsi qu'il est écrit dans le psaume second: «Tu es mon fils; je t'ai engendré aujourd'hui.»
sasa ameyatimiza kwetu sisi watoto wao, kwa kumfufua Yesu, kama ilivyoandikwa katika Zaburi ya pili: “‘Wewe ni Mwanangu; leo mimi nimekuzaa.’
34 Qu'il l'ait ressuscité des morts, de sorte qu'il ne saurait désormais tomber en corruption, c'est ce qu'il a déclaré en disant: «Je vous tiendrai fidèlement les promesses sacrées, faites à David.
Kwa kuwa Mungu alimfufua kutoka kwa wafu asioze kamwe, alitamka maneno haya: “‘Nitakupa wewe baraka takatifu zilizo za hakika nilizomwahidi Daudi.’
35 Aussi dit-il encore dans un autre endroit: «Tu ne permettras pas que ton Saint voie la corruption.»
Kama ilivyosemwa mahali pengine katika Zaburi, “‘Hutamwacha Aliye Mtakatifu wako kuona uharibifu.’
36 En effet, David, après avoir servi en son temps aux desseins de Dieu, est mort; il a été recueilli avec ses pères, et il a vu la corruption.
“Kwa maana Daudi akiisha kulitumikia kusudi la Mungu katika kizazi chake, alilala; akazikwa pamoja na baba zake na mwili wake ukaoza.
37 Mais celui que Dieu a ressuscité, n'a pas vu la corruption.
Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu hakuona uharibifu.
38 Sachez-le donc, frères, c'est par lui que la rémission des péchés vous est annoncée;
“Kwa hiyo ndugu zangu, nataka ninyi mjue kwamba kwa kupitia huyu Yesu msamaha wa dhambi unatangazwa kwenu.
39 et c'est par lui que tout croyant est justifié de tout ce dont vous ne pouviez être justifiés par la loi de Moïse.
Kwa kupitia yeye, kila mtu amwaminiye anahesabiwa haki kwa kila kitu ambacho asingeweza kuhesabiwa haki kwa sheria ya Mose.
40 Prenez donc garde qu'il ne vous arrive ce qui est dit dans les prophètes:
Kwa hiyo jihadharini ili yale waliyosema manabii yasiwapate:
41 «Voyez, hommes dédaigneux, soyez étonnés, et disparaissez; car je vais faire une oeuvre en vos jours, une oeuvre que vous ne croiriez point, si on vous la racontait.»
“‘Angalieni, enyi wenye dhihaka, mkastaajabu, mkaangamie, kwa maana nitatenda jambo wakati wenu ambalo hamtasadiki, hata kama mtu akiwaambia.’”
42 Lorsqu'ils sortirent, on les pria de parler, le sabbat suivant, sur les mêmes sujets.
Paulo na Barnaba walipokuwa wakitoka nje ya sinagogi, watu wakawaomba wazungumze tena mambo hayo Sabato iliyofuata.
43 Et après que l'assemblée se fut séparée, plusieurs Juifs et prosélytes pieux suivirent Paul et Barnabas, qui s'entretinrent avec eux et les exhortèrent à demeurer attachés à la grâce de Dieu.
Baada ya kusanyiko la Sinagogi kutawanyika, wengi wa Wayahudi na waongofu wa dini ya Kiyahudi wakawafuata Paulo na Barnaba, wakazungumza nao na kuwahimiza wadumu katika neema ya Mungu.
44 Le sabbat suivant, presque toute la ville se rassembla pour entendre la parole du Seigneur.
Sabato iliyofuata, karibu watu wote wa mji walikuja kusikiliza neno la Bwana.
45 Mais les Juifs, voyant cette foule, furent remplis de jalousie; ils s'opposèrent à ce que Paul disait, en l'injuriant.
Lakini Wayahudi walipoona ule umati mkubwa wa watu walijawa na wivu, wakayakanusha maneno Paulo aliyokuwa akisema.
46 Alors Paul et Barnabas leur dirent hardiment: C'était à vous, les premiers, qu'il fallait annoncer la parole de Dieu; mais puisque vous la rejetez et que vous vous jugez vous-mêmes indignes de la vie éternelle, nous nous tournons vers les Païens. (aiōnios g166)
Ndipo Paulo na Barnaba wakawajibu kwa ujasiri, wakisema, “Ilitupasa kunena nanyi neno la Mungu kwanza. Lakini kwa kuwa mmelikataa, mkajihukumu wenyewe kuwa hamstahili uzima wa milele, sasa tunawageukia watu wa Mataifa. (aiōnios g166)
47 Car le Seigneur nous l'a ainsi commandé: «Je t'ai établi pour être la lumière des nations, afin que tu portes le salut jusqu'aux extrémités de la terre.»
Kwa maana hili ndilo Bwana alilotuamuru: “‘Nimewafanya ninyi kuwa nuru kwa watu wa Mataifa, ili mpate kuuleta wokovu hadi miisho ya dunia.’”
48 Les Païens, en les entendant parler, étaient remplis de joie et donnaient gloire à la parole du Seigneur, et tous ceux qui étaient destinés à la vie éternelle, crurent. (aiōnios g166)
Watu wa Mataifa waliposikia haya wakafurahi na kulitukuza neno la Bwana; nao wote waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. (aiōnios g166)
49 La parole du Seigneur se répandait dans tout le pays.
Neno la Bwana likaenea katika eneo lile lote.
50 Mais les Juifs excitèrent les femmes dévotes de haut rang et les principaux habitants de la ville; ils provoquèrent une persécution contre Paul et Barnabas, et ils les chassèrent de leur territoire.
Lakini Wayahudi wakawachochea wanawake wenye kumcha Mungu, wenye vyeo pamoja na watu maarufu katika mji, wakachochea mateso dhidi ya Paulo na Barnaba na kuwafukuza kutoka eneo hilo.
51 Ceux-ci, ayant secoué contre eux la poussière de leurs pieds, allèrent à Iconium.
Hivyo Paulo na Barnaba wakakungʼuta mavumbi ya miguu yao ili kuwapinga, nao wakaenda Ikonio.
52 Quant aux disciples, ils étaient remplis de joie et du Saint-Esprit.
Wanafunzi wakajawa na furaha na Roho Mtakatifu.

< Actes 13 >