< Romains 12 >

1 Je vous exhorte donc, frères, au nom du Dieu des compassions, à lui offrir vos personnes en sacrifice vivant, saint, acceptable; ce serait de votre part un culte raisonnable.
Kwa hiyo, ndugu zangu, maadam Mungu ni mwenye huruma nyingi, nawasihi kwa moyo wote: jitoleeni nafsi zenu kwa Mungu kama tambiko iliyo hai, takatifu na yenye kupendeza. Hii ndiyo njia yenu halisi ya kumwabudu.
2 Ne suivez pas les errements de notre siècle; au contraire, que votre esprit se transforme en se renouvelant, de manière à bien vous pénétrer de ce qu'est la volonté de Dieu: volonté qui est bonne, acceptable, parfaite. (aiōn g165)
Msiige mitindo ya ulimwengu huu, bali Mungu afanye mabadiliko ndani yenu kwa kuzigeuza fikira zenu. Hapo ndipo mtakapoweza kuyajua mapenzi ya Mungu, kutambua jambo lililo jema, linalompendeza na kamilifu. (aiōn g165)
3 Ainsi je vous dis à tous, m'autorisant de la grâce qui m'a été accordée, de ne pas vous exagérer votre valeur, mais de rester dans les limites d'une juste appréciation, chacun selon la mesure de foi que Dieu lui a départie;
Kutokana na neema aliyonijalia Mungu, nawaambieni ninyi nyote: msijione kuwa ni kitu zaidi kuliko mnavyopaswa kuwa. Fikira zenu na ziwe na kiasi kufuatana na kipimo cha imani Mungu aliyomgawia kila mmoja.
4 car de même que notre corps, qui est un, a plusieurs membres et que tous les membres n'ont pas la même fonction,
Mwili una viungo vingi, kila kimoja na kazi yake.
5 de même, tous, tant que nous sommes, nous ne faisons qu'un seul corps en Christ, et nous sommes tous membres les uns des autres,
Hali kadhalika ingawa sisi ni wengi, tu mwili mmoja kwa kuungana na Kristo, na kila mmoja ni kiungo cha mwenzake.
6 possédant des dons divers chacun selon la grâce qui lui a été accordée; l'un a le don de prophétie, en proportion de sa foi;
Basi, tunavyo vipaji mbalimbali kufuatana na neema tuliyopewa. Mwenye kipaji cha unabii na akitumie kadiri ya imani yake.
7 l'autre a, dans son ministère, le don du diaconat; ici c'est un docteur qui a le don de l'enseignement;
Mwenye kipaji cha utumishi na atumikie. mwenye kipaji cha kufundisha na afundishe.
8 là un prédicateur qui a le don de la parole; le bienfaiteur doit donner avec générosité; le supérieur, présider avec zèle; celui qui est chargé des oeuvres de miséricorde, remplir ses fonctions avec joie.
Mwenye kipaji cha kuwafariji wengine na afanye hivyo. Mwenye kumgawia mwenzake alicho nacho na afanye hivyo kwa ukarimu. Msimamizi na asimamie kwa bidii; naye mwenye kutenda jambo la huruma na afanye hivyo kwa furaha.
9 Que votre amour soit sans hypocrisie. Ayez horreur du mal; soyez fermement attachés au bien.
Mapendo yenu na yawe bila unafiki wowote. Chukieni jambo lolote ovu, zingatieni jema.
10 Comme des frères, soyez pleins d'affection les uns pour les autres; estimez-vous; ayez des prévenances réciproques.
Pendaneni kidugu; kila mmoja amfikirie mwenzake kwanza kwa heshima.
11 Ne ralentissez pas votre zèle, ayez de l'ardeur d'âme, mettez-vous au service du Seigneur.
Msilegee katika bidii, muwe wachangamfu rohoni katika kumtumikia Bwana.
12 Soyez joyeux dans l'espérance, patients dans l'affliction, persévérants dans la prière.
Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida na kusali daima.
13 Subvenez aux besoins des fidèles. Exercez l'hospitalité avec empressement.
Wasaidieni watu wa Mungu katika mahitaji yao; wapokeeni wageni kwa ukarimu.
14 Bénissez vos persécuteurs, oui, bénissez, ne maudissez pas.
Watakieni baraka wote wanaowadhulumu ninyi; naam, watakieni baraka na wala msiwalaani.
15 Soyez heureux avec les heureux, pleurez avec ceux qui pleurent.
Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
16 Vivez ensemble en bonne intelligence. Gardez-vous de l'orgueil; marchez avec ceux qui sont humbles.
Muwe na wema uleule kwa kila mtu. Msijitakie makuu, bali jishugulisheni na watu wadogo. Msijione kuwa wenye hekima sana.
17 «Ne vous croyez pas meilleurs que vous ne l'êtes.» Ne rendez à personne le mal pour le mal. «Intéressez-vous à ce qui est bien aux yeux de tous les hommes.»
Msilipe ovu kwa ovu. Zingatieni mambo mema mbele ya wote.
18 Autant que possible et, dans la mesure où cela dépend de vous, vivez en paix avec tout le monde.
Kadiri inavyowezekana kwa upande wenu, muwe na amani na watu wote.
19 Ne vous vengez pas vous-mêmes, mes bien aimés; laissez faire la colère dont il est écrit: «La vengeance est à moi, c'est moi qui rétribuerai, dit le Seigneur.»
Wapenzi wangu, msilipize kisasi, bali mwachieni Mungu jambo hilo; maana Maandiko Matakatifu yasema: “Kulipiza kisasi ni shauri langu; mimi nitalipiza asema Bwana.”
20 Ainsi donc: «Si ton ennemi a faim donne-lui à manger, S'il a soif donne-lui à boire; En faisant cela tu entasseras sur sa tête des charbons ardents.»
Tena, Maandiko yasema: “Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe kinywaji. Maana kwa kufanya hivyo utamfanya apate aibu kali kama makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
21 Ne te laisse pas vaincre par le mal, mais sache vaincre le mal par le bien.
Usikubali kushindwa na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.

< Romains 12 >