< Apocalypse 15 >
1 Et je vis un autre prodige dans le ciel, un grand, un merveilleux prodige: sept anges ayant en main les sept dernières plaies par lesquelles doit se consommer la colère de Dieu.
Kisha nikaona ishara nyingine mbinguni, kubwa na ya kushangaza. Palikuwa hapo malaika saba wenye mabaa makubwa saba ya mwisho. Kwa mabaa hayo makubwa saba, ghadhabu ya Mungu imekamilishwa.
2 Et je vis comme une mer cristalline, mêlée de feu, et ceux qui avaient été vainqueurs de la bête, et de son image, et du chiffre de son nom, placés sur cette mer cristalline, tenaient les harpes de Dieu.
Kisha nikaona kitu kama bahari ya kioo, imechanganywa na moto. Nikawaona pia wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake na ambaye jina lake lilitajwa kwa ile tarakimu. Watu hao walikuwa wamesimama kando ya hiyo bahari ya kioo, wakiwa na vinubi walivyopewa na Mungu.
3 Et ils chantaient le cantique de Moïse, le serviteurs de Dieu, et le cantique de l'agneau en disant: «Grandes et merveilleuses sont tes oeuvres, Seigneur Dieu Tout-Puissant Justes et vraies sont tes voies »,
Walikuwa wakiimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwanakondoo: “Bwana Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makuu mno! Ewe Mfalme wa mataifa, njia zako ni za haki na za kweli!
4 roi des nations, Qui ne craindrait, ô Seigneur, qui ne glorifierait ton nom? Car toi seul es saint Et toutes les nations viendront se prosterner devant toi, » car tes jugements se sont manifestés.
Bwana, ni nani asiyekucha wewe? Nani asiyelitukuza jina lako? Wewe peke yako ni Mtakatifu. Mataifa yote yatakujia na kukuabudu maana matendo yako ya haki yameonekana na wote.”
5 Et après cela je regardai, et le Temple du tabernacle céleste du témoignage s'ouvrit,
Baada ya hayo nikaona Hekalu limefunguliwa mbinguni, na ndani yake hema ionyeshayo kuwapo kwa Mungu.
6 et les sept anges ayant en main les sept plaies en sortirent vêtus de lin pur et éclatant et ceints sur la poitrine de ceintures d'or.
Basi, wale malaika saba wenye mabaa saba wakatoka humo Hekaluni, wakiwa wamevaa nguo za kitani safi zenye kung'aa, na kanda za dhahabu vifuani mwao.
7 Et l'un des quatre animaux donna aux sept anges sept coupes d'or pleines de la colère du Dieu qui vit aux siècles des siècles; (aiōn )
Kisha, mmojawapo wa vile viumbe vinne akawapa hao malaika saba mabakuli ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, aishiye milele na milele. (aiōn )
8 et le Temple se remplit de la fumée de la majesté et de la puissance divine, et personne ne pouvait entrer dans le sanctuaire tant que les sept plaies des sept anges ne s'étaient pas accomplies.
Hekalu likajaa moshi uliosababishwa na utukufu na nguvu ya Mungu, na hakuna mtu aliyeweza kuingia Hekaluni mpaka mwisho wa mabaa makubwa saba ya wale malaika saba.