< Matthieu 27 >

1 Le jour s'étant levé, tous les chefs des prêtres et les Anciens du peuple tinrent conseil sur les moyens de mettre Jésus à mort.
Kulipopambazuka, makuhani wakuu wote na wazee wa watu walifanya mashauri juu ya Yesu wapate kumwua.
2 Et l'ayant chargé de liens, ils l’emmenèrent et le livrèrent à Pilate, le procurateur.
Wakamfunga pingu, wakamchukua, wakamkabidhi kwa Pilato, mkuu wa mkoa.
3 En voyant qu'il était condamné, celui qui l'avait livré, Judas, poussé par le remords, rapporta aux chefs des prêtres et aux Anciens les trente sicles d'argent,
Hapo, Yuda ambaye ndiye aliyemsaliti, alipoona kwamba wamekwisha mhukumu Yesu, akajuta, akawarudishia makuhani wakuu zile sarafu thelathini za fedha.
4 disant: «J'ai péché en livrant un sang innocent. » Ils répondirent: «Que nous importe? c'est ton affaire.»
Akawaambia, “Nimekosa kwa kumtoa mtu asiye na hatia auawe.” Lakini wao wakasema, “Yatuhusu nini sisi? Hilo ni shauri lako.”
5 Jetant alors les pièces d'argent dans le sanctuaire, Judas partit et il alla se pendre.
Naye akazitupa zile fedha Hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.
6 Mais les chefs des prêtres ramassèrent la somme, disant: «Il n'est pas permis de la verser dans le Korban, puisque c'est le prix du sang.»
Makuhani wakuu wakazichukua zile fedha, wakasema, “Haifai kuziweka katika hazina ya Hekalu kwa maana ni fedha za damu.”
7 Et après en avoir conféré ensemble, ils en achetèrent le «Champ-du-Potier» pour la sépulture des étrangers.
Basi, wakashauriana, wakazitumia kununua shamba la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
8 De là le nom de «Champ-du-Sang» qu'on lui donne encore aujourd'hui.
Ndiyo maana mpaka leo shamba hilo linaitwa Shamba la Damu.
9 (C'est ainsi que fut accomplie la parole du prophète Jérémie: «Et ils ont reçu les trente pièces d'argent, prix de celui qui avait été évalué, évalué par les enfants d'Israël,
Hivyo maneno ya nabii Yeremia yakatimia: “Walizichukua sarafu thelathini za fedha, thamani ya yule ambaye watu wa Israeli walipanga bei,
10 et ils les ont données pour le champ du potier, ainsi que me l'avait ordonné le Seigneur. »)
wakanunua nazo shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza.”
11 Jésus comparut devant le procurateur, et celui-ci l'interrogea: «C'est toi qui es le Roi des Juifs?» demanda-t-il. Jésus lui répondit: «Tu le dis.»
Yesu alisimamishwa mbele ya mkuu wa mkoa. Basi, mkuu wa mkoa akamwuliza, “Je, wewe ndiwe Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akamwambia, “Wewe umesema.”
12 Mais lorsque les chefs des prêtres et les Anciens l'acculèrent, il ne répondit rien.
Lakini makuhani wakuu na wazee walipokuwa wanamshtaki, hakujibu neno.
13 Alors Pilate lui dit: «Est-ce que tu n'entends pas tout ce dont ils t'accusent?»
Hivyo Pilato akamwuliza, “Je, husikii mashtaka hayo yote wanayotoa juu yako?”
14 Jésus ne lui répondit sur aucun point, ce dont le procurateur fut extrêmement surpris.
Lakini Yesu hakumjibu hata neno moja; hata huyo mkuu wa mkoa akashangaa sana.
15 Or à chaque fête il avait coutume de remettre en liberté un prisonnier, celui que le peuple choisissait.
Ilikuwa kawaida wakati wa Sikukuu ya Pasaka mkuu wa mkoa kuwafungulia Wayahudi mfungwa mmoja waliyemtaka.
16 Il y en avait un fameux détenu à ce moment, du nom de Bar-Abbas.
Wakati huo kulikuwa na mfungwa mmoja, jina lake Baraba.
17 Alors Pilate, qui savait que c'était par une haine jalouse que les chefs des prêtres et les Anciens lui avaient livré Jésus,
Hivyo, watu walipokusanyika pamoja, Pilato akawauliza, “Mwataka nimfungue yupi kati ya wawili hawa, Baraba ama Yesu aitwae Kristo?”
18 leur dit, pendant qu'ils étaient rassemblés: «Lequel voulez-vous que je vous délivre? Bar-Abbas ou Jésus, celui qu'on appelle Christ?»
Alisema hivyo maana alijua wazi kwamba walimleta kwake kwa sababu ya wivu.
19 (Tandis qu'il siégeait ainsi à son tribunal, sa femme lui envoya dire ceci: «Qu'il n'y ait rien entre toi et ce juste; car j'ai eu aujourd'hui, dans mon sommeil, un affreux cauchemar à son sujet.»)
Pilato alipokuwa amekaa katika kiti cha hukumu, mke wake akampelekea ujumbe: “Usijitie katika shauri la mtu huyu mwema, maana leo nimeteseka sana katika ndoto kwa sababu yake.”
20 Les chefs des prêtres et les Anciens persuadèrent à la foule de demander Bar-Abbas et de perdre Jésus.
Lakini makuhani wakuu na wazee wakawashawishi watu waombe Baraba afunguliwe na Yesu auawe.
21 Le procurateur reprit sa question: «Lequel des deux voulez-vous que je vous délivre?» — Bar-Abbas! répondirent-ils.
Mkuu wa mkoa akawauliza, “Ni yupi kati ya hawa wawili mnayetaka nimfungue?” Wakamjibu, “Baraba!”
22 Pilate leur dit: «Et Jésus, celui qu'on appelle Christ, qu'en ferai-je donc?» Ils répondirent tous: «Qu'il soit crucifié!» —
Pilato akawauliza, “Sasa, nifanye nini na Yesu aitwaye Kristo?” Wote wakasema, “Asulubiwe!”
23 «Mais qu'a-t-il fait de mal?» dit encore Pilate. Et ils n'en criaient que plus fort: «Qu'il soit crucifié!»
Pilato akauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Wao wakazidi kupaaza sauti: “Asulubiwe!”
24 Voyant qu'il n'obtenait rien et que, au contraire, le tumulte augmentait, Pilate demanda de l'eau, se lava les mains devant la foule et dit: «Je ne suis pas responsable du sang de cet homme, à vous d'en répondre!»
Basi, Pilato alipotambua kwamba hafanikiwi chochote na kwamba maasi yalikuwa yanaanza, alichukua maji, akanawa mikono mbele ya ule umati wa watu, akasema, “Mimi sina lawama juu ya kifo cha mtu huyu; shauri lenu wenyewe.”
25 Et tout le peuple répliqua par ces mots: «Le sang de cet homme! qu'il retombe sur nous et sur nos enfants!»
Watu wote wakasema, “Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!”
26 Pilate leur délivra alors Bar-Abbas. Quant à Jésus, l’ayant fait flageller, il l'abandonna au supplice de la croix.
Hapo Pilato akawafungulia Baraba kutoka gerezani, lakini akamtoa Yesu asulubiwe.
27 Les soldats du procurateur, emmenant Jésus dans le prétoire, assemblèrent autour de lui toute la cohorte.
Kisha askari wa mkuu wa mkoa wakamwingiza Yesu ndani ya ikulu, wakamkusanyikia kikosi kizima.
28 Ils lui ôtèrent ses vêtements, l'affublèrent d'un manteau militaire de couleur rouge.
Wakamvua nguo zake, wakamvika joho la rangi nyekundu.
29 Puis, tressant une couronne avec des épines, ils la lui mirent sur la tête, ainsi qu'un roseau dans la main droite; après quoi, se mettant à genoux devant lui, ils le bafouaient en disant: «Salut, le roi des Juifs!»
Kisha wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani, wakamwekea pia mwanzi katika mkono wake wa kulia. Wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki wakisema, “Shikamoo mfalme wa Wayahudi!”
30 Ils crachaient sur lui; ils lui prenaient le roseau et lui en donnaient des coups sur la tête.
Wakamtemea mate, wakauchukua ule mwanzi, wakampiga nao kichwani.
31 Quand ils eurent fini de se moquer de lui, ils lui ôtèrent le manteau, lui remirent ses vêtements et l'emmenèrent pour le crucifier.
Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
32 En s'en allant, ils rencontrèrent un homme de Cyrène, nommé Simon; et ils l'obligèrent à porter la croix de Jésus.
Walipokuwa wakienda, wakamkuta mtu mmoja jina lake Simoni, mwenyeji wa Kurene, wakamlazimisha kuuchukua msalaba wake Yesu.
33 Ils arrivèrent à un endroit nommé Golgotha, c'est-à-dire place du Crâne.
Walipofika mahali paitwapo Golgotha, maana yake, “Mahali pa Fuvu la kichwa,”
34 Ils lui donnèrent à boire du vin mêlé de fiel, et l'ayant goûté, il refusa de le boire.
wakampa mchanganyiko wa divai na nyongo. Lakini Yesu alipoonja akakataa kunywa.
35 Après l'avoir mis en croix, les soldats se partagèrent ses vêtements, en les tirant au sort.
Walimsulubisha, kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
36 Ils s'étaient assis et le gardaient.
Wakaketi, wakawa wanamchunga.
37 Au-dessus de sa tête ils avaient placé une inscription indiquant son crime: CELUI-CI EST JÉSUS, LE ROI DES JUIFS.
Juu ya kichwa chake wakaweka shtaka dhidi yake lilioandikwa, “Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi.”
38 On crucifia avec lui deux brigands, l'un à sa droite, l'autre à sa gauche.
Wanyang'anyi wawili walisulubishwa pia pamoja naye, mmoja upande wa kushoto na mwingine upande wa kulia.
39 Les passants l'injuriaient; ils lui disaient, en gesticulant de la tête:
Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana wakitikisa vichwa vyao na kusema,
40 «Toi qui détruis le Temple, et en trois jours le rebâtis, sauve-toi donc toi-même si tu es fils de Dieu!» — et: — «Descends de la croix!»
“Wewe! Si ulijidai kulivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu? Sasa jiokoe mwenyewe. Kama wewe ni Mwana wa Mungu, basi shuka msalabani!”
41 Les chefs des prêtres, avec les Scribes et les Anciens, se moquaient aussi de lui et disaient:
Hali kadhalika na makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria na wazee walimdhihaki wakisema,
42 «Il en a sauvé d'autres et il ne peut pas se sauver lui-même!»— «Ah! il est roi d'Israël! que maintenant il descende de la croix et nous croirons en lui!» -
“Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi! Eti yeye ni mfalme wa Wayahudi! Basi, sasa na ashuke msalabani, nasi tutamwamini.
43 Il a mis sa confiance en Dieu! que Dieu maintenant le délivre! s'il veut de lui!» En effet, il a dit: Je suis fils de Dieu.»
Alimtumainia Mungu na kusema eti yeye ni Mwana wa Mungu; basi, Mungu na amwokoe kama anamtaka.”
44 De même, les brigands que l'on avait crucifiés avec lui l'insultaient.
Hali kadhalika na wale waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana.
45 Depuis la sixième jusqu'à la neuvième heure, des ténèbres se firent sur tout le pays.
Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa, nchi yote ikawa katika giza.
46 Vers la neuvième heure Jésus jeta un cri et dit d'une voix forte: «Helei! Helei! Lema sabachthanei?» C'est-à-dire: «Mon Dieu! Mon Dieu! pourquoi m'as-tu abandonné?
Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kubwa, “Eli, Eli, lema sabakthani?” Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
47 Quelques-uns de ceux qui étaient là l'entendant: «Il appelle Élie, celui-là!» dirent-ils.
Lakini wale waliosimama pale waliposikia hivyo wakasema, “Anamwita Eliya.”
48 L'un d'entre eux courut aussitôt prendre une éponge, la trempa dans du vinaigre, et l'attachant à un roseau, il lui donna à boire. Mais les autres disaient:
Mmoja wao akakimbia, akachukua sifongo, akaichovya katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe.
49 «Laisse donc! voyons si Élie viendra le délivrer.»
Wengine wakasema, “Acha tuone kama Eliya anakuja kumwokoa.”
50 Jésus, jetant de nouveau un grand cri, rendit l'esprit.
Basi, Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akakata roho.
51 Et voilà que le rideau du Temples se déchira en deux depuis le haut jusqu'en bas; la terre trembla; les rochers se fendirent;
Hapo pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili, toka juu mpaka chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
52 les tombeaux s'ouvrirent; plusieurs des saints qui étaient morts ressuscitèrent en leurs corps;
makaburi yakafunguka na watu wengi wa Mungu waliokufa wakafufuliwa;
53 et sortant de leurs tombeaux après la résurrection de Jésus, ils entrèrent dans la ville sainte et apparurent à plusieurs.
nao, baada ya kufufuka kwake, wakatoka makaburini, wakaingia katika Mji Mtakatifu, wakaonekana na watu wengi.
54 Voyant le tremblement de terre et tout ce qui se passait, le centurion et ceux qui, avec lui, gardaient Jésus, furent frappés d'épouvante et dirent: «Cet homme-là était véritablement fils de Dieu.»
Basi, jemadari na wale waliokuwa wakimlinda Yesu walipoona tetemeko la ardhi na yale mambo yaliyotukia, wakaogopa sana, wakasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
55 Or il y avait là plusieurs femmes qui regardaient de loin c'étaient celles qui, depuis la Galilée, avaient suivi Jésus afin de le servir.
Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia.
56 Parmi elles, Marie-Magdeleine, Marie, mère de Jacques et de Joseph, ainsi que la mère des fils de Zébédée.
Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo.
57 Sur le soir arriva un homme riche, originaire d'Arimathée, nommé Joseph. Il était, lui aussi, un disciple de Jésus.
Ilipokuwa jioni, akaja mtu mmoja tajiri mwenyeji wa Armathaya, jina lake Yosefu. Yeye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
58 Il alla trouver Pilate et demanda le corps de Jésus. Pilate ordonna de le lui remettre.
Akamwendea Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu. Basi, Pilato akaamuru apewe.
59 Et Joseph, prenant le corps, l'ensevelit dans un linceul blanc
Yosefu akauchukua ule mwili akauzungushia sanda safi ya kitani,
60 et le déposa dans un sépulcre neuf, qu'il avait taillé dans le roc, et qui lui appartenait. Il roula une pierre énorme contre la porte du tombeau et s'en alla.
akauweka ndani ya kaburi lake jipya alilokuwa amelichonga katika mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.
61 Or Marie-Magdeleine et l'autre Marie étaient là, assises en face du sépulcre.
Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwa wameketi kulielekea kaburi.
62 Le lendemain (qui était le jour après la Préparation) les chefs des prêtres et les Pharisiens se rendirent ensemble chez Pilate
Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalio, makuhani wakuu na Mafarisayo walimwendea Pilato,
63 et lui dirent: «Seigneur, nous nous sommes souvenus que, de son vivant, cet imposteur disait: «Après trois jours, je ressusciterai.»
Wakasema, “Mheshimiwa, tunakumbuka kwamba yule mdanganyifu alisema kabla ya kufa ati, Baada ya siku tatu nitafufuka.
64 Ordonne donc que la tombe soit soigneusement surveillée jusqu'au troisième jour, de peur que ses disciples ne viennent voler le corps et ne disent ensuite au peuple: Il est ressuscité des morts. Imposture dernière qui serait pire que la première.»
Kwa hiyo amuru kaburi lilindwe mpaka siku ya tatu ili wanafunzi wake wasije wakamwiba na kuwaambia watu kwamba amefufuka. Uongo huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa awali.”
65 Pilate leur répondit: «Vous avez des gardes; allez, surveillez comme vous l'entendez.»
Pilato akawaambia, “Haya, mnao walinzi; nendeni mkalinde kadiri mjuavyo.”
66 Alors ils allèrent s'assurer du sépulcre, en scellant la pierre en présence de la garde.
Basi, wakaenda, wakalilinda kaburi, wakatia mhuri juu ya lile jiwe na kuacha hapo askari walinzi.

< Matthieu 27 >