< Marc 9 >

1 Il ajouta: «En vérité, je vous le dis, quelques-uns sont ici présents qui ne goûteront point la mort avant d'avoir vu venir, en puissance, le Royaume de Dieu.»
Yesu akaendelea kuwaambia, “Kweli nawaambieni, wako wengine papa hapa ambao hawatakufa kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu ukija kwa enzi.”
2 Six jours après, emmenant seuls avec lui Pierre, Jacques et Jean, Jésus les conduisit sur une haute montagne, à l'écart. Et alors, devant eux, il fut transfiguré:
Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane juu ya mlima mrefu peke yao. Huko, Yesu akageuka sura mbele yao,
3 ses vêtements devinrent resplendissants et d'une éblouissante blancheur. Nul foulon ici-bas ne saurait en produire une semblable.
mavazi yake yakang'aa, yakawa meupe sana, jinsi dobi yeyote duniani asingeweza kuyafanya meupe.
4 Élie leur apparut; avec lui était Moïse; et ils s'entretinrent avec Jésus.
Eliya na Mose wakawatokea, wakazungumza na Yesu.
5 Pierre alors, s'adressant à Jésus, lui dit: «Rabbi!, qu'il nous est bon d'être ici! Dressons trois tentes, une pour toi, une pour Moïse, une pour Élie...»
Petro akamwambia Yesu, “Mwalimu, ni vizuri sana kwamba tuko hapa. Basi, afadhali tujenge vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya.”
6 Il ne savait que dire; ils étaient, en effet, terrifiés.
Yeye na wenzake waliogopa hata hakujua la kusema.
7 Une nuée survint qui les enveloppa, et de cette nuée sortit une voix: «Celui-ci est mon Fils, le bien-aimé, écoutez-le!»
Kisha likatokea wingu likawafunika, na sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu, “Huyu ni Mwanangu mpendwa, msikilizeni.”
8 Immédiatement ils regardèrent autour d'eux, et ne virent plus personne; Jésus seul était avec eux.
Mara wanafunzi hao wakatazama tena, lakini hawakumwona mtu mwingine, ila Yesu peke yake pamoja nao.
9 Comme ils descendaient de la montagne, il leur ordonna de ne raconter à personne ce qu'ils venaient de voir, si ce n'est lorsque le Fils de l'homme serait ressuscité d'entre les morts.
Walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwakataza wasimwambie mtu yeyote mambo waliyoyaona, mpaka Mwana wa Mtu atakapokuwa amefufuka kutoka wafu.
10 Ils retinrent ces mots: «ressuscité d'entre les morts», et se demandaient, à part eux, ce qu'ils signifiaient;
Basi, wakashika agizo hilo, lakini wakawa wanajadiliana wao kwa wao maana ya kufufuka kutoka wafu.
11 et ils l'interrogèrent: «Comment les Scribes disent-ils: «Il faut, avant tout, qu'Élie vienne?»
Wakamwuliza Yesu, “Mbona walimu wa Sheria wanasema kwamba ni lazima Eliya aje kwanza?”
12 Il leur répondit: «Élie viendra avant tout et rétablira toutes choses; d'où vient alors qu'il est écrit du Fils de l'homme: il doit beaucoup souffrir et être méprisé?
Naye akawajibu, “Naam, Eliya anakuja kwanza kutayarisha yote. Hata hivyo, kwa nini basi imeandikwa katika Maandiko Matakatifu kwamba Mwana wa Mtu atapatwa na mateso mengi na kudharauliwa?
13 Eh bien, je vous le déclare, Élie est venu et ils lui ont fait tout ce qu'ils ont voulu, conformément à ce qui est écrit de lui.»
Lakini nawaambieni, Eliya amekwisha kuja, nao wakamtendea walivyotaka kama ilivyoandikwa juu yake.”
14 De retour auprès des disciples, ils les trouvèrent entourés d'une foule considérable; des Scribes discutaient avec eux.
Walipowafikia wale wanafunzi wengine, waliona umati mkubwa wa watu hapo. Na baadhi ya walimu wa Sheria walikuwa wanajadiliana nao.
15 Dès que la multitude aperçut Jésus, chacun fut en émoi; on accourut à lui, on le saluait.
Mara tu ule umati wa watu ulipomwona, wote walishangaa sana, wakamkimbilia wamsalimu.
16 Il les interrogea: «Qu'est-ce que cette discussion?»
Yesu akawauliza, “Mnajadiliana nini nao?”
17 L'un de ceux qui était dans la foule répondit: «Maître, je t'ai apporté mon fils; un Esprit muet le possède,
Hapo mtu mmoja katika ule umati wa watu akamjibu, “Mwalimu, nimemleta mwanangu kwako, ana pepo aliyemfanya kuwa bubu.
18 et partout où il s'empare de lui, il le renverse par terre; alors l'enfant écume, grince des dents et devient tout raide. J'ai demandé à tes disciples de le chasser: ils n'en ont pas eu la force.» —
Kila mara anapomvamia, humwangusha chini na kumfanya atokwe na povu kinywani, akisaga meno na kuwa mkavu mwili wote. Niliwaomba wanafunzi wako wamtoe huyo pepo lakini hawakuweza.”
19 «Ô génération sans foi, dit Jésus en leur répondant, jusqu'à quand serai-je au milieu de vous? Jusqu'à quand vous supporterai-je? Apportez-moi l'enfant.»
Yesu akawaambia, “Enyi kizazi kisicho na imani! Nitakaa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia mpaka lini? Mleteni kwangu.”
20 On le lui apporta. Mais à peine eut-il vu
Wakampeleka. Mara tu huyo pepo alipomwona Yesu, alimtia mtoto kifafa, naye mtoto akaanguka chini, akagaagaa na kutoka povu kinywani. Yesu akamwuliza baba yake huyo mtoto,
21 Jésus que l'Esprit lui donna des convulsions, et, tombant par terre, il se tordait en écumant. Jésus interrogea son père: «Combien y a-t-il de temps que cela lui arrive?» — «Depuis sa première enfance», répondit-il;
“Amepatwa na mambo hayo tangu lini?” Naye akamjibu, “Tangu utoto wake.
22 «et souvent l'Esprit l'a jeté tantôt dans le feu, tantôt dans l'eau pour le faire périr; si tu peux y faire quelque chose, aie pitié de nous, et viens à notre secours.»
Na mara nyingi pepo huyo amemwangusha motoni na majini, ili amwangamize kabisa. Basi, ikiwa waweza, utuhurumie na kutusaidia!”
23 Jésus lui répondit: «Tu me dis: si tu peux! Tout est possible à celui qui croit.»
Yesu akamwambia, “Eti ikiwa waweza! Mambo yote yanawezekana kwa mtu aliye na imani.”
24 Aussitôt le père de l'enfant s'écria: «Je crois! Viens en aide à mon incrédulité!»
Hapo, huyo baba akalia kwa sauti, “Naamini! Lakini imani yangu haitoshi, nisaidie!”
25 Jésus, voyant la foule accourir, fit des menaces à l'Esprit impur: il lui dit: «Esprit sourd et muet, c'est moi qui te l'ordonne, sors de cet enfant et désormais n'y rentre plus!»
Yesu alipouona umati wa watu unaongezeka upesi mbele yake, alimkemea yule pepo mchafu, “Pepo unayemfanya huyu mtoto kuwa bubu-kiziwi, nakuamuru, mtoke mtoto huyu wala usimwingie tena!”
26 L'Esprit jeta un cri et sortit, en agitant violemment l'enfant, qui devint comme mort; aussi un grand nombre disaient-ils: «Il est mort.»
Hapo huyo pepo alipaaza sauti, akamwangusha huyo mtoto chini, kisha akamtoka. Mtoto alionekana kama maiti, hata wengine walisema, “Amekufa!”
27 Mais Jésus le prit par la main, le releva; il revint à lui.
Lakini Yesu akamshika mkono, akamwinua, naye akasimama.
28 Quand Jésus fut entré dans une maison, ses disciples lui demandèrent en particulier: «Pourquoi, nous, avons-nous été impuissants à expulser cet Esprit?»
Yesu alipoingia nyumbani, wanafunzi wake walimwuliza kwa faragha, “Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa?”
29 Jésus leur répondit: «Il est d'une espèce, qui ne peut absolument se chasser que par la prière.»
Naye akawaambia, “Pepo wa aina hii hawezi kutoka isipokuwa kwa sala tu.”
30 Partis de là, ils traversèrent la Galilée, et il voulait que personne ne le sût,
Yesu na wanafunzi wake waliondoka hapo, wakaendelea na safari kupitia wilaya ya Galilaya. Yesu hakupenda watu wajue alipokuwa,
31 car il instruisait ses disciples; il leur disait: «Le Fils, de l'homme sera livrés entre les mains des hommes; ils le tueront; puis, une fois mis à mort, après trois jours, il ressuscitera.»
kwa sababu alikuwa anawafundisha wanafunzi wake. Aliwaambia, “Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa watu ambao watamuua; lakini siku ya tatu baada ya kuuawa atafufuka.”
32 Mais ils ne comprenaient pas ce langage et ils craignaient de l'interroger.
Wanafunzi hawakufahamu jambo hilo. Wakaogopa kumwuliza.
33 Ils arrivèrent à Capharnaüm; et quand il fut à la maison, il leur demanda: «De quoi vous entreteniez-vous pendant la route?»
Basi, walifika Kafarnaumu. Na alipokuwa nyumbani, aliwauliza, “Mlikuwa mnajadiliana nini njiani?”
34 Ils gardèrent le silence; car ils avaient discuté en chemin sur celui d'entre eux qui était le plus grand.
Lakini wao wakanyamaza, maana njiani walikuwa wamebishana ni nani aliye mkuu kati yao.
35 Jésus s'assit, appela les douze et leur dit: «Si quelqu'un veut être le premier, qu'il soit le dernier de tous et le serviteur de tous.»
Yesu akaketi chini, akawaita wale kumi na wawili, akawaambia, “Yeyote anayetaka kuwa wa kwanza lazima awe wa mwisho na kuwa mtumishi wa wote.”
36 Puis il prit un enfant, le plaça au milieu d'eux, et, après l'avoir embrassé, il leur dit:
Kisha akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha kati yao, akamku mbatia, halafu akawaambia,
37 «Qui reçoit en mon nom un enfant tel que celui-ci me reçoit. Et qui me reçoit, reçoit non pas moi, mais Celui qui m'a envoyé.»
“Anayempokea mtoto kama huyu kwa jina langu, ananipokea mimi; na anayenipokea mimi, hanipokei mimi tu, bali anampokea yule aliyenituma.”
38 «Maître, lui dit Jean, nous avons vu un homme chasser des démons en ton nom, et comme il ne nous suit pas, nous l'en avons empêché.»
Yohane akamwambia, “Mwalimu, tumemwona mtu mmoja akitoa pepo kwa kulitumia jina lako, nasi tukajaribu kumkataza kwa kuwa yeye si mmoja wetu.”
39 Jésus répondit: «Ne l'en empêchez point, car per sonne, après avoir, en mon nom, fait un miracle, ne peut aussitôt mal parler de moi.
Lakini Yesu akasema, “Msimkataze, maana hakuna mtu anayefanya muujiza kwa jina langu, na papo hapo akaweza kusema mabaya juu yangu.
40 En effet, qui n'est pas contre nous est pour nous.
Maana, asiyepingana nasi, yuko upande wetu.
41 Et quiconque, en mon nom et parce que vous êtes au Christ, vous aura donné à boire un verre d'eau, je vous le dis en vérité, ne perdra point sa récompense.»
Mtu yeyote atakeyewapeni kikombe cha maji ya kunywa kwa sababu ninyi ni watu wake Kristo, hakika hatakosa kupata tuzo lake.
42 «Quant à celui qui aura été une occasion de chute pour l'un de ces petits qui croient, il vaudrait mieux pour lui qu'on lui attachât au cou une de ces meules que tournent les ânes, et qu'on le jetât dans la mer.»
“Mtu yeyote atakayemfanya mmoja wa hawa wadogo wanaoniamini atende dhambi, ingekuwa afadhali kwa mtu huyo kufungiwa shingoni mwake jiwe kubwa la kusagia na kutupwa baharini.
43 «Si ta main est pour toi une occasion de chute, coupe-la; il t'est meilleur d'entrer mutilé dans la vie, que d'aller avec tes deux mains dans la Géhenne, dans le feu inextinguible. (Geenna g1067)
Mkono wako ukikukosesha, ukate! Afadhali kuingia kwenye uzima bila mkono mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili na kwenda katika moto wa Jehanamu. (Geenna g1067)
44 (où leur ver ne meurt point et où le feu ne s'éteint point).
Humo, wadudu wake hawafi na moto hauzimiki.
45 Si ton pied est pour toi une occasion de chute, coupe-le; il t'est meilleur d'entrer estropié dans la vie que d'être jeté avec tes deux pieds dans la Géhenne. (Geenna g1067)
Na mguu wako ukikukosesha, ukate! Afadhali kuingia katika uzima bila mguu mmoja, kuliko kuwa na miguu yote miwili na kutupwa katika moto wa Jehanamu. (Geenna g1067)
46 (où leur ver ne meurt point et où le feu ne s'éteint point).
Humo, wadudu wake hawafi na moto hauzimiki.
47 Si ton oeil est pour toi une occasion de chute, arrache-le; il t'est meilleur d'entrer borgne dans le Royaume de Dieu que d'être jeté, avec tes deux yeux, dans la Géhenne (Geenna g1067)
Na jicho lako likikukosesha, ling'oe! Afadhali kuingia katika utawala wa Mungu ukiwa na jicho moja tu, kuliko kuwa na macho yako yote mawili na kutupwa katika moto wa Jehanamu. (Geenna g1067)
48 où: «Leur ver ne meurt pas et le feu ne s'éteint pas.»
Humo wadudu wake hawafi, na moto hauzimiki.
49 Car tous seront salés par le feu.
“Maana kila mmoja atakolezwa kwa moto.
50 Le sel est bon: mais si le sel devient insipide, avec quoi l'assaisonnerez-vous? En vous-mêmes ayez du sel, et, entre vous, vivez en paix.»
Chumvi ni nzuri, lakini ikipoteza ladha yake, itakolezwa na nini? Muwe na chumvi ndani yenu na kudumisha amani kati yenu.”

< Marc 9 >