< Marc 9 >

1 Il ajouta: «En vérité, je vous le dis, quelques-uns sont ici présents qui ne goûteront point la mort avant d'avoir vu venir, en puissance, le Royaume de Dieu.»
Na alisema kwao, “Hakika nasema kwenu, baadhi yenu kuna watu waliosimama hapa hawataonja mauti kabla ya kuuona ufalme wa Mungu ukija kwa nguvu.”
2 Six jours après, emmenant seuls avec lui Pierre, Jacques et Jean, Jésus les conduisit sur une haute montagne, à l'écart. Et alors, devant eux, il fut transfiguré:
Na baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohana pamoja naye mlimani, pekee yao. Ndipo alianza kubadilika mbele yao.
3 ses vêtements devinrent resplendissants et d'une éblouissante blancheur. Nul foulon ici-bas ne saurait en produire une semblable.
Mavazi yake yakaanza kung'aa sana, meupe zaidi, meupe kuliko mng'arishaji yeyote duniani.
4 Élie leur apparut; avec lui était Moïse; et ils s'entretinrent avec Jésus.
Ndipo Eliya pamoja na Musa walitokea mbele yao, na walikuwa wakiongea na Yesu.
5 Pierre alors, s'adressant à Jésus, lui dit: «Rabbi!, qu'il nous est bon d'être ici! Dressons trois tentes, une pour toi, une pour Moïse, une pour Élie...»
Petro alijibu akamwambia Yesu, “Mwalimu, ni vyema sisi kuwa hapa, na tujenge vibanda vitatu, kimoja kwa ajili yako, kimoja kwa ajili Musa na kingine kwa ajili ya Eliya.”
6 Il ne savait que dire; ils étaient, en effet, terrifiés.
(Kwa kuwa hakujua nini cha kusema, waliogopa sana.)
7 Une nuée survint qui les enveloppa, et de cette nuée sortit une voix: «Celui-ci est mon Fils, le bien-aimé, écoutez-le!»
Wingu lilitokea na kuwafunika. Ndipo sauti ikatoka mawinguni ikisema, “Huyu ni mwanangu mpendwa. Msikieni yeye.”
8 Immédiatement ils regardèrent autour d'eux, et ne virent plus personne; Jésus seul était avec eux.
Ghafla, walipokuwa wakitazama, hawakumuona yeyote pamoja nao, isipokuwa Yesu tu.
9 Comme ils descendaient de la montagne, il leur ordonna de ne raconter à personne ce qu'ils venaient de voir, si ce n'est lorsque le Fils de l'homme serait ressuscité d'entre les morts.
Walipokuwa wanateremka kutoka mlimani, aliwaamuru kutokumwambia mtu yeyote yale yote waliyoyaona, mpaka Mwana wa Adamu atakapofufuka kutoka kwa wafu.
10 Ils retinrent ces mots: «ressuscité d'entre les morts», et se demandaient, à part eux, ce qu'ils signifiaient;
Ndipo waliyatunza mambo wao wenyewe. Lakini walijadiliana wao kwa wao ni nini maana yake “kufufuliwa kutoka kwa wafu”
11 et ils l'interrogèrent: «Comment les Scribes disent-ils: «Il faut, avant tout, qu'Élie vienne?»
Walimwuliza Yesu,”Kwa nini waandishi husema lazima Eliya aje kwanza?”
12 Il leur répondit: «Élie viendra avant tout et rétablira toutes choses; d'où vient alors qu'il est écrit du Fils de l'homme: il doit beaucoup souffrir et être méprisé?
Akawaambia, “hakika Eliya atakuja kwanza kuokoa vitu vyote. Kwa nini imeandikwa Mwana wa Adamu lazima apate mateso mengi na achukiwe?
13 Eh bien, je vous le déclare, Élie est venu et ils lui ont fait tout ce qu'ils ont voulu, conformément à ce qui est écrit de lui.»
Lakini nasema kwenu Eliya alikwisha kuja, na walimfanya kama walivyopenda, kama vile maandiko yasemavyo kuhusu yeye.”
14 De retour auprès des disciples, ils les trouvèrent entourés d'une foule considérable; des Scribes discutaient avec eux.
Na waliporudi kwa wanafunzi, waliona kundi kubwa limewazunguka na Masadukayo walikuwa wanabishana nao.
15 Dès que la multitude aperçut Jésus, chacun fut en émoi; on accourut à lui, on le saluait.
Na mara walipomwona, kundi lote lilishangaa na kumkimbilia kumsalimia.
16 Il les interrogea: «Qu'est-ce que cette discussion?»
Aliwauliza wanafunzi wake, “Mnabishana nao juu ya nini?”
17 L'un de ceux qui était dans la foule répondit: «Maître, je t'ai apporté mon fils; un Esprit muet le possède,
Mmoja wao katika kundi alimjibu, “Mwalimu, nilimleta mwanangu kwako; ana roho chafu ambayo humfanya asiweze kuongea,
18 et partout où il s'empare de lui, il le renverse par terre; alors l'enfant écume, grince des dents et devient tout raide. J'ai demandé à tes disciples de le chasser: ils n'en ont pas eu la force.» —
na humsababishia kutetemeka na kumwangusha chini, na kutoka povu mdomoni na kusaga meno na kukakamaa. Niliwaomba wanafunzi wako kumtoa pepo, lakini hawakuweza.
19 «Ô génération sans foi, dit Jésus en leur répondant, jusqu'à quand serai-je au milieu de vous? Jusqu'à quand vous supporterai-je? Apportez-moi l'enfant.»
Aliwajibu, “Kizazi kisichoamini, nitakaa nanyi kwa muda gani? Nitachukuliana nanyi hadi lini? Mleteni kwangu.”
20 On le lui apporta. Mais à peine eut-il vu
Walimleta mtoto wake. Roho mchafu alipomwona Yesu, ghafla ilimtia katika kutetemeka. Mvulana alianguka chini na kutoa povu mdomoni.
21 Jésus que l'Esprit lui donna des convulsions, et, tombant par terre, il se tordait en écumant. Jésus interrogea son père: «Combien y a-t-il de temps que cela lui arrive?» — «Depuis sa première enfance», répondit-il;
Yesu alimwuliza baba yake, “Amekuwa katika hali hii kwa muda gani?” Baba alisema, “Tangu utoto.
22 «et souvent l'Esprit l'a jeté tantôt dans le feu, tantôt dans l'eau pour le faire périr; si tu peux y faire quelque chose, aie pitié de nous, et viens à notre secours.»
Mara nyingine huanguka katika moto au kwenye maji, na kujaribu kumwangamiza. Kama unaweza kufanya chochote tuhurumie na utusaidie.”
23 Jésus lui répondit: «Tu me dis: si tu peux! Tout est possible à celui qui croit.»
Yesu alimwambia, “Kama uko tayari? Kila kitu kinawezekana kwa yeyote aaminiye.”
24 Aussitôt le père de l'enfant s'écria: «Je crois! Viens en aide à mon incrédulité!»
Ghafla baba wa mtoto alilia na kusema, “Naamini! Nisaidie kutokuamini kwangu.”
25 Jésus, voyant la foule accourir, fit des menaces à l'Esprit impur: il lui dit: «Esprit sourd et muet, c'est moi qui te l'ordonne, sors de cet enfant et désormais n'y rentre plus!»
Wakati Yesu alipoona kundi linakimbilia kwao, alimkemea roho mchafu na kusema, “wewe roho bubu na kiziwi, nakuamuru mwache, usiingie kwake tena.”
26 L'Esprit jeta un cri et sortit, en agitant violemment l'enfant, qui devint comme mort; aussi un grand nombre disaient-ils: «Il est mort.»
Alilia kwa nguvu na kumhangaisha mtoto na roho alimtoka. Mtoto alionekana kama amekufa, Ndipo wengi walisema, “Amekufa,”
27 Mais Jésus le prit par la main, le releva; il revint à lui.
Lakini Yesu alimchukua kwa mkono akamwinua, na mtoto alisimama.
28 Quand Jésus fut entré dans une maison, ses disciples lui demandèrent en particulier: «Pourquoi, nous, avons-nous été impuissants à expulser cet Esprit?»
Wakati Yesu alipoingia ndani, wanafunzi wake walimwuliza faragha, “Kwa nini hatukuweza kumtoa?”
29 Jésus leur répondit: «Il est d'une espèce, qui ne peut absolument se chasser que par la prière.»
Aliwaambia, “kwa namna hii hatoki isipokuwa kwa maombi.”
30 Partis de là, ils traversèrent la Galilée, et il voulait que personne ne le sût,
Walitoka pale na kupitia Galilaya. Hakutaka mtu yeyote ajue walipo,
31 car il instruisait ses disciples; il leur disait: «Le Fils, de l'homme sera livrés entre les mains des hommes; ils le tueront; puis, une fois mis à mort, après trois jours, il ressuscitera.»
kwa kuwa alikuwa anafundisha wanafunzi wake. Aliwaambia, “Mwana wa Adamu atafikishwa mikononi mwa watu, na watamuua. Atakapokuwa amekufa, baada ya siku tatu atafufuka tena.”
32 Mais ils ne comprenaient pas ce langage et ils craignaient de l'interroger.
Lakini hawakuelewa maelezo haya, na waliogopa kumwuliza.
33 Ils arrivèrent à Capharnaüm; et quand il fut à la maison, il leur demanda: «De quoi vous entreteniez-vous pendant la route?»
Ndipo walifika Karperinaumu. Wakati akiwa ndani ya nyumba aliwauliza, ''Mlikuwa mnajadili nini njiani”?
34 Ils gardèrent le silence; car ils avaient discuté en chemin sur celui d'entre eux qui était le plus grand.
Lakini walikuwa kimya. Kwani walikuwa wanabishana njiani kwamba nani alikuwa mkubwa zaidi.
35 Jésus s'assit, appela les douze et leur dit: «Si quelqu'un veut être le premier, qu'il soit le dernier de tous et le serviteur de tous.»
Alikaa chini akawaita kumi na wawili pamoja, na alisema nao, “Kama yeyote anataka kuwa wa kwanza, ni lazima awe wa mwisho na mtumishi wa wote.”
36 Puis il prit un enfant, le plaça au milieu d'eux, et, après l'avoir embrassé, il leur dit:
Alimchukua mtoto mdogo akamweka katikati yao. Akamchukua katika mikono yake, akasema,
37 «Qui reçoit en mon nom un enfant tel que celui-ci me reçoit. Et qui me reçoit, reçoit non pas moi, mais Celui qui m'a envoyé.»
“Yeyote ampokeaye mtoto kama huyu kwa jina langu, pia amenipokea mimi, na ikiwa mtu amenipokea, hanipokei mimi tu, lakini pia aliyenituma.”
38 «Maître, lui dit Jean, nous avons vu un homme chasser des démons en ton nom, et comme il ne nous suit pas, nous l'en avons empêché.»
Yohana alimwambia, “Mwalimu tulimwona mtu anatoa pepo kwa jina lako na tukamzuia, kwa sababu hatufuati.”
39 Jésus répondit: «Ne l'en empêchez point, car per sonne, après avoir, en mon nom, fait un miracle, ne peut aussitôt mal parler de moi.
Lakini Yesu alisema, “Msimzuie, kwa kuwa hakuna atakayefanya kazi kubwa kwa jina langu na ndipo baadaye aseme neno baya lolote juu yangu.
40 En effet, qui n'est pas contre nous est pour nous.
Yeyote asiyekuwa kinyume nasi yuko upande wetu.
41 Et quiconque, en mon nom et parce que vous êtes au Christ, vous aura donné à boire un verre d'eau, je vous le dis en vérité, ne perdra point sa récompense.»
Yeyote atakayekupa kikombe cha maji ya kunywa kwa sababu uko na Kristo, kweli nawaambia, hatapoteza thawabu yake.
42 «Quant à celui qui aura été une occasion de chute pour l'un de ces petits qui croient, il vaudrait mieux pour lui qu'on lui attachât au cou une de ces meules que tournent les ânes, et qu'on le jetât dans la mer.»
Yeyote anayewakosesha hawa wadogo waniaminio mimi, ingekuwa vyema kwake kufungiwa jiwe la kusagia shingoni na kutupwa baharini.
43 «Si ta main est pour toi une occasion de chute, coupe-la; il t'est meilleur d'entrer mutilé dans la vie, que d'aller avec tes deux mains dans la Géhenne, dans le feu inextinguible. (Geenna g1067)
Kama mkono wako ukikukosesha ukate. Ni heri kuingia katika uzima bila mkono kuliko kuingia kwenye hukumu ukiwa na mikono yote. Katika moto “usiozimika”. (Geenna g1067)
44 (où leur ver ne meurt point et où le feu ne s'éteint point).
(Zingatia: Mstari hii, “Mahali ambapo funza hawafi na moto usiozimika.” haumo katika nakala za kale).
45 Si ton pied est pour toi une occasion de chute, coupe-le; il t'est meilleur d'entrer estropié dans la vie que d'être jeté avec tes deux pieds dans la Géhenne. (Geenna g1067)
Kama mguu wako ukikukosesha, ukate. Ni vyema kwako kuingia uzimani ukiwa kilema, kuliko kutupwa hukumuni na miguu miwili. (Geenna g1067)
46 (où leur ver ne meurt point et où le feu ne s'éteint point).
(Zingatia: Mstari huu, “Mahali ambapo funza hawafi na moto usioweza kuzimika” haumo kwenye nakala za kale).
47 Si ton oeil est pour toi une occasion de chute, arrache-le; il t'est meilleur d'entrer borgne dans le Royaume de Dieu que d'être jeté, avec tes deux yeux, dans la Géhenne (Geenna g1067)
Kama jicho lako likikukosesha ling'oe. Ni vyema kwako kuingia katika Ufalme wa Mungu ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili na kutupwa kuzimu. (Geenna g1067)
48 où: «Leur ver ne meurt pas et le feu ne s'éteint pas.»
Mahali palipo na funza wasiokufa, na moto usiozimika.
49 Car tous seront salés par le feu.
Kwa kuwa kila mmoja atakolezwa na moto.
50 Le sel est bon: mais si le sel devient insipide, avec quoi l'assaisonnerez-vous? En vous-mêmes ayez du sel, et, entre vous, vivez en paix.»
Chumvi ni nzuri, kama chumvi ikipoteza ladha yake, utaifanyaje iwe na ladha yake tena? Muwe na chumvi miongoni mwenu wenyewe, na muwe na amani kwa kila mmoja.”

< Marc 9 >