< Luc 6 >

1 Il arriva — un jour de sabbat — que Jésus passa par des blés; ses disciples cueillaient les épis et, les froissant dans leurs mains, en mangeaient les grains.
Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
2 «Pourquoi faites-vous, dirent quelques-uns des Pharisiens, ce qu'au jour du sabbat il n'est pas permis de faire?»
Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?”
3 Jésus leur répondit par ces paroles: «N'avez-vous pas lu ce que fit David quand il eut faim et ce que firent ses compagnons?
Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4 Comment il entra dans la maison de Dieu, prit les pains de proposition, en mangea et en donna à ceux qui étaient avec lui, quand il n'est permis qu'aux prêtres seuls d'en manger?» —
Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo.”
5 «Le Fils de l'homme, ajouta-t-il, est maître aussi du sabbat.»
Hivyo akawaambia, “Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato.”
6 Un autre jour de sabbat, il entra dans la synagogue et il y enseigna. Il s'y trouvait un homme dont la main droite était paralysée.
Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7 Les Scribes et les Pharisiens l'observaient pour voir si, un jour de sabbat, il le guérirait, et pour tirer de là quelque prétexte à accusation.
Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
8 Quant à lui, il connaissait leurs pensées. «Lève-toi, dit-il, à l'homme dont la main était paralysée, et tiens-toi debout au milieu de nous tous! L'homme se leva et se tint debout.
Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka, simama katikati.” Yule mtu akaenda akasimama katikati.
9 «Je vous le demande, leur dit alors Jésus, est-il permis aux jours de sabbat de faire le bien ou de faire le mal? de sauver une vie ou de la perdre?»
Kisha Yesu akawaambia, “Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
10 Ayant sur eux tous promené son regard, il dit à l'homme: «Étends ta main.»
Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
11 Il le fit et sa main fut guérie. Quant à eux, ils étaient fous de rage, et ils parlaient entre eux de ce qu'ils pourraient bien faire à Jésus.
Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
12 En ces jours-là, il se retira sur la montagne pour prier et passa la nuit à prier Dieu.
Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
13 Quand il fit jour, il convoqua ses disciples; et il choisit douze d'entre eux, auxquels il donna le nom d'apôtres;
Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
14 ce furent Simon, qu'il nomma Pierre, et André son frère; — Jacques et Jean; — Philippe et Barthélemi; —
Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
15 Matthieu et Thomas; — Jacques, fils d'Alphée, et Simon (celui qu'on appelle le zélateur);
Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
16 Judas, frère de Jacques, et Judas l'Iskariôte, qui fut un traître.
Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
17 Descendant de la montagne, avec eux, il s'arrêta sur un terrain uni. Là se trouvait, avec une foule considérable de ses disciples, une multitude immense de peuple, venue pour l'entendre et se faire guérir de ses maux, de toute la Judée, de Jérusalem et du littoral de Tyr et de Sidon.
Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
18 Ceux qui étaient tourmentés par des Esprits impurs en étaient délivrés
Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
19 et chacun dans la foule cherchait à le toucher, parce qu'il sortait de lui une vertu qui les guérissait tous.
Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
20 Jésus, levant les yeux sur ses disciples, dit: «Heureux êtes-vous, ô pauvres, parce qu'à vous appartient le Royaume de Dieu!»
Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: “Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
21 «Heureux, ô vous qui avez faim maintenant, parce que vous serez rassasiés!» «Heureux, ô vous qui pleurez maintenant, parce que vous rirez!»
Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
22 «Heureux serez-vous lorsque les hommes vous haïront, vous réprouveront, vous outrageront, proscriront votre nom comme maudit à cause du Fils de l’homme!
“Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
23 En ce jour-là réjouissez-vous et sautez de joie! parce que votre récompense sera grande dans le ciel; car c'est de même façon que leurs pères traitaient les prophètes.»
Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
24 «Malheur à vous cependant, riches, parce que vous avez aujourd'hui votre consolation!»
Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
25 «Malheur à vous qui maintenant avez tout à satiété, parce que vous aurez faim!» «Malheur à vous qui maintenant riez, parce que vous tomberez dans le deuil et les larmes!»
Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
26 «Malheur! lorsque tous les hommes diront du bien de vous, car c'est de même façon que leurs pères traitaient les faux prophètes!»
Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
27 «Quant à vous qui m'écoutez, voici ce que je vous dis: Aimez vos ennemis; faites du bien à ceux qui vous haïssent;
“Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
28 bénissez ceux qui vous maudissent; priez pour ceux qui vous font injure.
Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
29 Si quelqu'un te frappe sur une joue, présente-lui aussi l'autre; et contre celui qui t'enlève ton manteau ne défends pas même ta tunique.»
Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
30 «A qui te demande, donne; et à qui s'empare de ce qui est à toi, ne réclame rien.»
Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
31 «Comme vous voulez que les hommes agissent envers vous, agissez vous-mêmes pareillement envers eux.
Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
32 Si vous aimez ceux qui vous aiment, quel gré vous en saura-t-on? les pécheurs aussi aiment ceux qui les aiment.
“Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
33 Et si vous faites du bien à ceux qui vous en font à vous-mêmes, quel gré vous en saura-t-on? Les pécheurs le font aussi.
Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
34 Et si vous prêtez à ceux dont vous espérez recevoir quelque chose, quel gré vous en saura-t-on? Les pécheurs aussi font des prêts aux pécheurs pour recevoir un jour le même service.
Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
35 Vous cependant aimez vos ennemis; faites du bien et prêtez sans espérer quoi que ce soit. Et votre récompense sera grande et vous serez fils du Très-Haut, parce qu'il est bon pour les ingrats et pour les méchants.»
Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
36 «Soyez miséricordieux, comme votre Père est miséricordieux.
Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
37 Ne jugez point et vous ne serez point jugés; ne condamnez point et vous ne serez point condamnés. Pardonnez, et il vous sera pardonné.
“Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
38 Donnez, et il vous sera donné; il sera versé dans votre sein une bonne mesure, pressée, tassée, débordante, car la mesure que vous faites aux autres sera votre mesure.»
Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu.”
39 Il leur dit aussi une parabole: «Un aveugle peut-il conduire un aveugle? Ne tomberont-ils pas tous deux dans une fosse?»
Akawaambia mfano huu: “Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
40 «Le disciple n'est pas au-dessus du maître; il sera parfait quand il sera pareil à son maître.»
Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
41 «Pourquoi regardes-tu la paille qui est dans l'oeil de ton frère? Et la poutre qui est dans ton oeil à toi, tu ne la remarques pas!
Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
42 Comment peux-tu dire à ton frère: «Mon frère, laisse-moi ôter cette paille qui est dans ton oeil», ne voyant pas toi-même la poutre qui est dans le tien? Hypocrite, ôte d'abord de ton oeil la poutre et alors tu verras à ôter la paille de l'oeil de ton frère!»
Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
43 «Un arbre qui produit de mauvais fruits n'est pas bon; à l'inverse, un arbre qui produit de bons fruits n'est pas mauvais;
“Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
44 car c'est par son fruit que chaque arbre se fait connaître. Sur des épines on ne cueille pas de figues; sur des ronces on ne vendange pas de raisin.»
Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
45 «Du bon trésor de son coeur l'homme bon tire le bien; de son mauvais trésor l'homme mauvais tire le mal; car c'est de l'abondance du coeur que la bouche parle.»
Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
46 «Pourquoi m'appelez-vous: «Seigneur! Seigneur!» et ne faites-vous pas ce que je dis?
“Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
47 Quiconque vient à moi, entendant mes paroles et les mettant en pratique, je vais vous montrer à qui il ressemble.
Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
48 Il ressemble à un homme qui, en construisant une maison, a creusé très avant et a établi ses fondations sur le roc. L'inondation est survenue; le torrent a fait irruption sur cette maison et il n'a pas eu la force de l'ébranler, parce qu'elle était bien construite.»
Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
49 «Quant à celui qui entend et ne met pas en pratique, il ressemble à un homme qui a bâti sa maison sur la terre sans fondations. Sur elle le torrent a fait irruption; soudain elle s'est écroulée; et la ruine de cette maison a été grande.
Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!”

< Luc 6 >