< Luc 21 >
1 Tout en regardant, il vit des riches qui mettaient leurs offrandes, dans le tronc.
Yesu alitazama kwa makini, akawaona matajiri walivyokuwa wanatia sadaka zao katika hazina ya Hekalu,
2 Il vit aussi une veuve indigente qui y mit deux leptes,
akamwona pia mama mmoja mjane akitumbukiza humo sarafu mbili ndogo.
3 et il dit: «En vérité, je vous le déclare, cette veuve pauvre a donné plus que tous.
Basi, akasema, “Nawaambieni kweli, mama huyu mjane ametia zaidi katika hazina kuliko wote.
4 Car tous ceux-là, pour leurs offrandes, ont puisé dans leur superflu; mais celle-ci a pris sur son indigence, elle a donné tout ce qu'elle possédait, tout ce qu'elle avait pour vivre.»
Kwa maana, wengine wote wametoa sadaka zao kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi.”
5 Quelques-uns faisaient remarquer, à propos du Temple, les pierres magnifiques et les offrandes dont il était orné.
Baadhi ya wanafunzi walikuwa wanazungumza juu ya Hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe ya thamani, pamoja na sadaka zilizotolewa kwa Mungu. Yesu akasema,
6 «Des jours viendront, dit-il, où de ce que vous voyez, il ne restera pas ici pierre sur pierre; tout sera renversé.»
“Haya yote mnayoyaona—zitakuja siku ambapo hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa.”
7 Alors ils le questionnèrent: «Maître, lui dirent-ils, quand donc ces choses arriveront-elles? et quel sera le signe qu'elles vont avoir lieu?»
Basi, wakamwuliza, “Mwalimu, mambo hayo yatatokea lini? Na ni ishara gani zitakazoonyesha kwamba karibu mambo hayo yatokee?”
8 Il répondit: «Prenez garde de vous laisser séduire; car plusieurs viendront en prenant mon nom, disant: «C'est moi!» et: «Le moment approche!». Ne marchez pas à leur suite.
Yesu akawajibu, “Jihadharini, msije mkadanganyika. Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye, na, Wakati ule umekaribia. Lakini ninyi msiwafuate!
9 Quand vous entendrez parler de guerres et de révolutions, n'en soyez pas effrayés. Il faut, en effet, que cela arrive d'abord; mais ce ne sera pas tout de suite la fin.»
Basi, mtakaposikia habari za vita na misukosuko, msitishike; maana ni lazima hayo yatokee kwanza, lakini mwisho wa yote, bado.”
10 Il continua ainsi: «Se soulèvera nation contre nation, royaume contre royaume;
Halafu akaendelea kusema: “Taifa moja litapigana na taifa lingine, na ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine.
11 il y aura de vastes tremblements de terre; ici et là des famines, des pestes, d'effrayantes choses et de grands prodiges au ciel.»
Kila mahali kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, kutakuwa na njaa na tauni. Kutakuwa na vituko vya kutisha na ishara kubwa angani.
12 «Mais, avant tout, on mettra la main sur vous, et l'on vous persécutera. Vous serez livrés aux synagogues, jetés en prison; et, à cause de mon nom, traînés devant des rois et des procurateurs.
Lakini kabla ya kutokea hayo yote, watawatieni nguvuni, watawatesa na kuwapelekeni katika masunagogi na kuwatia gerezani; mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya jina langu.
13 Cela vous arrivera pour que vous rendiez témoignage.
Hii itawapeni fursa ya kushuhudia Habari Njema.
14 Gravez bien dans vos coeurs que vous n'aurez pas à vous préoccuper de votre défense,
Muwe na msimamo huu mioyoni mwenu: hakuna kufikiria kabla ya wakati juu ya jinsi mtakavyojitetea,
15 car je vous donnerai, moi, un langage et une sagesse auxquels tous vos adversaires ne pourront ni résister ni répliquer.
kwa sababu mimi mwenyewe nitawapeni ufasaha wa maneno na hekima, hivyo kwamba zenu hawataweza kustahimili wala kupinga.
16 Vous serez livrés par vos pères et vos mères, par vos frères, par vos parents, par vos amis; ils feront mourir nombre d'entre vous;
Wazazi wenu, ndugu, jamaa na rafiki zenu watawasaliti ninyi; na baadhi yenu mtauawa.
17 et vous serez en haine à tout le monde à cause de mon nom.
Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu.
18 Et cependant pas un cheveu de votre tête ne doit périr;
Lakini, hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.
19 c'est par votre patience que vous sauverez vos vies.»
Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.
20 Lorsque vous verrez des armées camper autour de Jérusalem et l'investir, sachez alors qu'approche sa désolation.
“Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo mtambue ya kwamba wakati umefika ambapo mji huo utaharibiwa.
21 Que ceux qui seront dans la Judée fuient dans les montagnes, que ceux qui seront au milieu du pays en sortent, que ceux qui seront dans les contrées voisines n'y rentrent pas.
Hapo walioko Yudea wakimbilie milimani; wale walio mjini watoke; na wale walio mashambani wasirudi mjini.
22 Ces jours-là, en effet, seront des jours vengeurs où s'accomplira tout ce qui est écrit.
Kwa maana siku hizo ni siku za adhabu, ili yote yaliyoandikwa yatimie.
23 Malheur aux femmes qui seront enceintes et à celles qui allaiteront en ces jours-là! car il y aura sur la terre une calamité immense et une colère contre ce peuple;
Ole wao waja wazito na wanyonyeshao siku hizo! Kwa maana kutakuwa na dhiki kubwa katika nchi, na hasira ya Mungu itawajia watu hawa.
24 les hommes tomberont sous le tranchant du glaive, ils seront emmenés captifs dans toutes les nations, Jérusalem sera foulée aux pieds par les païens, jusqu'à ce que les temps des païens soient aussi accomplis.»
Wengine watauawa kwa upanga, wengine watachukuliwa mateka katika nchi zote; na mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa mataifa mengine, hadi nyakati zao zitakapotimia.
25 «Il y aura des prodiges dans le soleil, dans la lune et dans les étoiles; il y en aura sur la terre: angoisse des peuples jetés dans l'incertitude par le mugissement de la mer et des flots;
“Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari.
26 des hommes expirant de terreur dans l'attente de ce qui va arriver au monde, car les puissances des cieux seront ébranlées.
Watu watazirai kwa sababu ya uoga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
27 Et c'est alors qu'on verra le Fils de l'homme arrivant, au sein d'une nuée, en puissance et grande gloire.
Halafu, watamwona Mwana wa Mtu akija katika wingu, mwenye nguvu na utukufu mwingi.
28 Quand ces choses commenceront à arriver, regardez en haut, levez la tête, parce qu'approchera votre délivrance.»
Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia.”
29 Il se servit d'une comparaison: «Voyez le figuier, et tous les arbres.
Kisha akawaambia mfano: “Angalieni mtini na miti mingine yote.
30 Dès qu'ils commencent à pousser, vous savez de vous-mêmes, en les voyant, que l'été est proche.
Mnapoona kwamba imeanza kuchipua majani, mwatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
31 De même quand vous verrez arriver ces choses sachez que le royaume de Dieu est proche.
Vivyo hivyo, mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
32 En vérité, je vous le dis, cette génération ne passera pas que tout cela n'arrive.
Nawaambieni hakika, kizazi hiki cha sasa hakitapita kabla ya hayo yote kutendeka.
33 Le ciel et la terre passeront, mais mes paroles ne passeront point.»
Mbingu na dunia vitapita, lakini maneno yangu hayatapita.
34 «Veillez sur vous-mêmes, de peur que vos coeurs ne s'appesantissent dans la bonne chère, dans les excès de boisson, dans les soucis de ce monde, et que ce jour-là ne vous surprenne inopinément.
“Muwe macho, mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na shughuli za maisha haya. La sivyo, Siku ile itawajieni ghafla.
35 Car il surviendra comme un filet sur tous ceux qui habitent la surface de la terre.
Kwa maana itawajia kama mtego, wote wanaoishi duniani pote.
36 Soyez donc vigilants en tout temps, et priez afin que vous soyez rendus dignes d'échapper à toutes ces choses qui vont arriver et de subsister en présence du Fils de l'homme.»
Muwe waangalifu basi, na salini daima ili muweze kupata nguvu ya kupita salama katika mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Mtu.”
37 Le jour, il restait au Temple et y enseignait. Mais il allait passer les nuits hors de la ville sur la montagne appelée «Bois d'Oliviers»,
Wakati wa mchana, siku hizo, Yesu alikuwa akifundisha watu Hekaluni; lakini usiku alikuwa akienda katika mlima wa Mizeituni na kukaa huko.
38 et tout le peuple, de grand matin, venait au Temple pour l'entendre.
Watu wote walikuwa wanakwenda Hekaluni asubuhi na mapema, wapate kumsikiliza.