< Luc 18 >

1 Il leur raconta une parabole pour leur montrer qu'il faut prier toujours, et ne point se lasser:
Basi, Yesu aliwasimulia mfano kuonyesha kwamba ni lazima kusali daima bila kukata tamaa.
2 «Dans une certaine ville, dit-il, il y avait un juge qui n'avait ni crainte de Dieu, ni égards pour les hommes.
Alisema: “Katika mji mmoja kulikuwa na hakimu ambaye hakuwa anamcha Mungu wala kumjali binadamu.
3 Or, dans cette même ville, il y avait une veuve qui venait à lui et lui disait: «Fais-moi justice de mon adversaire.»
Katika mji huohuo, kulikuwa pia na mama mmoja mjane, ambaye alimwendea huyo hakimu mara nyingi akimwomba amtetee apate haki yake kutoka kwa adui yake.
4 Pendant longtemps, il ne le voulut pas.» «Enfin il se dit à lui-même: «Bien que je n'aie ni crainte de Dieu, ni égards pour les hommes,
Kwa muda mrefu huyo hakimu hakupenda kumtetea huyo mjane; lakini, mwishowe akajisemea: Ingawa mimi simchi Mungu wala simjali binadamu,
5 comme il est certain que cette veuve-là m'est à charge, je lui ferai justice, de peur qu'elle ne finisse par se livrer à quelque violence.»
lakini kwa vile huyu mjane ananisumbua, nitamtetea; la sivyo ataendelea kufika hapa, na mwisho atanichosha kabisa!”
6 Vous entendez, ajouta le Seigneur, ce que dit ce juge inique.
Basi, Bwana akaendelea kusema, “Sikieni jinsi alivyosema huyo hakimu mbaya.
7 Et Dieu ne ferait point justice à ses élus qui crient à lui nuit et jour? Il tarderait à les secourir?
Je, ndio kusema Mungu hatawatetea wale aliowachagua, ambao wanamlilia mchana na usiku? Je, atakawia kuwasikiliza?
8 Il leur fera prompte justice, je vous le déclare; mais le Fils de l'homme, à son retour, trouvera-t-il la foi sur la terre?»
Nawaambieni atawatetea upesi. Hata hivyo, je, kutakuwako na imani duniani wakati Mwana wa Mtu atakapokuja?”
9 Il raconta aussi la parabole suivante à quelques-uns très convaincus, à part eux, qu'ils étaient justes, et qui méprisaient les autres:
Halafu Yesu aliwaambia pia mfano wa wale ambao walijiona kuwa wema na kuwadharau wengine.
10 «Deux hommes montèrent au Temple pour prier; l'un Pharisien et l'autre publicain.
“Watu wawili walipanda kwenda Hekaluni kusali: mmoja Mfarisayo, na mwingine mtoza ushuru.
11 Le Pharisien, debout, priait ainsi en lui-même: «O Dieu, je te rends grâces de ce que je ne suis pas comme le reste des hommes, gens rapaces, iniques, adultères, de ce que je ne suis pas comme ce publicain-là.
Huyo Mfarisayo akasimama, akasali kimoyomoyo: Ee Mungu, nakushukuru kwa vile mimi si kama watu wengine: walafi, wadanganyifu au wazinzi. Nakushukuru kwamba mimi si kama huyu mtoza ushuru.
12 Je jeûne deux fois par semaine; je donne la dîme de tout ce que j'acquiers.»
Nafunga mara mbili kwa juma, natoa zaka sehemu ya kumi ya pato langu.
13 Quant au publicain, il se tenait à distance, il n'osait pas même lever les yeux vers le ciel, mais il se frappait la poitrine en disant: «Dieu, aie pitié de moi qui suis un pécheur!»
Lakini yule mtoza ushuru, akiwa amesimama kwa mbali bila hata kuinua macho yake mbinguni, ila tu akijipiga kifua kwa huzuni, alisema: Ee Mungu, unionee huruma mimi mwenye dhambi.
14 Celui-ci, je vous le déclare, rentra dans sa maison justifié, plutôt que l'autre; car quiconque s'élève lui-même sera abaissé, et quiconque s'abaisse lui-même sera élevé.»
Nawaambieni, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amesamehewa. Lakini yule mwingine, sivyo. Kwa maana kila anayejikweza atashushwa, na kila anayejishusha atakwezwa.”
15 On lui apportait même les tout petits enfants pour qu'il les touchât. Voyant cela, les disciples blâmèrent ceux qui les lui apportaient.
Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono yake. Wanafunzi walipowaona, wakawazuia kwa maneno makali.
16 Mais Jésus appela ces enfants: «Laissez, leur dit-il, les enfants venir à moi, et ne les en empêchez pas, car c'est à ceux qui leur ressemblent qu'appartient le Royaume de Dieu.
Lakini Yesu akawaita kwake akisema: “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu kama hawa.
17 En vérité, je vous le dis, qui ne recevra pas, comme un enfant, le Royaume de Dieu, n'y entrera pas.»
Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hataingia katika Ufalme huo.”
18 Un chef de synagogue lui posa une question: «Bon maître, lui dit-il, que dois-je faire pour acquérir la vie éternelle?» (aiōnios g166)
Kiongozi mmoja, Myahudi, alimwuliza Yesu, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niweze kuupata uzima wa milele?” (aiōnios g166)
19 Jésus lui dit: «Pourquoi m'appelles-tu bon? Nul n'est bon que Dieu seul!
Yesu akamwambia, “Mbona waniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
20 Tu connais les commandements: «Tu ne seras point adultère; tu ne seras point meurtrier; tu ne seras point voleur; tu ne rendras point de faux témoignages; honore ton père et ta mère.»
Unazijua amri: Usizini; usiue; usiibe; usitoe ushahidi wa uongo; waheshimu baba yako na mama yako.”
21 Il répondit: «Tout cela je l'ai observé dès ma jeunesse.»
Yeye akasema, “Hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu.”
22 Sur cette réponse, Jésus reprit: «Une chose te manque encore; vends tout ce que tu as; distribues-en le prix à des pauvres; tu auras alors un trésor dans les cieux; viens ensuite et suis-moi.»
Yesu aliposikia hayo akamwambia, “Unatakiwa bado kufanya kitu kimoja: uza kila ulicho nacho, wagawie maskini, na hivyo utakuwa na hazina yako mbinguni; halafu njoo unifuate.”
23 A ces mots, l'autre devint tout triste, car il était fort riche.
Lakini huyo mtu aliposikia hayo, alihuzunika sana kwa sababu alikuwa tajiri sana.
24 Voyant sa tristesse, Jésus dit: «Combien difficilement entreront dans le Royaume de Dieu ceux qui ont des richesses!
Yesu alipoona akihuzunika hivyo, akasema, “Jinsi gani ilivyo vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!
25 Il est plus facile à un chameau de passer par l'ouverture d'une aiguille qu'à un riche d'entrer dans le Royaume de Dieu.»
Naam, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
26 «Qui donc pourra être sauvé?» dirent-ils en l'entendant.
Wale watu waliposikia hayo, wakasema, “Nani basi, atakayeokolewa?”
27 Jésus répondit: «Ce qui est impossible aux hommes, est possible à Dieu.» —
Yesu akajibu, “Yasiyowezekana kwa binadamu, yanawezekana kwa Mungu.”
28 «Et nous, dit Pierre, c'est après avoir laissé tous nos biens, que nous t'avons suivi!»
Naye Petro akamwuliza, “Na sisi je? Tumeacha vitu vyote tukakufuata!”
29 Il leur répondit: «Je vous le dis en vérité: personne, à cause du Royaume de Dieu, ne quittera une maison, une femme, des frères, des parents, des enfants,
Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, mtu yeyote aliyeacha nyumba au mke au kaka au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,
30 qu'il ne reçoive dès le temps présent bien davantage, et dans le siècle à venir la vie éternelle.» (aiōn g165, aiōnios g166)
atapokea mengi zaidi wakati huu wa sasa, na kupokea uzima wa milele wakati ujao.” (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Prenant à part les douze, il leur dit: «Voilà que nous montons à Jérusalem et tout ce que les prophètes ont écrit du Fils de l'homme va s'accomplir:
Yesu aliwachukua kando wale kumi na wawili, akawaambia, “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu na huko kila kitu kilichoandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Mtu kitakamilishwa.
32 il sera livré aux païens, bafoué, outragé, couvert de crachats;
Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.
33 après l'avoir flagellé, ils le tueront, et le troisième jour il ressuscitera.»
Watampiga mijeledi, watamuua; lakini siku ya tatu atafufuka.”
34 A cela les disciples ne comprirent rien; le sens de ces paroles leur était caché; ils ne saisissaient pas ce qui leur était dit.
Lakini wao hawakuelewa hata kidogo jambo hilo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.
35 Il approchait de Jéricho. Un aveugle, assis au bord du chemin, mendiait.
Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.
36 Entendant le bruit d'une foule en marche, il demanda ce que c'était.
Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, “Kuna nini?”
37 On lui répondit: «C'est Jésus de Nazareth qui passe.»
Wakamwambia, “Yesu wa Nazareti anapita.”
38 Alors il s'écria: «Jésus, Fils de David, aie pitié de moi!»
Naye akapaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
39 Ceux qui étaient en avant le menaçaient pour le faire taire, mais lui n'en criait que plus fort: «Fils de David, aie pitié de moi!»
Wale watu waliotangulia wakamkemea wakimwambia anyamaze; lakini yeye akazidi kupaza sauti: “Mwana wa Daudi, nihurumie;”
40 Jésus s'arrêta et donna l'ordre de le lui amener. Quand l'homme fut près de lui, il lui demanda:
Yesu alisimama, akaamuru wamlete mbele yake. Yule kipofu alipofika karibu, Yesu akamwuliza,
41 «Que veux-tu que je fasse pour toi?» — «Seigneur, que j'y voie!» répondit l'aveugle.
“Unataka nikufanyie nini?” Naye akamjibu, “Bwana, naomba nipate kuona tena.”
42 Alors Jésus lui dit: «Vois! ta foi t'a sauvé!»
Yesu akamwambia, “Ona! Imani yako imekuponya.”
43 Immédiatement il vit, et il suivit Jésus en glorifiant Dieu. Tout le peuple, à ce spectacle, célébra les louanges de Dieu.
Na mara yule aliyekuwa kipofu akapata kuona, akamfuata Yesu akimtukuza Mungu. Watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.

< Luc 18 >