< Luc 10 >
1 Le Seigneur, après cela, désigna encore soixante et dix autres disciples, et il leur donna mission de le précéder deux par deux dans toute ville, dans tout endroit où lui-même devait aller.
Baada ya mambo hayo, Bwana akachagua sabini wengine, na kuwatuma wawili wawili wamtangulie katika kila mji na eneo alilotarajia kwenda.
2 Il leur disait: «La moisson est grande et les ouvriers en petit nombre; priez donc le maître de la moisson d'envoyer des ouvriers dans sa moisson.»
Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache. Hivyo basi muombeni Bwana wa mavuno, ili kwamba atume haraka wafanyakazi katika mavuno yake.
3 «Allez; voici que je vous envoie comme des agneaux au milieu de loups.»
Enendeni katika miji. Angalieni, ninawatuma kama kondoo katikati ya mbwa mwitu.
4 «N'emportez ni bourse, ni sac, ni chaussures, et en chemin ne saluez personne.
Msibebe mfuko wa pesa, wala mikoba ya wasafiri, wala viatu, wala msimsalimie yeyote njiani.
5 Dans toute maison où vous entrerez que votre première parole soit: «Paix à cette maison!»
Katika nyumba yeyote mtakayo ingia, kwanza semeni, 'Amani iwe katika nyumba hii.'
6 Et s'il s'y trouve quelque enfant de paix, sur lui reposera votre paix; sinon elle reviendra à vous.
kama mtu wa amani yupo pale, amani yenu itabaki juu yake, lakini kama sivyo, itarudi kwenu.
7 Demeurez dans cette maison-là, mangeant et buvant ce qui s'y trouvera, car l'ouvrier est digne de son salaire.» «Ne pérégrinez pas de maison en maison.»
Bakini katika nyumba hiyo, kuleni na mnywe watakachokitoa, kwa maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msihame kutoka nyumba hii kwenda nyingine.
8 «Dans toute ville où vous entrerez, et où l'on vous recevra, mangez ce qui vous sera offert;
Mji wowote muuingiao, na wakawapokea, kuleni chochote kitakachowekwa mbele yenu,
9 guérissez les malades qui sont dans la ville, et dites-leur: «Le Règne de Dieu s'est approché de vous.»
na ponyeni wagonjwa waliomo humo. Semeni kwao, 'Ufalme wa Mungu umekuja karibu yanu'
10 Dans toute ville où vous entrerez et où l'on ne vous recevra pas, sortez sur les places publiques et dites:
Lakini katika mji wowote mtakaoingia, na wasiwapokee, nendeni nje katika barabara na semeni,
11 «La poussière même de votre ville qui s'est attachée à nos pieds, nous la secouons pour vous la rendre; sachez cependant ceci: «Le Règne de Dieu approche!»
'Hata vumbi katika mji wenu lililonata miguu mwetu tunalikung'uta dhidi yenu! Lakini tambueni hili, Ufalme wa Mungu umekaribia.'
12 Je vous déclare qu'en ce jour-là! il y aura moins de rigueur pour Sodome que pour cette ville-là.
Ninawambieni kwamba siku ya hukumu itakuwa ni usitahamilivu zaidi kwa Sodoma kuliko mji huo.
13 Malheur à toi Chorazein, malheur à toi Bethsaïda, car, si les miracles faits au milieu de vous l'avaient été dans Tyr et dans Sidon, elles se seraient depuis longtemps repenties en se revêtant d'un sac et assises dans la cendre.
Ole kwako Korazini, Ole kwako Bethsaida! Kama kazi kuu zilizo fanyika ndani yako ingalifanyika Tiro na Sidoni, Wangelitubu zamani sana, wakikaa ndani ya nguo za gunia na majivu.
14 Aussi y aura-t-il au jugement moins de rigueur pour Tyr et pour Sidon que pour vous.
Lakini itakuwa usitahamilivu zaidi siku ya hukumu kwa Tiro na Sidoni zaidi yenu.
15 Et toi, Capharnaüm, crois-tu que tu seras élevée jusqu'au ciel? Tu seras abaissée jusqu'à la Demeure-des-morts.» (Hadēs )
Wewe Kapernaumu, Unafikiri utainuliwa mpaka Mbinguni? Hapana, utashushwa chini mpaka kuzimu (Hadēs )
16 «Qui vous écoute, m'écoute; qui vous méprise, me méprise; or qui me méprise, méprise Celui qui m'a envoyé.»
Atakaye wasikiliza ninyi anisikiliza mimi, na yeyote atakaye wakataa anikataa mimi, na yeyote anikataaye mimi anmtakaa aliyenituma”
17 Les soixante-dix revinrent pleins de joie; ils disaient: «Seigneur, les démons mêmes se soumettent à nous en ton nom.»
Wale sabini walirudi kwa furaha, wakisema, “Bwana, hata mapepo wanatutii katika jina lako.”
18 Il leur répondit: «Je voyais Satan tomber du ciel comme un éclair!
Yesu akawaambia, “Nilimwona Shetani akianguka kutoka mbinguni kama radi.
19 Oui, je vous ai donné la puissance de fouler aux pieds et des serpents et des scorpions et toutes les forces de l'Ennemi, et aucun mal ne vous arrivera.
Tazama, nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za adui, na hapana chochote kwa njia yoyote kitakachowadhuru.
20 Toutefois ne vous réjouissez pas de ce que les Esprits vous sont soumis; réjouissez-vous de ce que vos noms sont écrits dans les cieux!»
Hata hivyo msifurahi tu katika hili, kwamba roho zinawatii, lakini furahini zaidi kwamba majina yenu yameandikwa mbinguni.”
21 En ce moment même, il dit dans un transport de joie venu de l’Esprit saint: «Je te bénis, ô Père, ô Seigneur du ciel et de la terre, de ce que tu as caché ces choses à des sages et à des savants, et de ce que tu les as révélées à de petits enfants. Oui, Père, je te bénis de ce que tel a été ton bon plaisir.
Katika mda uleule alifurahi sana katika Roho Mtakatifu, na kusema, “Ninakusifu wewe, Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa sababu umeyaficha mambo haya kutoka kwa wenye hekima na akili, na kuyafunua kwa wasio fundishwa, kama watoto wadogo. Ndio, Baba, kwa kuwa ilipendeza katika machoni pako.”
22 Tout m'a été confié par mon Père, et personne ne sait qui est le Fils excepté le Père, et qui est le Père excepté le Fils et celui à qui il plaît au Fils de le révéler.»
“Kila kitu kimekabidhiwa kwangu na Baba yangu, na hakuna afahamuye Mwana ni nani ila Baba, na hakuna afahamuye Baba ni nani ila Mwana, na ye yote ambaye Mwana hutamani kujifunua kwake.”
23 Puis, se tournant vers les disciples, il leur dit en particulier: «Heureux les yeux qui voient ce que vous voyez!
Akawageukia wanafunzi, akasema faraghani, “Wamebarikiwa wayaonayo haya ambayo ninyi mnayaona.
24 Je vous déclare, en effet, que nombre de prophètes et de rois ont voulu voir ce que vous, vous voyez, et ne l'ont pas vu, entendre ce que vous entendez, et ne l'ont pas entendu.»
Ninawambia ninyi, kwamba manabii wengi na wafalme walitamani kuona mambo myaonayo, na hawakuyaona, na kusikia kusikia mnayoyaikia, na hawakuyasikia.”
25 Voulant le mettre à l'épreuve, un légiste se leva et lui dit: «Maître, que dois-je faire pour acquérir la vie éternelle?» — (aiōnios )
Tazama, mwalimu fulani wa sheria ya Kiyahudi alisimama na kumjaribu, akisema, “Mwalimu, nifanye nini niurithi izima wa milele?” (aiōnios )
26 «Qu'y a-t-il d'écrit dans la Loi? lui demanda Jésus; qu'est-ce que tu y lis?»
Yesu akamwambia, “Kimeandikwa nini katika sheria? Unaisoma je?”
27 Le légiste lui fit cette réponse: «Tu aimeras le Seigneur ton Dieu de tout ton coeur, de toute ton âme, de toute ta force, de toute ta pensée et ton prochain comme toi-même.» —
Akajibu akasema, “Utampenda Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote, na jirani yako kama nafsi yako mwenyewe.”
28 «Parfaitement répondu! dit Jésus; fais cela et tu vivras.»
Yesu akasema, “Umejibu kwa usahihi. Fanya hivi na utaishi.”
29 Mais le légiste, voulant se justifier lui-même, dit à Jésus: «Qui donc est «mon prochain?»;
Lakini mwalimu, akitamani kujihesabia haki mwenyewe, Akamwambia Yesu, “Na jirani yangu ni nani?”
30 Jésus reprit alors: «Un homme descendait de Jérusalem à Jéricho; il tomba entre les mains de brigands qui le dépouillèrent et partirent, le laissant couvert de blessures et à moitié mort.
Yesu akijibu akasema, “Mtu fulani alikuwa akitelemka kutoka Yerusalem kwenda Yeriko. Akaangukia kati ya wanyang'anyi, waliomnyang'anya mali yake, na kumpiga na kumuacha karibu akiwa nusu mfu.
31 Or un prêtre descendait, par hasard, par la même route; il vit l'homme, et il passa outre.
Kwa bahati kuhani fulani alikuwa akishuka katika njia hiyo, alipo muona alipita upande mwingine.
32 Un Lévite fit de même; arrivé à l'endroit, il vit, et il passa outre.
Vivyo hivyo Mlawi pia, alipofika mahali pale na kumuona, akapita upande mwingine.
33 Mais un certain Samaritain, qui était en voyage, arriva près de l'homme et fut, en le voyant, touché de compassion;
Lakini Msamaria mmoja, alipokuwa akisafiri, alipita pale alipokuwa mtu huyo. alipomuona, alisukumwa kwa huruma.
34 il s'approcha de lui, il banda ses plaies après y avoir versé de l'huile et du vin, puis il le plaça sur sa propre monture, l'amena dans une hôtellerie, et lui donna des soins.
Alimkaribia na kumfunga vidonda vyake, akimwiga mafuta na divai juu yake. Alimpandisha juu ya mnyama wake, na kumpeleka katika nyumba ya wageni na kumhudumia.
35 Le lendemain, il tira deux deniers, les remit à l'hôtelier et lui dit: «Tu prendras soin de cet homme; et ce que tu dépenseras de plus, moi-même, à mon retour, je te le rembourserai.»
Siku ilyofuata alichukua dinari mbili, na akampatia mmiliki wa nyumba ya wageni na kumwambia, 'Muhudumie na chochote cha ziada utakacho tumia, nitakulipa nitakaporudi.'
36 Lequel de ces trois te paraît avoir été le prochain de celui qui était tombé entre les mains des brigands?» —
Ni yupi kati ya hawa watatu, unafikiri, alikuwa ni jirani kwake yeye aliyeangukia kati ya wanyang'anyi?”
37 «C'est celui qui a été compatissant envers lui», répondit le Légiste. Jésus lui dit alors: «Va et agis de même, toi aussi.»
Mwalimu alisema, “Ni yule aliyeonesha huruma kwake.” Yesu akamwambia, “Nenda na ukafanye vivyo hivyo”
38 Dans un village où Jésus entra pendant qu'ils étaient en route, ce fut une femme nommée Marthe qui le reçut dans sa maison.
Sasa walipokuwa wakisafiri, waliingia katika kijiji fulani, na mwanamke mmoja jina lake Martha alimkaribisha nyumbani kwake.
39 Elle avait une soeur appelée Marie, qui, assise aux pieds du Seigneur, écoutait sa parole.
Alikuwa na dada aliyeitwa Mariamu, aliekaa miguuni pa Bwana na kusikiliza neno lake.
40 Marthe cependant était absorbée par toutes sorte de soins; elle s'arrêta pour dire: «Seigneur, n'as-tu aucun souci de ce que ma soeur m'a laissée servir toute seule? dis-lui donc de m'aider.»
Lakini Martha alijipa shughuli nyingi za kuandaa mlo. Alikwenda kwa Yesu, na kusema, “Bwana, haujali kwamba dada yangu ameniacha nihudumu peke yangu? Hivyo basi mwambie anisaidie.”
41 Mais le Seigneur lui fit cette réponse: «Marthe, Marthe, tu t'inquiètes, tu te troubles pour une multitude de choses;
Lakini Bwana alimjibu na kumwambia, “Martha, Martha, una sumbuka juu ya mambo mengi,
42 une seule chose est nécessaire. Marie a choisi la bonne part qui ne lui sera point ôtée.»
lakini ni kitu kimoja tu cha muhimu. Mariamu amechagua kilicho chema, ambacho hakitaondolewa kutoka kwake.”