< Jean 8 >

1 (Quant à Jésus, il alla au mont des Oliviers.)
lakini Yesu akaenda kwenye mlima wa Mizeituni.
2 Au point du jour, il revint au Temple. Tout le peuple accourait à lui. Jésus s'était assis et enseignait,
Kesho yake asubuhi na mapema alikwenda tena Hekaluni. Watu wote wakamwendea, naye akaketi akawa anawafundisha.
3 lorsque les Scribes et les Pharisiens lui amenèrent une femme qu'on avait surprise en adultère et la placèrent au milieu de tout le monde.
Basi, walimu wa Sheria na Mafarisayo wakamletea mwanamke mmoja aliyefumaniwa katika uzinzi. Wakamsimamisha katikati yao.
4 «Maître, dirent-ils à Jésus, cette femme a été saisie en flagrant délit d'adultère.
Kisha wakamwuliza Yesu, “Mwalimu! Mwanamke huyu alifumaniwa katika uzinzi.
5 Or, dans la Loi, Moïse [nous] a ordonné de lapider ces femmes-là. Et toi, quel est ton avis?»
Katika Sheria yetu Mose alituamuru mwanamke kama huyu apigwe mawe. Basi, wewe wasemaje?”
6 Ils parlaient ainsi pour le mettre à l'épreuve et avoir un prétexte à accusation.] Quant à Jésus, il s'était baissé et il écrivait sur le sol avec son doigt.
Walisema hivyo kumjaribu, wapate kisa cha kumshtaki. Lakini Yesu akainama chini, akaandika ardhini kwa kidole.
7 Ceux qui l'interrogeaient ayant persisté, il se releva et [leur] dit: «Que celui d'entre vous qui est sans péché lui jette la pierre le premier.»
Walipozidi kumwuliza, Yesu akainuka, akawaambia, “Mtu asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza kumpiga jiwe.”
8 Puis se penchant de nouveau, il continua d'écrire sur le sol.
Kisha akainama tena, akawa anaandika ardhini.
9 Mais, en entendant cette réponse, ils sortirent un à un, à commencer par les plus âgés. Et [Jésus] resta seul avec la femme, toujours là, au milieu.
Waliposikia hivyo, wakaanza kutoweka mmojammoja, wakitanguliwa na wazee. Yesu akabaki peke yake, na yule mwanamke amesimama palepale.
10 Alors il se leva et lui dit: «Femme, où sont-ils [tes accusateurs]? Est-ce qu'aucun ne t'a condamnée?» — «Aucun. Seigneur», répondit-elle.
Yesu alipoinuka akamwuliza huyo mwanamke, “Wako wapi wale watu? Je, hakuna hata mmoja aliyekuhukumu?”
11 Jésus lui dit: «Moi non plus je ne te condamne pas. Va et [désormais] ne pèche plus!»)
Huyo mwanamke akamjibu, “Mheshimiwa, hakuna hata mmoja!” Naye Yesu akamwambia, “Wala mimi sikuhukumu. Nenda zako; na tangu sasa usitende dhambi tena.”
12 Jésus leur parla de nouveau disant: «Je suis la lumière du, monde. Qui me suit ne marchera pas dans les ténèbres; mais il aura la lumière de la vie.»
Yesu alipozungumza nao tena, aliwaambia, “Mimi ndimi mwanga wa ulimwengu. Anayenifuata mimi hatembei kamwe gizani, bali atakuwa na mwanga wa uzima.”
13 Alors les Pharisiens lui dirent: «C'est toi-même qui témoignes de toi-même, ton témoignage n'est pas valable.»
Basi, Mafarisayo wakamwambia, “Wewe unajishuhudia mwenyewe; kwa hiyo ushahidi wako si halali.”
14 Jésus leur répondit par ces paroles: «Bien que je sois à moi-même mon propre témoin, mon témoignage est valable, parce que je sais d'où je suis venu et où je vais. Vous, vous ne savez ni d'où je viens, ni où je vais.
Yesu akawajibu, “Hata kama ninajishuhudia mwenyewe, ushahidi wangu ni wa kweli kwa sababu mimi najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda.
15 Vous, vous jugez selon la chair, moi, je ne juge personne.
Ninyi mnahukumu kwa fikira za kibinadamu, lakini mimi simhukumu mtu.
16 Et s'il m'arrive de juger, mon jugement est véritable, parce que je ne suis pas seul, mais avec moi est le Père qui m'a envoyé,
Hata nikihukumu, hukumu yangu ni ya haki kwa sababu mimi siko peke yangu; Baba aliyenituma yuko pamoja nami.
17 et il est écrit dans votre Loi que le témoignage de deux personnes est valable.
Imeandikwa katika Sheria yenu ya kwamba ushahidi wa watu wawili ni halali.
18 Or il y a moi qui me rends témoignage à moi-même, et il y a le Père qui m'a envoyé, et qui, lui aussi, me rend témoignage.» —
Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma, ananishuhudia pia.”
19 «Ton père, lui disaient-ils alors, où est-il?» — «Vous ne connaissez ni moi, ni mon Père, répondit Jésus; si vous me connaissiez, vous connaîtriez également mon Père.»
Hapo wakamwuliza, “Baba yako yuko wapi?” Yesu akawajibu “Ninyi hamnijui mimi wala hamumjui Baba. Kama mngenijua mimi, mngemjua na Baba yangu pia.”
20 Il prononça ces paroles dans le Trésor, lorsqu'il enseignait au Temple. Personne ne l'arrêta, parce que son heure n'était pas encore venue.
Yesu alisema maneno hayo kwenye chumba cha hazina alipokuwa anafundisha Hekaluni. Wala hakuna mtu aliyemtia nguvuni, kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
21 Il leur dit encore: «Je m'en vais; vous me chercherez et vous, mourrez dans votre péché. Au lieu où je vais, vous ne pouvez venir.» —
Yesu akawaambia tena, “Naenda zangu nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi, ninyi hamwezi kufika.”
22 «Est-ce qu'il se donnera la mort; se demandaient les Juifs, puisqu'il dit: «Au lieu où je vais, vous ne pouvez venir!»
Basi, viongozi wa Wayahudi wakasema, “Je, atajiua? Mbona anasema: Niendako ninyi hamwezi kufika?”
23 Jésus reprit: «Vous, vous êtes d'en bas; moi, je suis d'en haut; Vous, vous êtes de ce monde; moi, je ne suis pas de ce monde.
Yesu akawaambia, “Ninyi mmetoka papa hapa chini, mimi nimetoka juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
24 Aussi vous ai-je dit que vous mourrez dans vos péchés; car si vous ne croyez pas que c'est moi vous mourrez dans vos péchés.»
Ndiyo maana niliwaambieni mtakufa katika dhambi zenu. Kama msipoamini kwamba Mimi ndimi, mtakufa katika dhambi zenu.”
25 «Qui donc es-tu?» demandèrent-ils. Jésus leur répondit: «Avant tout, je suis ce que je vous dis.
Nao wakamwuliza, “Wewe ni nani?” Yesu akawajibu, “Nimewaambieni tangu mwanzo!
26 J'ai, sur vous, beaucoup à dire, j'ai beaucoup à juger, mais Celui qui m'a envoyé est véridique, et ce que j'ai entendu auprès de lui, je le proclame dans le monde.»
Ninayo mengi ya kusema na kuhukumu juu yenu. Lakini yule aliyenituma ni kweli; nami nauambia ulimwengu mambo yale tu niliyoyasikia kutoka kwake.”
27 Comme ils ne comprenaient pas qu'il leur parlait du Père,
Hawakuelewa kwamba Yesu alikuwa akisema nao juu ya Baba.
28 il ajouta: «Quand vous aurez élevé le Fils de l'homme, alors vous reconnaîtrez que c'est moi vous reconnaîtrez que je ne fais rien de moi-même, mais que je parle d'après les enseignements du Père.
Basi, Yesu akawaambia, “Mtakapokwisha mwinua Mwana wa Mtu hapo ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi, na kwamba sifanyi chochote mimi mwenyewe, ila nasema tu yale Baba aliyonifundisha.
29 Celui qui m'a envoyé est avec moi; il ne m'a pas laissé seul, parce que je fais toujours ce qui lui est agréable.»
Yule aliyenituma yuko pamoja nami; yeye hakuniacha peke yangu kwani nafanya daima yale yanayompendeza.”
30 Pendant qu'il parlait ainsi, plusieurs crurent en lui.
Baada ya kusema hayo watu wengi walimwamini.
31 Or, à ces Juifs qui avaient eu foi en lui, Jésus disait: «Si vous demeurez dans ma parole, vous êtes véritablement mes disciples;
Basi, Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkiyazingatia mafundisho yangu mtakuwa kweli wanafunzi wangu.
32 vous connaîtrez la vérité et la vérité vous rendra libres.»
Mtaujua ukweli, nao ukweli utawapeni uhuru.”
33 Ils lui répliquèrent: «Nous sommes du sang d'Abraham et nous n'avons jamais été les esclaves de qui que ce soit. Comment dis-tu: «Vous deviendrez libres.»
Nao wakamjibu, “Sisi ni wazawa wa Abrahamu, na hatujapata kamwe kuwa watumwa wa mtu yeyote yule. Una maana gani unaposema: mtakuwa huru?”
34 Jésus leur répondit: «En vérité, en vérité, je vous le dis, quiconque commet le péché est l'esclave du péché;
Yesu akawajibu, “Kweli nawaambieni, kila mtu anayetenda dhambi ni mtumwa wa dhambi.
35 or ce n'est pas pour toujours que l'esclave demeure dans la maison, le Fils y demeure toujours; (aiōn g165)
Mtumwa hana makao ya kudumu nyumbani, lakini mwana anayo makao ya kudumu. (aiōn g165)
36 si donc le Fils vous affranchit, vous serez véritablement libres.
Kama mwana akiwapeni uhuru mtakuwa huru kweli.
37 Je sais que vous êtes de la descendance d'Abraham; mais, parce que ma parole n'a pas prise sur vous, vous cherchez à me faire périr.
Najua kwamba ninyi ni wazawa wa Abrahamu. Hata hivyo, mnataka kuniua kwa sababu hamuyakubali mafundisho yangu.
38 Ce que j'ai vu auprès du Père, moi, je le dis; ce que vous avez appris de votre père, vous, vous le faites.»
Mimi nasema yale aliyonionyesha Baba, lakini ninyi mwafanya yale aliyowaambieni baba yenu.”
39 Ils répondirent par ces paroles: «Notre père à nous, c'est Abraham.» «Si vous étiez enfants d'Abraham, leur dit Jésus, vous feriez les oeuvres d'Abraham;
Wao wakamjibu, “Baba yetu ni Abrahamu!” Yesu akawaambia, “Kama ninyi mngekuwa watoto wa Abrahamu, mngefanya kama alivyofanya Abrahamu,
40 au lieu de cela, vous cherchez à me mettre à mort, moi, un homme qui vous ai dit la vérité, que j'ai entendue auprès de Dieu. Cela, Abraham ne l'a pas fait.
Mimi nimewaambieni ukweli niliousikia kwa Mungu; hata hivyo, ninyi mwataka kuniua. Abrahamu hakufanya hivyo!
41 Vous, vous faites les oeuvres de votre père.» «Nous ne sommes pas le produit de quelque fornication, répliquèrent-ils, nous avons un seul Père: Dieu.»
Ninyi mnafanya mambo yaleyale aliyofanya babu yenu.” Wao wakamwambia, “Sisi si watoto haramu! Tunaye baba mmoja tu, yaani Mungu.”
42 «Si Dieu était votre Père, reprit Jésus, vous m'aimeriez! car de Dieu je suis sorti et je viens; ce n'est pas, en effet, de moi-même que je suis venu; mais c'est lui qui m'a envoyé.
Yesu akawaambia, “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda mimi, maana mimi nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
43 Pourquoi ne reconnaissez-vous pas mon langage? parce que vous ne pouvez entendre s ma parole.
Kwa nini hamwelewi hayo ninayosema? Ni kwa kuwa hamwezi kuusikiliza ujumbe wangu.
44 Vous avez le diable pour père, et c'est aux convoitises de votre père que vous voulez obéir. Dès le commencement, celui-là fut homicide, et il ne se tient pas dans la vérité, parce qu'il n'y a point de vérité en lui. Quand il profère le mensonge, il parle de son propre fond, étant menteur et père du mensonge.
Ninyi ni watoto wa baba yenu Ibilisi na mnataka tu kutekeleza tamaa za baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo; hana msimamo katika ukweli, kwani ukweli haumo ndani yake. Kila asemapo uongo, husema kutokana na hali yake ya maumbile, maana yeye ni mwongo na baba wa uongo.
45 Quant à moi, c'est parce que je dis la vérité que vous ne me croyez pas.
Mimi nasema ukweli, na ndiyo maana ninyi hamniamini.
46 Qui de vous me convaincra de péché? Si je dis la vérité, pourquoi ne me croyez-vous pas?
Nani kati yenu awezaye kuthibitisha kuwa mimi nina dhambi? Ikiwa basi nasema ukweli, kwa nini hamniamini?
47 Celui qui est de Dieu, entend les paroles de Dieu. Voici pourquoi vous, vous n'entendez pas: c'est que vous n'êtes pas de Dieu.»
Aliye wa Mungu husikiliza maneno ya Mungu. Lakini ninyi hamsikilizi kwa sababu ninyi si (watu wa) Mungu.”
48 Les Juifs lui répondirent par ces paroles: «N'avons-nous pas raison de dire que tu es un Samaritain et un possédé du démon?»
Wayahudi wakamwambia, “Je, hatukusema kweli kwamba wewe ni Msamaria, na tena una pepo?”
49 «Je ne suis pas un possédé du démon, répliqua Jésus, mais j'honore mon Père, et vous, vous me déshonorez.
Yesu akajibu, “Mimi sina pepo; mimi namheshimu Baba yangu, lakini ninyi hamniheshimu.
50 Pour moi, je ne cherche pas ma gloire; il est quelqu'un qui la cherche et qui juge.
Mimi sijitafutii utukufu wangu mwenyewe; yuko mmoja mwenye kuutafuta utukufu huo, naye ni hakimu.
51 En vérité, en vérité, je vous le dis, si quelqu'un garde ma parole, il ne verra jamais la mort.» (aiōn g165)
Kweli nawaambieni, anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele.” (aiōn g165)
52 Nous sommes maintenant convaincus, lui dirent les Juifs, que tu es possédé du démon. Abraham est mort ainsi que les prophètes, et toi, tu dis: «Si quelqu'un garde ma parole, il ne goûtera jamais la mort.» (aiōn g165)
Basi, Wayahudi wakasema, “Sasa tunajua kweli kwamba wewe ni mwendawazimu! Abrahamu alikufa, na manabii pia walikufa, nawe wasema ati, Anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele! (aiōn g165)
53 Es-tu plus grand que notre père Abraham qui est mort? que les prophètes, qui sont morts? Qui prétends-tu être?»
Je, unajifanya mkuu zaidi kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa? Hata na manabii walikufa. Wewe unajifanya kuwa nani?”
54 Jésus répondit: «Si je me glorifie moi-même, ma gloire n'est rien. C'est mon Père qui me glorifie, mon Père dont vous dites qu'il est votre Dieu
Yesu akawajibu, “Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu. Baba yangu ambaye ninyi mwasema ni Baba yenu, ndiye anayenitukuza.
55 et que vous ne connaissez pas; pour moi, je le connais entièrement. Et si je disais que je ne le connais pas entièrement, je serais comme vous, un menteur; mais je le connais entièrement et je garde sa parole.
Ninyi hamjapata kumjua, lakini mimi namjua. Na, nikisema simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi. Mimi namjua na ninashika neno lake.
56 Abraham votre père a tressailli de joie dans l'espoir de voir mon jour; il l'a vu et il a été dans la joie.»
Abrahamu, baba yenu, alishangilia aione siku yangu; naye aliiona, akafurahi.”
57 «Tu n'as pas encore cinquante ans, repartirent les Juifs, et tu as vu Abraham!»
Basi, Wayahudi wakamwambia, “Wewe hujatimiza miaka hamsini bado, nawe umemwona Abrahamu?”
58 Jésus leur dit: «En vérité, en vérité, je vous le dis, avant qu'Abraham fût, moi, je suis.»
Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, kabla Abrahamu hajazaliwa, mimi niko.”
59 Alors ils prirent des pierres pour les lui jeter; mais Jésus se cacha et sortit du Temple.
Hapo wakaokota mawe ili wamtupie, lakini Yesu akajificha, akatoka Hekaluni.

< Jean 8 >