< Jean 7 >

1 Jésus, après ces choses, parcourait la Galilée, ne voulant pas, voyager en Judée, où les Juifs cherchaient à le faire périr.
Baada ya hayo, Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea mkoani Yudea kwa sababu viongozi wa Wayahudi walikuwa wanataka kumwua.
2 La fête juive dite des Tabernacles approchait cependant,
Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
3 et ses frères lui dirent: «Pars de ce pays-ci, transporte-toi en Judée, afin que les disciples que tu y comptes voient, eux aussi, les oeuvres que tu accomplis.
Basi ndugu zake wakamwambia, “Ondoka hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wazione kazi unazozifanya.
4 On n'agit pas en cachette quand on veut se faire connaître; si réellement tu fais ces choses, manifeste-toi toi-même au monde!»
Mtu hafanyi mambo kwa siri kama anataka kujulikana kwa watu. Maadam unafanya mambo haya, basi, jidhihirishe kwa ulimwengu.”
5 (En effet, ses frères non plus ne croyaient pas en lui.)
(Hata ndugu zake hawakumwamini!)
6 Jésus leur répondit: «Mon temps, à moi, n'est pas encore venu;
Basi, Yesu akawaambia, “Wakati wangu ufaao haujafika bado. Lakini kwenu ninyi kila wakati unafaa.
7 pour vous, que le monde ne peut haïr, le moment est toujours opportun; mais le monde me hait, moi, parce que je rends de lui le témoignage que ses oeuvres sont mauvaises.
Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini mimi wanichukia kwa sababu mimi nauambia wazi kwamba matendo yake ni maovu.
8 Rendez vous à la fête; quant à moi, je ne vais pas à cette fête, parce que mon temps n'est pas encore accompli.»
Ninyi nendeni kwenye sikukuu hiyo. Mimi siendi kwenye sikukuu hiyo, maana saa yangu ifaayo haijafika.”
9 Cela dit, il demeura en Galilée.
Alisema hayo kisha akabaki huko Galilaya.
10 Puis, lorsque ses frères furent partis pour la fête, lui-même s'y rendit aussi, mais ce n'était pas d'une façon ostensible, c'était comme en cachettes.
Baada ya ndugu zake kwenda kwenye sikukuu, Yesu naye alikwenda, lakini hakuenda kwa hadhara bali kwa siri.
11 Pendant la fête, cependant, les Juifs s'informaient de lui: «Où donc est-il», demandait-on.
Viongozi wa Wayahudi walikuwa wanamtafuta kwenye sikukuu hiyo; Wakauliza: “Yuko wapi?”
12 Dans la foule, une quantité de bruits couraient sur lui: «C'est un homme de bien», disaient ceux-ci. «Nullement, c'est tout le contraire», disaient ceux-là, «il égare la foule»;
Kulikuwa na minong'ono mingi katika umati wa watu. Baadhi yao walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “La! Anawapotosha watu.”
13 mais personne, par crainte des Juifs, n'osait s'exprimer tout haut sur son compte.
Hata hivyo hakuna mtu aliyethubutu kusema, habari zake hadharani kwa kuwaogopa viongozi wa Wayahudi.
14 On était déjà au milieu de la fête, lorsque Jésus monta au Temple;
Sikukuu hiyo ilipofikia katikati, Yesu naye alikwenda Hekaluni, akaanza kufundisha.
15 il se mit à enseigner au grand étonnement des Juifs. «Comment, disaient-ils, cet homme est-il si instruit, lui qui n'a pas étudié?»
Basi, Wayahudi wakashangaa na kusema “Mtu huyu amepataje elimu naye hakusoma shuleni?”
16 Jésus leur répondit par ces paroles: «Mon enseignement n'est pas de moi s, mais de Celui qui m'a envoyé.
Hapo Yesu akawajibu, “Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
17 Si quelqu'un veut faire sa volonté, il saura si mon enseignement est de Dieu s ou si je parle de mon chef.
Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe.
18 L'homme qui parle de son chef poursuit sa gloire propre; mais l'homme qui poursuit la gloire de celui qui l'a envoyé, est véridique, lui, et il n'y a en lui aucun manque de droiture.
Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
19 N'est-ce pas Moïse qui vous a donné la Loi? Et aucun de vous ne la met en pratique! Pourquoi cherchez-vous à me tuer?»
Je, Mose hakuwapeni Sheria? Hata hivyo, hakuna hata mmoja wenu anayeishika Sheria. Kwa nini mnataka kuniua?”
20 La foule répondit: «Tu es possédé d'un démon; qui est-ce qui, cherche à te tuer?»
Hapo watu wakamjibu, “Una wazimu wewe! Nani anataka kukuua?”
21 Jésus répliqua par ces paroles: «Une seule oeuvre accomplie par moi, vous a tous surpris.
Yesu akawajibu, “Kuna jambo moja nililofanya, nanyi mnalistaajabia.
22 Moïse vous a donné la circoncision (elle n'a pas été instituée par Moïse, elle vient des patriarches), cette circoncision vous la pratiquez le jour du sabbat.
Mose aliwapeni ile desturi ya kutahiri. (Si kwamba desturi hiyo ilitoka kwa Mose, bali ilitoka kwa mababu). Sasa ninyi humtahiri mtu hata siku ya Sabato.
23 Eh bien, si on peut, pour ne pas violer la loi de Moïse, pratiquer la circoncision le jour du sabbat, pourquoi vous irriter contre moi pour avoir, ce même jour de sabbat, rendu un homme entièrement sain?
Ikiwa basi, mtu hutahiriwa hata siku ya Sabato kusudi Sheria ya Mose isivunjwe, mbona mnanikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya Sabato?
24 Ne jugez pas sur l'apparence; jugez au contraire suivant la justice.»
Msihukumu mambo kwa nje tu; toeni hukumu ya haki.”
25 Parmi les habitants de Jérusalem quelques-uns disaient: «N'est-ce point cet homme que l'on cherche à faire périr?
Baadhi ya watu wa Yerusalemu walisema, “Je, yule mtu wanayemtafuta wamuue si huyu?
26 Le voici qui parle en toute liberté, et on ne lui dit rien! Les autorités auraient-elles vraiment reconnu qu'il est le Christ?
Tazameni sasa! Anawaonya hadharani, wala hakuna mtu anayemwambia hata neno. Je, yawezekana kuwa viongozi wametambua kweli kwamba huyu ndiye Kristo?
27 Nous savons pourtant d'où est celui-ci; or quand le Christ vient, personne ne sait d'où il est.»
Kristo atakapokuja hakuna mtu atakayejua mahali alikotoka, lakini sisi tunajua alikotoka mtu huyu!”
28 Alors Jésus, qui enseignait dans le Temple, s'écria: «Vous me connaissez! vous savez d'où je suis! mais je ne suis pas venu de moi-même. Il y en a un qui réellement m'a envoyé, et Celui-là vous ne le connaissez pas!
Basi, Yesu alipokuwa anafundisha Hekaluni alipaaza sauti na kusema, “Ati mnanijua; hata nilikotoka mnakujua! Hata hivyo, sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe; ila yeye aliyenituma mimi ni wa kweli, nanyi hamumjui.
29 Moi je le connais, parce que je viens de lui et que c'est lui qui m'a envoyé.»
Lakini mimi namjua kwa sababu nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma.”
30 Là-dessus, ils cherchèrent à l'arrêter; personne toutefois ne porta la main sur lui, parce que son heure n'était pas encore venue.
Basi, watu wakataka kumtia nguvuni, lakini hakuna mtu aliyethubutu kumkamata kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
31 Dans la foule un grand nombre crurent en lui. «Lorsque le Christ viendra, disaient-ils, fera-t-il plus de miracles que n'en a fait cet homme-là?»
Wengi katika ule umati wa watu walimwamini, wakasema, “Je, Kristo akija atafanya ishara kubwa zaidi kuliko alizozifanya huyu?”
32 Les Pharisiens entendirent ces rumeurs de la foule; aussi, de concert avec les chefs des prêtres, envoyèrent-ils des agents pour l'arrêter.
Mafarisayo waliwasikia watu wakinong'ona maneno hayo juu ya Yesu. Basi, wao pamoja na makuhani wakuu wakawatuma walinzi wamtie nguvuni.
33 Jésus dit alors: «Je suis encore avec vous pour un peu de temps; après quoi je retourne à Celui qui m'a envoyé.
Yesu akasema, “Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma.
34 Vous me chercherez et vous ne me trouverez pas et, au lieu où je suis, vous ne pouvez venir.»
Mtanitafuta lakini hamtaniona, maana pale nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika.”
35 Les Juifs se demandaient entre eux: «Où donc va-t-il aller, que nous ne le trouverons pas? Va-t-il aller chez les disséminés, parmi les païens et instruire les païens?
Viongozi wa Wayahudi wakasema wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi ambapo hatutaweza kumpata? Atakwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki, na kuwafundisha Wagiriki?
36 Qu'est-ce que ce mot qu'il a prononcé: «vous me chercherez et vous ne me trouverez pas; et au lieu où je suis vous ne pouvez venir.»
Ana maana gani anaposema: Mtanitafuta lakini hamtanipata, na mahali nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika?”
37 Durant le dernier jour de la fête, qui en est le plus solennel, Jésus, se tenant debout, s'écria: «Si quelqu'un a soif, qu'il vienne à moi et qu'il boive!
Siku ya mwisho ya sikukuu hiyo ilikuwa siku maalum. Yesu alisimama, akasema kwa sauti kubwa, “Aliye na kiu na aje kwangu anywe.
38 Comme dit l'Écriture: «Du sein de celui qui croit en moi jailliront des fleuves d'eau vives. »
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: Anayeniamini mimi, mito ya maji yenye uzima itatiririka kutoka moyoni mwake!”
39 Il disait cela de l'Esprit que devaient recevoir ceux qui avaient cru en lui. En effet, il n'y avait pas encore d'Esprit, parce que Jésus n'était pas encore glorifié.
(Alisema hayo kumhusu Roho ambaye wale waliomwamini yeye watampokea. Wakati huo Roho alikuwa hajafika kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.)
40 Dans la multitude, ceux qui avaient entendu ces paroles disaient: «C'est vraiment le prophète!»
Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, “Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!”
41 d'autres: «C'est le Christ!» d'autres encore:
Wengine wakasema, “Huyu ndiye Kristo!” Lakini wengine walisema, “Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya?
42 «Est-ce que le Christ doit sortir de la Gaulée? Est-ce que l'Écriture ne dit pas que le Christ sortira de la famille de David et du village de Bethléem d'où était David?»
Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!”
43 On était donc dans le peuple fort divisé à son sujet.
Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu.
44 Un certain nombre d'entre eux voulaient l'arrêter; mais aucun ne porta la main sur lui.
Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata.
45 Les agents retournèrent auprès des chefs des prêtres et des Pharisiens. «Pourquoi ne l'avez-vous pas amené!» demandèrent ceux-ci.»
Kisha wale walinzi wakarudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo; nao wakawauliza, “Kwa nini hamkumleta?”
46 A quoi les agents répondirent: «Jamais homme n'a parlé comme parle cet homme.» -
Walinzi wakawajibu, “Hakuna mtu aliyepata kamwe kusema kama asemavyo mtu huyu!”
47 «Vous êtes-vous aussi laissé séduire?» leur dirent les Pharisiens.
Mafarisayo wakawauliza, “Je, nanyi pia mmedanganyika?
48 «Est-ce qu'il y a un seul personnage ayant autorité qui ait cru en lui? Est-ce qu'il y a un seul Pharisien?
Je, mmekwisha mwona hata mmoja wa viongozi wa watu, au mmoja wa Mafarisayo aliyemwamini?
49 Il n'y a que cette maudite populace qui n'entend rien à la Loi!»
Lakini umati huu haujui Sheria ya Mose; umelaaniwa!”
50 Nicodème, un des leurs, celui qui était venu à Jésus tout d'abord, leur dit:
Mmoja wao alikuwa Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu. Basi, yeye akawaambia,
51 «Est-ce que notre Loi juge un homme sans qu'il soit entendu et sans qu'on se soit rendu compte de ses actes?»
“Je, Sheria yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza na kujua anafanya nini?”
52 Ils lui répondirent ainsi: «Serais-tu, toi aussi, de la Galilée? informe-toi, et tu verras que de la Galilée ne surgit pas de prophète.»
Nao wakamjibu, “Je, wewe pia umetoka Galilaya? Haya, kayachunguze Maandiko Matakatifu nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki kamwe nabii!”
53 (Après quoi, chacun d’eux retourna à sa maison.)
Basi, wote wakaondoka, kila mtu akaenda zake;

< Jean 7 >