< Jean 21 >

1 Après cela, sur le bord de la mer de Tibériade, Jésus se manifesta encore aux disciples. Voici comment:
Baada ya hayo Yesu aliwatokea tena wanafunzi wake kando ya ziwa Tiberia. Aliwatokea hivi:
2 Simon Pierre, Thomas appelé Didyme, Nathanaël de Cana en Galilée, les fils de Zébédée et deux autres disciples étaient ensemble.
Simoni Petro, Thoma (aitwaye Pacha), na Nathanieli mwenyeji wa Kana Galilaya, wana wawili wa Zebedayo na wanafunzi wake wengine wawili, walikuwa wote pamoja.
3 «Je vais pêcher», leur dit Simon Pierre. «Nous y allons avec toi» répondirent les autres. Ils partirent et montèrent dans la barque. Cette nuit-là ils ne prirent rien.
Simoni Petro aliwaambia, “Nakwenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Nasi tutafuatana nawe.” Basi, wakaenda, wakapanda mashua, lakini usiku huo hawakupata chochote.
4 Le matin venu, Jésus était là debout sur le rivage. Les disciples cependant ne savaient pas que c'était Jésus.
Kulipoanza kupambazuka, Yesu alisimama kando ya ziwa, lakini wanafunzi hawakujua kwamba alikuwa yeye.
5 «Enfants, leur dit-il, n'avez-vous rien à manger?» — Ils lui répondirent: «Non.» —
Basi, Yesu akawauliza, “Vijana, hamjapata samaki wowote sio?” Wao wakamjibu, “La! Hatujapata kitu.”
6 «Jetez le filet, dit Jésus, à droite de la barque, vous trouverez.» Ils le jetèrent et ils n'avaient plus la force de le retirer tellement il était plein de poissons.
Yesu akawaambia, “Tupeni wavu upande wa kulia wa mashua nanyi mtapata samaki.” Basi, wakatupa wavu lakini sasa hawakuweza kuuvuta tena kwa wingi wa samaki.
7 Alors le disciple que Jésus aimait dit à Pierre: «C'est le Seigneur!» A cette parole: «C'est le Seigneur», Simon Pierre qui n'était pas vêtu remit sa tunique et se jeta à l'eau.
Hapo yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, “Ni Bwana!” Simoni Petro aliposikia ya kuwa ni Bwana, akajifunga vazi lake (maana hakuwa amelivaa), akarukia majini.
8 Quant aux autres disciples ils vinrent avec la barque, et comme ils étaient peu éloignés de terre, — environ de deux cents coudées, — ils traînaient le filet plein de poissons.
Lakini wale wanafunzi wengine walikuja pwani kwa mashua huku wanauvuta wavu uliojaa samaki; hawakuwa mbali na nchi kavu, ila walikuwa yapata mita mia moja kutoka ukingoni.
9 Une fois descendus à terre, ils voient du charbon préparé, du, poisson dessus et du pain.
Walipofika nchi kavu waliona moto wa makaa umewashwa na juu yake pamewekwa samaki na mkate.
10 Jésus leur dit: «Apportez quelques-uns des poissons que vous venez de prendre.»
Yesu akawaambia, “Leteni hapa baadhi ya samaki mliovua.”
11 Simon Pierre monta alors dans la barque et tira à terre le filet. Il était plein de gros poissons; il y en avait cent cinquante-trois et malgré ce grand nombre le filet ne se déchira pas.
Basi, Simoni Petro akapanda mashuani, akavuta hadi nchi kavu ule wavu uliokuwa umejaa samaki wakubwa mia moja na hamsini na watatu. Na ingawa walikuwa wengi hivyo wavu haukukatika.
12 «Venez manger», dit Jésus aux disciples. Aucun d'eux n'osait lui poser cette question: «Qui es-tu?» Ils savaient que c'était le Seigneur.
Yesu akawaambia, “Njoni mkafungue kinywa.” Hakuna hata mmoja wao aliyethubutu kumwuliza: “Wewe ni nani?” Maana walijua alikuwa Bwana.
13 Jésus s'approche; prend le pain et le leur donne, ainsi que le poisson.
Yesu akaja, akatwaa mkate akawapa; akafanya vivyo hivyo na wale samaki.
14 C'était la troisième fois, depuis sa résurrection d'entre les morts, que Jésus se manifestait à ses disciples.
Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada ya kufufuka kutoka wafu.
15 Quand ils eurent mangé, Jésus dit à Simon Pierre: «Simon, fils de Jean, m'aimes-tu plus que ceux-ci?» —Il lui répondit: «Oui, Seigneur, tu sais que je t'aime.» Jésus lui dit: «Fais paître mes agneaux.»
Walipokwisha kula, Yesu alimwuliza Simoni Petro, “Simoni, mwana wa Yohane! Je, wanipenda mimi zaidi kuliko hawa?” Naye akajibu, “Naam, Bwana; wajua kwamba mimi nakupenda.” Yesu akamwambia, “Tunza wana kondoo wangu.”
16 Il lui dit une seconde fois: «Simon, fils de Jean, m'aimes-tu?» Il lui répondit: «Oui, Seigneur, tu sais que je t'aime.» Jésus lui dit: «Sois le pasteur de mes brebis.»
Kisha akamwambia mara ya pili, “Simoni mwana wa Yohane! Je, wanipenda?” Petro akamjibu, “Naam, Bwana; wajua kwamba nakupenda.” Yesu akamwambia, “Tunza kondoo wangu.”
17 Il lui dit pour la troisième fois: «Simon, fils de Jean, M'aimes-tu?» Pierre fut attristé de ce qu'il lui disait pour la troisième fois: «M'aimes-tu?» et lui répondit: «Seigneur, tu sais tout; tu sais que je t'aime. Jésus lui dit: «Fais paître mes brebis.
Akamwuliza mara ya tatu, “Simoni mwana wa Yohane! Je, wanipenda?” Hapo Petro akahuzunika kwa sababu alimwuliza mara ya tatu: “Wanipenda?” akamwambia, “Bwana, wewe wajua yote; wewe wajua kwamba mimi nakupenda.” Yesu akamwambia, “Tunza kondoo wangu!
18 En vérité, en vérité, je te le dis, lorsque tu étais plus jeune, tu te ceignais toi-même et tu allais où tu voulais; mais quand tu seras vieux, tu étendras les mains, un autre te ceindra, et te mènera où tu ne voudras pas.
Kweli nakwambia, ulipokuwa kijana ulizoea kujifunga mshipi na kwenda kokote ulikotaka. Lakini utakapokuwa mzee utanyosha mikono yako, na mtu mwingine atakufunga na kukupeleka usikopenda kwenda.”
19 (Il dit cela pour indiquer par quel genre de mort Pierre devait glorifier Dieu); et après avoir ainsi parlé, il ajouta: «Suis-moi.»
(Kwa kusema hivyo, alionyesha jinsi Petro atakavyokufa na kumtukuza Mungu.) Kisha akamwambia, “Nifuate.”
20 Pierre, se retournant, voit le suivre le disciple que Jésus aimait, celui qui, pendant le repas, s'était penché sur sa poitrine et lui avait dit: «Seigneur qui est celui qui te livrera?»
Hapo Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda, anafuata (Huyu mwanafunzi ndiye yule ambaye wakati wa chakula cha jioni, alikaa karibu sana na Yesu na kumwuliza: “Bwana ni nani atakayekusaliti?”)
21 Le voyant, Pierre dit à Jésus: «Seigneur, et celui-ci, que lui arrivera-t-il?»
Basi, Petro alipomwona huyo akamwuliza Yesu, “Bwana, na huyu je?”
22 Jésus lui répond: «Si je veux qu'il attende jusqu'à ce que je vienne, que t'importe? Toi, suis-moi.»
Yesu akamjibu, “Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, yakuhusu nini? Wewe nifuate mimi.”
23 Alors le bruit se répandit parmi les frères que ce disciple-là ne mourrait pas. Cependant Jésus n'a pas dit à Pierre: «Il ne mourra pas; » mais: «Si je veux qu'il attende jusqu'à ce que je vienne, que t'importe.»
Basi, habari hiyo ikaenea miongoni mwa wale ndugu kwamba mwanafunzi huyo hafi. Lakini Yesu hakumwambia kwamba mwanafunzi huyo hafi, ila, “Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, yakuhusu nini?”
24 C'est ce disciple-là même qui atteste ces choses et qui les a écrites, et nous savons que son témoignage est véridique.
Huyo ndiye yule aliyeshuhudia mambo haya na kuyaandika. Nasi twajua kwamba aliyoyasema ni kweli.
25 Il y a encore beaucoup d'autres choses que Jésus a faites. Si on les écrivait l'une après l'autre, je crois que le monde entier ne pourrait contenir les livres qu'on écrirait.
Kuna mambo mengine mengi aliyofanya Yesu, ambayo kama yangeandikwa yote, moja baada ya lingine, nadhani hata ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa.

< Jean 21 >