< Hébreux 3 >

1 En conséquence, mes saints frères, vous qui êtes appelés à aller au ciel, fixez les yeux sur l'apôtre et le grand-prêtre de la foi que nous professons,
Ndugu zangu watu wa Mungu ambao mmeitwa na Mungu, fikirini juu ya Yesu ambaye Mungu alimtuma awe Kuhani Mkuu wa imani tunayoiungama.
2 sur Jésus, qui était «fidèle» à celui qui l'avait institué, comme Moïse l'était dans toute sa maison ».
Yeye alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua kufanya kazi yake kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
3 - Mais Jésus a été jugé digne de surpasser Moïse en éclat de toute la distance qui sépare une maison de son constructeur.
Mjenzi wa nyumba hupata heshima zaidi kuliko hiyo nyumba yenyewe. Hali kadhalika naye Yesu anastahili heshima kubwa zaidi kuliko Mose.
4 (Toute maison a un architecte; Celui qui a tout construit c'est Dieu.)
Kila nyumba hujengwa na mjenzi fulani—na Mungu ndiye mjenzi wa vitu vyote.
5 Moïse, lui, a été fidèle «DANS toute sa maison, comme un serviteurs», par le témoignage qu'il a rendu à ce qui devait être révélé plus tard;
Mose alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Bwana kama mtumishi, na alinena juu ya mambo ambayo Mungu atayasema hapo baadaye.
6 Christ l'était comme un fils, «SUR sa maison»; et sa maison à lui c'est nous, si toutefois nous persistons fermement, jusqu'à la fin dans l'assurance et l'espérance qui font notre gloire.)
Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana mwenye mamlaka juu ya nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba yake kama tukizingatia uhodari wetu na uthabiti wetu katika kile tunachotumainia.
7 — Ainsi, comme le dit l'Esprit saint: «Si vous entendez aujourd'hui sa voix,
Kwa hiyo, basi, kama asemavyo Roho Mtakatifu: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo,
8 N'endurcissez pas vos coeurs, comme au jour de la révolte Et de la provocation dans le désert,
msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu; kama walivyokuwa siku ile kule jangwani,
9 Quand vos pères m'ont provoqué et m'ont mis à l'épreuve, Eux qui avaient vu mes oeuvres pendant quarante ans!
Huko wazee wenu walinijaribu na kunichunguza, asema Bwana, ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu kwa miaka arobaini.
10 Voilà pourquoi je me suis irrité contre cette génération Et j'ai dit: leurs coeurs s'égarent toujours. Ils n'ont point reconnu mes voies;
Kwa sababu hiyo niliwakasirikia watu hao nikasema, Fikira za watu hawa zimepotoka, hawajapata kamwe kuzijua njia zangu.
11 Et voici le serment que j'ai fait dans ma colère: Jamais ils n'entreront dans mon repos!»
Basi, nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko.”
12 Que personne de vous, mes frères, prenez-y garde, n'ait un mauvais coeur, ne soit incrédule, ne se sépare du Dieu vivant.
Basi ndugu, jihadharini asije akawako yeyote miongoni mwenu aliye na moyo mbaya hivyo na asiyeamini hata kujitenga na Mungu aliye hai.
13 Mais exhortez-vous les uns les autres, tous les jours, tant que l'on peut dire: «aujourd'hui», et qu'aucun de vous ne se laisse séduire et «endurcir» par le péché.
Maadamu hiyo “Leo” inayosemwa katika Maandiko bado inatuhusu sisi, mnapaswa kusaidiana daima, ili mtu yeyote miongoni mwenu asidanganywe na dhambi na kuwa mkaidi.
14 Car nous n'avons notre part du Christ que si nous gardons notre assurance première, fermement, jusqu'à la fin,
Maana sisi tunashirikiana na Kristo ikiwa tutazingatia kwa uthabiti tumaini tulilokuwa nalo mwanzoni.
15 aussi longtemps qu'on peut dire: «Si vous entendez aujourd'hui sa voix N'endurcissez pas vos coeurs, comme au jour de la révolte.»
Maandiko yasema hivi: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu.”
16 Lesquels, après avoir entendu, «se sont révoltés»? N'est-ce pas tous ceux que Moïse avait conduits hors d'Égypte?
Ni akina nani basi, waliosikia sauti ya Mungu wakamwasi? Ni wale wote walioongozwa na Mose kutoka Misri.
17 Et contre qui «Dieu s'irrita-t-il pendant quarante ans»? N'est-ce pas contre ceux qui péchaient et dont «les corps jonchaient le désert»?
Mungu aliwakasirikia akina nani kwa miaka arobaini? Aliwakasirikia wale waliotenda dhambi, maiti zao zikatapakaa kule jangwani.
18 Et à qui «jura-t-il qu'ils n'entreraient pas dans son repos?» N'est-ce pas à ceux qui désobéissaient?
Mungu alipoapa: “Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko,” alikuwa anawasema akina nani? Alikuwa anasema juu ya hao walioasi.
19 Nous voyons, en effet, que leur incrédulité les empêcha d'y entrer.
Basi, twaona kwamba hawakuingia huko kwa sababu hawakuamini.

< Hébreux 3 >