< Galates 2 >
1 Ensuite, quatorze années plus tard, je montai de nouveau à Jérusalem, avec Barnabas; je pris aussi Tite avec moi.
Baada ya miaka kumi na minne, nilikwenda tena Yerusalemu pamoja na Barnaba; nilimchukua pia Tito pamoja nami.
2 J'y montai sur une révélation; je leur communiquai l'Évangile tel que je le prêche aux païens. J'eus des entretiens particuliers avec les plus considérés d'entre eux, de peur que mes courses passées ou présentes ne fussent inutiles.
Kwenda kwangu kulitokana na ufunuo alionipa Mungu. Katika kikao cha faragha niliwaeleza hao viongozi ujumbe wa Habari Njema niliohubiri kwa watu wa mataifa. Nilifanya hivyo kusudi kazi yangu niliyokuwa nimefanya, na ile ninayofanya sasa isije ikawa bure.
3 Eh bien, on n'exigea pas même que Tite qui, m'accompagnait, et qui était Grec, se fit circoncire.
Lakini, hata mwenzangu Tito, ambaye ni Mgiriki, hakulazimika kutahiriwa,
4 Cependant, par égard pour les intrus, les faux frères qui s'étaient glissés parmi nous pour espionner la liberté dont nous jouissons grâce à Jésus-Christ et qui voudraient nous remettre en esclavage...
ingawa kulikuwa na ndugu wengine wa uongo waliotaka atahiriwe. Watu hawa walijiingiza kwa ujanja na kupeleleza uhuru wetu tulio nao katika kuungana na Kristo Yesu, ili wapate kutufanya watumwa.
5 Nous ne leur avons pas cédé, nous ne nous sommes pas soumis un seul instant, afin que la vérité de l'Évangile fût maintenue pour vous.
Hatukukubaliana nao hata kidogo ili ukweli wa Habari Njema ubaki nanyi daima.
6 Quant à ceux que l'on considérait comme des personnages (ce qu'ils étaient jadis peu m'importe, Dieu ne fait pas acception de personnes)... ceux, dis-je, qui étaient considérés comme des personnages ne m'apprirent rien de plus.
Lakini watu hawa wanaosemekana kuwa ni viongozi—kama kweli walikuwa hivyo au sivyo, kwangu si kitu, maana Mungu hahukumu kwa kuangalia mambo ya nje—watu hawa hawakuwa na kitu cha kuongeza katika Habari hii Njema kama niihubirivyo.
7 Au contraire, voyant que l'évangélisation des non-circoncis m'était confiée, comme l'était à Pierre celle des circoncis
Badala yake, walitambua kwamba Mungu alikuwa amenituma kuhubiri Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kama vile Petro alivyokuwa ametumwa kuihubiri kwa Wayahudi.
8 (car Celui qui a donné à Pierre la force d'être apôtre des circoncis m'a donné aussi à moi la force d'être apôtre des païens),
Maana, yule aliyemwezesha Petro kuwa mtume kwa Wayahudi, ndiye aliyeniwezesha nami pia kuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine.
9 connaissant, dis-je, la grâce qui m'avait été accordée, Jacques, Képhas et Jean, qui passaient pour les colonnes de l'Église, nous donnèrent la main, à Barnabas et à moi, en signe d'union, afin que nous fussions, pour les païens, ce qu'ils étaient pour les circoncis.
Basi, Yakobo, Kefa na Yohane, ambao waonekana kuwa viongozi wakuu, walitambua kwamba Mungu alinijalia neema hiyo, wakatushika sisi mkono, yaani Barnaba na mimi, iwe ishara ya ushirikiano. Sisi ilitupasa tukafanye kazi kati ya watu wa mataifa mengine, na wao kati ya Wayahudi.
10 Ils nous prièrent seulement de nous souvenir des pauvres; aussi me suis-je empressé de le faire.
Wakatuomba lakini kitu kimoja: tuwakumbuke maskini; jambo ambalo nimekuwa nikijitahidi kutekeleza.
11 Quand Képhas vint à Antioche, je lui résistai en face, parce qu’il avait évidemment tort.
Lakini Kefa alipofika Antiokia nilimpinga waziwazi maana alikuwa amekosea.
12 En effet, avant l'arrivée de certains individus, envoyés par Jacques, il mangeait avec les païens; après leur arrivée, il se tint à l'écart, il s'isola, parce qu'il avait peur des partisans de la circoncision. Les autres Juifs firent les hypocrites avec lui,
Awali, kabla ya watu kadhaa waliokuwa wametumwa na Yakobo kuwasili hapo, Petro alikuwa akila pamoja na watu wa mataifa mengine. Lakini, baada ya hao watu kufika, aliacha kabisa kula pamoja na watu wa mataifa mengine, kwa kuogopa kikundi cha waliosisitiza tohara.
13 si bien que Barnabas lui-même fut entraîné dans cette hypocrisie.
Hata ndugu wengine Wayahudi walimuunga mkono Petro katika kitendo hiki cha unafiki, naye Barnaba akakumbwa na huo unafiki wao.
14 Alors, quand je vis qu'ils ne marchaient pas dans le droit chemin de la vérité de l'Évangile, je dis à Képhas devant tout le monde: «Si toi qui es Juif, tu agis comme les païens et non comme les Juifs, comment peux-tu obliger les païens à faire comme les Juifs?
Basi, nilipoona kuwa msimamo wao kuhusu ukweli wa Habari Njema haukuwa umenyooka, nikamwambia Kefa mbele ya watu wote: “Ingawa wewe ni Myahudi, unaishi kama watu wa mataifa mengine na si kama Myahudi! Unawezaje, basi kujaribu kuwalazimisha watu wa mataifa mengine kuishi kama Wayahudi?”
15 Nous autres, nous sommes Juifs de naissance; nous ne sommes pas des pécheurs comme tous ces païens...»
Kweli, sisi kwa asili ni Wayahudi, na si watu wa mataifa mengine hao wenye dhambi!
16 Sachant cependant que l'homme n'est pas justifié par les oeuvres de la Loi, mais qu'il l'est uniquement par la foi en Jésus-Christ. nous avons cru en Jésus-Christ pour être justifiés par cette foi. Ce n'est pas par les oeuvres de la Loi, parce que les oeuvres de la Loi Ne justifient aucune créatures.»
Lakini, tunajua kwa hakika kwamba mtu hawezi kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa kuitii Sheria, bali tu kwa kumwamini Yesu Kristo. Na sisi pia tumemwamini Yesu Kristo ili tupate kukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani yetu kwa Kristo, na si kwa kuitii Sheria.
17 S'il se trouve alors que nous, qui cherchons notre justification en Christ, nous sommes aussi des pécheurs, Christ aura été (ce qu'à Dieu ne plaise) un ministre de péché!
Sasa, ikiwa katika kutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu kwa kuungana na Kristo sisi tunaonekana kuwa wenye dhambi, je, jambo hili lina maana kwamba Kristo anasaidia utendaji wa dhambi? Hata kidogo!
18 Si je rebâtis ce que j'avais abattu, je me constitue moi-même prévaricateur!
Lakini ikiwa ninajenga tena kile nilichokwisha bomoa, basi nahakikisha kwamba mimi ni mhalifu.
19 Pour moi, c'est par égard pour la Loi que je suis mort à la Loi, afin de vivre à Dieu.
Maana, kuhusu Sheria hiyo, mimi nimekufa; Sheria yenyewe iliniua, nipate kuishi kwa ajili ya Mungu. Mimi nimeuawa pamoja na Kristo msalabani,
20 J'ai été crucifié avec Christ; je ne vis plus, c'est Christ qui vit en moi. Le reste de vie que je traîne en la chair, je le vis dans la foi au Fils de Dieu a qui m'a aimé et s'est livré pour moi.
na sasa naishi, lakini si mimi tena, bali Kristo anaishi ndani yangu. Maisha haya ninayoishi sasa naishi kwa imani, imani katika Mwana wa Mungu aliyenipenda hata akayatoa maisha yake kwa ajili yangu.
21 Je ne veux pas anéantir la grâce de Dieu, et si la justice s'obtient par la Loi, alors Christ est mort pour rien!
Sipendi kuikataa neema ya Mungu. Kama mtu huweza kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa njia ya Sheria, basi, Kristo alikufa bure!