< Éphésiens 6 >
1 Vous, enfants, obéissez à vos parents selon le Seigneur; c'est justice:
Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.
2 «Respecte ton père et ta mère.» Voilà un commandement capital à cause de cette promesse:
“Waheshimu Baba na mama yako,” hii ndiyo amri ya kwanza ambayo imeongezewa ahadi, yaani,
3 «afin d'être heureux et de vivre longtemps sur la terre.»
“Upate fanaka na miaka mingi duniani.”
4 Et vous, qui êtes pères, n'irritez pas vos enfants, mais élevez-les en les instruisant et les avertissant selon le Seigneur.
Nanyi akina baba, msiwachukize watoto wenu ila waleeni katika nidhamu na mafundisho ya Kikristo.
5 Vous, qui êtes esclaves, obéissez à ceux qui sont vos maîtres sur la terre, dans la crainte, dans l'humilité, dans la droiture de votre coeur, comme au Christ,
Enyi watumwa, watiini mabwana zenu hapa duniani kwa hofu na tetemeko; fanyeni hivyo kwa unyofu wa moyo kana kwamba mnamtumikia Kristo.
6 et non pas seulement quand ils ont l'oeil sur vous, comme si vous n'aviez à satisfaire que des hommes, mais, esclaves de Christ, faites la volonté de Dieu de toute votre âme.
Fanyeni hivyo si tu wakati wanapowatazama ili mjipendekeze kwao, bali tumikieni kwa moyo kama atakavyo Mungu kwa sababu ninyi ni watumishi wa Kristo.
7 Servez-les avec affection, comme s'il s'agissait du Seigneur et non pas d'hommes,
Muwe radhi kutumikia kwa ajili ya Bwana na si kwa ajili ya watu.
8 et sachez, que chacun sera récompensé par le Seigneur selon le bien qu'il aura fait, qu'il soit esclave ou qu'il soit libre.
Kumbukeni kwamba kila mtu mwenye kutenda mema, awe mtumwa au mtu huru, atapokea tuzo lake kutoka kwa Bwana.
9 Et vous, maîtres, agissez de même envers eux, laissez là les menaces, car vous savez que leur maître et le vôtre est dans les cieux, et qu'il n'a pas égard à la condition des personnes.
Nanyi mnaotumikiwa, watendeeni vivyo hivyo watumwa wenu, na acheni kutumia vitisho. Kumbukeni kwamba ninyi pia kama vile wao, mnaye Bwana yuleyule mbinguni, kwake cheo cha mtu si kitu.
10 Enfin, cherchez votre force dans le Seigneur, dans sa vertu, dans sa puissance.
Hatimaye, nawatakeni muwe imara katika kuungana na Bwana na kwa msaada wa nguvu yake kuu.
11 Revêtez l'armure de Dieu afin de pouvoir résister aux manoeuvres du Diable.
Vaeni silaha anazowapeni Mungu mpate kuzipinga mbinu mbaya za Ibilisi.
12 Car nous avons à combattre, non contre des adversaires de chair et de sang, mais contre les chefs, les souverains, les dominateurs de ce monde de ténèbres, contre les mauvais Esprits des régions célestes. (aiōn )
Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu huu wa giza. (aiōn )
13 Prenez donc l'armure de Dieu afin de pouvoir résister dans les mauvais jours et rester debout après avoir triomphé de tout.
Kwa sababu hiyo, vaeni silaha za Mungu ili siku ile itakapofika muweze kuyapinga mashambulio ya adui; na mkisha pigana mpaka mwisho, muwe bado thabiti.
14 Tenez ferme; «Que la vérité soit la ceinture de vos reins.» «Que la justice soit votre cuirasse.»
Basi, simameni imara! Ukweli uwe kama ukanda kiunoni mwenu, uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani,
15 «Que vos pieds aient pour chaussures la préparation à suivre Évangile de paix. »
na hamu ya kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.
16 Par-dessus tout, prenez le bouclier de la foi; avec lui vous pourrez éteindre tous les traits enflammés du Malin.
Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.
17 Saisissez aussi «le casque du salut» et «l'épée de l'Esprit», c'est-à-dire la Parole de Dieu.
Upokeeni wokovu kama kofia yenu ya chuma, na neno la Mungu kama upanga mnaopewa na Roho Mtakatifu.
18 Priez Dieu ardemment, suppliez-le en toute occasion et par l'Esprit. Montrez là de la vigilance, beaucoup de persévérance; priez pour tous les fidèles,
Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.
19 ainsi que pour moi; qu'il me soit donné, quand j'ouvre la bouche, de parler courageusement, de faire connaître le mystère de l'Évangile
Niombeeni nami pia ili niongeapo Mungu anijalie cha kusema, niweze kuwajulisha watu fumbo la Habari Njema kwa uthabiti.
20 (moi, son ambassadeur, et qui suis aux fers); oui, que j'en parle avec assurance, comme je le dois.
Mimi ni balozi kwa ajili ya Habari Njema hiyo ingawa sasa niko kifungoni. Ombeni, basi, ili niweze kuwa hodari katika kuitangaza kama inipasavyo.
21 Pour que vous sachiez, vous aussi, où j'en suis et ce que je fais, le bien-aimé frère Tychique, un fidèle ministre du Seigneur, vous dira tout.
Tukiko, ndugu yetu mpenzi na mtumishi mwaminifu wa Bwana, atawapeni habari zangu zote mpate kujua ninachofanya.
22 Je vous l'envoie dans ce but; vous saurez par lui où nous en sommes, et il consolera vos coeurs.
Namtuma kwenu awapeni habari zetu mpate kuwa na moyo.
23 La paix soit avec les frères, et l'amour, uni à la foi, accordé par Dieu notre Père et par le Seigneur Jésus-Christ.
Ninawatakieni ninyi ndugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
24 La grâce soit avec tous ceux qui aiment notre Seigneur Jésus-Christ d'une manière inaltérable.
Nawatakia neema ya Mungu wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa mapendo yasiyo na mwisho.