< Actes 3 >
1 Pierre et Jean montaient un jour au Temple pour la prière de la neuvième heure;
Siku moja, saa tisa alasiri, Petro na Yohane walikuwa wanakwenda Hekaluni, wakati wa sala.
2 or, il y avait un homme estropié de naissance que, tous les jours, on apportait et on déposait à la porte du Temple dite «La Belle», pour demander l'aumône à ceux qui entraient.
Na pale karibu na mlango wa Hekalu uitwao “Mlango Mzuri”, palikuwa na mtu mmoja, kiwete tangu kuzaliwa. Watu walimbeba huyo mtu kila siku na kumweka hapo ili aombe chochote kwa wale waliokuwa wakiingia Hekaluni.
3 Voyant Pierre et Jean qui allaient pénétrer dans le Temple, il s'adressa à eux pour recevoir une aumône.
Alipowaona Petro na Yohane wakiingia Hekaluni, aliwaomba wampe chochote.
4 Pierre arrêta sur lui son regard, ainsi que Jean: «Regarde-nous, lui dit-il.»
Petro na Yohane walimkodolea macho, naye Petro akamwambia, “Tutazame!”
5 Lui les fixait attentivement, s'attendant à recevoir quelque chose.
Naye akawageukia, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
6 Mais Pierre continua: «Je n'ai ni argent ni or, mais ce que j'ai, je te le donne; au nom de Jésus-Christ de Nazareth, marche!»
Kisha Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu lakini kile nilicho nacho nitakupa. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!”
7 En même temps il lui prenait la main droite et le levait; immédiatement ses pieds et ses chevilles devinrent fermes;
Halafu, akamshika mkono wa kulia, akamwinua. Papo hapo miguu na magoti yake yakapata nguvu.
8 d'un saut il se mit debout; il marchait! et il entra avec eux dans le Temple, marchant, sautant et louant Dieu.
Akaruka, akasimama na kuanza kutembea. Halafu akaingia pamoja nao Hekaluni, akitembea na kurukaruka huku akimtukuza Mungu.
9 Tout le peuple le vit marcher et louer Dieu,
Watu wote waliokuwa hapo walimwona akitembea na kumsifu Mungu.
10 chacun le reconnaissait; c'était bien lui, l'homme qui demandait l'aumône assis à «La Belle Porte» du Temple; complète était la stupéfaction comme l'enthousiasme de ce qui lui était arrivé.
Walipomtambua kuwa ndiye yule aliyekuwa anaombaomba karibu na ule “Mlango Mzuri” wa Hekalu, wakashangaa mno hata wasiweze kuelewa yaliyompata.
11 Cet homme ne quittant pas Pierre et Jean, c'est vers eux, au portique dit de Salomon, qu'accourut tout le peuple, confondu de surprise.
Watu wote, wakiwa na mshangao mkubwa wakaanza kukimbilia mahali palipoitwa “Ukumbi wa Solomoni,” ambapo yule mtu alikuwa bado anaandamana na Petro na Yohane.
12 Voyant cela, Pierre s'adressa ainsi à la foule: «Hommes d'Israël, Pourquoi vous étonnez-vous de ce qui vient de se passer? Pourquoi nous regardez-vous avec cette insistance, comme si c'était nous, par nos propres forces ou par notre piété, qui avions fait, marcher cet homme?
Basi, Petro alipowaona watu hao akawaambia, “Wananchi wa Israeli, kwa nini mnashangazwa na jambo hili? Mbona mnatukodolea macho kana kwamba ni kwa nguvu zetu au utakatifu wetu sisi wenyewe tumemfanya mtu huyu aweze kutembea?
13 Le Dieu d'Abraham, d'Isaac et de Jacob, le Dieu de nos pères a glorifié son serviteur Jésus que vous, vous avez livré et que vous avez renié devant Pilate, et cela, quand lui, il voulait le relâcher!
Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Yesu mtumishi wake. Yeye ndiye yuleyule mliyemtia mikononi mwa wakuu na kumkataa mbele ya Pilato hata baada ya Pilato kuamua kumwacha huru.
14 Oui, vous avez renié le Saint et le Juste, et vous avez demandé la grâce d'un meurtrier,
Alikuwa mtakatifu na mwema; lakini ninyi mlimkataa, mkataka mtu mwingine aliyekuwa muuaji afunguliwe.
15 vous avez tué l'auteur de la vie, que Dieu a ressuscité d'entre les morts, et nous, nous sommes ses témoins.
Basi, mlimuua yule ambaye ni chanzo cha uzima. Lakini Mungu alimfufua, na sisi ni mashahidi wa tukio hilo.
16 C'est par la foi en son nom que ce nom a guéri l'homme que vous voyez et connaissez; la foi qui agit par lui a donné à cet homme, et en votre présence à tous, une guérison complète.»
Jina la Yesu na imani katika jina hilo ndivyo vilivyompa nguvu mtu huyu mnayemwona na kumfahamu. Imani kwa Yesu ndiyo iliyomponya kabisa mtu huyu kama mnavyoona nyote.
17 «Je sais d'ailleurs, frères, que vous avez fait tout cela dans votre ignorance et vos magistrats aussi.
“Sasa ndugu zangu, nafahamu kwamba ninyi na wakuu wenu mlitenda hayo kwa sababu ya kutojua kwenu.
18 Dieu a accompli de cette manière ce qu'il avait prédit d'avance par la bouche de tous les prophètes, savoir que son Christ devait souffrir.
Lakini ndivyo Mungu alivyotimiza yale aliyotangaza zamani kwa njia ya manabii wote, kwamba ilikuwa lazima Kristo wake ateseke.
19 Repentez-vous donc et convertissez-vous pour que vos péchés soient effacés et alors pourront venir de la part du Seigneur des temps de rafraîchissement,
Basi, tubuni mkamrudie Mungu ili afute dhambi zenu.
20 et il vous enverra celui qu'il vous a destiné, Jésus-Christ,
Fanyeni hivyo ili Bwana awape nyakati za kuburudika rohoni na kuwaletea yule Kristo aliyemteua ambaye ndiye Yesu.
21 que le ciel doit recevoir jusqu'à l'époque du rétablissement universel dont Dieu a parlé autrefois par la bouche de ses saints prophètes.» (aiōn )
Ni lazima yeye abaki huko mbinguni mpaka utakapofika wakati wa kurekebishwa vitu vyote, kama Mungu alivyosema kwa njia ya manabii wake watakatifu wa tangu zamani. (aiōn )
22 «D'une part, Moïse a dit: «Le Seigneur notre Dieu vous suscitera d'entre vos frères un prophète semblable à moi, vous l'écouterez dans tout ce qu'il vous dira,
Kwa maana Mose alisema, Bwana Mungu wenu atawapelekeeni nabii kama mimi kutoka kati yenu ninyi wenyewe.
23 et quiconque n'écoutera pas ce prophète, sera exterminé du milieu du peuple.»
Yeyote yule ambaye hatamsikiliza nabii huyo atatengwa mbali na watu wa Mungu na kuangamizwa.
24 D'autre part, tous les prophètes, depuis Samuel et ses successeurs, ont parlé et ont annoncé ces jours-là.
Manabii wote, kuanzia Samweli na wale waliomfuata, walitangaza habari za mambo haya ambayo yamekuwa yakitendeka siku hizi.
25 Vous êtes les fils des prophètes et les héritiers de l'alliance que Dieu, a conclue avec nos pères, disant à Abraham: «Toutes les familles de la terre seront bénies en ta postérité.»
Ahadi zile Mungu alizotoa kwa njia ya manabii ni kwa ajili yenu; na mnashiriki lile agano Mungu alilofanya na babu zenu, kama alivyomwambia Abrahamu: Kwa njia ya wazawa wako, jamaa zote za dunia zitabarikiwa.
26 Pour vous, les premiers, Dieu a suscité son serviteur et l'a envoyé vous bénir en détournant chacun de vous de ses iniquités.»
Basi, ilikuwa kwa ajili yenu kwanza kwamba Mungu alimfufua mtumishi wake, alimtuma awabariki kwa kumfanya kila mmoja wenu aachane kabisa na maovu yake.”