< Actes 19 >
1 Pendant qu'Apollos était à Corinthe, Paul, qui venait de parcourir les parties les plus élevées du pays, descendit à Éphèse et y trouva quelques disciples. Il leur demanda: «Avez-vous reçu l'Esprit saint, quand vous êtes devenus croyants?»
Wakati Apolo alipokuwa Korintho, Paulo alisafiri sehemu za bara, akafika Efeso ambako aliwakuta wanafunzi kadhaa.
2 — «Nous n'avons pas entendu parler d'un Esprit saint, » lui répondirent-ils.
Akauliza, “Je, mlipopata kuwa waumini mlipokea Roho Mtakatifu?” Nao wakamjibu, “La! Hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatujasikia.”
3 Il reprit alors: «Quel baptême avez-vous donc reçu?» — «Le baptême de Jean, » répliquèrent-ils.
Naye akasema, “Sasa mlipata ubatizo wa namna gani?” Wakamjibu, “Ubatizo wa Yohane.”
4 Mais Paul: «Jean a baptisé; c'était un baptême de repentance, et il disait au peuple de croire en celui qui devait venir après lui, c'est-à-dire en Jésus.»
Naye Paulo akasema, “Ubatizo wa Yohane ulikuwa wa kuonyesha kwamba watu wametubu. Yohane aliwaambia watu wamwamini yule ambaye alikuwa anakuja baada yake, yaani Yesu.”
5 Apprenant cela, ils furent baptisés au nom du Seigneur Jésus;
Baada ya kusikia hayo, walibatizwa kwa jina la Bwana Yesu.
6 Paul leur imposa les mains, et l'Esprit saint descendit sur eux; ils se mirent à parler en langues étrangères et à prophétiser.
Basi, Paulo akawawekea mikono, na Roho Mtakatifu akawashukia, wakaanza kusema lugha mbalimbali na kutangaza ujumbe wa Mungu.
7 Ils étaient douze en tout environ.
Wote jumla, walikuwa watu wapatao kumi na wawili.
8 Paul se rendit à la synagogue, et il y prêcha en toute franchise sur le Royaume de Dieu. Pendant trois mois il s'efforça, par ses discours, de convaincre les Juifs.
Kwa muda wa miezi mitatu Paulo alikuwa akienda katika sunagogi, akawa na majadiliano ya kuvutia sana juu ya Ufalme wa Mungu.
9 Mais quelques-uns restèrent endurcis, incrédules, et se mirent à décrier l'enseignement de Paul devant la foule; alors il se sépara d'eux, et tous les jours il réunit à part ses disciples dans un endroit qu'on appelait: «École de Tyrannus».
Lakini wengine walikuwa wakaidi, wakakataa kuamini, wakaanza kuongea vibaya hadharani juu ya Njia ya Bwana. Hapo Paulo alivunja uhusiano nao, akawachukua pembeni wale wanafunzi wake, akawa anazungumza nao kila siku katika jumba la masomo la Turano.
10 Cela dura deux ans, de sorte que tous les habitants de l'Asie, Juifs et Grecs, entendirent la parole du Seigneur.
Aliendelea kufanya hivyo kwa muda wa miaka miwili hata wakazi wote wa Asia, Wayahudi na watu wa mataifa mengine, wakaweza kusikia neno la Bwana.
11 Dieu faisait par les mains de Paul des miracles extraordinaires;
Mungu alifanya miujiza ya ajabu kwa mikono ya Paulo.
12 au point qu'on mettait sur les malades le linge ou les vêtements qu'il avait portés, et ils étaient guéris de leurs maladies et délivrés des mauvais Esprits.
Watu walikuwa wakichukua leso na nguo nyingine za kazi ambazo Paulo alikuwa amezitumia, wakazipeleka kwa wagonjwa, nao wakaponywa magonjwa yao; na wale waliokuwa na pepo wabaya wakatokwa na pepo hao.
13 Alors quelques exorcistes juifs ambulants essayèrent d'invoquer le nom du Seigneur Jésus sur ceux qui étaient au pouvoir des mauvais Esprits. Ils disaient: «Je vous adjure par ce Jésus que prêche Paul.»
Wayahudi kadhaa wenye kupunga pepo wabaya, walisafiri huko na huko, wakijaribu kulitumia jina la Bwana Yesu kwa wale waliokuwa wamepagawa na pepo wabaya. Walikuwa wakisema: “Ninawaamuru kwa jina la Yesu ambaye Paulo anamhubiri.”
14 (C'étaient les sept fils d'un archiprêtre juif, Skevas, qui faisaient cela.)
Watoto saba wa Skewa, Kuhani Mkuu wa Kiyahudi, walikuwa miongoni mwa hao waliokuwa wanafanya hivyo.
15 Mais le mauvais Esprit leur répondit: «Je connais Jésus, et je sais qui est Paul; et vous, qui êtes-vous?»
Lakini pepo mbaya aliwajibu, “Ninamfahamu Yesu, ninamjua pia Paulo, lakini ninyi ni nani?”
16 Et puis, sautant sur eux, l'homme qui était possédé du mauvais Esprit en terrassa deux et eut si bien le dessus qu'ils durent s'enfuir de la maison sans vêtements et tout blessés.
Kisha yule mtu aliyepagawa aliwarukia wote kwa kishindo, akawashinda nguvu. Na hao watoto wa Skewa wakakimbia kutoka ile nyumba wakiwa uchi na wamejaa majeraha.
17 Le fait fut connu de tous les Juifs et de tous les Grecs qui habitaient Éphèse, et tous furent frappés de stupeur; on magnifiait le nom du Seigneur Jésus.
Kila mtu huko Efeso, Myahudi na asiye Myahudi, alisikia juu ya tukio hilo. Wote waliingiwa na hofu, wakalitukuza jina la Bwana Yesu.
18 Plusieurs de ceux qui étaient devenus croyants venaient confesser et reconnaître leurs pratiques.
Waumini wengi walijitokeza wakakiri hadharani mambo waliyokuwa wametenda.
19 Ceux qui s'étaient livrés à la magie vinrent en foule, apportèrent leurs livres et les brûlèrent publiquement. On en estima la valeur; elle se trouva être de cinquante mille pièces d'argent.
Wengine waliokuwa wameshughulikia mambo ya uchawi hapo awali, walikusanya vitabu vyao, wakavichoma mbele ya wote. Walikisia gharama ya vitabu hivyo, wakaona yafikia vipande vya fedha elfu hamsini.
20 C'était ainsi que la parole du Seigneur gagnait en force et en autorité.
Kwa namna hiyo, neno la Bwana lilizidi kuenea na kuwa na nguvu zaidi.
21 Après ces événements, Paul forma le projet de se rendre à Jérusalem en traversant la Macédoine et l'Achaïe. — «Quand j'aurai fait cela, disait-il, il faudra aussi que je voie Rome.»
Baada ya mambo hayo, Paulo aliamua kwenda Yerusalemu kwa kupitia Makedonia na Akaya. Alisema, “Baada ya kufika huko, itanilazimu kuona Roma pia.”
22 Puis il envoya en Macédoine deux de ses aides, Timothée et Éraste, mais lui-même resta encore quelque temps en Asie.
Hivyo, aliwatuma wawili wa wasaidizi wake, Timotheo na Erasto, wamtangulie kwenda Makedonia, naye akabaki kwa muda huko Asia.
23 Ce fut vers cette époque que la diffusion de l'Évangile fut l'occasion de troubles assez sérieux.
Wakati huo ndipo kulipotokea ghasia kubwa huko Efeso kwa sababu ya hiyo Njia ya Bwana.
24 Un orfèvre, du nom de Démétrius, fabriquait des réductions en argent du Temple d'Artémis. Ses ouvriers trouvaient à ce travail un profit considérable.
Kulikuwa na mfua fedha mmoja aitwaye Demetrio, ambaye alikuwa na kazi ya kutengeneza sanamu za nyumba ya mungu wa kike aitwaye Artemi. Shughuli hiyo iliwapatia mafundi faida kubwa.
25 Il les réunit un jour, avec tous les ouvriers du même état, et leur dit: «Éphésiens, «Vous savez que cette industrie fait notre fortune,
Demetrio aliwakusanya hao wafanyakazi pamoja na wengine waliokuwa na kazi kama hiyo, akawaambia, “Wananchi, mnafahamu kwamba kipato chetu kinatokana na biashara hii.
26 et vous voyez et entendez dire que non seulement à Éphèse, mais dans presque toute l'Asie, ce Paul a gagné et entraîné une foule de gens, en disant que les dieux faits de main d'homme ne sont pas de vrais dieux.
Sasa, mnaweza kusikia na kujionea wenyewe mambo Paulo anayofanya, si tu hapa Efeso, ila pia kote katika Asia. Yeye amewashawishi na kuwageuza watu wakakubali kwamba miungu ile iliyotengenezwa na watu si miungu hata kidogo.
27 Ce ne sont pas seulement nos intérêts qui vont être en souffrance, c'est le Temple même de notre grande déesse Artémis qui ne compte plus pour rien, et bientôt il ne sera plus question de la majesté de celle que toute l'Asie, que le monde entier adore.
Hivyo iko hatari kwamba biashara yetu itakuwa na jina baya. Si hivyo tu, bali pia jambo hilo linaweza kuifanya nyumba ya mungu Artemi kuwa si kitu cha maana. Hatimaye sifa zake huyo ambaye Asia na dunia yote inamwabudu, zitakwisha.”
28 Ces paroles les rendirent furieux et ils se mirent à crier: «Vive la grande Artémis d'Éphèse!»
Waliposikia hayo, waliwaka hasira, wakaanza kupiga kelele: “Mkuu ni Artemi, wa Efeso!”
29 L'agitation gagna la ville entière. Toute la foule se porta au théâtre en y entraînant Caïus et Aristarque, les Macédoniens qui accompagnaient Paul.
Mji wote ukajaa ghasia. Wakawavamia Gayo na Aristarko, wenyeji wa Makedonia, ambao walikuwa wasafiri wenzake Paulo, wakakimbia nao mpaka kwenye ukumbi wa michezo.
30 Lui-même voulait se montrer au peuple, mais les disciples le retinrent.
Paulo mwenyewe alitaka kuukabili huo umati wa watu, lakini wale waumini walimzuia.
31 Il y eut même des Asiarques de ses amis qui le firent prier de ne pas se présenter au théâtre.
Maofisa wengine wa huo mkoa wa Asia, waliokuwa rafiki zake, walimtumia Paulo ujumbe wakimsihi asijihatarishe kwa kwenda kwenye ukumbi wa michezo.
32 Chacun criait de son côté; aussi l'assemblée était-elle très confuse et le plus grand nombre ne savait pas même pourquoi on s'était réuni.
Wakati huo, kila mtu alikuwa anapayuka; wengine hili na wengine lile, mpaka hata ule mkutano ukavurugika. Wengi hawakujua hata sababu ya kukutana kwao.
33 Enfin, on fit sortir de la foule un certain Alexandre que les Juifs voulaient mettre en avant. Cet Alexandre, ayant fait signe de la main, se préparait à prendre devant le peuple la défense des siens.
Kwa vile Wayahudi walimfanya Aleksanda ajitokeze mbele, baadhi ya watu katika ule umati walidhani kuwa ndiye. Basi, Aleksanda aliwaashiria watu kwa mkono akitaka kujitetea mbele ya ule umati wa watu.
34 Mais la foule s'aperçut qu'il était juif, et alors elle se mit à crier d'une seule voix pendant près de deux heures: «Vive la grande Artémis d'Éphèse!»
Lakini walipotambua kuwa yeye ni Myahudi, wote kwa sauti moja walipiga kelele: “Mkuu ni Artemi wa Efeso!” Wakaendelea kupayukapayuka hivyo kwa muda wa saa mbili.
35 Le chancelier de la ville parvint enfin à l'apaiser, et prononça ces paroles: Habitants d'Éphèse, «Quel homme au monde ignore que votre ville d'Éphèse ne soit la gardienne du Temple de la grande Artémis et de sa statue tombée du ciel?
Hatimaye karani wa mji alifaulu kuwanyamazisha, akawaambia, “Wananchi wa Efeso, kila mtu anajua kwamba mji huu wa Efeso ni mlinzi wa nyumba ya mungu Artemi na mlinzi wa ile sanamu iliyoanguka kutoka mbinguni.
36 Cela est incontestable; il faut donc que vous restiez calmes et ne fassiez rien avec précipitation.
Hakuna anayeweza kukana mambo haya. Hivyo basi, tulieni; msifanye chochote bila hadhari.
37 Vous avez amené là ces hommes, mais ils ne sont coupables ni de sacrilège ni de blasphème envers votre déesse.
Mmewaita watu hawa hapa ingawaje hawakuikufuru nyumba ya mungu wala kumtukana mungu wetu wa kike.
38 Si Démétrius et ses ouvriers ont à se plaindre de quelqu'un, il y a des tribunaux, il y a des proconsuls, qu'on se fasse assigner!
Kama, basi Demetrio na wafanyakazi wake wana mashtaka yao kuhusu watu hawa, yapo mahakama na wakuu wa mikoa; wanaweza kushtakiana huko.
39 S'il s'agit d'autres choses, on peut les examiner dans une assemblée légalement convoquée.
Kama mna matatizo mengine, yapelekeni katika kikao halali.
40 Autrement nous risquons d'être accusés de sédition pour ce qui s'est passé aujourd'hui, car nous n'avons aucune bonne raison à donner pour expliquer notre rassemblement.»
Kwa maana tungaliweza kushtakiwa kwa kusababisha ghasia kutokana na vituko vya leo. Ghasia hii haina msingi halali na hatungeweza kutoa sababu za kuridhisha za ghasia hiyo.”
41 Là-dessus, il congédia l'assemblée.
Baada ya kusema hayo aliuvunja mkutano.