< Actes 18 >
1 Après cela, Paul partit d'Athènes et vint à Corinthe.
Baada ya hayo, Paulo aliondoka Athene, akaenda Korintho.
2 Il y trouva un Juif nommé Aquilas, originaire du Pont, et récemment arrivé d'Italie avec sa femme Priscille, chassé de Rome comme tous les Juifs par un édit de Claude. Il se réunit à eux
Huko Korintho, alimkuta Myahudi mmoja aitwaye Akula, mzaliwa wa Ponto. Akula pamoja na mkewe aitwaye Priskila, walikuwa wamerudi kutoka Italia siku hizohizo kwa sababu Kaisari Klaudio alikuwa ameamuru Wayahudi wote waondoke Roma. Paulo alikwenda kuwaona,
3 et comme ils étaient du même métier que lui, il demeura chez eux pour y travailler. Ils étaient, de leur état, fabricants de tentes.
na kwa vile wao walikuwa mafundi wa kushona mahema kama alivyokuwa yeye, Paulo alikaa nao akafanya kazi.
4 Chaque sabbat il parlait à la synagogue, et il gagnait des Juifs et des Grecs.
Kila Sabato alifanya majadiliano katika sunagogi akijaribu kuwavuta Wayahudi na Wagiriki.
5 Quand Silas et Timothée arrivèrent de Macédoine, Paul se consacrait uniquement à la prédication, affirmant aux Juifs que Jésus était le Christ.
Baada ya Sila na Timotheo kuwasili kutoka Makedonia, Paulo alianza kutumia wakati wake wote kwa ajili ya kuhubiri, akawathibitishia Wayahudi kwamba Yesu ndiye Kristo.
6 Mais ceux-ci s'opposaient à lui et l'insultaient; alors, secouant sur eux la poussière de ses vêtements, il leur dit: «Que votre sang retombe sur votre tête! J'en suis innocent et désormais je m'adresserai aux païens.»
Walipompinga na kuanza kumtukana, aliyakung'uta mavazi yake mbele yao akisema, “Mkipotea ni shauri lenu wenyewe; mimi sina lawama yoyote juu ya jambo hilo. Na tangu sasa nitawaendea watu na mataifa mengine.”
7 Il sortit de la salle et se rendit chez un certain Titius Justus, homme «craignant Dieu», dont la maison était contiguë à la synagogue.
Basi, akatoka hapo akaenda kukaa nyumbani kwa mtu mmoja mcha Mungu aitwaye Tito Yusto. Nyumba yake Tito ilikuwa karibu na lile sunagogi.
8 Crispus, le chef de la synagogue, crut au Seigneur avec toute sa maison, et plusieurs des Corinthiens qui entendaient Paul devenaient croyants et se faisaient baptiser.
Lakini Krispo, mkuu wa sunagogi, alimwamini Bwana yeye pamoja na jamaa yake yote. Wakorintho wengi waliusikiliza ujumbe huo, wakaamini na kubatizwa.
9 Une nuit, le Seigneur dit à Paul dans une vision: «Sois sans crainte, parle au contraire, ne cesse de parler, car je suis avec toi;
Siku moja usiku, Bwana alimwambia Paulo katika maono: “Usiogope, endelea kuhubiri tu bila kufa moyo,
10 personne ne mettra la main sur toi pour te faire du mal, parce que j'ai un grand peuple dans cette ville.»
maana mimi niko pamoja nawe. Hakuna mtu atakayejaribu kukudhuru maana hapa mjini pana watu wengi walio upande wangu.”
11 Paul alors s'établit à Corinthe pendant un an et demi, et il y prêcha la parole de Dieu.
Basi, Paulo alikaa huko akifundisha neno la Mungu kati yao kwa muda wa mwaka mmoja na nusu.
12 Pendant le proconsulat de Gallion en Achaïe, les Juifs, tous d'accord, se soulevèrent contre Paul et l'amenèrent devant le tribunal:
Lakini wakati Galio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Akaya, Wayahudi walimvamia Paulo kwa pamoja na kumpeleka mahakamani.
13 «Cet homme, dirent-ils, excite les gens à rendre à Dieu un culte contraire à la Loi.»
Wakasema, “Tunamshtaki mtu huyu kwa sababu ya kuwashawishi watu wamwabudu Mungu kwa namna inayopingana na Sheria.”
14 Paul ouvrait la bouche pour répondre, quand Gallion, s'adressant aux Juifs: «S'il s'agissait de quelque crime ou de quelque méfait, leur dit-il, j'accueillerais vos plaintes comme il convient, ô Juifs!
Kabla tu Paulo hajaanza kusema, Galio aliwaambia Wayahudi, “Sikilizeni enyi Wayahudi! Kama kweli jambo hili lingekuwa juu ya uhalifu au uovu ningekuwa tayari kuwasikilizeni.
15 mais s'il s'agit de vos discussions sur une doctrine, sur des noms propres, sur votre Loi particulière, regardez-y vous-mêmes; je ne veux pas juger ces questions-là.»
Lakini kama ni shauri la ubishi kuhusu maneno na majina ya Sheria yenu, amueni ninyi wenyewe. Mimi sitaki kuwa hakimu wa mambo haya!”
16 Et il les renvoya du tribunal.
Basi, akawafukuza kutoka mahakamani.
17 Tout le monde alors tomba sur Sosthènes, le chef de la synagogue, et l'on se mit à le battre devant le tribunal. Gallion ne s'en soucia nullement.
Nao wote wakamkamata Sosthene ambaye alikuwa kiongozi wa sunagogi, wakampiga palepale mbele ya mahakama. Lakini Galio hakujali kitendo hicho hata kidogo.
18 Paul resta encore longtemps à Corinthe; puis il prit congé des frères et s'embarqua pour la Syrie avec Priscille et Aquilas, après s'être fait raser la tête à Kenchrées; car il avait fait un voeu.
Paulo alikaa bado na wale ndugu huko Korintho kwa siku nyingi. Kisha aliwaaga, akapanda meli kwenda Siria pamoja na Priskila na Akula. Huko Kenkrea, alinyoa nywele zake kwa sababu ya nadhiri aliyokuwa ameweka.
19 On débarqua à Éphèse; Paul y laissa ses compagnons et se rendit à la synagogue, où il s'entretint avec les Juifs.
Walifika Efeso na hapo Paulo aliwaacha Priskila na Akula, akaenda katika sunagogi, akajadiliana na Wayahudi.
20 Mais quand ils lui demandèrent de prolonger son séjour, il n'y consentit pas
Walimwomba akae nao muda mrefu zaidi, lakini hakupenda.
21 et leur dit en prenant congé d'eux: «Je reviendrai une autre fois chez vous, s'il plaît à Dieu.» Il partit d'Éphèse,
Bali alipokuwa anaondoka, alisema, “Mungu akipenda nitakuja kwenu tena.” Akaondoka Efeso kwa meli.
22 débarqua à Césarée et, après être monté à Jérusalem pour saluer l'Église, il descendit à Antioche.
Meli ilitia nanga Kaisarea, naye Paulo akaenda Yerusalemu kulisalimia lile kanisa, kisha akaenda Antiokia.
23 Il en repartit après un court séjour et traversa successivement le pays des Galates et la Phrygie pour fortifier tous les disciples.
Alikaa huko muda mfupi, halafu akaendelea na safari kwa kupitia sehemu za Galatia na Frugia akiwatia moyo wafuasi wote.
24 Cependant un certain Juif, du nom d'Apollos, né à Alexandrie, un homme éloquent, arriva à Éphèse;
Myahudi mmoja aitwaye Apolo, mzaliwa wa Aleksandria, alifika Efeso. Alikuwa mtu mwenye ufasaha wa kuongea na mwenye ujuzi mkubwa wa Maandiko Matakatifu.
25 il connaissait à fond les Écritures. On l'avait instruit dans la doctrine du Seigneur; c'était une âme ardente qui prêchait et enseignait avec soin ce qui concerne Jésus, bien qu'il ne connût que le baptême de Jean.
Alikuwa amefundishwa juu ya hiyo njia ya Bwana, na akiwa motomoto, aliongea juu ya habari za Yesu. Akafundisha kwa usahihi ingawa alikuwa amepata ubatizo wa Yohane tu.
26 Quand il commença à parler librement dans la synagogue, Priscilla et Aquilas qui l'entendirent l'emmenèrent avec eux et lui exposèrent plus exactement la doctrine de Dieu.
Priskila na Akula walipomsikia akiongea kwa uhodari ndani ya sunagogi, walimchukua kwao wakamfundisha hiyo Njia ya Mungu kwa usahihi zaidi.
27 Lorsqu'il se proposa de passer en Achaïe, les frères l'y encouragèrent et écrivirent aux disciples de lui faire bon accueil. Une fois arrivé, il se rendit, par la grâce de Dieu, très utile aux croyants;
Apolo alipoamua kwenda Akaya, wale ndugu walimtia moyo kwa kuwaandikia wafuasi kule Akaya wampokee. Alipofika huko, aliweza kwa msaada wa neema ya Mungu, kuwasaidia sana wale ndugu waliopata kuwa waumini;
28 car il réfutait vigoureusement les Juifs en public, leur démontrant par les Écritures que Jésus est le Christ.
kwa maana aliendelea kwa uhodari kuwashinda Wayahudi hadharani akithibitisha kwa Maandiko Matakatifu kuwa Yesu ni Kristo.