< Actes 11 >
1 Les apôtres et les frères de Judée apprirent que les païens aussi avaient accepté la Parole de Dieu,
Mitume na ndugu kule Yudea walisikia kwamba watu wa mataifa mengine pia walikuwa wamelipokea neno la Mungu.
2 et Pierre, à son retour à Jérusalem, fut blâmé par les fidèles circoncis:
Basi, Petro aliporudi Yerusalemu, wale Wayahudi waumini waliopendelea watu wa mataifa mengine watahiriwe, walimlaumu wakisema:
3 «Tu es entré chez des incirconcis, lui dirent-ils, et tu as mangé avec eux!»
“Wewe umekwenda kukaa na watu wasiotahiriwa na hata umekula pamoja nao!
4 Mais Pierre leur raconta, en suivant l'ordre des faits, tout ce qui s'était passé:
Hapo Petro akawaeleza kinaganaga juu ya yale yaliyotendeka tangu mwanzo:
5 «J'étais, leur dit-il, dans la ville de Joppé, et pendant que je priais j'eus une extase et une vision m'apparut; c'était un objet descendant du ciel, ressemblant à une grande nappe nouée aux quatre coins et qui vint jusqu'à moi.
“Siku moja nikiwa nasali mjini Yopa, niliona maono; niliona kitu kama shuka kubwa likishushwa chini kutoka mbinguni likiwa limeshikwa pembe zake nne, likawekwa kando yangu.
6 Ayant regardé à l'intérieur, l'ayant bien examinée, j'y vis les quadrupèdes de la terre, les animaux sauvages, les reptiles et les oiseaux du ciel,
Nilichungulia ndani kwa makini nikaona wanyama wenye miguu minne, wanyama wa mwituni, wanyama watambaao na ndege wa angani.
7 et j'entendis une voix qui me disait: «Lève-toi, Pierre, tue et mange»;
Kisha nikasikia sauti ikiniambia: Petro amka, chinja, ule.
8 je répondis: «Nullement, Seigneur, parce que jamais rien de souillés ni d'impur n'est entré dans ma bouche».
Lakini mimi nikasema: La, Bwana; maana chochote kilicho najisi au kichafu hakijapata kamwe kuingia kinywani mwangu.
9 Une voix, venant du ciel, s'adressa à moi pour la seconde fois: «N'appelle pas souillés ce que Dieu a purifié.»
Ile sauti ikasikika tena kutoka mbinguni: Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.
10 Cela se répéta par trois fois, puis tout remonta au ciel.»
Jambo hilo lilifanyika mara tatu, na mwishowe vyote vilirudishwa juu mbinguni.
11 «Et voilà qu'à ce moment même trois hommes se présentèrent à la porte de la maison où j'étais; ils m'étaient envoyés de Césarée.
Ghafla, watu watatu waliokuwa wametumwa kwangu kutoka Kaisarea waliwasili kwenye nyumba niliyokuwa nakaa.
12 L'Esprit me dit d'aller avec eux sans aucun scrupule. Les six frères que voici m'accompagnèrent et nous entrâmes dans la maison de Cornélius.»
Roho aliniambia niende pamoja nao bila kusita. Hawa ndugu sita waliandamana nami pia kwenda Kaisarea na huko tuliingia nyumbani mwa Kornelio.
13 «Celui-ci nous raconta comment il avait vu dans sa maison l'ange se tenant devant lui et lui disant: «Envoie à Joppé et fais venir Simon, surnommé Pierre,
Yeye alitueleza jinsi alivyokuwa amemwona malaika amesimama nyumbani mwake na kumwambia: Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
14 il te dira des choses par lesquelles tu obtiendras le salut, toi et tous les tiens.»
Yeye atakuambia maneno ambayo kwayo wewe na jamaa yako yote mtaokolewa.
15 Lorsque je commençai à leur parler, l'Esprit saint descendit sur eux, comme sur nous à l'origine;
Na nilipoanza tu kuongea, Roho Mtakatifu aliwashukia kama alivyotushukia sisi pale awali.
16 et je me souvins de ce mot du Seigneur, quand il disait: «Jean baptisait d'eau, mais vous, vous serez baptisés d'Esprit saint.»
Hapo nilikumbuka yale maneno Bwana aliyosema: Yohane alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.
17 Si donc Dieu leur a accordé le même don qu'à nous, pour avoir cru au Seigneur Jésus-Christ, qui étais-je moi pour oser m'opposer à Dieu?»
Basi, kama Mungu amewapa pia watu wa mataifa mengine zawadi ileile aliyotupa sisi tulipomwamini Bwana Yesu Kristo, je, mimi ni nani hata nijaribu kumpinga Mungu?”
18 A l'ouïe de ces paroles, ils se calmèrent, et ils rendirent gloire à Dieu: «Ainsi, disaient-ils, Dieu a aussi accordé aux païens la repentance pour qu'ils aient la vie.»
Waliposikia hayo, waliacha ubishi, wakamtukuza Mungu wakisema, “Mungu amewapa watu wa mataifa mengine nafasi ya kutubu na kuwa na uzima!”
19 Ceux qui avaient été dispersés par la persécution, à la suite de la mort d'Étienne, allèrent jusqu'en Phénicie et atteignirent Chypre et Antioche, n'annonçant la parole à personne qu'aux Juifs.
Kutokana na mateso yaliyotokea wakati Stefano alipouawa, waumini walitawanyika. Wengine walikwenda mpaka Foinike, Kupro na Antiokia wakihubiri ule ujumbe kwa Wayahudi tu.
20 Mais quelques-uns d'eux qui étaient Chypriotes et Cyrénéens, arrivés à Antioche, parlèrent aussi aux Hellénistes et leur annoncèrent l'Évangile du Seigneur Jésus.
Lakini baadhi ya waumini waliotoka Kupro na Kurene, walikwenda Antiokia wakautangaza huo ujumbe kwa watu wa mataifa mengine wakiwahubiria ile Habari Njema juu ya Bwana Yesu.
21 La main du Seigneur fut avec eux et grand fut le nombre de ceux qui crurent et se convertirent au Seigneur.
Bwana aliwasaidia na idadi kubwa ya watu iliamini na kumgeukia Bwana.
22 Le bruit en parvint aux oreilles des membres de l'Église de Jérusalem et ils envoyèrent Barnabas jusqu'à Antioche.
Habari ya jambo hilo ikasikika kwa lile kanisa la Yerusalemu. Hivyo wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
23 Lorsque, à son arrivée, il vit la grâce de Dieu, il s'en réjouit et il les exhorta tous à rester, d'un coeur convaincu, fidèles au Seigneur,
Alipofika huko na kuona jinsi Mungu alivyowaneemesha wale watu, alifurahi na kuwahimiza wote wadumu katika uaminifu wao kwa Bwana.
24 parce qu'il était homme de bien, plein d'Esprit saint et de foi; et un grand nombre de personnes s'unirent au Seigneur.
Barnaba alikuwa mtu mwema na mwenye kujaa Roho Mtakatifu na imani. Kundi kubwa la watu lilivutwa kwa Bwana.
25 Barnabas se rendit ensuite à Tarse, y chercha Saul, le trouva et l'amena à Antioche.
Kisha, Barnaba alikwenda Tarso kumtafuta Saulo
26 Durant une année entière ils restèrent ensemble dans l'Église et instruisirent un grand nombre de personnes. Ce fut à Antioche qu'on donna pour la première fois aux disciples le nom de chrétiens.
Alipompata, alimleta Antiokia. Nao wote wawili walikaa na lile kanisa kwa mwaka wote mzima wakifundisha kundi kubwa la watu. Huko Antiokia, ndiko, kwa mara ya kwanza, wafuasi waliitwa Wakristo.
27 En ce temps-là, des prophètes se rendirent de Jérusalem à Antioche.
Wakati huohuo, manabii kadhaa walikuja Antiokia kutoka Yerusalemu.
28 L'un d'eux, nommé Agabus, se leva et annonça par l'Esprit qu'une grande famine régnerait sur toute la terre; elle arriva, en effet, sous Claude.
Basi, mmoja wao aitwaye Agabo alisimama, na kwa uwezo wa Roho akabashiri kwamba kutakuwa na njaa kubwa katika nchi yote (Njaa hiyo ilitokea wakati Klaudio alipokuwa akitawala).
29 Les disciples décidèrent d'envoyer, chacun selon son pouvoir, un secours aux frères demeurant en Judée;
Wale wanafunzi waliamua kila mmoja kwa kadiri ya uwezo wake apeleke chochote ili kuwasaidia wale ndugu waliokuwa wanaishi Yudea.
30 ce qu'ils firent en le remettant aux Anciens par l'entremise de Barnabas et de Saul.
Basi, wakafanya hivyo na kupeleka mchango wao kwa wazee wa kanisa kwa mikono ya Barnaba na Saulo.