< 3 Jean 1 >
1 L'ancien au bien-aimé Gaïus (que j'aime véritablement).
Mimi mzee nakuandikia wewe Gayo, rafiki yangu, ninayekupenda kweli.
2 Mon bien-aimé, je fais des voeux pour que tu prospères en toutes choses et que la santé de ton corps soit aussi bonne que celle de ton âme.
Mpenzi wangu, nakutakia mafanikio mema ya kila aina; nakutakia afya njema ya mwili kama ulivyo nayo rohoni.
3 J'ai été, en effet, bien heureux de voir des frères venir et rendre témoignage de la vérité qui est en toi; je veux dire rendre témoignage que tu marches dans la vérité.
Nimefurahi sana ndugu kadhaa walipofika hapa, wakaiambia juu ya uaminifu wako kuhusu ukweli; naam, wewe unaishi daima katika ukweli.
4 Je n'ai pas de plus grande joie que d'apprendre que mes enfants marchent dans la vérité.
Hakuna kitu kinachonifurahisha zaidi kuliko kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.
5 Mon bien-aimé, tu te montres fidèle dans ce que tu fais pour les frères, et ce sont des étrangers.
Mpenzi wangu, wewe ni mwaminifu kila mara unapowahudumia ndugu, hata kama ni wageni.
6 Ils ont rendu témoignage à ton amour devant toute l'Église. Tu feras bien de pourvoir à leur voyage d'une manière digne de Dieu;
Ndugu hao wamelieleza kanisa hapa habari za upendo wako. Tafadhali uwasaidie waendelee na safari yao kwa namna itakayompendeza Mungu,
7 car c'est pour le «nom» qu'ils sont partis sans rien recevoir des païens.
Maana wanaanza safari yao katika utumishi wa Kristo bila kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.
8 Aussi devons-nous accueillir de tels hommes, afin de nous mettre à l'oeuvre avec eux pour la vérité.
Basi, sisi tunapaswa kuwasaidia watu hawa, ili nasi tupate kushiriki katika kazi yao kwa ajili ya ukweli.
9 J'ai écrit quelques mots à l'Église, mais Diotréphès, qui affecte d'être leur chef, n'accepte rien de nous.
Niliandika barua fupi kwa hilo kanisa; lakini Diotrefe, ambaye hupenda kuwa kiongozi wao, hataki kabisa kunisikiliza.
10 Aussi, quand je viendrai, je signalerai les actes qu'il commet, comment il se répand contre nous en mauvais propos, et cela ne lui suffit pas, car non seulement il n'accueille pas les frères lui-même, mais il défend de les accueillir, et ceux qui seraient désireux de le faire, il les chasse de l'Église.
Basi, nitakapokuja nitayafichua mambo yote anayofanya, maneno mabaya anayotutolea na uongo anaosema juu yetu. Isitoshe, yeye hukataa kuwakaribisha hao ndugu walio safarini, na hata huwazuia watu wengine wanaotaka kuwakaribisha, na hujaribu kuwafukuzia nje ya kanisa.
11 Mon bien-aimé, n'imite pas le mal, mais le bien. Celui qui fait le bien est de Dieu. Celui qui fait le mal n'a pas vu Dieu.
Mpenzi wangu, usifuate mfano mbaya, bali mfano mwema. Kila atendaye mema ni wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hajapata kumwona Mungu.
12 Quant à Démétrius, tous, et la vérité elle-même, lui rendent un bon témoignage. Nous aussi nous lui rendons un bon témoignage, et tu sais que notre témoignage est véridique.
Kila mtu anamsifu Demetrio; naam, ukweli wenyewe unamsifu. Nasi pia tunatoa ushahidi wetu juu yake, nawe wajua kwamba tunachosema ni kweli.
13 J'aurais bien des choses à t'écrire; mais je ne veux pas te les faire savoir avec l'encre et la plume.
Ninayo bado mengi ya kukwambia, lakini sipendi kuyaandika kwa kalamu na wino.
14 J'espère te voir bientôt et nous nous entretiendrons de vive voix. La paix soit avec toi. Les amis te saluent. Salue les amis chacun en particulier.
Natumaini kukuona karibuni na hapo tutazungumza ana kwa ana. Nakutakia amani. Rafiki zako wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu wote kila mmoja binafsi.