< 2 Corinthiens 4 >
1 Voilà pourquoi, chargés par la miséricorde de Dieu d'un pareil ministère, nous ne faiblissons pas;
Basi, Mungu, kwa huruma yake, ametukabidhi kazi hii na hivyo hatufi moyo.
2 au contraire nous repoussons bien loin tout procédé secret et honteux, nous ne recourons pas à la ruse, nous ne falsifions pas la parole de Dieu, mais nous publions ouvertement la vérité, et ainsi nous nous recommandons nous-mêmes à toute conscience d'homme, et cela à la face de Dieu.
Tumeyaacha kabisa mambo yote ya aibu na ya kisirisiri. Hatuishi tena kwa udanganyifu, wala kwa kulipotosha neno la Mungu; bali tunaudhihirisha ukweli kwa kuufanya ukweli, na hivyo kujiweka chini ya uamuzi wa dhamiri za watu mbele ya Mungu.
3 (S'il reste encore un voile sur notre Évangile, c'est pour ceux qui vont périr que ce voile existe,
Maana, kama Habari Njema tunayohubiri imefichika, imefichika tu kwa wale wanaopotea.
4 pour les incrédules dont le dieu de ce monde a aveuglé les pensées, afin qu'ils ne soient point illuminés des splendeurs du glorieux Évangile du Christ, qui est l'image de Dieu.) (aiōn )
Hao hawaamini kwa sababu yule mungu wa ulimwengu huu amezitia giza akili zao wasipate kuuona wazi mwanga wa Habari Njema ya utukufu wa Kristo, ambaye ni mfano kamili wa Mungu. (aiōn )
5 Car nous ne nous prêchons pas nous-mêmes, mais Jésus-Christ le Seigneur; et nous-mêmes nous sommes vos serviteurs à cause de Jésus.
Maana hatujitangazi sisi wenyewe, ila tunamhubiri Yesu Kristo aliye Bwana, sisi wenyewe tukiwa watumishi wenu kwa ajili ya Yesu.
6 En effet, le Dieu qui a dit: «Que des ténèbres jaillisse la lumière», a fait aussi jaillir la lumière dans nos coeurs, pour que nous fassions resplendir la connaissance de la gloire de Dieu sur la face de Christ.
Mungu ambaye alisema, “Mwanga na uangaze kutoka gizani,” ndiye mwenye kuiangaza mioyo yetu, na kutupatia mwanga wa ujuzi wa utukufu wa Mungu uangazao katika uso wa Kristo.
7 Nous portons ce trésor dans des vases d'argile pour prouver que la puissance débordante de sa vertu vient de Dieu et non pas de nous;
Basi, sisi tulio na hazina hii tuko tu kama vyombo vya udongo, ili ionekane wazi kwamba nguvu hiyo kuu yatoka kwa Mungu wala si kwetu sisi wenyewe.
8 nous sommes toujours surchargés, jamais écrasés; tourmentés, jamais désespérés;
Daima twapata taabu, lakini hatugandamizwi; twapata mashaka, lakini hatukati tamaa;
9 persécutés, jamais vaincus; jetés à terre, jamais morts;
twateseka, lakini hatuachwi bila msaada; na ingawa tumeangushwa chini, hatukuangamizwa.
10 nous portons partout dans notre corps le martyre de Jésus, pour que, dans notre corps, se montre aussi sa vie.
Kila wakati tumekuwa tukichukua mwilini mwetu kifo cha Kristo, ili uhai wake Yesu pia udhihirike katika miili yetu.
11 Nous sommes toujours livrés vivants à la mort à cause de Jésus pour que, dans la mort de notre chair, se montre aussi sa vie.
Naam, katika maisha yetu yote tunakabiliwa na kifo daima kwa ajili ya Yesu, ili uzima wake Yesu udhihirike katika miili yetu inayokufa.
12 Ainsi la mort exerce son pouvoir sur nous et la vie agit en vous.
Hii ina maana kwamba ndani yetu kifo kinafanya kazi, lakini ndani yenu uhai unafanya kazi.
13 Nous avons le même Esprit de foi que dans ce passage de l'Écriture: «J'ai cru, c'est pourquoi j'ai parlé.» Nous croyons, nous aussi, voilà pourquoi nous parlons,
Maandiko Matakatifu yasema: “Niliamini, ndiyo maana nilinena.” Nasi pia, tukiwa na moyo huohuo wa imani, tunaamini, na kwa sababu hiyo twanena.
14 sachant que celui qui a ressuscité le Seigneur Jésus nous ressuscitera avec Jésus et nous fera paraître avec vous devant lui.
Tunajua kwamba yule aliyemfufua Bwana Yesu atatufufua sisi pia pamoja na Yesu na kutuweka mbele yake pamoja nanyi.
15 Tout cela à cause de vous et afin que la grâce de plus en plus abondante multiplie les actions de grâces d'un plus grand nombre d'entre vous pour la gloire de Dieu.
Yote haya ni kwa faida yenu; ili kama vile neema ya Mungu inavyoenea kwa watu wengi zaidi na zaidi vivyo hivyo watu wengi zaidi watoe shukrani nyingi kwa utukufu wa Mungu.
16 Aussi nous ne faiblissons pas; au contraire, si notre être extérieur tombe en ruines, notre être intérieur se renouvelle de jour en jour;
Kwa sababu hiyo hatufi moyo; na hata kama maumbile yetu ya nje yataoza, lakini kwa ndani tunafanywa wapya siku kwa siku.
17 car un moment de légères afflictions nous vaut une somme immense, incalculable de gloire éternelle, (aiōnios )
Taabu tunayopata ni kidogo, tena ya muda tu: lakini itatupatia utukufu upitao matazamio yote, utukufu ambao hauna mwisho. (aiōnios )
18 à nous qui ne regardons pas aux choses visibles, mais aux invisibles, parce que les choses visibles ne durent qu'un temps, les invisibles sont éternelles. (aiōnios )
Hivyo tunatazamia kwa makini si vitu vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Maana vinavyoonekana ni vya muda tu; lakini vile visivyoonekana ni vya milele. (aiōnios )