< 2 Corinthiens 3 >
1 Nous recommençons, n'est-ce pas, à faire nous-mêmes notre éloge? Aurions-nous peut-être besoin, comme certains individus, de lettres de recommandation pour vous ou de votre part?
Je, tunaanza tena kujipendekeza? Je, tunahitaji barua ya utambulisho kwenu, au kutoka kwenu, kama watu wengine?
2 notre lettre, c'est vous; écrite dans nos coeurs, reconnaissable et lisible pour tout le monde;
Ninyi wenyewe ni barua yetu; barua iliyoandikwa mioyoni mwetu kila mtu aione na kuisoma.
3 on sait bien que vous êtes une lettre de Christ rédigée par nous, écrite non à l'encre, mais par l'Esprit du Dieu vivant, non sur des tables de pierre, mais sur des tables de chair, sur vos coeurs.
Ni dhahiri kwamba ninyi ni barua ya Kristo aliyoipeleka kwa mikono yetu. Barua yenyewe imeandikwa si kwa wino, bali kwa Roho wa Mungu hai; imeandikwa si juu ya kipande cha jiwe, bali juu ya mioyo ya watu.
4 Une pareille assurance en Dieu, c'est du Christ que nous la tenons;
Tunaweza kusema hayo kwa sababu ya tumaini letu tulilo nalo kwa Mungu kwa njia ya Kristo.
5 par nous-mêmes nous sommes incapables de rien concevoir, de rien tirer de notre propre fonds,
Si kwamba sisi tunaweza kufanya chochote kwa nguvu zetu wenyewe, ila uwezo wetu wote hutoka kwa Mungu:
6 toute notre capacité vient de Dieu, qui nous a rendus capables d'être ministres d'une Nouvelle Alliance, qui n'est pas de lettre, mais d'esprit; car la lettre tue, et l'esprit vivifie.
maana yeye ndiye aliyetuwezesha kulihudumia Agano Jipya ambalo si agano la sheria iliyoandikwa, bali Agano la Roho. Maana sheria iliyoandikwa huleta kifo, lakini Roho huleta uzima.
7 Si le ministère de la mort, gravé en lettres sur la pierre, a été si entouré de gloire que les enfants d'Israël ne pouvaient fixer le visage de Moïse, tellement il resplendissait d'un éclat maintenant anéanti,
Sheria iliwekwa kwa kuandikwa juu ya vipande vya mawe. Ingawaje mwisho wake umekuwa kifo, utukufu wake ulikuwa mkuu mno hata wana wa Israeli wasiweze kuutazama uso wa Mose kwa sababu ya mng'ao wake. Tena mng'ao huo ulikuwa wa muda tu. Basi, ikiwa huduma ya kile ambacho kimesababisha kifo imefanyika kwa utukufu mwingi kiasi hicho,
8 combien le ministère de l'Esprit ne sera-t-il pas plus glorieux?
basi, huduma ya Roho ina utukufu mkuu zaidi.
9 Si le ministère de la condamnation a été glorieux, le ministère de la justice sera beaucoup plus glorieux encore;
Ikiwa basi, kulikuwa na utukufu katika huduma ile iliyoleta hukumu, ni wazi kwamba huduma ile iletayo kukubaliwa kuwa waadilifu itakuwa na utukufu mkuu zaidi.
10 on peut même dire, dans un sens, que ce qui a été glorifié autrefois ne l'a pas été, en comparaison d'une gloire supérieure.
Sasa utukufu mkuu zaidi umechukua nafasi ya ule utukufu uliokuja hapo awali, ambao fahari yake imekwisha toweka.
11 Si, en effet, ce qui est anéanti a été glorieux, à plus forte raison ce qui est éternel sera glorieux.
Maana ikiwa kile kilichokuwa cha muda tu kilikuwa na utukufu wake, bila shaka kile chenye kudumu milele kitakuwa na utukufu mkuu zaidi.
12 Cette espérance que nous avons nous remplit de hardiesse
Kwa vile hili ndilo tumaini letu, sisi twasema kwa uhodari mkuu.
13 et nous ne faisons pas comme Moïse «qui se voilait la face» pour cacher aux regards des enfants d'Israël la fin d'un éclat périssable.
Sisi hatufanyi kama Mose ambaye alilazimika kuufunika uso wake kwa kitambaa ili watu wa Israeli wasiuone ule mwisho wa mng'ao uliokuwa unafifia.
14 Leur intelligence s'obscurcit, et aujourd'hui encore ce voile est là quand on leur lit l'Ancienne Alliance; ils ne voient pas avec évidence que le Christ seul l'abolit.
Lakini akili zao zilipumbazwa. Mpaka leo hii lisomwapo Agano la Kale, kifuniko hicho bado kipo. Kifuniko hicho kitaondolewa tu mtu anapoungana na Kristo.
15 Oui, aujourd'hui encore, quand on leur lit Moïse, il y a un voile sur leur coeur.
Naam, mpaka hivi leo kila isomwapo Sheria ya Mose akili zao huwa zimefunikwa.
16 «Lorsqu'ils se convertissent au Seigneur, ce voile est enlevé ».
Lakini, wakati mtu amgeukiapo Bwana, kifuniko hicho huondolewa.
17 C'est le Seigneur qui est l'Esprit; là où est l'Esprit du Seigneur, là est la liberté;
Hapa “Bwana” ni Roho; na pale alipo Roho wa Bwana ndipo ulipo uhuru.
18 et nous tous qui, le visage découvert, contemplons dans un miroir la gloire du Seigneur, nous nous transformons à son image; sa gloire devient la nôtre comme cela doit se faire par l'Esprit du Seigneur.
Basi, sisi sote ambao nyuso zetu hazikufunikwa, twaonyesha kama katika kioo, utukufu wa Bwana; tunabadilishwa tufanane zaidi na huo mfano wake kwa utukufu mwingi zaidi. Hiyo ni kazi yake Roho wa Bwana.