< Psaumes 57 >

1 Au maître chantre. Sur « Ne détruis pas » Ecrit de David, quand, fuyant devant Saül, il se retira dans la caverne. Prends pitié de moi, ô Dieu! prends pitié de moi! Car mon âme cherche en toi son refuge; et je me réfugie à l'ombre de tes ailes, en attendant que la calamité passe,
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
2 J'invoque le Dieu suprême, le Dieu qui agit en ma faveur.
Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
3 Il enverra des Cieux, pour me sauver et confondre mes ennemis, (Pause) Dieu enverra sa grâce et sa fidélité.
Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
4 Je vis au milieu des lions, gisant parmi des hommes qui vomissent des flammes, des hommes dont les dents sont des dards et des flèches, et la langue, une épée tranchante.
Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
5 Montre, ô Dieu, que tu domines les Cieux! Que sur toute la terre apparaisse ta gloire!
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 Ils tendent un filet sous mes pas, mon âme succombe, ils creusent une fosse devant moi; ils y tombent eux-mêmes. (Pause)
Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
7 Mon cœur se rassure, ô Dieu! mon cœur se rassure. Je veux te célébrer par mes chants et mes accords.
Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
8 Èveille-toi, mon esprit, éveille-toi, mon luth, ma harpe! Je veux me lever avec l'aurore!
Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
9 Je te célébrerai parmi les peuples, Seigneur, je te chanterai parmi les nations;
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
10 car ta miséricorde est grande jusques aux Cieux, et ta fidélité jusques aux nues.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
11 Montre, ô Dieu, que tu domines les Cieux; et que sur toute la terre apparaisse ta gloire!
Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.

< Psaumes 57 >