< Psaumes 2 >

1 Pourquoi cette rumeur dans les nations, et chez les peuples, ces complots inutiles,
Kwa nini mataifa wanafanya dhoruba, kwa nini watu wanafanya njama ambazo zitafeli?
2 cette levée des rois de la terre, et ces princes en conseil assemblés contre l'Éternel et contre son Oint?
Wafalme wa nchi kwa pamoja hushikilia misimamo yao na watawala kwa pamoja hufanya njama kinyume na Yahwe na kinyume na Masihi, wakisema,
3 « Rompons leurs fers, et secouons leurs chaînes! » [disent-ils.]
“Ngoja tuzikate pingu walizo tufingia sisi na kuzitupa pingu zao.”
4 Sur son trône dans les Cieux Il se rit, le Seigneur se raille d'eux;
Yeye aketie katika mbingu atacheka kwa dharau mbele yao; Bwana atawadhihaki wao.
5 puis Il leur parle dans sa colère, et par son courroux Il les épouvante:
Kisha ataongea nao katika hasira yake na kuwaogofya kwa gadhabu yake, akisema,
6 « Moi-même j'ai oint mon Roi sur Sion, ma montagne sainte! »
“Mimi mwenyewe nilimpaka mafuta mfalme wa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 – « Que je redise le décret! L'Éternel m'a dit: Tu es mon fils, en ce jour je t'ai engendré.
Nami nitatangaza amri ya Yahwe. Yeye aliniambia, “wewe ni mwanangu! Leo hii nimekuwa baba yako.
8 Demande-moi, et je te donnerai les nations en héritage, et en propriété les extrémités de la terre;
Uniombe, nami nitakupa wewe taifa kwa ajili ya urithi na mikoa ya nchi iliyo bora kwa ajili ya umiliki wako.
9 tu les briseras d'un sceptre de fer, comme un vase de potier, tu les mettras en pièces. »
Wewe utawavunja wao kwa fimbo ya chuma; kama vile mtungi wa mfinyanzi, wewe utawavunja wao vipande vipande.”
10 Maintenant, ô rois, devenez sages, soyez avertis, juges de la terre!
Hivyo sasa, ninyi wafalme; mchukue tahadhari; mjirekebishe.
11 Soumettez-vous à l'Éternel avec crainte, soyez alarmés et tremblez!
Mwabuduni Yahwe kwa hofu na mfurahi mkitetemeka.
12 Embrassez le Fils, de peur qu'il ne s'irrite, et que vous ne vous perdiez en suivant votre voie. Car un instant encore, et sa colère s'allume. Heureux tous ceux qui mettent en lui leur confiance!
Mumbusu mwana vinginevyo atawakasirikia, na mtakufa pale pale hasira yake ikiwaka. Ni jinsi gani wamebarikiwa wale wote watafutao usalama ndani yake.

< Psaumes 2 >