< Psaumes 104 >

1 Mon âme, bénis l'Éternel! Éternel, mon Dieu, tu es très grand, tu es revêtu de splendeur et de majesté!
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
2 Il s'enveloppe de lumière comme d'un vêtement, Il déploie les Cieux comme une tenture;
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
3 Il élève sur les eaux le haut de sa demeure, Il fait des nuées son char, Il s'avance sur les ailes du vent.
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
4 Il fait des vents ses messagers, et ses ministres, du feu enflammé.
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
5 Il assit la terre sur ses bases, elle est inébranlable pour toujours, pour jamais.
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
6 Tu l'avais couverte de l'abîme comme d'un manteau, les eaux se tenaient sur les montagnes;
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
7 à ta menace elles ont fui, à la voix de ton tonnerre elles ont reculé:
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
8 les montagnes montèrent, les vallées descendirent à la place que tu leur assignas.
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
9 Tu posas des limites qu'elles ne franchiraient plus, afin qu'elles ne vinssent plus recouvrir la terre.
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
10 Tu fais jaillir des sources pour former les ruisseaux; ils s'écoulent entre les montagnes;
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
11 ils abreuvent toutes les bêtes des champs, les onagres y étanchent leur soif.
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
12 Sur leurs bords séjournent les oiseaux du ciel, entre les rameaux ils font entendre leur voix.
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
13 Du haut de sa demeure Il arrose les montagnes, et la terre se rassasie du fruit de tes œuvres.
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
14 Il fait croître l'herbe pour les quadrupèdes, et les plantes pour le service de l'homme, tirant ainsi le pain du sein de la terre;
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
15 et le vin qui réjouit le cœur de l'homme, et, plus que l'huile, fait resplendir son visage; et le pain qui fortifie le cœur de l'homme.
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
16 Les arbres de l'Éternel sont rassasiés, les cèdres du Liban qu'il a plantés,
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
17 où viennent nicher les oiseaux, la cigogne, qui habite les pins.
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
18 Les hautes montagnes sont pour les bouquetins, et les rochers sont l'asile des gerboises.
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
19 Il créa la lune pour marquer les temps; le soleil connaît son couchant.
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
20 Tu fais l'obscurité, et il est nuit: alors toutes les bêtes des forêts sont en mouvement;
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
21 les jeunes lions rugissent après la proie, et demandent à Dieu leur pâture.
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
22 Le soleil se lève: ils se retirent, et vont reposer dans leurs tanières.
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
23 L'homme se rend à son travail, et à son labour jusques au soir.
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
24 Que tes œuvres sont nombreuses, ô Éternel! Tu les as toutes faites avec sagesse; la terre est pleine de tes richesses.
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
25 Dans cette mer grande et vaste fourmillent sans nombre des animaux petits et grands.
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
26 Là circulent les navires, le Léviathan que tu formas pour s'y jouer.
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
27 Tous ils s'attendent à toi, pour que tu leur donnes la nourriture en son temps.
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
28 Tu leur donnes, ils recueillent; tu ouvres ta main, ils se rassasient de biens.
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
29 Tu caches ta face, ils sont éperdus; tu leur retires le souffle, ils expirent et rentrent dans leur poudre.
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30 Tu émets ton souffle, ils sont créés, et tu renouvelles la face de la terre.
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
31 La gloire de l'Éternel demeure à jamais; l'Éternel se réjouit de ses œuvres.
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
32 Il regarde la terre, et elle tremble; Il touche les montagnes, et elles sont fumantes.
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
33 Je veux chanter l'Etemel, tant que je vivrai, célébrer mon Dieu, tant que je serai.
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
34 Que mes chants lui soient agréables! Je fais mes délices de l'Éternel.
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
35 Que les pécheurs disparaissent de la terre, et que les impies cessent d'être! Mon âme, bénis l'Éternel! Alléluia!
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.

< Psaumes 104 >