< Psaumes 101 >
1 Cantique de David. Je vais chanter la bonté et la droiture; c'est toi, Éternel, que je célébrerai.
Nitaimba uaminifu wa agano lako na hukumu; kwako, Ee Yahwe, Nitakuimbia sifa.
2 Je m'appliquerai à suivre une voie innocente: ô puissé-je y parvenir! J'agirai dans l'innocence du cœur au sein de ma maison.
Nitatembea katika njia ya uadilifu. Oh, ni lini utakuja kwangu? Nitatembea kwa uadilifu ndani ya nyumba yangu.
3 Je ne mettrai devant mes yeux aucune chose indigne; je hais la conduite des transgresseurs, sur moi elle n'aura pas de prise.
Sitaweka matendo maovu mbele ya macho yangu; ninachukia uovu usio na maana; hauta shikamana nami.
4 Que le cœur pervers se tienne loin de moi, je ne veux pas connaître le méchant.
Watu waliopotoka wataniacha mimi; mimi sichangamani na uovu.
5 Je détruirai celui qui en secret calomnie son ami; je ne supporte pas celui dont l'œil est altier et le cœur enflé.
Nitamwangamiza yeyote amsengenyaye jirani yake kwa siri. Sitamvumilia yeyote mwenye kiburi.
6 Mes yeux se porteront vers les hommes sûrs du pays, pour les faire habiter avec moi; ceux qui suivent une voie innocente, seront mes serviteurs.
Nitawachagua walio waaminifu katika nchi wakae upande wangu. Wale watembeao katika njia ya uhadilifu watanitumikia.
7 Il ne s'assiéra pas dans ma maison celui qui fait des fraudes; celui qui ment ne pourra demeurer sous mes yeux.
Watu wadanganyifu hawatabaki ndani ya nyumba yangu; waongo hawatakaribishwa mbele ya macho yangu.
8 Chaque jour je veillerai à arracher les impies du pays, à bannir de la cité de l'Éternel tous ceux qui font le mal.
Asubuhi hata asubuhi nitawaangamiza waovu wote kutoka nchini; nitawaondoa watendao maovu wote katika mji wa Yahwe.