< Proverbes 27 >

1 Ne te vante pas du lendemain, car tu ignores ce qu'un jour enfante.
Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
2 Qu'un autre te loue, et non ta propre bouche, un étranger, et non tes propres lèvres!
Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
3 La pierre est lourde, et le sable pesant; mais l'humeur de l'insensé pèse plus que tous deux.
Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
4 La fureur est cruelle, et la colère impétueuse; mais qui pourra tenir devant la jalousie?
Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
5 Mieux vaut un reproche franc, qu'une affection dissimulée.
Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
6 Les coups d'un ami viennent de fidélité; mais un ennemi prodigue les baisers.
Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
7 L'homme rassasié foule le miel aux pieds; mais pour l'affamé tout ce qui est amer, est doux.
Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
8 Tel l'oiseau qui erre loin de son nid, tel est l'homme qui erre loin de ses lieux.
Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
9 L'huile et l'encens réjouissent le cœur, et par un conseil cordial l'ami est doux à l'homme.
Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
10 Ne quitte pas ton ami, ni l'ami de ton père, mais ne va pas chez ton frère le jour de ton malheur! Mieux vaut un voisin proche, qu'un parent éloigné.
Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
11 Sois sage, mon fils, et réjouis mon cœur, et je saurai que répondre à qui m'outragera.
Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
12 Le sage voit la calamité, et se met à l'abri; les inconsidérés vont en avant, et sont punis.
Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
13 Prends-lui son manteau, car il a cautionné autrui, et nantis-toi de lui plutôt que de l'étranger.
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
14 Quand de grand matin à haute voix on salue son prochain, cela est regardé comme une imprécation.
Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
15 L'eau d'une gouttière tombant sans relâche un jour de pluie, et la femme querelleuse sont choses pareilles;
Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
16 qui l'arrêterait, arrêterait le vent, et sa main appellerait [bientôt] l'huile à son secours.
Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
17 Le fer aiguise le fer, et l'un aiguise la colère de l'autre.
Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
18 Qui garde son figuier, en mange le fruit, et qui a des soins pour son maître, obtient de l'honneur.
Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
19 Comme dans les eaux un regard [répond] à un regard, ainsi le cœur de l'homme [répond] au cœur de l'homme.
Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
20 Les Enfers et l'abîme ne sont jamais rassasiés, et les yeux de l'homme ne sont jamais rassasiés. (Sheol h7585)
Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol h7585)
21 Ce qu'est le creuset pour l'argent, la fournaise pour l'or, que chacun le soit pour la bouche qui le loue!
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
22 Quand tu pilerais le fou dans le mortier, parmi les gruaux avec le pilon, sa folie ne le quittera pas.
Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
23 Examine l'aspect de ton bétail, et sois attentif à tes troupeaux!
Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
24 Car l'opulence n'est pas éternelle; et une couronne se transmet-elle dans tous les âges?
Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
25 L'herbe disparaît, et la tendre verdure se montre, et l'on recueille les herbes des montagnes;
Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
26 les agneaux te donnent des vêtements, et les boucs, le prix d'un champ;
wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
27 le lait des chèvres suffit à ta nourriture, à la nourriture de ta maison, et à l'entretien de tes servantes.
Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.

< Proverbes 27 >