< Proverbes 25 >

1 Ce sont aussi des Proverbes de Salomon, que recueillirent les hommes d'Ezéchias, roi de Juda.
Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
2 La gloire de Dieu, c'est de cacher ses desseins, et la gloire des rois, de les pénétrer.
Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
3 Comme les Cieux en hauteur, la terre en profondeur, que le cœur du roi soit insondable!
Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
4 De l'argent enlève les scories, et il en sort pour l'orfèvre un vase;
Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
5 ôte l'impie des alentours du roi, et par la justice son trône s'affermira.
Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
6 Ne fais pas le glorieux devant un roi, et ne te mets pas au rang des Grands;
Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
7 car mieux vaut qu'on te dise: Monte ici! que d'être humilié devant le prince que tes yeux voient.
ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
8 Ne te hâte pas d'entrer en procès, de peur de ce qu'à la fin tu pourrais faire, si ta partie t'outrage!
usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
9 Plaide ton procès contre ta partie, mais ne révèle pas le secret d'autrui;
Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
10 de peur que celui qui t'entendrait, ne te fasse honte, et que ton infamie ne s'efface pas.
ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
11 Des pommes d'or sur une ciselure d'argent, tel est un mot dit à propos.
Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
12 Anneau d'or, collier d'or fin, tel est le sage moniteur pour l'oreille docile.
Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
13 Le frais de la neige au temps de la moisson, tel est le messager sûr pour celui qui le dépêche: il restaure l'âme de son maître.
Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
14 Nuage et vent, mais point de pluie, c'est l'homme qui se vante en mentant de donner.
Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
15 A la patience un prince se laisse gagner, et la langue, toute molle qu'elle est, brise des os.
Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
16 Si tu trouves du miel, manges-en ce qui t'est suffisant, de peur d'en avoir à satiété, et de le rejeter.
Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
17 Mets rarement le pied dans la maison de ton ami, de peur qu'il ne se lasse de toi, et ne te prenne en aversion.
Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
18 Un marteau, une épée, une flèche aiguë, c'est l'homme qui dépose contre son frère en faux témoin.
Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
19 Une dent cassée, un pied vacillant, c'est au jour de détresse le perfide en qui l'on se lie.
Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
20 Oter son manteau au jour de la froidure, verser du vinaigre sur du natron, c'est chanter des chansons à un cœur triste.
Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
21 Si ton ennemi a faim, donne-lui du pain à manger, s'il a soif, donne-lui de l'eau à boire,
Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
22 car ainsi tu lui mets sur la tête des charbons ardents, et l'Éternel te récompensera.
Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
23 Le vent du nord produit la pluie, et la calomnie sourde, le visage irrité.
Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
24 Mieux vaut habiter le coin d'un toit, que près d'une femme querelleuse, et le même logis.
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
25 Une eau fraîche pour un homme fatigué, c'est une bonne nouvelle venant d'un pays lointain.
Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
26 Une source troublée, et un puits gâté, c'est le juste succombant sous l'impie.
Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
27 Il n'est pas bon de manger trop de miel, et sonder les choses difficiles est trop difficile.
Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
28 Une ville forcée et sans murs, tel est l'homme qui n'a pas l'empire de son cœur.
Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.

< Proverbes 25 >