< Nombres 28 >
1 Et l'Éternel parla à Moïse en ces termes:
Bwana akamwambia Mose,
2 Transmets ce commandement aux enfants d'Israël: Vous veillerez à m'offrir à leurs époques fixes, mes oblations, mon ordinaire pour mes sacrifices ignés, mon parfum agréable.
“Wape Waisraeli agizo hili na uwaambie: ‘Hakikisheni kwamba mnaniletea mimi kwa wakati uliowekwa chakula kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, kama harufu nzuri ya kupendeza.’
3 Et dis-leur: Voici le sacrifice igné que vous offrirez à l'Éternel: deux agneaux d'un an sans défaut, chaque jour, comme holocauste continuel.
Waambie: ‘Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto mnayomtolea Bwana: wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasio na dosari, kama sadaka ya kawaida ya kuteketezwa kila siku.
4 Tu sacrifieras l'un des agneaux le matin et le second dans la soirée;
Andaa mwana-kondoo mmoja asubuhi na mwingine jioni,
5 et pour l'offrande un dixième d'épha de fleur de farine trempée d'un quart de hin d'huile d'olives concassées.
kila mmoja atolewe pamoja na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa pamoja na robo ya hini ya mafuta ya zeituni.
6 C'est l'holocauste continuel sacrifié sur le mont de Sinaï pour être un parfum agréable comme sacrifice igné à l'Éternel.
Hii ni sadaka ya kawaida ya kuteketezwa iliyoanzishwa katika Mlima Sinai kama harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
7 Et tu ajouteras à chaque agneau une libation d'un quart de hin [de vin]; dans le Sanctuaire verse une libation de cervoise à l'Éternel.
Sadaka ya kinywaji itakayotolewa pamoja na kila mwana-kondoo ni robo ya hini ya kinywaji kilichochachuka. Mimina sadaka ya kinywaji kwa Bwana mahali patakatifu.
8 Et tu sacrifieras le second des deux agneaux dans la soirée. Comme l'offrande du matin avec sa libation tu offriras un sacrifice igné, parfum agréable à l'Éternel.
Andaa yule mwana-kondoo wa pili jioni, pamoja na sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kama ulivyofanya kwa ile sadaka nyingine ya asubuhi. Hii ni sadaka iliyotolewa kwa kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
9 Et le jour du Sabbat deux agneaux d'un an sans défaut, et comme offrande deux dixièmes de fleur de farine trempée d'huile et sa libation en sus.
“‘Siku ya Sabato, utatoa sadaka ya wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari pamoja na sadaka yake ya kinywaji na sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta.
10 C'est l'holocauste sabbatique à offrir chaque sabbat outre l'holocauste continuel et sa libation.
Hii ni sadaka ya kuteketezwa itakayotolewa kwa ajili ya kila Sabato, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya kinywaji.
11 Et au commencement de vos mois vous offrirez en holocauste à l'Éternel deux jeunes taureaux et un bélier, sept agneaux d'un an sans défaut,
“‘Siku ya kwanza ya kila mwezi, mtamletea Bwana sadaka ya kuteketezwa ya fahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasiokuwa na dosari.
12 avec offrande de trois dixièmes de fleur de farine trempée d'huile pour chaque taureau, et de deux dixièmes de fleur de farine trempée d'huile pour un bélier,
Pamoja na kila fahali, kutakuwa na sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa, uliochanganywa na mafuta, pamoja na kondoo dume mmoja, sadaka ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta;
13 et pour offrande un dixième de fleur de farine trempée d'huile pour chaque agneau, en holocauste, parfum agréable, sacrifice igné à l'Éternel.
pamoja na kila mwana-kondoo, sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na mafuta. Hii ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri, sadaka ya kuteketezwa iliyotolewa kwa moto kwa Bwana.
14 Et les libations à y ajouter: un demi-hin pour chaque taureau, et un tiers de hin pour le bélier, et un quart de hin de vin par agneau. Tel est l'holocauste mensuel qu'on offrira à chaque nouvelle lune de l'année.
Pamoja na kila fahali kutakuwa na sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai; pamoja na kila kondoo dume, theluthi moja ya hini, na pamoja na kila mwana-kondoo robo hini. Hii ni sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi itakayotolewa kila mwandamo wa mwezi kwa mwaka.
15 Et un bouc sera sacrifié à l'Éternel comme victime expiatoire, en sus de l'holocauste continuel, et sa libation.
Zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya kinywaji, mbuzi mmoja dume atatolewa kwa Bwana kama sadaka ya dhambi.
16 Et au premier mois, le quatorzième jour du mois, il y aura Pâque en l'honneur de l'Éternel.
“‘Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, itafanyika Pasaka ya Bwana.
17 Et le quinzième jour de ce mois, il y aura fête; pendant sept jours on mangera des azymes.
Katika siku ya kumi na tano ya mwezi huo itakuwa sikukuu; kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
18 Le premier jour, sainte convocation: vous vous abstiendrez de toute œuvre de travail,
Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, msifanye kazi za kawaida.
19 et vous offrirez le sacrifice igné d'un holocauste à l'Éternel, deux jeunes taureaux et un bélier et sept agneaux d'un an, qui soient sans défaut,
Leteni mbele za Bwana sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo dume saba wenye umri wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
20 avec une offrande de fleur de farine trempée d'huile, trois dixièmes pour chaque taureau, et deux dixièmes pour le bélier, c'est ce que vous offrirez;
Pamoja na kila fahali, andaa sadaka ya nafaka sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa;
21 puis vous offrirez un dixième pour chacun des sept agneaux,
pia pamoja na kila mmoja wa wale wana-kondoo saba, andaa sehemu ya kumi ya efa.
22 et un bouc expiatoire en propitiation pour vous.
Pia mtoe beberu mmoja kama sadaka ya dhambi ambaye atafanya upatanisho kwa ajili yenu.
23 Vous les sacrifierez outre l'holocauste du matin qui sert à l'holocauste continuel;
Andaa hizi licha ya zile sadaka za kawaida za kuteketezwa za kila asubuhi.
24 vous l'offrirez ainsi chacun des sept jours comme nourriture, en sacrifice igné d'un parfum agréable à l'Éternel, en sus de l'holocauste continuel et sa libation.
Kwa njia hii andaa chakula cha sadaka ya kuteketezwa kila siku, kwa siku saba kama harufu nzuri impendezayo Bwana. Hii itaandaliwa licha ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji.
25 Et le septième jour vous aurez sainte convocation; vous vous abstiendrez de toute œuvre de travail.
Siku ya saba mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
26 Et au jour des premiers fruits, lorsque vous offrirez à l'Éternel une offrande nouvelle après vos semaines [de moisson], vous aurez sainte convocation; vous vous abstiendrez de toute œuvre de travail.
“‘Siku ya malimbuko, mnapomletea Bwana sadaka ya nafaka mpya wakati wa Sikukuu ya Majuma, mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
27 Et vous offrirez en holocauste d'un parfum agréable à l'Éternel deux jeunes taureaux, un bélier, sept agneaux d'un an,
Mlete sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na pia wana-kondoo saba wenye umri wa mwaka mmoja, kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
28 avec une offrande de fleur de farine trempée d'huile, trois dixièmes pour chaque taureau, deux dixièmes pour le bélier,
Pamoja na kila fahali itatolewa sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini;
29 un dixième pour chacun des sept agneaux,
na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba.
30 un bouc pour votre expiation;
Ongeza beberu mmoja kwa kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
31 vous les offrirez en sus de l'holocauste continuel et de l'offrande qui l'accompagne; qu'ils soient sans défaut, et ajoutez-y les libations.
Andaa hizi sadaka pamoja na sadaka zake za vinywaji, kuwa nyongeza ya sadaka za kawaida za kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya nafaka. Hakikisha kuwa wanyama hao hawana dosari.