< Job 36 >
1 Et Elihu poursuivit et dit:
Elihu akaendelea kusema:
2 Accorde-moi un peu de patience, et je t'instruirai! car en faveur de Dieu j'ai encore à parler.
“Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
3 Je prendrai mes preuves de haut, et je justifierai mon Créateur.
Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
4 Car mes discours certes ne seront pas menteurs, et tu trouveras en moi droiture de pensée.
Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
5 Voici, Dieu est grand, mais Il est sans dédain, Il est grand par sa puissante intelligence.
“Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
6 Il ne laisse pas vivre le méchant, et Il fait droit au misérable.
Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
7 Du juste Il ne détourne pas ses yeux, et avec les rois sur le trône pour toujours Il le place, afin qu'il soit élevé.
Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
8 Mais s'il est captif dans les fers, retenu dans les chaînes de l'adversité,
Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
9 c'est que Dieu veut lui dévoiler sa conduite et ses péchés, car il fut orgueilleux;
huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
10 faire que son oreille s'ouvre aux leçons, et lui dire de renoncer au mal.
Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
11 S'il écoute et se soumet, il achève sa vie dans la félicité, et ses années dans les délices;
Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
12 mais, s'il n'écoute pas, il court au devant de la flèche, et il périt, faute d'avoir voulu comprendre.
Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
13 Les impies nourrissent la colère, ne prient point, quand Dieu les enchaîne;
“Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
14 leur âme meurt dans le premier âge, et ils perdent la vie, comme les victimes de l'infamie.
Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
15 Mais Il retire les malheureux de leurs maux, se révélant à eux par les afflictions.
Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
16 Il te tirera de même des serres de l'angoisse, pour te mettre au large, où il n'y aura plus de gêne; et des mets succulents seront servis sur ta table.
“Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
17 Mais si tu te remplis de la pensée de l'impie, le châtiment suivra de près ta pensée.
Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
18 Que la colère de Dieu ne te pousse pas au blasphème! Une grosse rançon ne te ferait pas échapper:
Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
19 ta richesse y suffirait-elle? Ici l'or et les moyens de l'opulence ne font rien.
Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
20 Ne soupire pas après la nuit qui arrache des peuples de leur sol!
Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
21 Veille sur toi! ne prends pas le parti du mal… Car il te semble préférable au malheur.
Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
22 Voici, Dieu est élevé par sa puissance; est-il un maître pareil à Lui?
“Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 Qui lui prescrira ses voies? et qui lui dira: Tu fais mal?
Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
24 Pense à exalter ses œuvres, que les hommes célèbrent par leurs chants!
Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
25 Tous les humains les admirent, quoiqu'un mortel ne les voie que de loin!
Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
26 Voici, Dieu est grand, nous ne Le concevons pas, le nombre de ses ans ne peut être trouvé.
Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
27 Quand Il attire les gouttes de l'eau, la vapeur qu'il en forme distille la pluie,
“Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
28 que versent les nuages qui l'épanchent sur la foule des hommes.
mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
29 Qui comprendra les déchirements de la nue, et le fracas dont Sa tente retentit?
Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
30 Voici, autour de Lui Il déploie la clarté, et prend pour se couvrir la mer jusques dans ses racines.
Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
31 Car tels sont ses moyens pour châtier les peuples, et pour donner la nourriture avec abondance.
Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
32 Il arme ses mains de flammes, et à son ordre elles fondent sur les rebelles:
Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
33 Son grondement l'annonce, annonce aux troupeaux son approche.
Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.