< Job 30 >
1 Et maintenant je suis la risée de mes cadets, dont je ne daignais pas associer les pères aux chiens de mes troupeaux.
“Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
2 Aussi bien la force de leurs mains, qu'eût-elle été pour moi? Pour ces hommes il n'y a jamais d'âge mûr:
Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
3 desséchés par la disette et la faim, ils rongent la steppe, le vieux désert et la solitude;
Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
4 ils cueillent l'arroche le long des haies, et la racine du genêt est leur pain;
Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
5 ils sont bannis de la société; on crie après eux, comme après les larrons;
Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
6 réduits à habiter des ravins affreux, les antres de la terre et des rochers,
Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
7 parmi les buissons ils poussent des hurlements, et pêle-mêle se blottissent sous les ronces,
Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
8 impies, hommes sans nom, qui furent chassés du pays!
Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
9 Et maintenant je suis leur chanson, et le sujet de leurs discours;
“Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
10 ils me maudissent, puis me quittent, et devant moi ne s'abstiennent pas de cracher.
Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
11 Bien plus, ils déceignent leur corde, et m'en frappent, et ils secouent tout frein devant moi.
Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
12 A ma droite leur engeance se lève; ils ne me laissent pas prendre pied, et se fraient jusqu'à moi une voie pour me nuire;
Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
13 ils ruinent mon sentier, aident à ma perte, eux que personne ne soutient.
Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
14 Ils viennent comme par une large brèche, se précipitent avec fracas.
Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
15 Toutes les terreurs se tournent contre moi; c'est comme un ouragan qui poursuit ma grandeur, et, comme un nuage, mon bonheur a passé.
Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
16 Aussi, maintenant mon âme en moi épanche sa plainte; les jours de malheur m'ont saisi.
“Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
17 La nuit perce mes os et les détache, et le mal qui me ronge, ne sommeille pas.
Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
18 Sous Ses coups puissants mon manteau se déforme, comme ma tunique il s'applique à mon corps.
Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
19 Il m'a jeté dans la boue, et assimilé à la poudre et à la cendre.
Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
20 Je crie à Toi, et Tu ne m'écoutes pas! je suis là debout, et Tu me regardes!
“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
21 Tu T'es changé pour moi en cruel ennemi, et Tu m'opposes la force de ton bras.
Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
22 Tu me soulèves sur la tempête et m'emportes avec elle, et pour moi tu anéantis tout espoir de salut.
Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
23 Car, je le sais, c'est à la mort que tu me mènes, au rendez-vous de tous les vivants.
Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
24 Cependant du sein des décombres ne tend-on pas la main? Quand on périt, ne crie-t-on pas au secours?
“Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
25 Oui, je pleurai sur ceux pour qui les temps étaient durs, et les indigents attristaient mon âme.
Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
26 Et pourtant! j'attendais le bonheur, et le malheur est venu; j'espérais la clarté, et les ténèbres sont arrivées.
Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
27 Mes entrailles bouillonnent, et n'ont aucun repos, des jours de chagrin me sont survenus.
Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
28 Je marche noirci, mais non par le soleil; debout dans l'assemblée, je me lamente,
Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
29 devenant ainsi le frère des chacals, et l'égal de l'autruche.
Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
30 Ma peau noircit et tombe, et mes os brûlent d'inflammation.
Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
31 Ainsi le deuil a remplacé mon luth, et des sons lugubres, ma cornemuse.
Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.