< Jérémie 39 >

1 Et lorsque Jérusalem fut prise, (la neuvième année de Sédécias, roi de Juda, le dixième mois, Nébucadnézar, roi de Babel, avec toute son armée, vint devant Jérusalem, et l'assiégea;
Hivi ndivyo Yerusalemu ilivyotwaliwa: Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Mfalme Sedekia wa Yuda, katika mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu na akauzunguka mji.
2 la onzième année de Sédécias, le quatrième mois, le neuvième jour du mois, la ville fut forcée; )
Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne wa mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Sedekia, ukuta wa mji ulibomolewa.
3 alors vinrent tous les généraux du roi de Babel, et ils se placèrent à la Porte du milieu; c'étaient Nergal-Scharétser, Samgar-Nébo, Sareskim, chef des eunuques, Nergal-Scharétser, chef des mages, et tous les autres chefs du roi de Babel.
Kisha maafisa wote wa mfalme wa Babeli wakaja na kuketi kwenye Lango la Kati, nao ni: Nergal-Shareza wa Samgari, Nebo-Sarsekimu afisa mkuu, Nergal-Shareza afisa mwenye cheo cha juu, na maafisa wengine wote wa mfalme wa Babeli.
4 Et lorsque Sédécias, roi de Juda, et tous les gens de guerre les virent, ils s'enfuirent, et sortirent nuitamment de la ville par le chemin des jardins du roi, et passant la porte entre les deux murailles, ils sortirent du côté de la plaine.
Mfalme Sedekia wa Yuda na askari wote walipowaona, wakakimbia na kuondoka mjini usiku kwa njia ya bustani ya mfalme, kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili, wakaelekea Araba.
5 Alors l'armée des Chaldéens se mit à leur poursuite, et ils atteignirent Sédécias dans les campagnes de Jéricho, et ils le prirent, et le menèrent à Nébucadnézar, roi de Babel, à Ribla dans le pays de Hamath, lequel prononça son jugement sur lui.
Lakini jeshi la Wakaldayo likawafuatia na kumpata Sedekia katika sehemu tambarare za Yeriko. Wakamkamata na kumpeleka kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu.
6 Et le roi de Babel égorgea les fils de Sédécias à Ribla sous ses yeux; et le roi de Babel égorgea aussi tous les nobles de Juda,
Huko Ribla, mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake, na pia akawaua wakuu wote wa Yuda.
7 et il creva les yeux à Sédécias, et le lia de chaînes pour le mener à Babel.
Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia na kumfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
8 Et les Chaldéens brûlèrent par le feu la maison du roi et les maisons du peuple, et abattirent les murs de Jérusalem.
Jeshi la Wakaldayo likachoma moto jumba la kifalme na nyumba za watu, na kuzibomoa kuta za Yerusalemu.
9 Et le reste du peuple demeuré dans la ville, et les transfuges qui avaient passé à lui, le reste du peuple, Nébuzaradan, chef des satellites, les déporta à Babel;
Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme akawachukua na kuwapeleka uhamishoni Babeli watu waliokuwa wamebaki ndani ya mji, pamoja na wale waliokuwa wamejisalimisha kwake, na watu wengine wote.
10 mais Nébuzaradan, chef des satellites, laissa dans le pays de Juda les petits d'entre le peuple qui ne possédaient rien, et il leur donna des vignes et des champs dans ce temps-là.
Lakini Nebuzaradani kiongozi wa walinzi aliwabakiza baadhi ya watu maskini katika nchi ya Yuda, ambao hawakuwa na kitu. Naye wakati huo akawapa mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
11 Et Nébucadnézar, roi de Babel, donna ses ordres quant à Jérémie par Nébuzaradan, chef des satellites, et dit:
Basi, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa ametoa maagizo kuhusu Yeremia kupitia Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme akisema:
12 Prends-le, et aie soin de lui, et ne lui fais aucun mal, et traite-le, ainsi qu'il te le dira.
“Mchukue umtunze. Usimdhuru, lakini umfanyie chochote anachotaka.”
13 Alors Nébuzaradan, chef des satellites, et Nébuschasban, chef des eunuques, et Nergal-Scharétser, chef des mages, et tous les chefs du roi de Babel,
Basi Nebuzaradani kiongozi wa walinzi, Nebushazbani afisa mkuu, Nergal-Shareza afisa wa cheo cha juu, na maafisa wengine wote wa mfalme wa Babeli
14 envoyèrent chercher Jérémie du vestibule de la prison, et le remirent à Gédalia, fils d'Achikam, fils de Schaphan, pour le conduire dans sa maison. Et ainsi il demeura au milieu du peuple.
wakatuma watu kumwondoa Yeremia kutoka ua wa walinzi. Wakamkabidhi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani, ili amrudishe nyumbani kwake. Kwa hiyo akabaki miongoni mwa watu wake mwenyewe.
15 Et la parole de l'Éternel fut adressée à Jérémie, pendant qu'il était détenu dans le vestibule de la prison, en ces mots:
Wakati Yeremia alipokuwa amezuiliwa katika ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia kusema:
16 Va, et parle à Ebedmélech, l'Éthiopien, et lui dis: Ainsi parle l'Éternel des armées, Dieu d'Israël: Vois, je vais faire arriver ce que j'ai prononcé sur cette ville, du mal et non du bien, et tu seras témoin de ces événements en ce temps-là.
“Nenda ukamwambie Ebed-Meleki Mkushi, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Ninakaribia kutimiza maneno yangu dhidi ya mji huu kwa njia ya maafa, wala si kwa kuwafanikisha. Wakati huo hayo yatatimizwa mbele ya macho yako.
17 Mais je te délivrerai en ce jour-là, dit l'Éternel, et tu ne seras point livré aux mains des hommes que tu redoutes,
Lakini siku hiyo nitakuokoa, asema Bwana; hutatiwa mikononi mwa wale unaowaogopa.
18 car je veux te sauver, et tu ne tomberas point sous le glaive, tu auras ta vie pour ton butin, parce que tu as eu confiance en moi, dit l'Éternel.
Nitakuokoa; hutaanguka kwa upanga, lakini maisha yako yatakuwa salama, kwa sababu unanitumaini, asema Bwana.’”

< Jérémie 39 >