< Jérémie 35 >
1 La parole qui fut adressée à Jérémie par l'Éternel, dans le temps de Jéhojakim, fils de Josias, roi de Juda, en ces mots:
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, wakati wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda:
2 Rends-toi auprès de la maison des Réchabites, et parle-leur, et amène-les dans la maison de l'Éternel, dans l'une des chambres, et offre-leur du vin à boire.
“Nenda kwa jamaa ya Warekabi, uwaalike waje kwenye moja ya vyumba vya pembeni vya nyumba ya Bwana, na uwape divai wanywe.”
3 Et je pris Jaasénia, fils de Jérémie, fils de Habazinia, et ses frères et tous ses fils, et toute la maison des Réchabites,
Basi nikaenda kumwita Yaazania mwana wa Yeremia, mwana wa Habazinia, na ndugu zake na wanawe wote, yaani jamaa nzima ya Warekabi.
4 et je les amenai à la maison de l'Éternel, dans la chambre des fils de Hanan, fils de Gédalia, homme de Dieu, laquelle est à côté de la chambre des princes, au-dessus de la chambre de Mahaséïa, fils de Sallum, garde du seuil.
Nikawaleta katika nyumba ya Bwana, ndani ya chumba cha wana wa Hanani mwana wa Igdalia mtu wa Mungu. Kilikuwa karibu na chumba cha maafisa, ambacho kilikuwa juu ya kile cha Maaseya mwana wa Shalumu, aliyekuwa bawabu.
5 Et je plaçai devant les fils de la maison des Réchabites des coupes pleines de vin, et des calices, et je leur dis: « Buvez du vin! »
Kisha nikaweka mabakuli yaliyojaa divai na baadhi ya vikombe mbele ya watu wa jamaa ya Warekabi na kuwaambia, “Kunyweni divai.”
6 Mais ils dirent: Nous ne buvons pas de vin; car Jonadab, fils de Réchab, notre père, nous a donné ce commandement: Vous ne boirez point de vin, ni vous, ni vos fils, à perpétuité;
Lakini wao wakajibu, “Sisi hatunywi divai, kwa sababu baba yetu Yonadabu mwana wa Rekabu, alitupa agizo hili: ‘Ninyi wala wazao wenu kamwe msinywe divai.
7 et vous ne bâtirez point de maisons, et ne sèmerez aucune semence, et ne planterez ni ne posséderez des vignes; mais vous habiterez sous des tentes toute votre vie, afin que vous viviez longtemps dans le pays où vous séjournez.
Pia msijenge nyumba kamwe, wala kuotesha mbegu au kupanda mashamba ya mizabibu. Kamwe msiwe na kitu chochote katika hivi, lakini siku zote lazima muishi kwenye mahema. Ndipo mtakapoishi kwa muda mrefu katika nchi ambayo ninyi ni wahamiaji.’
8 Et nous sommes dociles à la voix de Jonadab, fils de Réchab, notre père, en tout ce qu'il nous a prescrit, de sorte que nous ne buvons pas de vin durant toute notre vie, ni nous, ni nos femmes, ni nos fils, ni nos filles,
Tumetii kila kitu ambacho baba yetu Yonadabu mwana wa Rekabu alituamuru. Sisi wenyewe wala wake zetu wala wana wetu na binti zetu kamwe hatujanywa divai
9 et que nous ne bâtissons pas de maisons pour nous loger, et que nous ne possédons ni vignes, ni champs, ni terre ensemencée,
wala kujenga nyumba za kuishi au kuwa na mashamba ya mizabibu, mashamba au mazao.
10 et nous habitons sous des tentes, et nous écoutons et nous pratiquons tout ce que nous a prescrit Jonadab, notre père.
Tumeishi katika mahema na tumetii kikamilifu kila kitu alichotuamuru baba yetu Yonadabu.
11 Et, quand Nébucadnézar, roi de Babel, s'avança dans le pays, nous dîmes: Venez, et fuyons à Jérusalem devant l'armée des Chaldéens et devant l'armée de Syrie; c'est ainsi que nous habitons dans Jérusalem.
Lakini wakati Nebukadneza mfalme wa Babeli alipoivamia nchi hii, tulisema, ‘Njooni, lazima twende Yerusalemu ili kukimbia majeshi ya Wakaldayo na ya Washamu.’ Kwa hiyo tumeishi Yerusalemu.”
12 Alors la parole de l'Éternel fut adressée à Jérémie en ces mots:
Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
13 Ainsi parle l'Éternel des armées, Dieu d'Israël: Va et dis aux hommes de Juda et aux habitants de Jérusalem: De là ne tirerez-vous pas cette leçon, qu'il vous faut obéir à mes paroles? dît l'Éternel.
“Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliye Mungu wa Israeli, asemalo: Nenda ukawaambie watu wa Yuda na watu wa Yerusalemu, ‘Je, hamwezi kujifunza kutoka kwa wana wa Rekabu, na kuyatii maneno yangu?’ asema Bwana.
14 On accomplit les préceptes de Jonadab, fils de Réchab, lesquels il a donnés comme règle à ses fils, de ne point boire de vin, et ils n'en ont pas bu jusques aujourd'hui, car ils sont dociles à l'ordre de leur père; et moi je vous ai parlé dès le matin, et vous ne m'obéissez pas!
‘Yonadabu mwana wa Rekabu aliwaagiza wanawe wasinywe divai, na agizo hilo wamelishika mpaka leo hawanywi divai, kwa sababu wanatii amri ya baba yao. Lakini nimenena nanyi tena na tena, lakini hamkunitii mimi.
15 Et je vous ai envoyé tous mes serviteurs, les prophètes, dès le matin, pour vous dire: Renoncez donc chacun à votre mauvaise voie, et amendez votre conduite, et n'allez plus après d'autres dieux pour les servir; alors vous resterez dans le pays que j'ai donné à vous et à vos pères; mais vous n'avez point prêté l'oreille, et ne m'avez point obéi.
Tena na tena nimewatuma watumishi wangu wote manabii kwenu. Wakasema, “Kila mmoja wenu ni lazima ageuke na kuacha njia zake mbaya, na kuyatengeneza matendo yake. Msifuate miungu mingine ili kuitumikia. Ndipo mtakapoishi katika nchi niliyowapa ninyi na baba zenu.” Lakini hamkujali wala kunisikiliza.
16 Oui, les fils de Jonadab, fils de Réchab, observent la règle que leur donna leur père, et ce peuple ne m'obéit pas!
Wazao wa Yonadabu mwana wa Rekabu walitimiza amri ambayo baba yao aliwapa, lakini watu hawa hawakunitii mimi.’
17 C'est pourquoi, ainsi parle l'Éternel, Dieu des armées, Dieu d'Israël: Voici, j'amène sur Juda et sur tous les habitants de Jérusalem tous les maux dont je les ai menacés, parce que je leur ai parlé, et qu'ils n'ont point écouté; et que je les ai appelés, et qu'ils n'ont point répondu.
“Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Sikilizeni! Nitaleta juu ya Yuda na juu ya kila mmoja aishiye Yerusalemu kila aina ya maafa niliyotamka dhidi yao. Nilinena nao, lakini hawakusikiliza. Niliwaita, lakini hawakujibu.’”
18 Et Jérémie dit à la maison des Réchabites: Ainsi parle l'Éternel des armées, Dieu d'Israël: Parce que vous êtes dociles au commandement de Jonadab votre père, et que vous observez tous ses commandements et que vous faites selon tout ce qu'il vous a commandé,
Kisha Yeremia akaiambia jamaa ya Warekabi, “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: ‘Mmetii amri ya baba yenu Yonadabu, na mmefuata mafundisho yake yote na mmefanya kila kitu alichowaamuru.’
19 à cause de cela, ainsi prononce l'Éternel des armées, Dieu d'Israël: Il ne manquera point à Jonadab, fils de Réchab, d'un homme qui se tienne en ma présence, dans tous les âges.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Yonadabu mwana wa Rekabu hatakosa kamwe kuwa na mtu wa kunitumikia mimi.’”